Maombolezo 1 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Maombolezo 1:1-22

1 Sura hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 11:1 Isa 47:7-8; Ezr 4:20; Eze 5:5; Isa 3:26; Yer 42:2; Law 26:43; Mao 1:9Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa,

mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu!

Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane,

ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa!

Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo

sasa amekuwa mtumwa.

21:2 Za 6:6; Yer 4:30; Mik 7:5; Yer 30:14; 13:17; Mao 1:16; Ay 7:3Kwa uchungu, hulia sana usiku,

machozi yapo kwenye mashavu yake.

Miongoni mwa wapenzi wake wote

hakuna yeyote wa kumfariji.

Rafiki zake wote wamemsaliti,

wamekuwa adui zake.

31:3 Yer 13:19; Kum 28:64-65; Kut 15:9; Law 26:14, 32, 33Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili,

Yuda amekwenda uhamishoni.

Anakaa miongoni mwa mataifa,

hapati mahali pa kupumzika.

Wote ambao wanamsaka wamemkamata

katikati ya dhiki yake.

41:4 Isa 27:10; Yer 9:11; Yoe 1:8-13Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza,

kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja

kwenye sikukuu zake zilizoamriwa.

Malango yake yote yamekuwa ukiwa,

makuhani wake wanalia kwa uchungu,

wanawali wake wanahuzunika,

naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu.

51:5 Isa 22:5; Yer 10:20; 39:9; 30:14; Mao 3:39; Yer 30:15; 52:28-30; Za 5:10; Mao 2:17Adui zake wamekuwa mabwana zake,

watesi wake wana raha.

Bwana amemletea huzuni

kwa sababu ya dhambi zake nyingi.

Watoto wake wamekwenda uhamishoni,

mateka mbele ya adui.

61:6 Yer 13:18; Za 9:14; Law 26:36Fahari yote imeondoka

kutoka kwa Binti Sayuni.

Wakuu wake wako kama ayala

ambaye hapati malisho,

katika udhaifu wamekimbia

mbele ya anayewasaka.

71:7 2Fal 14:26; Yer 37:7; Mik 4:11; Mao 4:17; Yer 2:26Katika siku za mateso yake na kutangatanga,

Yerusalemu hukumbuka hazina zote

ambazo zilikuwa zake siku za kale.

Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui,

hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia.

Watesi wake walimtazama

na kumcheka katika maangamizi yake.

81:8 Isa 59:2-13; Za 38:8; Yer 13:22-26; 2:22Yerusalemu ametenda dhambi sana

kwa hiyo amekuwa najisi.

Wote waliomheshimu wanamdharau,

kwa maana wameuona uchi wake.

Yeye mwenyewe anapiga kite

na kugeukia mbali.

91:9 Isa 47:7; Eze 24:13; Yer 13:18; Mhu 4:1; Yer 16:7; Za 25:18; Kum 32:29Uchafu wake umegandamana na nguo zake;

hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye.

Anguko lake lilikuwa la kushangaza,

hapakuwepo na yeyote wa kumfariji.

“Tazama, Ee Bwana, teso langu,

kwa maana adui ameshinda.”

101:10 Neh 13:1; Kum 23:3; Yer 51:51; Isa 64:11; Za 74:7-8Adui ametia mikono

juu ya hazina zake zote,

aliona mataifa ya kipagani

wakiingia mahali patakatifu pake,

wale uliowakataza kuingia

kwenye kusanyiko lako.

111:11 Za 38:8; Yer 38:9; 37:21; 52:6Watu wake wote wanalia kwa uchungu

watafutapo chakula;

wanabadilisha hazina zao kwa chakula

ili waweze kuendelea kuishi.

“Tazama, Ee Bwana, ufikiri,

kwa maana nimedharauliwa.”

121:12 Yer 18:16; Isa 10:4; Yer 30:24; Dan 9:12; Isa 13:13; Mit 24:21; Lk 21:22“Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando?

Angalieni kote mwone.

Je, kuna maumivu kama maumivu yangu

yale yaliyotiwa juu yangu,

yale Bwana aliyoyaleta juu yangu

katika siku ya hasira yake kali?

131:13 Ay 30:30; Za 102:3; Hab 3:16; Yer 44:6; Eze 12:13; Ay 18:8; Za 66:11; Hos 7:12“Kutoka juu alipeleka moto,

akaushusha katika mifupa yangu.

Aliitandia wavu miguu yangu

na akanirudisha nyuma.

Akanifanya mkiwa,

na mdhaifu mchana kutwa.

141:14 Isa 47:6; Yer 15:12; 32:5“Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira,

kwa mikono yake zilifumwa pamoja.

Zimefika shingoni mwangu

na Bwana ameziondoa nguvu zangu.

Amenitia mikononi mwa wale

ambao siwezi kushindana nao.

151:15 Yer 37:10; Isa 41:2; 28:1; Yer 18:21; Ufu 14:19; Yer 14:17; Amu 6:11; Isa 63:3“Bwana amewakataa wapiganaji wa vita

wote walio kati yangu,

ameagiza jeshi dhidi yangu

kuwaponda vijana wangu wa kiume.

Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga

Bikira Binti Yuda.

161:16 Za 119:136; Ay 7:3; Yer 16:7; 13:17; 14:17; Isa 22:4; Mao 3:48-49“Hii ndiyo sababu ninalia

na macho yangu yanafurika machozi.

Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji,

hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu.

Watoto wangu ni wakiwa

kwa sababu adui ameshinda.”

