Marko 13 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 13:1-37

Dalili Za Siku Za Mwisho

(Mathayo 24:1-2; Luka 21:5-6)

113:1 Mt 24:1; Lk 21:5Yesu alipokuwa akitoka Hekaluni, mmojawapo wa wanafunzi wake akamwambia, “Mwalimu! Tazama jinsi mawe haya yalivyo makubwa, na majengo haya yalivyo mazuri!”

213:2 Lk 19:44Ndipo Yesu akajibu akasema, “Je, unayaona majengo haya yalivyo makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali yote yatabomolewa.”

Mateso Yatabiriwa

(Mathayo 24:3-14; Luka 21:7-19)

313:3 Mt 21:1; 4:21Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni mkabala na Hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamuuliza faraghani, 413:4 Mt 24:3; Lk 21:7“Tafadhali tuambie, mambo haya yatatukia lini? Nayo dalili ya kuwa hayo yote yanakaribia kutimia itakuwa gani?”

513:5 Yer 29:8; 1Tim 4:1Yesu akawaambia: “Jihadharini mtu yeyote asiwadanganye. 6Wengi watakuja kwa Jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye,’ nao watawadanganya wengi. 7Msikiapo habari za vita na uvumi wa vita, msiwe na hofu. Mambo haya hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado. 813:8 Mt 24:8; Isa 19:2; 2Nya 15:6Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na mitetemeko sehemu mbalimbali na njaa. Haya yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.

913:9 Mt 10:17“Lakini ninyi jihadharini. Kwa maana watawapeleka katika mabaraza yao na kupigwa mijeledi katika masinagogi. Mtashtakiwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwa ushuhuda kwao. 1013:10 Mt 10:19-20Nayo habari njema lazima ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote kabla ule mwisho haujawadia. 1113:11 Lk 12:11-12Mtakapokamatwa na kushtakiwa, msisumbuke awali kuhusu mtakalosema. Semeni tu lolote mtakalopewa wakati huo, kwa kuwa si ninyi mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho Mtakatifu.

1213:12 Mik 7:6; Lk 12:51-53“Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, naye baba atamsaliti mtoto wake. Watoto nao wataasi dhidi ya wazazi wao na kusababisha wauawe. 1313:13 Yn 15:21; Mt 10:22Watu wote watawachukia kwa ajili ya Jina langu. Lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.

Chukizo La Uharibifu

(Mathayo 24:15-28; Luka 21:20-24)

1413:14 Dan 11:31; 12:11“Mtakapoona ‘chukizo la uharibifu’ limesimama mahali pasipolipasa (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani. 15Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke au kuingia ndani ili kuchukua chochote. 16Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. 1713:17 Lk 22:39; 21:23Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! 18Ombeni mambo haya yasitokee wakati wa baridi. 1913:19 Mk 10:6; Dan 9:26; Yoe 2:2Kwa maana siku hizo zitakuwa za dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo, hapo Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka leo, na wala haitakuwako tena kamwe. 20Kama Bwana asingelifupisha siku hizo, kamwe asingeliokoka mtu yeyote. Lakini kwa ajili ya wateule, wale aliowachagua, amezifupisha siku hizo. 2113:21 Lk 17:23; 21:8Wakati huo mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristo13:21 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. huyu hapa!’ au, ‘Tazama, yuko kule,’ msisadiki. 2213:22 Mt 7:15; Yn 4:48; 2The 2:9-10Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara na maajabu ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule. 2313:23 2Pet 3:17Hivyo jihadharini. Nimekwisha kuwaambia mambo haya yote mapema kabla hayajatukia.

Kuja Kwa Mwana Wa Adamu

(Mathayo 24:29-31; Luka 21:25-28)

2413:24 Isa 13:10“Lakini katika siku hizo, baada ya hiyo dhiki,

“ ‘jua litatiwa giza

nao mwezi hautatoa nuru yake;

2513:25 Isa 34:4; Mt 24:9nazo nyota zitaanguka kutoka angani,

na nguvu za anga zitatikisika.’

2613:26 Dan 7:13; Ufu 1:7“Ndipo watu wote watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu. 2713:27 Zek 2:6Naye atawatuma malaika wake wawakusanye wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka miisho ya dunia hadi miisho ya mbingu.

Somo Kuhusu Mtini

(Mathayo 24:32-35; Luka 21:29-33)

2813:28 Mt 24:32; Lk 21:29“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia. 29Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni. 3013:30 Lk 17:25; Mk 9:11Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia. 3113:31 Mt 5:18Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa

(Mathayo 24:36-44)

3213:32 Mdo 1:7; 1The 5:1-2“Kwa habari ya siku ile na saa hakuna yeyote ajuaye, hata malaika walio mbinguni wala Mwana, ila Baba peke yake. 33Jihadharini! Kesheni! Kwa maana hamjui wakati ule utakapowadia. 3413:34 Mt 25:14Ni kama mtu anayesafiri. Anaiacha nyumba yake na kuwaachia watumishi wake kuiangalia, kila mtu na kazi yake, kisha akamwamuru yule bawabu aliye mlangoni akeshe.

3513:35 Mt 24:42, 44“Basi kesheni kwa sababu hamjui ni lini mwenye nyumba atakaporudi: iwapo ni jioni, au ni usiku wa manane, au alfajiri awikapo jogoo, au mapambazuko. 36Kama akija ghafula, asije akawakuta mmelala. 3713:37 Lk 12:35-40Lile ninalowaambia ninyi, nawaambia watu wote: ‘Kesheni!’ ”

La Bible du Semeur

Marc 13:1-37

De la destruction de Jérusalem à la venue du Fils de l’homme

(Mt 24.1-3 ; Lc 21.5-7)

1Comme Jésus sortait du Temple, un de ses disciples lui dit : Regarde, Maître, quelles belles pierres ! Quel édifice magnifique !

