Luka 23 – NEN & HHH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 23:1-56

Yesu Apelekwa Kwa Pilato

(Mathayo 27:1-14; Marko 15:1-5; Yohana 18:28-38)

123:1 Mk 15:1; Yn 18:28Kisha umati wote wa watu ukainuka na kumpeleka Yesu kwa Pilato. 223:2 Lk 20:22; Yn 18:28Nao wakaanza kumshtaki wakisema: “Tumemwona huyu mtu akipotosha taifa letu, akiwazuia watu wasilipe kodi kwa Kaisari na kujiita kuwa yeye ni Kristo,23:2 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. mfalme.”

323:3 Mt 27:11; 1Tim 6:13Basi Pilato akamuuliza Yesu, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”

Yesu akajibu, “Wewe wasema.”

423:4 1Tim 6:13; 2Kor 5:21Pilato akawaambia viongozi wa makuhani na watu wote waliokuwepo, “Sioni sababu ya kutosha kumshtaki mtu huyu!”

523:5 Mk 1:14Lakini wao wakakazana kusema, “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika Uyahudi yote, tangu Galilaya alikoanzia, hadi sehemu hii!”

Yesu Apelekwa Kwa Herode

623:6 Lk 22:59Pilato aliposikia hayo akauliza, “Huyu mtu ni Mgalilaya?” 723:7 Mk 14:1; Lk 3:1Alipofahamu kwamba Yesu alikuwa chini ya mamlaka ya Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa pia Yerusalemu.

823:8 Lk 9:9Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amesikia mambo mengi kumhusu yeye. Pia alitarajia kumwona akifanya miujiza kadha wa kadha. 923:9 Mk 14:61Herode akamuuliza maswali mengi, lakini Yesu hakumjibu lolote. 10Wakati huo viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwepo wakitoa mashtaka yao kwa nguvu sana. 1123:11 Mk 15:17-19; Yn 19:2-3Herode na askari wake wakamdhihaki Yesu na kumfanyia mzaha. Wakamvika vazi zuri sana, wakamrudisha kwa Pilato. 1223:12 Mdo 4:27Siku hiyo, Herode na Pilato wakawa marafiki; kabla ya jambo hili walikuwa na uadui kati yao.

Yesu Ahukumiwa Kifo

(Mathayo 27:15-26; Marko 15:6-15; Yohana 18:39–19:16)

1323:13 Mt 27:23; Mk 15:14; Yn 18:38Basi Pilato akawaita pamoja viongozi wa makuhani, viongozi wengine na watu, 1423:14 Lk 23:1, 2, 4akawaambia, “Ninyi mlimleta huyu mtu kwangu kana kwamba ni mtu anayewachochea watu ili waasi. Nimemhoji mbele yenu nami nimeona hakuna msingi wowote wa mashtaka yenu dhidi yake. 15Wala Herode hakumwona na kosa lolote, ndiyo sababu amemrudisha kwetu. Kama mnavyoona, mtu huyu hakufanya jambo lolote linalostahili kifo. 1623:16 Mdo 16:37; 2Kor 11:23-24Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi na kumwachia.” [ 1723:17 Mt 27:15; Mk 15:6; Yn 18:39Kwa kuwa ilikuwa lazima kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa Sikukuu.]

1823:18 Mdo 3:13-14Ndipo watu wote wakapiga kelele kwa pamoja, “Mwondoe mtu huyo! Tufungulie Baraba!” 19(Baraba alikuwa amefungwa gerezani kwa sababu ya maasi yaliyokuwa yametokea mjini, na kwa ajili ya uuaji.)

20Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena. 21Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”

2223:22 Lk 23:18Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”

23Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda. 2423:24 Mt 27:26; Mk 15:15; Yn 19:17Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe. 25Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.

Kusulubiwa Kwa Yesu

(Mathayo 27:32-44; Marko 15:21-32; Yohana 19:17-27)

2623:26 Mt 27:32; Mk 15:21; Yn 19:17Walipokuwa wakienda naye, wakamkamata mtu mmoja aitwaye Simoni mwenyeji wa Kirene, aliyekuwa anapita zake kuingia mjini kutoka shambani. Wakambebesha msalaba, wakamlazimisha auchukue nyuma ya Yesu. 2723:27 Lk 8:52Idadi kubwa ya watu wakamfuata Yesu, wakiwamo wanawake waliokuwa wakimlilia na kumwombolezea. 2823:28 Lk 19:41-44; 21:23-24Yesu akawageukia, akawaambia, “Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi bali jililieni ninyi wenyewe na watoto wenu. 2923:29 Mt 24:19Kwa maana wakati utafika mtakaposema, ‘Wamebarikiwa wanawake tasa, ambao matumbo yao hayakuzaa, wala matiti yao hayakunyonyesha!’ 3023:30 Hos 10:8; Ufu 6:16Ndipo

“ ‘wataiambia milima, “Tuangukieni!”

na vilima, “Tufunikeni!” ’

3123:31 Eze 20:47Kwa maana kama wamefanya hivi kwa mti mbichi, kwa mti mkavu itakuwaje?”

