Luka 4 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 4:1-44

Yesu Ajaribiwa Na Shetani

(Mathayo 4:1-11; Marko 1:12-13)

14:1 Lk 1:15-45; 3:3-21; Eze 37:1; Lk 2:27Yesu, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akarudi kutoka Yordani. Akaongozwa na Roho Mtakatifu hadi nyikani, 24:2 Kut 34:28; 1Fal 19:8mahali ambako kwa siku arobaini alikuwa akijaribiwa na ibilisi. Kwa siku zote hizo hakula chochote, hivyo baada ya muda huo akaona njaa.

34:3 Mt 4:3Ibilisi akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru jiwe hili liwe mkate.”

44:4 Kum 8:3Yesu akajibu akamwambia, “Imeandikwa: ‘Mtu haishi kwa mkate tu.’ ”

54:5 Mt 24:14Ibilisi akampeleka hadi juu ya mlima mrefu akamwonyesha milki zote za dunia kwa mara moja. 64:6 Yn 14:30Akamwambia, “Nitakupa mamlaka juu ya milki hizi na fahari zake zote, kwa maana zimekabidhiwa mkononi mwangu nami ninaweza kumpa yeyote ninayetaka. 7Hivyo ikiwa utanisujudia na kuniabudu, vyote vitakuwa vyako.”

84:8 Kum 6:3Yesu akamjibu, “Imeandikwa: ‘Mwabudu Bwana Mungu wako na umtumikie yeye peke yake.’ ”

94:9 Mt 4:5Kisha ibilisi akampeleka mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya mnara mrefu wa Hekalu, akamwambia, “Kama wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa, 104:10 Za 91:11, 12kwa maana imeandikwa:

“ ‘Atakuagizia malaika zake

ili wakulinde;

114:11 Za 91:12nao watakuchukua mikononi mwao,

usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.’ ”

124:12 Kum 6:12Yesu akamjibu, “Imesemwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ”

134:13 Ebr 4:15; Yn 14:30Ibilisi alipomaliza kila jaribu, akamwacha Yesu mpaka wakati mwingine ufaao.

Mwanzo Wa Huduma Ya Galilaya

(Mathayo 4:12-17; Marko 1:14-15)

144:14 Mt 4:12; 9:26Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando. 154:15 Mt 4:23Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.

Yesu Akataliwa Nazareti

(Mathayo 13:53-58; Marko 6:1-6)

164:16 Mt 2:23; 13:54Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome, 174:17 Isa 61:1, 2; 58:6naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:

184:18 Yn 3:34“Roho wa Bwana yu juu yangu,

kwa sababu amenitia mafuta

kuwahubiria maskini habari njema.

Amenituma kuwatangazia wafungwa

kufunguliwa kwao,

na vipofu kupata kuona tena,

kuwaweka huru wanaoonewa,

19na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”

204:20 Mt 26:55Kisha akakifunga kitabu, akamrudishia mtumishi na akaketi. Watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 214:21 Mt 1:22Ndipo akaanza kwa kuwaambia, “Leo Andiko hili limetimia mkiwa mnasikia.”

224:22 Yn 6:42; 7:15Wote waliokuwako wakamsifu na kuyastaajabia maneno yake yaliyojaa neema, wakaulizana, “Je, huyu si mwana wa Yosefu?”

234:23 Mt 2:23; Mk 1:21-28; 2:1-12Yesu akawaambia, “Bila shaka mtatumia mithali hii: ‘Tabibu, jiponye mwenyewe! Mambo yale tuliyosikia kwamba uliyafanya huko Kapernaumu, yafanye na hapa kwenye mji wako.’ ”

244:24 Mt 13:57; Yn 4:44Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna nabii anayekubalika katika mji wake mwenyewe. 254:25 1Fal 18:1; Ufu 11:6Lakini ukweli ni kwamba palikuwa na wajane wengi katika Israeli wakati wa Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita pakawa na njaa kuu katika nchi nzima. 264:26 1Fal 17:8-16; Mt 11:21Hata hivyo Eliya hakutumwa hata kwa mmoja wao, bali kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni. 274:27 2Fal 5:1-14Pia palikuwa na wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa, isipokuwa Naamani mtu wa Shamu.”4:27 Shamu hapa inamaanisha Syria.

28Watu wote katika sinagogi waliposikia maneno haya, wakakasirika sana. 294:29 Hes 15:35; Ebr 13:12Wakasimama, wakamtoa nje ya mji, wakamchukua hadi kwenye kilele cha mlima mahali ambapo mji huo ulikuwa umejengwa, ili wamtupe chini kutoka kwenye mteremko mkali. 304:30 Yn 8:59; 10:39Lakini yeye akapita papo hapo katikati ya huo umati wa watu akaenda zake.

