Luka 22 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 22:1-71

Yuda Akubali Kumsaliti Yesu

(Mathayo 26:14-16; Marko 14:10-11)

122:1 Yn 11:55Wakati huu Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa imekaribia. 222:2 Mt 12:14Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wanatafuta njia ya kumuua Yesu, kwa sababu waliwaogopa watu. 322:3 Mt 4:10; Mk 14:10, 1122:3 Mt 4:10; Yn 13:2; Mt 10:4Shetani akamwingia Yuda, aliyeitwa Iskariote, mmoja wa wale Kumi na Wawili. 422:4 Mdo 4:1; 5:24Yuda akaenda kwa viongozi wa makuhani na kwa maafisa wa walinzi wa Hekalu, akazungumza nao jinsi ambavyo angeweza kumsaliti Yesu. 522:5 Zek 11:12Wakafurahi na wakakubaliana kumpa fedha. 6Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.

Maandalizi Ya Pasaka

(Mathayo 26:17-25; Marko 14:12-21; Yohana 13:21-30)

722:7 Kum 16:5-8; Mk 4:12Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa. 822:8 Mdo 3:1, 11; 4:13-19Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”

9Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”

10Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia. 11Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’ 12Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”

1322:13 Lk 19:32Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.

Kuanzishwa Kwa Meza Ya Bwana

(Mathayo 26:31-35; Marko 14:27-31; Yohana 13:36-38)

1422:14 Mk 6:30; Mt 26:20; Mk 14:17-18Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake. 1522:15 Mt 16:21Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu. 1622:16 Lk 14:15; Ufu 19:9Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”

17Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote. 1822:18 Mt 26:29; Mk 14:29Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”

1922:19 Mt 14:19Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”

2022:20 Zek 9:11; 2Kor 3:6Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu. 2122:21 Za 41:9Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami. 2222:22 Mt 8:20; Mdo 2:23; 4:29Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.” 2322:23 Mt 26:22; Yn 13:22, 25Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.

Mabishano Kuhusu Ukuu

2422:24 Mk 9:34; Lk 9:46Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao. 25Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’ 2622:26 1Pet 5:5; Mk 9:35; Lk 12:37Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye. 2722:27 Mt 20:28; Lk 12:37Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye. 2822:28 Ebr 4:15Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu. 2922:29 Mt 25:34; 2Tim 2:12Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi, 30ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”

Yesu Atabiri Kuwa Petro Atamkana

3122:31 Ay 16:12; Amo 9:9Yesu akasema, “Simoni, Simoni, sikiliza, Shetani ameomba kuwapepeta ninyi wote kama ngano. 3222:32 Yn 17:9-15; Rum 8:34; Yn 21:15-17Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe, nawe ukiisha kunirudia, uwaimarishe ndugu zako.”

3322:33 Yn 11:16Petro akajibu, “Bwana, niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na hata kifoni.”

3422:34 Mt 26:34; Mk 14:30; Yn 13:38Yesu akamjibu, “Ninakuambia Petro, kabla jogoo hajawika usiku wa leo, utakana mara tatu kwamba hunijui mimi.”

Mfuko, Mkoba Na Upanga

3522:35 Mt 10:9-10; Lk 9:3Kisha Yesu akawauliza, “Nilipowatuma bila mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu chochote?”

Wakajibu, “La, hatukupungukiwa na kitu chochote.”

36Akawaambia, “Lakini sasa, aliye na mfuko na auchukue, na aliye na mkoba vivyo hivyo. Naye asiye na upanga, auze joho lake anunue mmoja. 3722:37 Isa 53:12Kwa sababu, nawaambia, andiko hili lazima litimizwe juu yangu, kwamba, ‘Alihesabiwa pamoja na wakosaji’; kwa kweli yaliyoandikwa kunihusu mimi hayana budi kutimizwa.”

38Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, tazama hapa kuna panga mbili.”

Akawajibu, “Inatosha.”