3223:32 Isa 53:12; Mt 27:38Watu wengine wawili wahalifu, walipelekwa pamoja na Yesu ili wakasulubiwe. 33Walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, hapo ndipo walipomsulubisha Yesu pamoja na hao wahalifu, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wake wa kushoto. 3423:34 Mt 11:25; 5:44; Za 22:18Yesu akasema, “Baba, wasamehe, kwa maana hawajui walitendalo!” Wakagawana nguo zake kwa kupiga kura.

3523:35 Za 22:17; Isa 42:1; Zek 12:10; Mt 27:39; Mk 15:29Watu wakasimama hapo wakimwangalia, nao viongozi wa Wayahudi wakamdhihaki wakisema, “Aliokoa wengine! Ajiokoe mwenyewe basi, kama yeye ndiye Kristo wa Mungu, Mteule wake.”

3623:36 Za 22:7; 69:21; Mt 27:48Askari nao wakaja, wakamdhihaki. Wakamletea siki ili anywe, 3723:37 Lk 4:3, 9na wakamwambia, “Kama wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”

3823:38 Mt 2:2Kwenye msalaba juu ya kichwa chake, kulikuwa na maandishi haya: Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi.

Maandishi haya yalikuwa yameandikwa kwa lugha za Kiyunani, Kilatini na Kiebrania.

3923:39 Mt 27:44; Mk 15:32Mmoja wa wale wahalifu waliosulubiwa pamoja naye akamtukana, akasema: “Wewe si ndiye Kristo? Jiokoe mwenyewe na utuokoe na sisi.”

40Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake, akasema, “Je, wewe humwogopi Mungu, wakati uko kwenye adhabu iyo hiyo? 4123:41 Lk 23:4Sisi tumehukumiwa kwa haki kwa kuwa tunapata tunayostahili kwa ajili ya matendo yetu. Lakini huyu mtu hajafanya kosa lolote.”

4223:42 Mt 16; 27Kisha akasema, “Yesu, unikumbuke utakapokuja katika Ufalme wako.”

4323:43 1Kor 12:3-4; Ufu 2:7Yesu akamjibu, “Amin, nakuambia, leo hii utakuwa pamoja nami Paradiso.”23:43 Paradiso maana yake bustani nzuri, hapa ina maana mahali zinapokwenda roho za wacha Mungu, yaani watakatifu.

Kifo Cha Yesu

(Mathayo 27:45-56; Marko 15:33-41; Yohana 19:28-30)

4423:44 Amo 8:9Ilikuwa kama saa sita mchana, nalo giza likafunika nchi yote hadi saa tisa, 4523:45 Kut 26:31-33; Ebr 3:8; 10:19-20kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili. 4623:46 Mt 27:50; Za 31:5; 1Pet 2:23; Yn 19:30Yesu akapaza sauti yake akasema, “Baba, mikononi mwako naikabidhi roho yangu.” Baada ya kusema haya, akakata roho.

4723:47 Mt 9:8Yule jemadari alipoona yaliyotukia, akamsifu Mungu, akasema, “Hakika, mtu huyu alikuwa mwenye haki.” 4823:48 Lk 18:13Watu wote waliokuwa wamekusanyika hapo kushuhudia tukio hili walipoyaona hayo, wakapigapiga vifua vyao kwa huzuni na kwenda zao. 4923:49 Lk 8:2; Za 38:11Lakini wale wote waliomfahamu, pamoja na wale wanawake waliokuwa wamemfuata kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali wakiyatazama mambo haya.

Maziko Ya Yesu

(Mathayo 27:57-61; Marko 15:42-47; Yohana 19:38-42)

5023:50 Mt 27:59; Mk 15:46Basi kulikuwa na mtu mmoja mwema na mwenye haki, jina lake Yosefu. Yeye alikuwa mjumbe wa Baraza la Wayahudi,23:50 Baraza la Wayahudi hapa ina maana ya Sanhedrin ambalo lilikuwa ndilo baraza la juu kabisa la utawala wa Kiyahudi, lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. 5123:51 Lk 2:25, 38lakini yeye hakuwa amekubaliana na maamuzi na vitendo vya viongozi wenzake. Huyu alikuwa mwenyeji wa Arimathaya huko Uyahudi, naye alikuwa anaungojea Ufalme wa Mungu kwa matarajio makubwa. 52Yosefu alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu. 53Akaushusha kutoka msalabani, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi, na kuuweka katika kaburi lililochongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limezikiwa mtu mwingine bado. 5423:54 Mt 27:62Ilikuwa Siku ya Maandalizi, nayo Sabato ilikuwa karibu kuanza.

