Luka 3 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 3:1-38

Yohana Mbatizaji Aanza Kuhubiri

(Mathayo 3:1-12; Marko 1:1-8; Yohana 1:19-28)

13:1 Mt 27:2Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene, 23:2 Yn 18:13; Mdo 4:6; Mt 3:1nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani. 33:3 Mk 3:16; Mal 1:4Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi. 43:4 Isa 40:3-5; Mt 3:3; Mk 1:3; Yn 1:23Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:

“Sauti ya mtu aliaye nyikani,

‘Itengenezeni njia ya Bwana,

yanyoosheni mapito yake.

5Kila bonde litajazwa,

kila mlima na kilima vitashushwa.

Njia zilizopinda zitanyooshwa,

na zilizoparuza zitasawazishwa.

63:6 Za 98:2; Lk 2:30Nao watu wote watauona

wokovu wa Mungu.’ ”

73:7 Mt 12:34; 23:33; Rum 1:18Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja? 83:8 Isa 51:7; Gal 3:7Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya. 93:9 Mt 3:10Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”

103:10 Mdo 2:37; 16:30Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”

113:11 Isa 58:7; Eze 18:7Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”

123:12 Lk 7:29Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”

133:13 Lk 19:8Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”

143:14 Law 19:11Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?”

Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”

153:15 Mt 3:1; Yn 1:19-20; Mdo 13:25Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.3:15 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. 163:16 Mk 1:4; Yn 1:26, 33; Mdo 11:16Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji.3:16 Tafsiri nyingine zinasema ndani ya maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto. 173:17 Isa 30:24; Mt 13:30; 25:41Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.” 18Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.

193:19 Mt 14:1Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya, 203:20 Mt 14:3-4Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.

Kubatizwa Kwa Bwana Yesu

(Mathayo 3:13-17; Marko 1:9-11)

213:21 Mt 14:23; Mk 1:35Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka. 223:22 Isa 42:1; Yn 1:32-33; Mt 3:17Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”

Ukoo Wa Bwana Yesu

(Mathayo 1:1-17)

233:23 Mt 4:17; Lk 1:27Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu,

Yosefu alikuwa mwana wa Eli,

24Eli alikuwa mwana wa Mathati,

Mathati alikuwa mwana wa Lawi,

Lawi alikuwa mwana wa Melki,

Melki alikuwa mwana wa Yanai,

Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,

25Yosefu alikuwa mwana wa Matathia,

Matathia alikuwa mwana wa Amosi,

Amosi alikuwa mwana wa Nahumu,

Nahumu alikuwa mwana wa Esli,

Esli alikuwa mwana wa Nagai,

26Nagai alikuwa mwana wa Maathi,

Maathi alikuwa mwana wa Matathia,

Matathia alikuwa mwana wa Semeini,

Semeini alikuwa mwana wa Yoseki,

Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,

273:27 Mt 1:12; 1Nya 3:17Yoda alikuwa mwana wa Yoanani,

Yoanani alikuwa mwana wa Resa,

Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli,

Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli,

Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,

28Neri alikuwa mwana wa Melki,

Melki alikuwa mwana wa Adi,

Adi alikuwa mwana wa Kosamu,

Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu,

Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,

29Eri alikuwa mwana wa Yoshua,

Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri,

Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu,

Yorimu alikuwa mwana wa Mathati,

Mathati alikuwa mwana wa Lawi,

30Lawi alikuwa mwana wa Simeoni,

Simeoni alikuwa mwana wa Yuda,

Yuda alikuwa mwana wa Yosefu,

Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu,

Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu,

Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,

313:31 2Sam 5:14; 1Nya 3:5Melea alikuwa mwana wa Mena,

Mena alikuwa mwana wa Matatha,

Matatha alikuwa mwana wa Nathani,

Nathani alikuwa mwana wa Daudi,

323:32 Rut 4:22; 1Nya 2:10Daudi alikuwa mwana wa Yese,

Yese alikuwa mwana wa Obedi,

Obedi alikuwa mwana wa Boazi,

Boazi alikuwa mwana wa Salmoni,

Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,

333:33 Rut 4:18-22; 1Nya 2:10Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu,

Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu,

Aramu alikuwa mwana wa Hesroni,

Hesroni alikuwa mwana wa Peresi,

Peresi alikuwa mwana wa Yuda,

343:34 Mwa 11:24-26Yuda alikuwa mwana wa Yakobo,

Yakobo alikuwa mwana wa Isaki,

Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu,

Abrahamu alikuwa mwana wa Tera,

Tera alikuwa mwana wa Nahori,

35Nahori alikuwa mwana wa Serugi,

Serugi alikuwa mwana wa Reu,

Reu alikuwa mwana wa Pelegi,

Pelegi alikuwa mwana wa Eberi,

Eberi alikuwa mwana wa Sala,

363:36 Mwa 5:28-32; 11:12Sala alikuwa mwana wa Kenani,

Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi,

Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu,

Shemu alikuwa mwana wa Noa,

Noa alikuwa mwana wa Lameki,

373:37 Mwa 5:12-25Lameki alikuwa mwana wa Methusela,

Methusela alikuwa mwana wa Enoki,

Enoki alikuwa mwana wa Yaredi,

Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli,

Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,

383:38 Mwa 5:19Kenani alikuwa mwana wa Enoshi,

Enoshi alikuwa mwana wa Sethi,

Sethi alikuwa mwana wa Adamu,

Adamu alikuwa mwana wa Mungu.