Yesu Atoa Pepo Mchafu

(Marko 1:21-28)

314:31 Mt 4:13Kisha Yesu akashuka kwenda Kapernaumu, mji wa Galilaya, na katika siku ya Sabato akawa anafundisha. 324:32 Mt 7:28-29Wakashangazwa sana na mafundisho yake, maana maneno yake yalikuwa na mamlaka.

334:33 Mk 1:23Ndani ya sinagogi palikuwa na mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu. Naye akapiga kelele kwa nguvu akisema, 344:34 Mt 8:28-29; Mk 1:24; Yak 2:19“Tuache! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Ninakujua wewe ni nani. Wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu!”

354:35 Mt 8:26; Lk 8:24Basi Yesu akamkemea yule pepo mchafu, akisema, “Nyamaza kimya! Nawe umtoke!” Yule pepo mchafu akamwangusha yule mtu chini mbele yao wote, akatoka pasipo kumdhuru. 364:36 Mt 7:28-29; 10:1Watu wote wakashangaa, wakaambiana, “Mafundisho haya ni ya namna gani? Anawaamuru pepo wachafu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!” 374:37 Mt 9:26Habari zake zikaanza kuenea kila mahali katika sehemu ile.

Yesu Awaponya Wengi

(Mathayo 8:14-17; Marko 1:29-34)

384:38 Mt 8:14; Mk 1:29Yesu akatoka katika sinagogi, akaenda nyumbani kwa Simoni. Basi huko alimkuta mama mkwe wa Simoni akiwa ameshikwa na homa kali, nao wakamwomba Yesu amsaidie. 394:39 Lk 4:35, 41Hivyo Yesu akamwinamia na kukemea ile homa, nayo ikamwacha. Akaamka saa ile ile, naye akaanza kuwahudumia.

404:40 Mk 5:23; Mt 4:23Jua lilipokuwa linatua, watu wakamletea Yesu watu wote waliokuwa na maradhi mbalimbali, naye akaweka mikono yake juu ya kila mgonjwa, naye akawaponya. 414:41 Mt 4:3; 8:4Pepo wachafu pia wakawatoka watu wengi, nao walipokuwa wakitoka wakapiga kelele, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakemea na kuwazuia wasiseme, kwa maana walimjua kuwa yeye ndiye Kristo.4:41 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta.

424:42 Mk 1:35Kesho yake, kulipopambazuka, Yesu alikwenda mahali pa faragha. Watu wengi wakawa wanamtafuta kila mahali, nao walipomwona wakajaribu kumzuia asiondoke. 434:43 Mt 3:2Lakini yeye akawaambia, “Imenipasa kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika miji mingine pia, kwa maana kwa kusudi hili nilitumwa.” 444:44 Mt 4:23Naye aliendelea kuhubiri katika masinagogi ya Uyahudi.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Lucas 4:1-44

Tentación de Jesús

4:1-13Mt 4:1-11; Mr 1:12-13

1Jesús, lleno del Espíritu Santo, volvió del Jordán y fue llevado por el Espíritu al desierto. 2Allí estuvo cuarenta días y fue tentado por el diablo. No comió nada durante esos días, pasados los cuales tuvo hambre.

3―Si eres el Hijo de Dios —le propuso el diablo—, dile a esta piedra que se convierta en pan.

4Jesús le respondió:

―Escrito está: “No solo de pan vive el hombre”.4:4 Dt 8:3

5Entonces el diablo lo llevó a un lugar alto y le mostró en un instante todos los reinos del mundo.

6―Sobre estos reinos y todo su esplendor —le dijo—, te daré la autoridad, porque a mí me ha sido entregada, y puedo dársela a quien yo quiera. 7Así que, si me adoras, todo será tuyo.

Jesús le contestó:

8―Escrito está: “Adora al Señor tu Dios y sírvele solamente a él”.4:8 Dt 6:13

9El diablo lo llevó luego a Jerusalén e hizo que se pusiera de pie en la parte más alta del templo, y le dijo:

―Si eres el Hijo de Dios, ¡tírate de aquí! 10Pues escrito está:

»“Ordenará que sus ángeles te cuiden.

Te sostendrán en sus manos

11para que no tropieces con piedra alguna”».4:10-11 Sal 91:11,12

12―También está escrito: “No pongas a prueba al Señor tu Dios”4:12 Dt 6:16 —le replicó Jesús.

13Así que el diablo, habiendo agotado todo recurso de tentación, lo dejó hasta otra oportunidad.

