Luka 22 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 22:1-71

Yuda Akubali Kumsaliti Yesu

(Mathayo 26:14-16; Marko 14:10-11)

122:1 Yn 11:55Wakati huu Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa imekaribia. 222:2 Mt 12:14Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wanatafuta njia ya kumuua Yesu, kwa sababu waliwaogopa watu. 322:3 Mt 4:10; Mk 14:10, 1122:3 Mt 4:10; Yn 13:2; Mt 10:4Shetani akamwingia Yuda, aliyeitwa Iskariote, mmoja wa wale Kumi na Wawili. 422:4 Mdo 4:1; 5:24Yuda akaenda kwa viongozi wa makuhani na kwa maafisa wa walinzi wa Hekalu, akazungumza nao jinsi ambavyo angeweza kumsaliti Yesu. 522:5 Zek 11:12Wakafurahi na wakakubaliana kumpa fedha. 6Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.

Maandalizi Ya Pasaka

(Mathayo 26:17-25; Marko 14:12-21; Yohana 13:21-30)

722:7 Kum 16:5-8; Mk 4:12Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa. 822:8 Mdo 3:1, 11; 4:13-19Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”

9Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”

10Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia. 11Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’ 12Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”

1322:13 Lk 19:32Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.

Kuanzishwa Kwa Meza Ya Bwana

(Mathayo 26:31-35; Marko 14:27-31; Yohana 13:36-38)

1422:14 Mk 6:30; Mt 26:20; Mk 14:17-18Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake. 1522:15 Mt 16:21Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu. 1622:16 Lk 14:15; Ufu 19:9Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”

17Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote. 1822:18 Mt 26:29; Mk 14:29Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”

1922:19 Mt 14:19Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”

2022:20 Zek 9:11; 2Kor 3:6Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu. 2122:21 Za 41:9Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami. 2222:22 Mt 8:20; Mdo 2:23; 4:29Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.” 2322:23 Mt 26:22; Yn 13:22, 25Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.

Mabishano Kuhusu Ukuu

2422:24 Mk 9:34; Lk 9:46Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao. 25Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’ 2622:26 1Pet 5:5; Mk 9:35; Lk 12:37Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye. 2722:27 Mt 20:28; Lk 12:37Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye. 2822:28 Ebr 4:15Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu. 2922:29 Mt 25:34; 2Tim 2:12Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi, 30ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”

Yesu Atabiri Kuwa Petro Atamkana

3122:31 Ay 16:12; Amo 9:9Yesu akasema, “Simoni, Simoni, sikiliza, Shetani ameomba kuwapepeta ninyi wote kama ngano. 3222:32 Yn 17:9-15; Rum 8:34; Yn 21:15-17Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe, nawe ukiisha kunirudia, uwaimarishe ndugu zako.”

3322:33 Yn 11:16Petro akajibu, “Bwana, niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na hata kifoni.”

3422:34 Mt 26:34; Mk 14:30; Yn 13:38Yesu akamjibu, “Ninakuambia Petro, kabla jogoo hajawika usiku wa leo, utakana mara tatu kwamba hunijui mimi.”

Mfuko, Mkoba Na Upanga

3522:35 Mt 10:9-10; Lk 9:3Kisha Yesu akawauliza, “Nilipowatuma bila mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu chochote?”

Wakajibu, “La, hatukupungukiwa na kitu chochote.”

36Akawaambia, “Lakini sasa, aliye na mfuko na auchukue, na aliye na mkoba vivyo hivyo. Naye asiye na upanga, auze joho lake anunue mmoja. 3722:37 Isa 53:12Kwa sababu, nawaambia, andiko hili lazima litimizwe juu yangu, kwamba, ‘Alihesabiwa pamoja na wakosaji’; kwa kweli yaliyoandikwa kunihusu mimi hayana budi kutimizwa.”

38Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, tazama hapa kuna panga mbili.”

Akawajibu, “Inatosha.”