5523:55 Lk 8:2; Mk 15:47Wale wanawake waliokuwa wamekuja pamoja na Yesu wakimfuata kutoka Galilaya wakamfuata Yosefu, wakaliona kaburi na jinsi mwili wa Yesu ulivyolazwa. 5623:56 Mk 16:1; Lk 24:1; Kut 12:16; 20:11Kisha wakarudi nyumbani, wakaandaa manukato na marhamu ya kuupaka huo mwili. Lakini wakapumzika siku ya Sabato kama ilivyoamriwa.

Habrit Hakhadasha/Haderekh

הבשורה על-פי לוקס 23:1-56

1ראשי הכוהנים, הסופרים, זקני העם וחברי הסנהדרין הוליכו את ישוע אל פילטוס, 2ומיד החלו להאשים אותו: ”האיש הזה מסית את העם לא לשלם מס לקיסר הרומאי, וטוען שהוא המשיח, כלומר מלך!“

3”האם אתה מלך היהודים?“ שאל פילטוס את ישוע. ”אתה אומר“, ענה ישוע.

4פילטוס פנה אל ראשי הכוהנים ואל ההמון וקרא: ”מה אתם רוצים ממנו? הוא לא עבר על שום חוק!“

5אולם הם התעקשו: ”אבל הוא מסית את העם בכל אזור יהודה נגד השלטון. הוא החל בכך בגליל, ועכשיו הוא בא לירושלים.“

6”האם הוא תושב הגליל?“ שאל פילטוס.

7”כן“, השיבו לו. מאחר שהגליל היה במחוז שיפוטו של הורדוס, החליט פילטוס לשלוח את ישוע אליו. מלבד זאת, באותה העת היה הורדוס בירושלים.

8הורדוס שמח מאוד לראות את ישוע, מכיוון ששמע עליו ניסים ונפלאות, ומזה זמן רב השתוקק לפגוש אותו פנים אל פנים ולחזות בניסים שחולל.

9הורדוס שאל את ישוע שאלות רבות, אולם ישוע לא השיב דבר. 10בינתיים ראשי הכוהנים והסופרים הטיחו את האשמותיהם בישוע.

11גם הורדוס וחייליו בזו לישוע וצחקו לו; הם הלבישו אותו גלימת פאר ושלחוהו חזרה אל פילטוס. 12הורדוס ופילטוס, שהיו עד אז אויבים, הפכו באותו יום לידידים.

13פילטוס אסף את ראשי הכוהנים, ומנהיגים אחרים ואת העם, 14והודיע להם: ”הבאתם לפני את האיש הזה וטענתם שהוא מסית את העם למרוד בשלטון. חקרתי אותו היטב בנוכחותכם ולא מצאתי כל יסוד להאשמותיכם! 15גם הורדוס לא מצא כל אשמה בישוע, ולכן שלח אותו אלינו. האיש הזה לא עשה כל מעשה שדינו מוות! 16משום כך אלקה אותו בשוט ואשחרר אותו.“ 17מדי שנה בחג הפסח, נהג פילטוס לשחרר אסיר יהודי אחד.

18אך כולם צעקו פה אחד: ”קחו אותו מכאן! שחרר לנו את בר־אבא!“ 19(בר־אבא היה במאסר באשמת רצח והסתה למרד בירושלים). 20פילטוס רצה לשחרר את ישוע, ולכן ניסה להתווכח עם הקהל. 21אבל הקהל התעקש: ”צלוב אותו! צלוב אותו!“

22פילטוס שאל אותם פעם שלישית: ”מדוע? מה הוא עשה? לא מצאתי כל סיבה להוציאו להורג. אלקה אותו בשוט ואשחרר אותו.“ 23אבל הם המשיכו לצעוק ולהפציר בו לצלוב את ישוע, וצעקותיהם הכריעו את הנידון.

24פילטוס נכנע לדרישתם ודן את ישוע למוות. 25על־פי בקשתם שחרר את בר־אבא, שהיה אסור באשמת רצח ומרידה, ומסר לידיהם את ישוע כדי שיעשו בו כרצונם.

