Malaki 1 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Malaki 1:1-14

11:1 Nah 1:1; Mdo 7:38; Rum 3:1-2; 1Pet 4:11Ujumbe: Neno la Bwana kwa Israeli kupitia kwa Malaki.

Yakobo Alipendwa, Esau Alichukiwa

21:2 Kum 4:37; Mal 2:14-17; 3:7-13; Yer 46:27; Rum 9:13; Mwa 25:23; 28:13Bwana asema, “Nimewapenda ninyi.”

“Lakini ninyi mnauliza, ‘Wewe umetupendaje?’ ”

Bwana asema, “Je, Esau hakuwa ndugu yake Yakobo? Hata hivyo nimempenda Yakobo, 31:3 Lk 14:26; Eze 35:3; Isa 34:10; 13:22lakini nikamchukia Esau, nami nimeifanya milima yake kuwa ukiwa, na urithi wake nimewapa mbweha wa jangwani.”

41:4 Isa 11:14; 34:11; 9:10; 34:5; Mao 4:22; Eze 25:12-14; 26; 14Edomu anaweza kusema, “Ingawa tumepondapondwa, tutajenga upya magofu.”

Lakini hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Wanaweza kujenga, lakini nitabomoa. Wataitwa Nchi Ovu, watu ambao siku zote wapo chini ya ghadhabu ya Bwana. 51:5 Za 35:17; 48:1; Mik 5:4; Isa 45:22; 52:10; Amo 1:11-12; Za 83:18Mtayaona kwa macho yenu wenyewe na kusema, ‘Bwana ni mkuu, hata nje ya mipaka ya Israeli!’

Dhabihu Zilizo Na Mawaa

61:6 Law 20:9; Mt 15:14; 23:9; Lk 6:46; Ay 5:17; Kum 31; 12; 20:12; 5:16; Efe 6:2; Lk 18:20“Mwana humheshimu baba yake, naye mtumishi humheshimu bwana wake. Kama mimi ni baba, iko wapi heshima ninayostahili? Kama mimi ni bwana, iko wapi heshima ninayostahili?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau Jina langu.

“Lakini mnauliza, ‘Tumelidharau Jina lako kwa namna gani?’

71:7 Law 21:6; Eze 23; 41; 41:22“Mnatoa sadaka chakula kilichotiwa unajisi juu ya madhabahu yangu.

“Lakini ninyi mnauliza, ‘Tumekutia unajisi kwa namna gani?’

“Kwa kusema kuwa meza ya Bwana ni ya kudharauliwa. 81:8 Law 1:3; Kum 15:21; Mwa 32:20; Isa 43:23; Ay 42:8Wakati mletapo dhabihu za wanyama walio vipofu, je, hilo si kosa? Mnapoleta dhabihu zilizo vilema au wanyama wagonjwa, je, hilo si kosa? Jaribuni kuvitoa kwa mtawala wenu! Je, angefurahishwa nanyi? Je, atawakubalia?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

91:9 Law 23:33-44; Za 51:17; Mik 6:6-8; Rum 12; 1; Ebr 13:16; Yer 6:20; Hos 13:9“Basi mwombeni Mungu awe na neema kwetu. Je, kwa sadaka kama hizo kutoka mikononi mwenu, atawapokea?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

101:10 2Nya 28:24; Hos 5:6; Mal 2:12; Law 22; 20; Isa 1:11-14; Yer 14:12; 1Kor 9:13; Flp 3:18-19“Laiti mmoja wenu angalifunga milango ya Hekalu, ili msije mkawasha moto usiokuwa na faida juu ya madhabahu yangu! Sina furaha nanyi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, “nami sitaikubali sadaka toka mikononi mwenu. 111:11 Isa 24:15; 56:6; 6:3; 12:4; 60:6-7; 19:21; Za 113:3; Mt 8:11; Ufu 5:8; Ebr 13:15; Isa 59:19; 66:19; Yn 4:21; 1Tim 2:8Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa, kuanzia mawio ya jua hata machweo yake. Kila mahali uvumba na sadaka safi zitaletwa kwa Jina langu, kwa sababu Jina langu litakuwa kuu miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