Yesu Aomba Kwenye Mlima Wa Mizeituni

(Mathayo 26:36-46; Marko 14:32-42)

3922:39 Lk 21:37; Mt 21:1Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata. 4022:40 Mt 6:13; 26:41; Mk 14:38Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.” 4122:41 Lk 18:11Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba 4222:42 Mt 20:22; 26:39akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.” 4322:43 Mt 4:11; 1:13Malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu. 4422:44 Yn 12:27Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii, nalo jasho lake likawa kama matone ya damu yakidondoka ardhini.

45Baada ya kuomba, akawarudia wanafunzi wake akawakuta wamelala, wakiwa wamechoka kutokana na huzuni. 4622:46 Lk 22:40Naye akawauliza, “Mbona mmelala? Amkeni, mwombe ili msije mkaingia majaribuni.”

Yesu Akamatwa

(Mathayo 26:47-56; Marko 14:43-50; Yohana 18:3-11)

4722:47 Mt 26:47-57; Mk 14:43-49; Yn 18:2-11Yesu alipokuwa bado anazungumza, umati mkubwa wa watu ukaja. Uliongozwa na Yuda, ambaye alikuwa mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili. Akamkaribia Yesu ili ambusu. 48Lakini Yesu akamwambia, “Yuda, je, unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu?”

49Wafuasi wa Yesu walipoona yale yaliyokuwa yanakaribia kutokea, wakasema, “Bwana, tuwakatekate kwa panga zetu?” 5022:50 Mt 26:51; Mk 14:47; Yn 18:10Mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa upanga, akamkata sikio la kuume.

51Lakini Yesu akasema, “Acheni!” Akaligusa lile sikio la yule mtu na kumponya.

5222:52 Mt 26:55; Mk 14:14-48Kisha Yesu akawaambia wale viongozi wa makuhani, maafisa wa walinzi wa Hekalu, pamoja na wazee waliokuwa wamekuja kumkamata, “Mmekuja na panga na marungu, kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi? 5322:53 Mt 26:55; Yn 12:27; Mt 8:12; Yn 3:20Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi Hekaluni lakini hamkunikamata. Lakini hii ni saa yenu, wakati giza linatawala!”

Petro Amkana Yesu

(Mathayo 26:57-75; Marko 14:53-72; Yohana 18:12-27)

5422:54 Mt 26:57; Mk 14:53; Mt 26:58; Yn 18:15Kisha wakamkamata Yesu, wakamchukua, wakaenda naye mpaka nyumbani kwa kuhani mkuu. Lakini Petro akafuata kwa mbali. 5522:55 Mt 26:69; Mk 14:66Walipokwisha kuwasha moto katikati ya ua na kuketi pamoja, Petro naye akaketi pamoja nao. 56Mtumishi mmoja wa kike akamwona kwa mwanga wa moto akiwa ameketi pale. Akamtazama sana, akasema, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja na Yesu!”

57Lakini Petro akakana, akasema, “Ewe mwanamke, hata simjui!”

5822:58 Mt 26:71; Mk 14:69; Yn 18:26Baadaye kidogo, mtu mwingine alimwona Petro akasema, “Wewe pia ni mmoja wao!” Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sio mmoja wao!”

5922:59 Lk 23:6Baada ya muda wa kama saa moja hivi, mtu mwingine akazidi kusisitiza, “Kwa hakika huyu mtu naye alikuwa pamoja na Yesu, kwa maana yeye pia ni Mgalilaya.”

60Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sijui unalosema!” Wakati huo huo, akiwa bado anazungumza, jogoo akawika. 6122:61 Lk 7:13Naye Bwana akageuka, akamtazama Petro. Ndipo Petro akakumbuka lile neno ambalo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.” 62Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.

Walinzi Wamdhihaki Yesu Na Kumpiga

(Mathayo 26:67-68; Marko 14:65)

6322:63 Mt 26:67, 68; Mk 14:6522:63 Mt 26:67, 68; Mk 14:65Watu waliokuwa wanamlinda Yesu wakaanza kumdhihaki na kumpiga. 64Wakamfunga kitambaa machoni na kumuuliza, “Tabiri! Tuambie ni nani aliyekupiga?” 6522:65 Mt 16:21Wakaendelea kumtukana kwa matusi mengi.