26בהוליכם את ישוע אל מקום הצליבה פגשו בדרך את שמעון הקוריני, שחזר מן השדה, ואילצוהו ללכת אחרי ישוע ולשאת את צלבו. 27בין הקהל הרב שהלך אחרי ישוע היו גם נשים רבות שספדו עליו. 28ישוע פנה אליהן ואמר: ”בנות ירושלים, אל תבכינה עלי, כי אם על עצמכן ועל ילדיכן, 29כי תבוא העת שבה נשים שאין להן ילדים תיחשבנה לבנות מזל.23‏.29 כג 29 כלשונו: ”הנה ימים באים ויאמרו: ’אשרי העקרות ואשרי המעיים אשר לא ילדו ואשרי השדיים אשר לא הניקו‘.“ 30בעת ההיא יתחננו בני־האדם לפני ההרים שיפלו עליהם ויכסו אותם, ולפני הגבעות – שתקבורנה אותם. 31שהרי אם זהו גורלו של אדם חף מפשע, מה נורא יהיה גורלם של האשמים באמת!“23‏.31 כג 31 כלשונו: ”אם ככה יעשו בעץ הלח, מה ייעשה ביבש?“

32יחד עם ישוע הובלו למוות גם שני פושעים. 33בהגיעם אל המקום שנקרא ”מקום הגולגולת“ – הם צלבו את השלושה: את ישוע במרכז, ואת שני הפושעים לימינו ולשמאלו.

34”אבי, סלח להם,“ קרא ישוע, ”כי אינם יודעים מה הם עושים!“ בינתיים ערכו החיילים הגרלה וחילקו ביניהם את בגדי ישוע. 35ההמון עמד והביט במתרחש, ואילו מנהיגי העם לעגו לו וקראו: ”הוא ’הושיע‘ כל־כך הרבה אנשים? אם הוא באמת המשיח בחיר האלוהים, הבה נראה כיצד יושיע את עצמו!“

36גם החיילים התלו בו; הם נתנו לו לשתות חומץ 37וקראו: ”אם אתה באמת מלך היהודים, הושע את עצמך!“

38מעל ראשו של ישוע תלו שלט: ”זהו מלך היהודים“.

39אחד הפושעים שהיה תלוי לצידו של ישוע לעג לו ואמר: ”אם אתה באמת המשיח, מדוע אינך מציל את עצמך ואותנו לפני שיהיה מאוחר מדי?“

40הפושע השני גער בחברו ואמר: ”האם גם במותך אינך ירא את האלוהים? 41אנחנו נענשים בעונש שמגיע לנו על מעשינו הרעים, אולם האדם הזה חף מפשע!“ 42הוא פנה אל ישוע ואמר: ”ישוע, זכור אותי כשתבוא אל מלכותך.“

43”עוד היום אתה תהיה איתי בגן־עדן“, ענה לו ישוע.

44בשעה שתים־עשרה בצהריים כיסה חושך את כל הארץ למשך שלוש שעות. 45אור השמש חשך, והפרוכת התלויה לפני קודש הקודשים בבית־המקדש נקרעה לשניים.

46לאחר מכן קרא ישוע בקול גדול: ”אבי, אני מפקיד את רוחי בידך.“ ונפח את נשמתו.

47קצין רומאי אחד, אשר ראה את המתרחש, נמלא יראת אלוהים וקרא: ”האיש הזה באמת היה צדיק!“

48משנוכחו האנשים שבאו לחזות בצליבה כי ישוע מת, הצטערו צער רב והלכו לבתיהם. 49כל חבריו וידידיו של ישוע, וביניהם הנשים שהלכו אחריו מהגליל, עמדו במרחק מה והביטו במתרחש.

50‏-51בין ידידיו של ישוע היה גם אדם בשם יוסף מהעיירה היהודית רמתיים. יוסף היה איש טוב וישר והאמין בביאת המשיח. למרות שהיה חבר הסנהדרין לא הסכים עם החלטתם ופעולתם.

52יוסף הלך אל פילטוס וביקש ממנו את גופתו של ישוע. 53לאחר שהוריד את הגופה מן הצלב עטף אותה יוסף בסדין, וקבר אותה בקבר חדש חצוב בסלע, שטרם נקבר בו איש. 54כל זה התרחש ביום שישי בערב, לפני כניסת השבת.

55הנשים אשר באו עם ישוע מהגליל הלכו אחרי יוסף וראו היכן שקבר את הגופה. 56לאחר מכן הלכו והכינו מרקחת בשמים, אולם לא שבו מיד אל הקבר, כי בינתיים נכנסה השבת והן לא רצו לחלל אותה.