171:17 Yer 4:31; Kut 23:21; Law 18:25-28Sayuni ananyoosha mikono yake,

lakini hakuna yeyote wa kumfariji.

Bwana ametoa amri kwa ajili ya Yakobo

kwamba majirani zake wawe adui zake;

Yerusalemu umekuwa

kitu najisi miongoni mwao.

181:18 1Sam 12:14; Kum 28:32; Neh 9:33; Ezr 9:15; Kut 9:27; Dan 9:7Bwana ni mwenye haki,

hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake.

Sikilizeni, enyi mataifa yote,

tazameni maumivu yangu.

Wavulana wangu na wasichana wangu

wamekwenda uhamishoni.

191:19 Mao 2:20; Yer 14:15; 22:20“Niliita washirika wangu

lakini walinisaliti.

Makuhani wangu na wazee wangu

waliangamia mjini

walipokuwa wakitafuta chakula

ili waweze kuishi.

201:20 Yer 4:19; Kum 32:25; Eze 7:15; Ay 20:2; Mao 2:11; Isa 16:11; Hos 11:8“Angalia, Ee Bwana, jinsi nilivyo katika dhiki!

Nina maumivu makali ndani yangu,

nami ninahangaika moyoni mwangu,

kwa kuwa nimekuwa mwasi sana.

Huko nje, upanga unaua watu,

ndani, kipo kifo tu.

211:21 Za 38:8; Mao 2:15; Yer 30:16; Isa 47:11; Za 6:6“Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu,

lakini hakuna yeyote wa kunifariji.

Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu,

wanafurahia lile ulilolitenda.

Naomba uilete siku uliyoitangaza

ili wawe kama mimi.

221:22 Neh 4:5; Za 6:6“Uovu wao wote na uje mbele zako;

uwashughulikie wao

kama vile ulivyonishughulikia mimi

kwa sababu ya dhambi zangu zote.

Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi

na moyo wangu umedhoofika.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

耶利米哀歌 1:1-22

凄惨的耶路撒冷

1从前人烟稠密的城,

现在何其荒凉!

从前扬威万邦的强国,

现在竟像寡妇一样。

从前在诸省做公主的,

现在却沦为奴婢。

2她在夜间痛哭,泪流满面。

情人中没有一个前来安慰。

朋友都出卖她,与她为敌。

3犹大饱受苦难和奴役,

被掳往远方,流落异邦,

找不到安居之所。

她在走投无路之际被追敌擒获。

4通往锡安1:4 锡安”又称“耶路撒冷”。的道路满目凄凉,

因为无人前去过节。

她的城门冷落,

她的祭司悲叹,

她的少女哀伤,她痛苦不已。

5敌人做了她的主人,

兴旺发达。

因为她作恶多端,

耶和华叫她饱受困苦,

她的孩子被敌人掳去。

6锡安的尊荣消逝,

她的首领像找不到草吃的鹿,

无力逃脱敌人的追赶。

7在困苦流离中,

耶路撒冷想起昔日的荣华。

如今,她的人民落在敌人手中,

无人援救。

仇敌看见她,都嘲笑她的灭亡。

8耶路撒冷罪大恶极,

沦为污秽之物。

从前尊重她的人看见她赤身裸体,就蔑视她。

她只能哀叹、退避。

9她的裙子沾满污秽,

她未曾想过自己的结局。

她的败落无比凄惨,

无人安慰。

她哭喊道:“耶和华啊,

仇敌已经获胜,

求你垂顾我的苦难!”

10敌人伸手夺去她的一切珍宝。

她目睹外族人闯入圣殿——那是耶和华禁止他们进入的地方。

11她的人民呻吟着四处觅食,

用珍宝换取粮食维生。

耶路撒冷的哀叹

她说:“耶和华啊,求你眷顾我,

因为我被人蔑视。

12“路人啊,你们都无动于衷吗?

你们看看,

耶和华向我发烈怒,降祸于我,

还有谁比我更痛苦呢?

13“祂从高天降下火来,

焚烧我的骨头;

祂在我脚前设下网罗,

使我返回;

祂使我凄凉孤寂,终日痛苦。

14“我的罪恶连接成轭,

祂亲手把它们编在一起,

绑在我的颈项上,

使我筋疲力尽。

主把我交给我无力抵挡的敌人。

15“主藐视我所有的勇士,

召集军队攻击我,

打垮我的青年。

主践踏犹大1:15 犹大人”希伯来文是“犹大的纯洁少女”。

如同在榨酒池踩踏。

16“我为此哭泣,

泪流满面,

却无人安慰、鼓励我。

我的儿女凄凉孤苦,

因为仇敌已经得胜。”

17锡安伸手求助,却无人理睬。

耶和华已命四周邻国与雅各为敌。

耶路撒冷在他们当中成了污秽之物。

18“但耶和华是公义的,

因为我违背了祂的命令。

万国啊,请听我的话,

看看我的痛苦!

我的年轻男女都被掳去。

19“我向情人们求助,

他们却欺骗我。

我的祭司和长老在觅食求生时,

倒毙在城中。

20“耶和华啊,

看看我是多么痛苦!

我的内脏搅动,

我的心灵翻腾,

因为我背叛了你。

街上有屠杀,

家中有死亡。

21“人们听见我的哀叹,

却无人安慰我。

敌人看见你降给我的灾难,

都幸灾乐祸。

愿你应许的审判之日来临,

叫他们像我一样受苦!

22“愿他们的恶行都摆在你眼前!

你怎样因我的罪恶而惩罚我,

愿你也照样惩罚他们!

我叹息不绝,心中哀伤。”