Swedish Contemporary Bible

Lukas 3:1-38

Johannes döparen banar väg för Jesus

(Matt 3:1-12; Mark 1:2-8; Joh 1:19-28)

1Det var nu kejsaren Tiberius femtonde regeringsår. Pontius Pilatus var landshövding i Judeen, Herodes var tetrark över Galileen, hans bror Filippos över Itureen och Trachonitis och Lysanias över Abilene. 2Hannas och Kajafas var överstepräster.

Vid den här tiden kom Guds ord till Johannes, Sakarias son, i ödemarken. 3Han gav sig iväg till trakterna kring Jordanfloden och förkunnade omvändelsens dop för syndernas förlåtelse, 4så som det står skrivet i boken om profeten Jesajas ord:

”En röst ropar i ödemarken:

’Bana väg för Herren!

Jämna vägen för honom!

5Varje dal ska fyllas,

alla berg och höjder sänkas,

krokiga stigar rätas

och steniga vägar jämnas.

6Då ska alla människor få se Guds räddning.’ ”3:6 Se Jes 40:3-5; 52:10.

7När stora mängder människor nu kom till Johannes för att bli döpta, sa han till dem: ”Ni huggormsyngel, tror ni att ni kan klara er undan den kommande vreden? 8Nej, handla3:8 Ordagrant: Bär då sådan frukt. som det anstår en som är omvänd! Tänk inte att ni bara kan säga: ’Abraham är vår stamfar.’ Jag säger er att Gud kan förvandla de här stenarna till Abrahams ättlingar! 9Yxan är redan satt till roten på träden. Varje träd som inte bär god frukt ska huggas ner och kastas i elden!”

10Då frågade folket: ”Vad ska vi då göra?”

11Han svarade: ”Om någon har två skjortor, ska han ge bort en av dem till någon som ingen har. Och den som har mat ska göra likadant.”

12Även tullindrivare3:12 Tullindrivarna var judar som arbetade med att ta in skatt åt romarna, och de var avskydda av alla. kom för att döpas, och de frågade: ”Mästare, vad ska vi göra?”

13Han svarade: ”Kräv inte mer än vad ni fått order om.”

14”Och vi då, vad ska vi göra?” frågade några soldater.

Johannes svarade: ”Tvinga inte till er pengar genom hot och våld, utan nöj er med er lön.”

15Hela folket levde i väntan, och alla undrade i sina hjärtan om inte Johannes kunde vara Messias. 16Men Johannes svarade dem alla: ”Jag döper er med vatten, men snart kommer en som är starkare än jag. Jag är inte ens värdig att knyta upp hans sandalremmar.3:16 Detta var en slavs uppgift. Han ska döpa er i den heliga Anden och eld. 17Han har kastskoveln i sin hand för att rensa upp sin tröskplats och samla vetet i ladan, men agnarna ska han bränna upp i en eld som aldrig slocknar.”

18På många olika sådana sätt förmanade Johannes folket när han framförde sitt budskap för dem.

Herodes sätter Johannes i fängelse

19Johannes riktade också direkt kritik mot Herodes, tetrarken i Galileen, för hans förhållande med sin brors hustru Herodias och för allt annat ont han gjort. 20Därför lät Herodes sätta Johannes i fängelse, och gjorde på det viset ännu en ond gärning.

Jesus blir döpt

(Matt 3:13-17; Mark 1:9-11; Joh 1:32-34)

21Men när nu allt folket kom för att bli döpta, och också Jesus hade blivit döpt och stod där och bad, öppnades himlen. 22Den heliga Anden sänkte sig ner över honom i form av en duva, och en röst från himlen sa: ”Du är min älskade Son, du är min glädje.”

Jesus släkttavla

(Matt 1:1-17)

23Jesus var runt trettio år när han började sin verksamhet. Han ansågs vara son till Josef,

som var son till Eli, 24son till Mattat,

son till Levi, son till Melki,

son till Jannaj, son till Josef,

25son till Mattatias, son till Amos,

son till Nahum, son till Hesli,

son till Naggaj, 26son till Machat,

son till Mattatias, son till Shimi,

son till Josek, son till Joda,

27son till Jochanan, son till Resa,

son till Serubbabel, son till Shealtiel,

son till Ner, 28son till Melki,

son till Addi, son till Kosam,

son till Elmadam, son till Er,

29son till Josua, son till Elieser,

son till Jorim, son till Mattat,

son till Levi, 30son till Symeon,

son till Juda, son till Josef,

son till Jonam, son till Eljakim,

31son till Melea, son till Menna,

son till Mattatta, son till Natan,

son till David, 32son till Jishaj,

son till Oved, son till Boas,

son till Salma, son till Nachshon,

33son till Amminadav, son till Admin,

son till Arni, son till Hesron,

son till Peres, son till Juda,

34son till Jakob, son till Isak,

son till Abraham, son till Terach,

son till Nachor, 35son till Serug,

son till Regu, son till Peleg,

son till Ever, son till Shelach,

36son till Kenan, son till Arpakshad,

son till Sem, son till Noa,

son till Lemek, 37son till Metushelach,

son till Henok, son till Jered,

son till Mahalalel, son till Kenan,

38son till Enosh, son till Set,

son till Adam, son till Gud.