2Jésus lui répondit : Oui, regarde bien ces grandes constructions : il ne restera pas une pierre sur une autre, tout sera démoli.

3Puis il alla s’asseoir sur les pentes du mont des Oliviers, en face du Temple.

Pierre, Jacques, Jean et André le prirent à part et lui demandèrent : 4Dis-nous : quand cela se produira-t-il et à quel signe reconnaîtra-t-on que tous ces événements seront près de s’accomplir13.4 Autre traduction : quel signe annoncera la fin de toutes choses ? ?

(Mt 24.4-14 ; Lc 21.8-19)

5Là-dessus, Jésus leur dit : Faites attention que personne ne vous induise en erreur. 6Plusieurs viendront sous mon nom en disant : « C’est moi le Messie ! », et ils tromperont beaucoup de gens.

7Quand vous entendrez parler de guerres et de menaces de guerres, ne vous laissez pas troubler, car cela doit arriver, mais ce ne sera pas encore la fin. 8En effet, on verra se dresser une nation contre une nation, un royaume contre un autre13.8 Voir Es 19.2., il y aura en divers lieux des tremblements de terre et des famines, mais ce ne seront que les premières douleurs de l’enfantement.

9Quant à vous, faites attention à vous-mêmes : on vous traduira devant les tribunaux des Juifs, on vous fouettera dans les synagogues, vous comparaîtrez devant des gouverneurs et des rois à cause de moi, pour leur apporter un témoignage. 10Il faut, avant tout, que la Bonne Nouvelle de l’Evangile soit annoncée à tous les peuples. 11Quand on vous emmènera pour vous traduire devant les autorités, ne vous inquiétez pas à l’avance de ce que vous direz, mais dites simplement ce qui vous sera donné au moment même : car ce n’est pas vous qui parlerez, mais l’Esprit Saint. 12Le frère livrera son propre frère pour le faire condamner à mort, et le père livrera son enfant. Des enfants se dresseront contre leurs parents et les feront mettre à mort. 13Tout le monde vous haïra à cause de moi. Mais celui qui tiendra bon jusqu’au bout sera sauvé.

(Mt 24.15-31 ; Lc 21.20-28 ; 17.23-24)

14Quand vous verrez l’abominable profanation13.14 Dn 9.27 ; 11.31 ; 12.11. établie dans le lieu où elle ne doit pas être – que celui qui lit comprenne ! – alors, que ceux qui sont en Judée s’enfuient dans les montagnes. 15Si quelqu’un est sur son toit en terrasse, qu’il ne rentre pas à l’intérieur de sa maison pour emporter quelque bien qui s’y trouve. 16Que celui qui sera dans les champs ne retourne pas chez lui pour aller chercher son manteau. 17Malheur, en ces jours-là, aux femmes enceintes et à celles qui allaitent ! 18Priez pour que cela n’arrive pas en hiver, 19car ce seront des jours de détresse comme on n’en a pas connus depuis que Dieu a créé le monde13.19 Dn 12.1. et comme jamais plus on n’en verra de semblables.

20Vraiment, si le Seigneur n’avait pas décidé de réduire le nombre de ces jours, personne n’en réchapperait ; mais, à cause de ceux qu’il a choisis, il abrégera ce temps.

21Si quelqu’un vous dit alors : « Voyez, le Messie est ici ! » ou : « Il est là ! » ne le croyez pas. 22De faux messies surgiront, ainsi que de faux prophètes. Ils produiront des signes miraculeux et des prodiges au point de tromper, si c’était possible, ceux que Dieu a choisis. 23Vous donc, faites attention, je vous ai prévenus !

24Cependant, en ces jours-là, après ce temps de détresse,

le soleil s’obscurcira,

la lune perdra sa clarté,

25les étoiles tomberont du ciel ;

les puissances célestesseront ébranlées13.25 Es 13.10 ; 34.4..

(Mt 24.32-36 ; Lc 21.29-33)

26Alors on verra le Fils de l’homme venir sur les nuées13.26 Dn 7.13. avec beaucoup de puissance et de gloire. 27Il enverra ses anges rassembler ses élus des quatre coins du monde, d’un bout à l’autre de l’univers.

28Que l’exemple du figuier vous serve d’enseignement : quand ses rameaux deviennent tendres et que ses feuilles poussent, vous savez que l’été est proche. 29De même, quand vous verrez se produire ces événements, sachez que le Fils de l’homme est proche, comme aux portes de la ville. 30Vraiment, je vous assure que cette génération-ci ne passera pas jusqu’à ce que tout cela vienne à se réaliser. 31Le ciel et la terre passeront, mais mes paroles ne passeront jamais. 32Quant au jour ou à l’heure, personne ne sait quand cela se produira, ni les anges du ciel, ni même le Fils ; seul, le Père le sait.

(Mt 24.42)

33Soyez vigilants, restez sur vos gardes, puisque vous ne savez pas quand viendra le moment.

34Les choses se passeront comme lorsqu’un homme quitte sa maison pour un long voyage et en laisse la responsabilité à ses serviteurs, en confiant à chacun sa tâche. Il commande au portier de veiller. 35Tenez-vous donc vous aussi en éveil ! Car vous ne savez pas quand le maître de la maison doit revenir : sera-ce tard ? à minuit ? au chant du coq ? ou le matin ? 36Qu’il ne vous trouve pas en train de dormir s’il revient à l’improviste ! 37Ce que je dis là, je vous le dis à tous : Tenez-vous en éveil !