121:12 Eze 41:22“Lakini mnalinajisi Jina langu kwa kusema kuhusu meza ya Bwana, ‘Imetiwa unajisi pamoja na chakula chake. Ni ya kudharauliwa.’ 131:13 Isa 43:22-24; Hes 14:11; Kum 15:21; Law 22:20; Isa 1:12Nanyi mnasema, ‘Mzigo gani huu!’ Nanyi mnaidharau kwa kiburi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

“Wakati mnapowaleta wanyama mliopokonya kwa nguvu, walio vilema au walio wagonjwa na kuwatoa kama dhabihu, je, niwakubali kutoka mikononi mwenu?” asema Bwana. 141:14 Kut 12:5; Za 95:3; 72:6-11; Oba 1:21; Law 22:18-21; Mdo 5:1“Amelaaniwa yeye adanganyaye, aliye na mnyama wa kiume anayekubalika katika kundi lake na kuweka nadhiri ya kumtoa, lakini akatoa dhabihu ya mnyama aliye na dosari kwa Bwana. Kwa kuwa mimi ni Mfalme Mkuu, nalo Jina langu linapaswa kuogopwa miongoni mwa mataifa,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.

Swedish Contemporary Bible

Malaki 1:1-14

1Profetia.

Herrens ord till Israel genom Malaki.

Herren älskar sitt folk

2”Jag har älskat er, säger Herren. Men ni säger: ’På vilket sätt har du älskat oss?’ Var inte Jakob och Esau bröder? säger Herren. Jag älskade Jakob 3men hatade Esau. Jag gjorde hans berg till en ödemark och gav hans arv åt öknens schakaler.”

4Om Edom säger: ”Vi är krossade, men vi ska åter bygga upp ruinerna,” så säger härskarornas Herre: ”Låt dem bygga, jag kommer ändå att riva ner det. Det ska kallas ondskans land och folket som Herren vredgas på för evigt. 5Ni får se det med egna ögon, och då ska ni säga: ’Herren är stor, även bortom Israels gränser!’

Israels otrohet

(1:6—2:16)

Herren kräver felfria offer

6En son hedrar sin far och en tjänare sin herre. Om jag är en far, var är min heder? Och om jag är en herre, var är min respekt? Detta säger härskarornas Herre till er präster, som föraktar mitt namn.

Då frågar ni: ’På vilket sätt har vi föraktat ditt namn?’

7Genom att ni har burit fram oren mat på mitt altare.

Ni frågar: ’På vilket sätt har vi gjort dig oren?’

Genom att säga att Herrens bord kan föraktas. 8När ni bär fram ett blint offerdjur, är det inte något ont? När ni bär fram ett halt och sjukt offerdjur, är det inte något ont? Försök komma med sådana offer till din ståthållare! Skulle han gilla dig och ta emot dig välvilligt? säger härskarornas Herre.

9Nu vädjar ni till Gud att han ska vara nådig mot oss! Skulle han, när ni nu har sådant i era händer, vara välvilligt inställd mot er?” säger härskarornas Herre.

10”Om ändå någon av er ville stänga tempeldörrarna och låta bli att i onödan tända eld på mitt altare! Jag vill inte veta av er, säger härskarornas Herre, och jag kan inte ta emot era offer. 11Från öster till väster ska mitt namn bli stort bland folken. På alla platser ska man bära fram rökelse och rena offer åt mitt namn, för mitt namn är stort bland folken, säger härskarornas Herre.

12Ni däremot vanhelgar det och säger att Herrens bord är orent och hans mat är värd förakt. 13Ni säger: ’Så besvärligt!’ och fnyser bara, säger härskarornas Herre. Ni kommer med stulna, halta och sjuka djur för att offra. Skulle jag kunna ta emot sådant av er? säger Herren. 14Förbannad är den bedräglige som lovar att offra ett handjur från sin hjord och sedan ändå offrar ett missbildat djur åt Herren. För jag är en stor kung, säger härskarornas Herre, och mitt namn är fruktat bland folken.