Luka 24 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 24:1-53

Kufufuka Kwa Yesu

(Mathayo 28:1-10; Marko 16:1-8; Yohana 20:1-10)

124:1 Lk 23:56; Mt 28:1; Mk 16; 1; Yn 20:2Mnamo siku ya kwanza ya juma, alfajiri na mapema, wale wanawake walichukua yale manukato waliyokuwa wameyaandaa, wakaenda kaburini. 224:2 Mt 24:2; Mk 16:5Wakakuta lile jiwe limevingirishwa kutoka kwenye kaburi, 324:3 Lk 24:23; Mk 16:5lakini walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu. 424:4 Yn 20:12; Mdo 1:10Walipokuwa wanashangaa juu ya jambo hili, ghafula watu wawili waliokuwa wamevaa mavazi yanayongʼaa kama umeme wakasimama karibu nao. 5Wale wanawake, wakiwa na hofu, wakainamisha nyuso zao mpaka chini. Lakini wale watu wakawaambia, “Kwa nini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu? 624:6 Mt 17:22-23; Mk 9:30-31Hayuko hapa; amefufuka! Kumbukeni alivyowaambia alipokuwa bado yuko pamoja nanyi huko Galilaya kwamba: 724:7 Mt 8:20; 16:21‘Ilikuwa lazima Mwana wa Adamu atiwe mikononi mwa watu wenye dhambi na waovu ili asulubiwe, na siku ya tatu afufuke.’ ” 824:8 Yn 2:22Ndipo wakayakumbuka maneno ya Yesu.

924:9 Mt 28:8; Mk 16:10Waliporudi kutoka huko kaburini, wakawaeleza wale wanafunzi kumi na mmoja pamoja na wengine wote mambo haya yote. 1024:10 Lk 8:1-3; Mk 6:30Basi Maria Magdalene, Yoana, na Maria mama yake Yakobo, pamoja na wanawake wengine waliofuatana nao ndio waliwaelezea mitume habari hizi. 1124:11 Mk 16:11Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi. 1224:12 Yn 20:3-7; 20:10Hata hivyo, Petro akainuka na kukimbia kwenda kule kaburini. Alipoinama kuchungulia, akaona vile vitambaa vya kitani, ila hakuona kitu kingine. Naye akaenda zake akijiuliza nini kilichotokea.

Njiani Kwenda Emau

(Marko 16:12-13)

1324:13 Mk 16:12Ikawa siku iyo hiyo, wanafunzi wawili wa Yesu walikuwa njiani wakienda kijiji kilichoitwa Emau, yapata maili saba24:13 Maili saba ni kama kilomita 11.2. kutoka Yerusalemu. 14Walikuwa wakizungumza wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotukia. 1524:15 Mt 18:20Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akaja akatembea pamoja nao, 1624:16 Yn 20:14; 21:4lakini macho yao yakazuiliwa ili wasimtambue.

17Akawauliza, “Ni mambo gani haya mnayozungumza wakati mnatembea?”

Wakasimama, nyuso zao zikionyesha huzuni. 1824:18 Yn 19:25Mmoja wao, aliyeitwa Kleopa, akamuuliza, “Je, wewe ndiye peke yako mgeni huku Yerusalemu ambaye hufahamu mambo yaliyotukia humo siku hizi?”

1924:19 Mk 1:24Akawauliza, “Mambo gani?”

Wakamjibu, “Mambo ya Yesu wa Nazareti. Yeye alikuwa nabii, mwenye uwezo mkuu katika maneno yake na matendo yake, mbele za Mungu na mbele ya wanadamu wote. 2024:20 Lk 23:13Viongozi wa makuhani na viongozi wetu walimtoa ahukumiwe kufa, nao wakamsulubisha. 2124:21 Lk 1:68; 2:38; Mt 16:21Lakini tulikuwa tumetegemea kwamba yeye ndiye angelikomboa Israeli. Zaidi ya hayo, leo ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee. 2224:22 Mt 28:8; Mk 16:10; Lk 24:9, 10; Yn 20:18Isitoshe, baadhi ya wanawake katika kundi letu wametushtusha. Walikwenda kaburini leo alfajiri, 23lakini hawakuukuta mwili wake. Walirudi wakasema wameona maono ya malaika ambao waliwaambia kwamba Yesu yu hai. 2424:24 Lk 24:12; Yn 20:3-19Kisha baadhi ya wenzetu walikwenda kaburini wakalikuta kama vile wale wanawake walivyokuwa wamesema, lakini yeye hawakumwona.”