Yesu Aomba Kwenye Mlima Wa Mizeituni

(Mathayo 26:36-46; Marko 14:32-42)

3922:39 Lk 21:37; Mt 21:1Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata. 4022:40 Mt 6:13; 26:41; Mk 14:38Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.” 4122:41 Lk 18:11Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba 4222:42 Mt 20:22; 26:39akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.” 4322:43 Mt 4:11; 1:13Malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu. 4422:44 Yn 12:27Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii, nalo jasho lake likawa kama matone ya damu yakidondoka ardhini.

45Baada ya kuomba, akawarudia wanafunzi wake akawakuta wamelala, wakiwa wamechoka kutokana na huzuni. 4622:46 Lk 22:40Naye akawauliza, “Mbona mmelala? Amkeni, mwombe ili msije mkaingia majaribuni.”

Yesu Akamatwa

(Mathayo 26:47-56; Marko 14:43-50; Yohana 18:3-11)

4722:47 Mt 26:47-57; Mk 14:43-49; Yn 18:2-11Yesu alipokuwa bado anazungumza, umati mkubwa wa watu ukaja. Uliongozwa na Yuda, ambaye alikuwa mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili. Akamkaribia Yesu ili ambusu. 48Lakini Yesu akamwambia, “Yuda, je, unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu?”

49Wafuasi wa Yesu walipoona yale yaliyokuwa yanakaribia kutokea, wakasema, “Bwana, tuwakatekate kwa panga zetu?” 5022:50 Mt 26:51; Mk 14:47; Yn 18:10Mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa upanga, akamkata sikio la kuume.

51Lakini Yesu akasema, “Acheni!” Akaligusa lile sikio la yule mtu na kumponya.

5222:52 Mt 26:55; Mk 14:14-48Kisha Yesu akawaambia wale viongozi wa makuhani, maafisa wa walinzi wa Hekalu, pamoja na wazee waliokuwa wamekuja kumkamata, “Mmekuja na panga na marungu, kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? 5322:53 Mt 26:55; Yn 12:27; Mt 8:12; Yn 3:20Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi Hekaluni lakini hamkunikamata. Lakini hii ni saa yenu, wakati giza linatawala!”

Petro Amkana Yesu

(Mathayo 26:57-75; Marko 14:53-72; Yohana 18:12-27)

5422:54 Mt 26:57; Mk 14:53; Mt 26:58; Yn 18:15Kisha wakamkamata Yesu, wakamchukua, wakaenda naye mpaka nyumbani kwa kuhani mkuu. Lakini Petro akafuata kwa mbali. 5522:55 Mt 26:69; Mk 14:66Walipokwisha kuwasha moto katikati ya ua na kuketi pamoja, Petro naye akaketi pamoja nao. 56Mtumishi mmoja wa kike akamwona kwa mwanga wa moto akiwa ameketi pale. Akamtazama sana, akasema, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja na Yesu!”

57Lakini Petro akakana, akasema, “Ewe mwanamke, hata simjui!”

5822:58 Mt 26:71; Mk 14:69; Yn 18:26Baadaye kidogo, mtu mwingine alimwona Petro akasema, “Wewe pia ni mmoja wao!” Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sio mmoja wao!”

5922:59 Lk 23:6Baada ya muda wa kama saa moja hivi, mtu mwingine akazidi kusisitiza, “Kwa hakika huyu mtu naye alikuwa pamoja na Yesu, kwa maana yeye pia ni Mgalilaya.”

60Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sijui unalosema!” Wakati huo huo, akiwa bado anazungumza, jogoo akawika. 6122:61 Lk 7:13Naye Bwana akageuka, akamtazama Petro. Ndipo Petro akakumbuka lile neno ambalo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.” 62Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.

Walinzi Wamdhihaki Yesu Na Kumpiga

(Mathayo 26:67-68; Marko 14:65)

6322:63 Mt 26:67, 68; Mk 14:6522:63 Mt 26:67, 68; Mk 14:65Watu waliokuwa wanamlinda Yesu wakaanza kumdhihaki na kumpiga. 64Wakamfunga kitambaa machoni na kumuuliza, “Tabiri! Tuambie ni nani aliyekupiga?” 6522:65 Mt 16:21Wakaendelea kumtukana kwa matusi mengi.

