Maombolezo 5 – Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) NEN

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Maombolezo 5:1-22

15:1 Za 44:13-16; 89:50Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata,

tazama, nawe uione aibu yetu.

25:2 Za 79:1; Sef 1:13; Yer 17:4Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni,

na nyumba zetu kwa wageni.

35:3 Kut 22:24; Yer 15:8; 18:21Tumekuwa yatima wasio na baba,

mama zetu wamekuwa kama wajane.

45:4 Isa 55:1; Eze 4:16-17; Isa 3:1Ni lazima tununue maji tunayokunywa,

kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.

55:5 Isa 47:6; Neh 9:37; Yos 1:13Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu,

tumechoka na hakuna pumziko.

65:6 Yer 2:36; Mwa 24:2; Hos 5:13; 7:11; Yer 50:15; Hos 12:1Tumejitolea kwa Misri na Ashuru

tupate chakula cha kutosha.

75:7 Yer 14:20; 16:12; Eze 8:2; Yer 31:29; Eze 18:2; Mt 23:32Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena,

na sisi tunachukua adhabu yao.

85:8 Neh 5:15; Zek 11:6Watumwa wanatutawala

na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.

9Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu

kwa sababu ya upanga jangwani.

105:10 Ay 30:30; Mao 4:8-9Ngozi yetu ina joto kama tanuru,

kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.

115:11 Mwa 34:29; Zek 14:2; Isa 13:16Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni,

na mabikira katika miji ya Yuda.

12Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao,

wazee hawapewi heshima.

135:13 Amu 13:16; 16:21Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia,

wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.

145:14 Isa 24:8; Yer 7:34; 2Fal 25:18Wazee wameondoka langoni la mji,

vijana wameacha kuimba nyimbo zao.

155:15 Amu 8:10; Yer 25:10Furaha imeondoka mioyoni mwetu,

kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.

165:16 Yer 13:18; 14:20; Za 89:39; Ay 19:9; Isa 3:11Taji imeanguka kutoka kichwani petu.

Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!

175:17 Ay 17:7; Za 6:7; 16:8; Yer 8:18Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia,

kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,

185:18 Isa 27:10; Mik 3:12; Za 74:2-4kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa,

nao mbweha wanatembea juu yake.

195:19 1Nya 16:31; Za 45:6; 102:22-27Wewe, Ee Bwana unatawala milele,

kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi.

205:20 Za 13:1; 44:24; 71:11Kwa nini watusahau siku zote?

Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu?

215:21 Isa 60:20-22; Za 80:3Turudishe kwako mwenyewe, Ee Bwana,

ili tupate kurudi.

Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale,

225:22 Isa 64:9; Yer 6:30; Za 53:5; 60:12isipokuwa uwe umetukataa kabisa

na umetukasirikia pasipo kipimo.