25Yesu akawaambia, “Ninyi ni wajinga kiasi gani, nanyi ni wazito mioyoni mwenu kuamini mambo yote yaliyonenwa na manabii! 2624:26 Ebr 2:10; 1Pet 1:11Je, haikumpasa Kristo24:26 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. kuteswa kwa njia hiyo na kisha aingie katika utukufu wake?” 2724:27 Mwa 3:15; Hes 2:19; Mk 7:20; Mal 3:1; Yn 1:45Naye akianzia na Sheria ya Mose na Manabii wote, akawafafanulia jinsi Maandiko yalivyosema kumhusu yeye.

2824:28 Mwa 32:26; 42:7; Mk 6:49Nao walipokaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, Yesu akawa kama anaendelea mbele. 2924:29 Mwa 19:3; Mdo 16:15Lakini wao wakamsihi sana akae nao, wakisema, “Kaa hapa nasi, kwa maana sasa ni jioni na usiku unaingia.” Basi akaingia ndani kukaa nao.

3024:30 Mt 14:19Alipokuwa mezani pamoja nao, akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akaanza kuwagawia. 3124:31 Za 39:3; Lk 24:16Ndipo macho yao yakafumbuliwa, nao wakamtambua, naye akatoweka machoni pao. Hawakumwona tena. 3224:32 Za 39:3; Lk 24:27, 28Wakaulizana wao kwa wao, “Je, mioyo yetu haikuwakawaka kwa furaha ndani yetu alipokuwa anazungumza nasi njiani na kutufafanulia Maandiko?”

33Wakaondoka mara, wakarudi Yerusalemu. Wakawakuta wale wanafunzi kumi na mmoja na wale waliokuwa pamoja nao, wamekusanyika 3424:34 1Kor 15:5wakisema, “Ni kweli! Bwana amefufuka, naye amemtokea Simoni.” 3524:35 Lk 24:30, 31Kisha wale wanafunzi wawili wakaeleza yaliyotukia njiani na jinsi walivyomtambua Yesu alipoumega mkate.

Yesu Awatokea Wanafunzi Wake

(Mathayo 28:16-20; Marko 16:14-18; Yohana 20:19-23; Matendo 1:6-8)

3624:36 Yn 20:19, 21, 26; 14:27Walipokuwa bado wanazungumza hayo, Yesu mwenyewe akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”

3724:37 Mk 6:49Wakashtuka na kuogopa wakidhani kwamba wameona mzuka. 38Lakini Yesu akawauliza, “Kwa nini mnaogopa? Kwa nini mna shaka mioyoni mwenu? 3924:39 Yn 20:27; 1Yn 1:1Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”

40Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake. 4124:41 Mwa 45:26; Yn 21:5Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”

42Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa, 4324:43 Mdo 10:40naye akakichukua na kukila mbele yao.

4424:44 Lk 24:26; Mt 1:22; 16:21; Za 110Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”

4524:45 Mdo 16:14Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko. 4624:46 Lk 24:26; Isa 50:6; 53:2Akawaambia, “Haya ndiyo yaliyoandikwa: Kristo atateswa na siku ya tatu atafufuka kutoka kwa wafu. 4724:47 Mdo 10:43; 13:38; Mt 28:19; Mk 13:10Toba na msamaha wa dhambi zitatangaziwa mataifa yote kupitia jina lake kuanzia Yerusalemu. 4824:48 Yn 15:27; 1Pet 5:1Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.

Kuahidiwa Kwa Roho Mtakatifu

4924:49 Yn 14:16; Mdo 1:4“Tazama nitawatumia ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini hadi mtakapovikwa uwezo utokao juu.”

Kupaa Kwa Yesu Mbinguni

(Marko 16:19-20; Matendo 1:9-11)

5024:50 Mt 21:11Akiisha kuwaongoza mpaka kwenye viunga vya Bethania, akainua mikono yake juu na kuwabariki. 5124:51 2Fal 2:11Alipokuwa anawabariki, akawaacha, akachukuliwa mbinguni. 5224:52 Mt 28:9, 17Kisha wakamwabudu na kurudi Yerusalemu wakiwa wamejawa na furaha kuu. 5324:53 Mdo 2:46Nao wakadumu ndani ya Hekalu wakimtukuza Mungu. Amen.