Yesu Apelekwa Mbele Ya Baraza

(Mathayo 26:59-66; Marko 14:55-64; Yohana 18:28-38)

6622:66 Mt 5:22; 27:1; Mk 15:1; Mdo 4:26; 22:5Kulipopambazuka, baraza la wazee wa watu,22:66 Baraza la wazee hapa ina maana ya Sanhedrin ambalo lilikuwa ndilo Baraza la juu kabisa la utawala wa Kiyahudi, lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. yaani viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, wakakutana pamoja, naye Yesu akaletwa mbele yao. 6722:67 Mt 26:63; Mk 14:61Wakamwambia, “Kama wewe ndiye Kristo,22:67 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. tuambie.”

Yesu akawajibu, “Hata nikiwaambia hamtaamini. 6822:68 Lk 20:3-8Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu. 6922:69 Mk 16:19Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”

7022:70 Mt 26:65; 27:11; Lk 23:3Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?”

Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”

7122:71 Mt 26:65; Mk 14:62Kisha wakasema, “Tuna haja gani tena ya ushahidi zaidi? Tumesikia wenyewe kutoka kinywani mwake.”

New International Version – UK

Luke 22:1-71

Judas agrees to betray Jesus

1Now the Festival of Unleavened Bread, called the Passover, was approaching, 2and the chief priests and the teachers of the law were looking for some way to get rid of Jesus, for they were afraid of the people. 3Then Satan entered Judas, called Iscariot, one of the Twelve. 4And Judas went to the chief priests and the officers of the temple guard and discussed with them how he might betray Jesus. 5They were delighted and agreed to give him money. 6He consented, and watched for an opportunity to hand Jesus over to them when no crowd was present.

The Last Supper

7Then came the day of Unleavened Bread on which the Passover lamb had to be sacrificed. 8Jesus sent Peter and John, saying, ‘Go and make preparations for us to eat the Passover.’

9‘Where do you want us to prepare for it?’ they asked.

10He replied, ‘As you enter the city, a man carrying a jar of water will meet you. Follow him to the house that he enters, 11and say to the owner of the house, “The Teacher asks: where is the guest room, where I may eat the Passover with my disciples?” 12He will show you a large room upstairs, all furnished. Make preparations there.’

13They left and found things just as Jesus had told them. So they prepared the Passover.

14When the hour came, Jesus and his apostles reclined at the table. 15And he said to them, ‘I have eagerly desired to eat this Passover with you before I suffer. 16For I tell you, I will not eat it again until it finds fulfilment in the kingdom of God.’

17After taking the cup, he gave thanks and said, ‘Take this and divide it among you. 18For I tell you I will not drink again from the fruit of the vine until the kingdom of God comes.’

19And he took bread, gave thanks and broke it, and gave it to them, saying, ‘This is my body given for you; do this in remembrance of me.’

20In the same way, after the supper he took the cup, saying, ‘This cup is the new covenant in my blood, which is poured out for you.22:19,20 Some manuscripts do not have given for you… poured out for you. 21But the hand of him who is going to betray me is with mine on the table. 22The Son of Man will go as it has been decreed. But woe to that man who betrays him!’ 23They began to question among themselves which of them it might be who would do this.

24A dispute also arose among them as to which of them was considered to be greatest. 25Jesus said to them, ‘The kings of the Gentiles lord it over them; and those who exercise authority over them call themselves Benefactors. 26But you are not to be like that. Instead, the greatest among you should be like the youngest, and the one who rules like the one who serves. 27For who is greater, the one who is at the table or the one who serves? Is it not the one who is at the table? But I am among you as one who serves. 28You are those who have stood by me in my trials. 29And I confer on you a kingdom, just as my Father conferred one on me, 30so that you may eat and drink at my table in my kingdom and sit on thrones, judging the twelve tribes of Israel.