Yesu Apelekwa Mbele Ya Baraza

(Mathayo 26:59-66; Marko 14:55-64; Yohana 18:28-38)

6622:66 Mt 5:22; 27:1; Mk 15:1; Mdo 4:26; 22:5Kulipopambazuka, baraza la wazee wa watu,22:66 Baraza la wazee hapa ina maana ya Sanhedrin ambalo lilikuwa ndilo Baraza la juu kabisa la utawala wa Kiyahudi, lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. yaani viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, wakakutana pamoja, naye Yesu akaletwa mbele yao. 6722:67 Mt 26:63; Mk 14:61Wakamwambia, “Kama wewe ndiye Kristo,22:67 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. tuambie.”

Yesu akawajibu, “Hata nikiwaambia hamtaamini. 6822:68 Lk 20:3-8Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu. 6922:69 Mk 16:19Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”

7022:70 Mt 26:65; 27:11; Lk 23:3Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?”

Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”

7122:71 Mt 26:65; Mk 14:62Kisha wakasema, “Tuna haja gani tena ya ushahidi zaidi? Tumesikia wenyewe kutoka kinywani mwake.”

New International Reader’s Version

Luke 22:1-71

Judas Agrees to Hand Jesus Over

1The Feast of Unleavened Bread, called the Passover, was near. 2The chief priests and the teachers of the law were looking for a way to get rid of Jesus. They were afraid of the people. 3Then Satan entered Judas, who was called Iscariot. Judas was one of the 12 disciples. 4He went to the chief priests and the officers of the temple guard. He talked with them about how he could hand Jesus over to them. 5They were delighted and agreed to give him money. 6Judas accepted their offer. He watched for the right time to hand Jesus over to them. He wanted to do it when no crowd was around.

The Last Supper

7Then the day of Unleavened Bread came. That was the time the Passover lamb had to be sacrificed. 8Jesus sent Peter and John on ahead. “Go,” he told them. “Prepare for us to eat the Passover meal.”

9“Where do you want us to prepare for it?” they asked.

10Jesus replied, “When you enter the city, a man carrying a jar of water will meet you. Follow him to the house he enters. 11Then say to the owner of the house, ‘The Teacher asks, “Where is the guest room? Where can I eat the Passover meal with my disciples?” ’ 12He will show you a large upstairs room with furniture already in it. Prepare for us to eat there.”

13Peter and John left. They found things just as Jesus had told them. So they prepared the Passover meal.

14When the hour came, Jesus and his apostles took their places at the table. 15He said to them, “I have really looked forward to eating this Passover meal with you. I wanted to do this before I suffer. 16I tell you, I will not eat the Passover meal again until it is celebrated in God’s kingdom.”

17After Jesus took the cup, he gave thanks. He said, “Take this cup and share it among yourselves. 18I tell you, I will not drink wine with you again until God’s kingdom comes.”

19Then Jesus took bread. He gave thanks and broke it. He handed it to them and said, “This is my body. It is given for you. Every time you eat it, do this in memory of me.”

20In the same way, after the supper he took the cup. He said, “This cup is the new covenant in my blood. It is poured out for you. 21But someone here is going to hand me over to my enemies. His hand is with mine on the table. 22The Son of Man will go to his death, just as God has already decided. But how terrible it will be for the one who hands him over!” 23The apostles began to ask one another about this. They wondered which one of them would do it.

24They also started to argue. They disagreed about which of them was thought to be the most important person. 25Jesus said to them, “The kings of the Gentiles hold power over their people. And those who order them around call themselves Protectors. 26But you must not be like that. Instead, the most important among you should be like the youngest. The one who rules should be like the one who serves. 27Who is more important? Is it the one at the table, or the one who serves? Isn’t it the one who is at the table? But I am among you as one who serves. 28You have stood by me during my troubles. 29And I give you a kingdom, just as my Father gave me a kingdom. 30Then you will eat and drink at my table in my kingdom. And you will sit on thrones, judging the 12 tribes of Israel.

31“Simon, Simon! Satan has asked to sift all of you disciples like wheat. 32But I have prayed for you, Simon. I have prayed that your faith will not fail. When you have turned back, help your brothers to be strong.”