Rechazan a Jesús en Nazaret

14Jesús regresó a Galilea en el poder del Espíritu, y se extendió su fama por toda aquella región. 15Enseñaba en las sinagogas, y todos lo admiraban.

16Fue a Nazaret, donde se había criado, y un sábado entró en la sinagoga, como era su costumbre. Se levantó para hacer la lectura, 17y le entregaron el libro del profeta Isaías. Al desenrollarlo, encontró el lugar donde está escrito:

18«El Espíritu del Señor está sobre mí,

por cuanto me ha ungido

para anunciar buenas nuevas a los pobres.

Me ha enviado a proclamar libertad a los cautivos

y dar vista a los ciegos,

a poner en libertad a los oprimidos,

19a pregonar el año del favor del Señor».4:19 Is 61:1,2

20Luego enrolló el libro, se lo devolvió al ayudante y se sentó. Todos los que estaban en la sinagoga lo miraban detenidamente, 21y él comenzó a hablarles: «Hoy se cumple esta Escritura en vuestra presencia».

22Todos dieron su aprobación, impresionados por las hermosas palabras4:22 Todos … palabras. Lit. Todos daban testimonio de él y estaban asombrados de las palabras de gracia. que salían de su boca. «¿No es este el hijo de José?», se preguntaban.

23Jesús continuó: «Seguramente me vais a citar el proverbio: “¡Médico, cúrate a ti mismo! Haz aquí en tu tierra lo que hemos oído que hiciste en Capernaún”. 24Pues bien, os aseguro que a ningún profeta lo aceptan en su propia tierra. 25No cabe duda de que en tiempos de Elías, cuando el cielo se cerró por tres años y medio, de manera que hubo una gran hambre en toda la tierra, muchas viudas vivían en Israel. 26Sin embargo, Elías no fue enviado a ninguna de ellas, sino a una viuda de Sarepta, en los alrededores de Sidón. 27Así mismo, había en Israel muchos enfermos de lepra en tiempos del profeta Eliseo, pero ninguno de ellos fue sanado, sino Naamán el sirio».

28Al oír esto, todos los que estaban en la sinagoga se enfurecieron. 29Se levantaron, lo expulsaron del pueblo y lo llevaron hasta la cumbre de la colina sobre la que estaba construido el pueblo, para tirarlo por el precipicio. 30Pero él pasó por en medio de ellos y se fue.

Jesús expulsa a un espíritu maligno

4:31-37Mr 1:21-28

31Jesús pasó a Capernaún, un pueblo de Galilea, y el sábado enseñaba a la gente. 32Estaban asombrados de su enseñanza, porque les hablaba con autoridad.

33Había en la sinagoga un hombre que estaba poseído por un espíritu maligno, quien gritó con todas sus fuerzas:

34―¡Ah! ¿Por qué te entrometes, Jesús de Nazaret? ¿Has venido a destruirnos? Yo sé quién eres tú: ¡el Santo de Dios!

35―¡Cállate! —lo reprendió Jesús—. ¡Sal de ese hombre!

Entonces el demonio derribó al hombre en medio de la gente y salió de él sin hacerle ningún daño.

36Todos se asustaron y se decían unos a otros: «¿Qué clase de palabra es esta? ¡Con autoridad y poder da órdenes a los espíritus malignos, y salen!» 37Y se extendió su fama por todo aquel lugar.

Jesús sana a muchos enfermos

4:38-41Mt 8:14-17

4:38-43Mr 1:29-38

38Cuando Jesús salió de la sinagoga, se fue a casa de Simón, cuya suegra estaba enferma con una fiebre muy alta. Le pidieron a Jesús que la ayudara, 39así que se inclinó sobre ella y reprendió a la fiebre, la cual se le fue. Ella se levantó en seguida y se puso a servirles.

40Al ponerse el sol, la gente llevó a Jesús todos los que padecían de diversas enfermedades; él puso las manos sobre cada uno de ellos y los sanó. 41Además, de muchas personas salían demonios que gritaban: «¡Tú eres el Hijo de Dios!» Pero él los reprendía y no los dejaba hablar porque sabían que él era el Cristo.

42Cuando amaneció, Jesús salió y se fue a un lugar solitario. La gente andaba buscándolo y, cuando llegaron adonde él estaba, procuraban detenerlo para que no se fuera. 43Pero él les dijo: «Es preciso que anuncie también a los demás pueblos las buenas nuevas del reino de Dios, porque para esto fui enviado».

44Y siguió predicando en las sinagogas de los judíos.4:44 los judíos. Lit. Judea. Var. Galilea.