31‘Simon, Simon, Satan has asked to sift all of you as wheat. 32But I have prayed for you, Simon, that your faith may not fail. And when you have turned back, strengthen your brothers.’

33But he replied, ‘Lord, I am ready to go with you to prison and to death.’

34Jesus answered, ‘I tell you, Peter, before the cock crows today, you will deny three times that you know me.’

35Then Jesus asked them, ‘When I sent you without purse, bag or sandals, did you lack anything?’

‘Nothing,’ they answered.

36He said to them, ‘But now if you have a purse, take it, and also a bag; and if you don’t have a sword, sell your cloak and buy one. 37It is written: “And he was numbered with the transgressors”22:37 Isaiah 53:12; and I tell you that this must be fulfilled in me. Yes, what is written about me is reaching its fulfilment.’

38The disciples said, ‘See, Lord, here are two swords.’

‘That’s enough!’ he replied.

Jesus prays on the Mount of Olives

39Jesus went out as usual to the Mount of Olives, and his disciples followed him. 40On reaching the place, he said to them, ‘Pray that you will not fall into temptation.’ 41He withdrew about a stone’s throw beyond them, knelt down and prayed, 42‘Father, if you are willing, take this cup from me; yet not my will, but yours be done.’ 43An angel from heaven appeared to him and strengthened him. 44And being in anguish, he prayed more earnestly, and his sweat was like drops of blood falling to the ground.22:43,44 Many early manuscripts do not have verses 43 and 44.

45When he rose from prayer and went back to the disciples, he found them asleep, exhausted from sorrow. 46‘Why are you sleeping?’ he asked them. ‘Get up and pray so that you will not fall into temptation.’

Jesus arrested

47While he was still speaking a crowd came up, and the man who was called Judas, one of the Twelve, was leading them. He approached Jesus to kiss him, 48but Jesus asked him, ‘Judas, are you betraying the Son of Man with a kiss?’

49When Jesus’ followers saw what was going to happen, they said, ‘Lord, should we strike with our swords?’ 50And one of them struck the servant of the high priest, cutting off his right ear.

51But Jesus answered, ‘No more of this!’ And he touched the man’s ear and healed him.

52Then Jesus said to the chief priests, the officers of the temple guard, and the elders, who had come for him, ‘Am I leading a rebellion, that you have come with swords and clubs? 53Every day I was with you in the temple courts, and you did not lay a hand on me. But this is your hour – when darkness reigns.’

Peter disowns Jesus

54Then seizing him, they led him away and took him into the house of the high priest. Peter followed at a distance. 55And when some there had kindled a fire in the middle of the courtyard and had sat down together, Peter sat down with them. 56A servant-girl saw him seated there in the firelight. She looked closely at him and said, ‘This man was with him.’

57But he denied it. ‘Woman, I don’t know him,’ he said.

58A little later someone else saw him and said, ‘You also are one of them.’

‘Man, I am not!’ Peter replied.

59About an hour later another asserted, ‘Certainly this fellow was with him, for he is a Galilean.’

60Peter replied, ‘Man, I don’t know what you’re talking about!’ Just as he was speaking, the cock crowed. 61The Lord turned and looked straight at Peter. Then Peter remembered the word the Lord had spoken to him: ‘Before the cock crows today, you will disown me three times.’ 62And he went outside and wept bitterly.

The guards mock Jesus

63The men who were guarding Jesus began mocking and beating him. 64They blindfolded him and demanded, ‘Prophesy! Who hit you?’ 65And they said many other insulting things to him.

Jesus before Pilate and Herod

66At daybreak the council of the elders of the people, both the chief priests and the teachers of the law, met together, and Jesus was led before them. 67‘If you are the Messiah,’ they said, ‘tell us.’

Jesus answered, ‘If I tell you, you will not believe me, 68and if I asked you, you would not answer. 69But from now on, the Son of Man will be seated at the right hand of the mighty God.’

70They all asked, ‘Are you then the Son of God?’

He replied, ‘You say that I am.’

71Then they said, ‘Why do we need any more testimony? We have heard it from his own lips.’