Malaki 3 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Malaki 3:1-18

13:1 Hes 27:21; 2Nya 36:15; Isa 40:3; 63:9; Mt 11; 10; 3:3; Lk 7:27; Mik 5:2; 1Sam 9:20; Mdo 7:38; Hag 2:7“Angalieni, nitamtuma mjumbe wangu, atakayeiandaa njia mbele yangu. Ndipo ghafula Bwana mnayemtafuta atakuja hekaluni mwake. Mjumbe wa Agano, ambaye mnamwonea shauku, atakuja,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

23:2 Eze 7:7; 22:14; Ufu 6:17; Dan 7:13; Yoe 2:31; Mt 16:27; Yak 5:8; 2Pet 3:4; 1Sam 6:20; Isa 1:31; 30:30; 4:4; Zek 13:9; Mt 3:10-12; Ay 9:30Lakini ni nani atakayeweza kustahimili hiyo siku ya kuja kwake? Ni nani awezaye kusimama atakapotokea? Kwa kuwa atakuwa kama moto wa mfua fedha au kama sabuni ya afuaye nguo. 33:3 Eze 12:10; 1Kor 3:13; 1Nya 23:28; Isa 1:25; Ay 28:1; Za 12:6; 132:9; Ufu 3:18; Zek 13:9; Rum 15:16; 1Pet 2:5Ataketi kama mfuaji na asafishaye fedha. Atawatakasa Walawi, naye atawasafisha kama dhahabu na fedha. Kisha Bwana atakuwa na watu watakaoleta sadaka katika haki, 43:4 2Nya 7:3; 7:12; Za 51:19; Eze 20:40; Mal 1:11nazo sadaka za Yuda na Yerusalemu zitakubalika kwa Bwana, kama katika siku zilizopita, kama katika miaka ya zamani.

53:5 Kut 7:11; 20:14; Yak 2:11; 5:4-9; Isa 1:2; 47:9; 2Pet 2:12-14; Law 19:11-13; Yer 7:9; Yak 5:4; Kut 22:21-22; Kum 24:19; 31:12; Eze 22:7“Basi nitakuja karibu nanyi ili kuhukumu. Nami nitakuwa mwepesi kushuhudia dhidi ya wachawi, wazinzi, waapao kwa uongo, wanaopunja vibarua malipo yao, wanaowaonea wajane na yatima, na wanaowanyima wageni haki, lakini hawaniogopi mimi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

Kumwibia Mungu

63:6 Hes 23:19; Ebr 7:21; Yak 1:17; Ay 34:15; Hos 11:9; 1Sam 15:29; Rum 11:29; Mao 3:22“Mimi Bwana sibadiliki. Kwa hiyo ninyi, enyi uzao wa Yakobo, hamjaangamizwa. 73:7 Kut 32:8; Mdo 7:51; Yer 7:26; Isa 44:22; Kum 30:1-4; Isa 55:6-7; Eze 18:32; Yak 4:8; Zek 1:3Tangu wakati wa baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu nanyi hamkuzishika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

“Lakini mnauliza, ‘Tutarudi kwa namna gani?’

83:8 Zek 5:3; Law 27:30; Hes 18:21; Neh 13:10-12; Lk 18:12“Je, mwanadamu atamwibia Mungu? Hata hivyo mnaniibia mimi.

“Lakini mnauliza, ‘Tunakuibia kwa namna gani?’

“Mnaniibia zaka na dhabihu. 93:9 Kum 28:15-68; 11:26; Zek 5:3Mko chini ya laana, ninyi taifa lote, kwa sababu mnaniibia mimi. 103:10 Kut 22:29; Neh 13:12; 2Fal 7:2; Isa 44:3; Yoe 2:14, 24; 2Kor 9:8-11; Law 25:21; Mit 3:9; Mwa 7:11; 1Nya 26:29Leteni zaka kamili ghalani, ili kuwe na chakula katika nyumba yangu. Nijaribuni katika hili,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nanyi mwone kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagieni baraka nyingi mpaka mkose nafasi ya kutosha. 113:11 Kut 10:15; 23:26; Kum 28:39; Amo 4:9Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu, wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. 123:12 Kum 28:3-12; Isa 61:9; 62:4; Eze 20:6; Dan 8:9; 2Nya 31:10“Ndipo mataifa yote yatawaita mliobarikiwa, kwa maana nchi yenu itakuwa ya kupendeza sana,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

133:13 Mal 2:17“Mmesema vitu vigumu dhidi yangu,” asema Bwana.

“Hata hivyo mnauliza, ‘Tumesema nini dhidi yako?’