33But Simon replied, “Lord, I am ready to go with you to prison and to death.”

34Jesus answered, “I tell you, Peter, you will say three times that you don’t know me. And you will do it before the rooster crows today.”

35Then Jesus asked the disciples, “Did you need anything when I sent you without a purse, bag or sandals?”

“Nothing,” they answered.

36He said to them, “But now if you have a purse, take it. And also take a bag. If you don’t have a sword, sell your coat and buy one. 37It is written, ‘He was counted among those who had committed crimes.’ (Isaiah 53:12) I tell you that what is written about me must come true. Yes, it is already coming true.”

38The disciples said, “See, Lord, here are two swords.”

“Two swords are enough!” he replied.

Jesus Prays on the Mount of Olives

39Jesus went out as usual to the Mount of Olives. His disciples followed him. 40When they reached the place, Jesus spoke. “Pray that you won’t fall into sin when you are tempted,” he said to them. 41Then he went a short distance away from them. There he got down on his knees and prayed. 42He said, “Father, if you are willing, take this cup of suffering away from me. But do what you want, not what I want.” 43An angel from heaven appeared to Jesus and gave him strength. 44Because he was very sad and troubled, he prayed even harder. His sweat was like drops of blood falling to the ground.

45After that, he got up from prayer and went back to the disciples. He found them sleeping. They were worn out because they were very sad. 46“Why are you sleeping?” he asked them. “Get up! Pray that you won’t fall into sin when you are tempted.”

Jesus Is Arrested

47While Jesus was still speaking, a crowd came up. The man named Judas was leading them. He was one of the 12 disciples. Judas approached Jesus to kiss him. 48But Jesus asked him, “Judas, are you handing over the Son of Man with a kiss?”

49Jesus’ followers saw what was going to happen. So they said, “Lord, should we use our swords against them?” 50One of them struck the slave of the high priest and cut off his right ear.

51But Jesus answered, “Stop this!” And he touched the man’s ear and healed him.

52Then Jesus spoke to the chief priests, the officers of the temple guard, and the elders. They had all come for him. “Am I leading a band of armed men against you?” he asked. “Do you have to come with swords and clubs? 53Every day I was with you in the temple courtyard. And you didn’t lay a hand on me. But this is your hour. This is when darkness rules.”

Peter Says He Does Not Know Jesus

54Then the men arrested Jesus and led him away. They took him into the high priest’s house. Peter followed from far away. 55Some people there started a fire in the middle of the courtyard. Then they sat down together. Peter sat down with them. 56A female servant saw him sitting there in the firelight. She looked closely at him. Then she said, “This man was with Jesus.”

57But Peter said he had not been with him. “Woman, I don’t know him,” he said.

58A little later someone else saw Peter. “You also are one of them,” he said.

“No,” Peter replied. “I’m not!”

59About an hour later, another person spoke up. “This fellow must have been with Jesus,” he said. “He is from Galilee.”

60Peter replied, “Man, I don’t know what you’re talking about!” Just as he was speaking, the rooster crowed. 61The Lord turned and looked right at Peter. Then Peter remembered what the Lord had spoken to him. “The rooster will crow today,” Jesus had said. “Before it does, you will say three times that you don’t know me.” 62Peter went outside. He broke down and cried.

The Guards Make Fun of Jesus

63There were men guarding Jesus. They began laughing at him and beating him. 64They blindfolded him. They said, “Prophesy! Who hit you?” 65They also said many other things to make fun of him.

Jesus Is Brought to Pilate and Herod

66At dawn the elders of the people met together. These included the chief priests and the teachers of the law. Jesus was led to them. 67“If you are the Messiah,” they said, “tell us.”

Jesus answered, “If I tell you, you will not believe me. 68And if I asked you, you would not answer. 69But from now on, the Son of Man will be seated at the right hand of the mighty God.”

70They all asked, “Are you the Son of God then?”

He replied, “You say that I am.”

71Then they said, “Why do we need any more witnesses? We have heard it from his own lips.”