King James Version

Luke 24:1-53

1Now upon the first day of the week, very early in the morning, they came unto the sepulchre, bringing the spices which they had prepared, and certain others with them. 2And they found the stone rolled away from the sepulchre. 3And they entered in, and found not the body of the Lord Jesus. 4And it came to pass, as they were much perplexed thereabout, behold, two men stood by them in shining garments: 5And as they were afraid, and bowed down their faces to the earth, they said unto them, Why seek ye the living among the dead? 6He is not here, but is risen: remember how he spake unto you when he was yet in Galilee, 7Saying, The Son of man must be delivered into the hands of sinful men, and be crucified, and the third day rise again. 8And they remembered his words, 9And returned from the sepulchre, and told all these things unto the eleven, and to all the rest. 10It was Mary Magdalene, and Joanna, and Mary the mother of James, and other women that were with them, which told these things unto the apostles. 11And their words seemed to them as idle tales, and they believed them not. 12Then arose Peter, and ran unto the sepulchre; and stooping down, he beheld the linen clothes laid by themselves, and departed, wondering in himself at that which was come to pass.

13¶ And, behold, two of them went that same day to a village called Emmaus, which was from Jerusalem about threescore furlongs. 14And they talked together of all these things which had happened. 15And it came to pass, that, while they communed together and reasoned, Jesus himself drew near, and went with them. 16But their eyes were holden that they should not know him. 17And he said unto them, What manner of communications are these that ye have one to another, as ye walk, and are sad? 18And the one of them, whose name was Cleopas, answering said unto him, Art thou only a stranger in Jerusalem, and hast not known the things which are come to pass there in these days? 19And he said unto them, What things? And they said unto him, Concerning Jesus of Nazareth, which was a prophet mighty in deed and word before God and all the people: 20And how the chief priests and our rulers delivered him to be condemned to death, and have crucified him. 21But we trusted that it had been he which should have redeemed Israel: and beside all this, to day is the third day since these things were done. 22Yea, and certain women also of our company made us astonished, which were early at the sepulchre; 23And when they found not his body, they came, saying, that they had also seen a vision of angels, which said that he was alive. 24And certain of them which were with us went to the sepulchre, and found it even so as the women had said: but him they saw not. 25Then he said unto them, O fools, and slow of heart to believe all that the prophets have spoken: 26Ought not Christ to have suffered these things, and to enter into his glory? 27And beginning at Moses and all the prophets, he expounded unto them in all the scriptures the things concerning himself. 28And they drew nigh unto the village, whither they went: and he made as though he would have gone further. 29But they constrained him, saying, Abide with us: for it is toward evening, and the day is far spent. And he went in to tarry with them. 30And it came to pass, as he sat at meat with them, he took bread, and blessed it, and brake, and gave to them. 31And their eyes were opened, and they knew him; and he vanished out of their sight. 32And they said one to another, Did not our heart burn within us, while he talked with us by the way, and while he opened to us the scriptures? 33And they rose up the same hour, and returned to Jerusalem, and found the eleven gathered together, and them that were with them, 34Saying, The Lord is risen indeed, and hath appeared to Simon. 35And they told what things were done in the way, and how he was known of them in breaking of bread.

36¶ And as they thus spake, Jesus himself stood in the midst of them, and saith unto them, Peace be unto you. 37But they were terrified and affrighted, and supposed that they had seen a spirit. 38And he said unto them, Why are ye troubled? and why do thoughts arise in your hearts? 39Behold my hands and my feet, that it is I myself: handle me, and see; for a spirit hath not flesh and bones, as ye see me have. 40And when he had thus spoken, he shewed them his hands and his feet. 41And while they yet believed not for joy, and wondered, he said unto them, Have ye here any meat? 42And they gave him a piece of a broiled fish, and of an honeycomb. 43And he took it, and did eat before them. 44And he said unto them, These are the words which I spake unto you, while I was yet with you, that all things must be fulfilled, which were written in the law of Moses, and in the prophets, and in the psalms, concerning me. 45Then opened he their understanding, that they might understand the scriptures, 46And said unto them, Thus it is written, and thus it behoved Christ to suffer, and to rise from the dead the third day: 47And that repentance and remission of sins should be preached in his name among all nations, beginning at Jerusalem. 48And ye are witnesses of these things.

49¶ And, behold, I send the promise of my Father upon you: but tarry ye in the city of Jerusalem, until ye be endued with power from on high.

50¶ And he led them out as far as to Bethany, and he lifted up his hands, and blessed them. 51And it came to pass, while he blessed them, he was parted from them, and carried up into heaven. 52And they worshipped him, and returned to Jerusalem with great joy: 53And were continually in the temple, praising and blessing God. Amen.