143:14 Za 73:13; 100:2; Isa 1:14; 57:10; 58:3; Yn 12:26; Rum 12:11; Yos 22:5; Sef 1:12; Ay 21:14“Mmesema, ‘Ni bure kumtumikia Mungu. Tumepata faida gani kwa kushika maagizo yake na kwenda kama waombolezaji mbele za Bwana Mwenye Nguvu Zote? 153:15 Za 119:21; 14:1; 36:1-2; Yer 7:10; Ay 21:7Lakini sasa wenye kiburi wanabarikiwa. Hakika watenda mabaya wanastawi, pia hata wale wanaoshindana na Mungu ndio wanaosalimika.’ ”

163:16 Za 34:15; 56:8; 87:6; 33:18; Kut 32:32; Lk 10:20; Mit 1:7; Ebr 3:13; Kum 31:12; Ufu 11:18; Mwa 22:12; 1Fal 18:3, 12Ndipo wale waliomcha Bwana wakasemezana wao kwa wao, naye Bwana akasikiliza na akasikia. Kitabu cha kumbukumbu kikaandikwa mbele yake kuhusu wale ambao walimcha Bwana na kuliheshimu jina lake.

173:17 Isa 43:21; 26:20; Kut 8:22; Kum 7:6; Tit 2:14; Neh 13:22; Rum 8:14, 32; Za 103:13; Lk 15:1-32“Nao watakuwa watu wangu,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “katika siku ile nitakapowafanya watu kuwa hazina yangu. Nitawahurumia, kama vile kwa huruma mtu amhurumiavyo mwanawe anayemtumikia. 183:18 Mwa 18:25; Kum 32:4; Mt 25:32-33Kwa mara nyingine tena utaona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia.

King James Version

Malachi 3:1-18

1Behold, I will send my messenger, and he shall prepare the way before me: and the Lord, whom ye seek, shall suddenly come to his temple, even the messenger of the covenant, whom ye delight in: behold, he shall come, saith the LORD of hosts. 2But who may abide the day of his coming? and who shall stand when he appeareth? for he is like a refiner’s fire, and like fullers’ soap: 3And he shall sit as a refiner and purifier of silver: and he shall purify the sons of Levi, and purge them as gold and silver, that they may offer unto the LORD an offering in righteousness. 4Then shall the offering of Judah and Jerusalem be pleasant unto the LORD, as in the days of old, and as in former years.3.4 former: or, ancient 5And I will come near to you to judgment; and I will be a swift witness against the sorcerers, and against the adulterers, and against false swearers, and against those that oppress the hireling in his wages, the widow, and the fatherless, and that turn aside the stranger from his right, and fear not me, saith the LORD of hosts.3.5 oppress: or, defraud 6For I am the LORD, I change not; therefore ye sons of Jacob are not consumed.

7¶ Even from the days of your fathers ye are gone away from mine ordinances, and have not kept them. Return unto me, and I will return unto you, saith the LORD of hosts. But ye said, Wherein shall we return?

8¶ Will a man rob God? Yet ye have robbed me. But ye say, Wherein have we robbed thee? In tithes and offerings. 9Ye are cursed with a curse: for ye have robbed me, even this whole nation. 10Bring ye all the tithes into the storehouse, that there may be meat in mine house, and prove me now herewith, saith the LORD of hosts, if I will not open you the windows of heaven, and pour you out a blessing, that there shall not be room enough to receive it.3.10 pour…: Heb. empty out 11And I will rebuke the devourer for your sakes, and he shall not destroy the fruits of your ground; neither shall your vine cast her fruit before the time in the field, saith the LORD of hosts.3.11 destroy: Heb. corrupt 12And all nations shall call you blessed: for ye shall be a delightsome land, saith the LORD of hosts.

13¶ Your words have been stout against me, saith the LORD. Yet ye say, What have we spoken so much against thee? 14Ye have said, It is vain to serve God: and what profit is it that we have kept his ordinance, and that we have walked mournfully before the LORD of hosts?3.14 ordinance: Heb. observation3.14 mournfully: Heb. in black 15And now we call the proud happy; yea, they that work wickedness are set up; yea, they that tempt God are even delivered.3.15 are set up: Heb. are built

16¶ Then they that feared the LORD spake often one to another: and the LORD hearkened, and heard it, and a book of remembrance was written before him for them that feared the LORD, and that thought upon his name. 17And they shall be mine, saith the LORD of hosts, in that day when I make up my jewels; and I will spare them, as a man spareth his own son that serveth him.3.17 jewels: or, special treasure 18Then shall ye return, and discern between the righteous and the wicked, between him that serveth God and him that serveth him not.