Luka 19 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 19:1-48

Zakayo Mtoza Ushuru

119:1 Lk 18:35Yesu akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji. 2Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo. 3Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo. 419:4 1Fal 10:27; 1Nya 27:28; Lk 18:37Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.

5Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!” 6Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.

719:7 Mt 9:11Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, “Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.’ ”

819:8 Lk 7:13; 3:12-13; Hes 5:7; Eze 33:14-15Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, “Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango.”

919:9 Rum 4:16; Gal 3:17Ndipo Yesu akamwambia, “Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Abrahamu. 1019:10 Eze 34:12-16; Yn 3:17Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”

Mfano Wa Fedha

(Mathayo 25:14-30)

1119:11 Lk 17:20; Mt 3:2; Mdo 1:6Walipokuwa wanasikiliza haya, Yesu akaendelea kuwaambia mfano, kwa sababu alikuwa anakaribia Yerusalemu na watu walikuwa wakidhani ya kuwa Ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja saa iyo hiyo. 1219:12 Mk 13:34; Mt 25:14Hivyo akawaambia: “Mtu mmoja mwenye cheo kikubwa alisafiri kwenda nchi ya mbali ili akapokee madaraka ya kuwa mfalme, kisha arudi. 1319:13 Mk 13:34Hivyo akawaita kumi miongoni mwa watumishi wake, na akawapa kila mmoja fungu la fedha. Akawaambia, ‘Fanyeni biashara na fedha hizi mpaka nitakaporudi.’

1419:14 Yn 1:11“Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’

15“Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.

16“Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’

17“Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’

18“Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’

19“Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’

20“Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa. 2119:21 Mit 27:18; Lk 16:10Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’

2219:22 2Sam 1:16; Ay 15:6; Mt 25:26“Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda, 23kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’

24“Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’

25“Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’

2619:26 Mt 13:12; 25:29“Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa. 27Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’ ”

Yesu Aingia Yerusalemu Kwa Ushindi

(Mathayo 21:1-11; Marko 11:1-11; Yohana 12:12-19)

2819:28 Mk 10:32; Lk 9:51Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu. 2919:29 Mt 21:1, 1719:29 Mt 21:1-9; Mk 11:1-10; Yn 12:12-16Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia, 30“Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa. 31Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’ ”

3219:32 Lk 22:13Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia. 3319:33 2Fal 9:13Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”

34Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”

3519:35 2Fal 9:13; Mt 21:7; Mk 11:7; Yn 12:14Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake. 3619:36 Mt 21:18Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.

3719:37 Mt 21:1Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:

3819:38 Za 118:26; Lk 13:35; 2:14“Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!”

“Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”

3919:39 Mt 21:15-16Baadhi ya Mafarisayo waliokuwamo miongoni mwa ule umati wa watu wakamwambia, “Mwalimu, waamuru wanafunzi wako wanyamaze.”

4019:40 Ebr 2:11Yesu akawajibu, “Nawaambia ninyi, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapiga kelele.”

Yesu Anaulilia Mji Wa Yerusalemu

4119:41 Isa 22:4; Lk 13:34-35Alipokaribia Yerusalemu na kuuona mji, aliulilia, 4219:42 Kum 32:29; Mt 13:14; Yn 12:38akisema, “Laiti ungalijua hata wewe leo yale ambayo yangeleta amani, lakini sasa yamefichika machoni pako. 4319:43 Yer 6:6; Lk 21:20Hakika siku zinakujia, ambazo adui zako watakuzingira, nao watakuzunguka pande zote na kukuzuilia ndani. 4419:44 Za 137:9; Mt 24:2; Mk 13:2; 1Pet 2:12Watakuponda chini, wewe na watoto walioko ndani ya kuta zako. Nao hawataacha hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukutambua wakati wa kujiliwa kwako.”

Yesu Atakasa Hekaluni

(Mathayo 21:12-17; Marko 11:15-19; Yohana 2:13-22)

4519:45 Mt 21:12; Mk 11:11, 15; Yn 2:14, 15Ndipo akaingia eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza vitu humo. 4619:46 Isa 56:7; Yer 7:11Naye akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’ ”

4719:47 Mt 26:55; 12:14; Mk 11:18Kila siku alikuwa akifundisha Hekaluni. Lakini viongozi wa makuhani, walimu wa sheria na viongozi wa watu walikuwa wakitafuta njia ili kumuua. 48Lakini hawakupata nafasi kwa sababu watu wote walimfuata wakiyasikiliza maneno yake kwa usikivu mwingi.

Knijga O Kristu

Luka 19:1-48

Isus i Zakej

1Isus uđe u Jerihon. Dok je prolazio gradom, 2dođe čovjek imenom Zakej, utjecajan Židov koji je radio za rimsku poreznu upravu i vrlo se obogatio. 3Želio je vidjeti Isusa, ali je bio prenizak rastom da bi ga mogao vidjeti preko mnoštva. 4On zato potrči naprijed te se popne na smokvu pokraj koje je Isus trebao proći da s nje promatra.

5Kad je Isus stigao do njega, pogleda gore i reče mu: “Zakeju, brzo siđi! Danas moram k tebi u goste.”

6Zakej žurno siđe s drveta i primi ga u goste sav radostan. 7Ali mnoštvo koje je to promatralo počne prigovarati: “Otišao je takvom grešniku u goste!”

8A Zakej ustane i reče Gospodinu: “Gospodine, polovicu svojega imanja dat ću siromasima, a svakome koga sam prevario četverostruko ću vratiti.”

9“Danas je u ovu kuću došlo spasenje jer je i ovaj čovjek Abrahamov sin! 10Ja, Sin Čovječji, došao sam tražiti i spasiti izgubljene.”

Prispodoba o desetorici slugu

(Mt 25:14-30)

11Mnoštvo je sve to slušalo. Kako je već bio nadomak Jeruzalemu, mislili su da će se kraljevstvo Božje odmah pojaviti. Isus im zato ispriča prispodobu: 12“Neki je ugledan čovjek trebao otputovati u daleku zemlju da ga ondje okrune za kralja, a zatim se vratiti. 13Pozove zato desetoricu svojih slugu, dade svakomu pola kilograma srebra19:13 U grčkome: 10 mina (svakome jednu minu, što je u to doba iznosilo otprilike tri mjesečne plaće). te im reče: ‘Trgujte s njime dok ne dođem.’ 14Ali njegovi su ga građani mrzili i poslali su za njim poslanike s porukom: ‘Ne želimo da on kraljuje nad nama.’

15Kad se vratio kao kralj, zapovjedi da mu pozovu sluge kojima je dao novac. Htio je znati koliko je koji zaradio. 16Prvi sluga dođe i reče: ‘Gospodaru, udeseterostručio sam iznos koji si mi dao.’ 17‘Odlično! Dobar si sluga’, reče mu on. ‘Zato što si bio vjeran u najmanjemu, dajem ti da vladaš nad deset gradova.’

18Drugi sluga dođe i reče: ‘Upeterostručio sam iznos, gospodaru.’ 19‘Dobro! Vladaj nad pet gradova’, reče i njemu.

20Ali treći sluga dođe bez zarade i reče: ‘Gospodaru, evo ti srebra. Držao sam ga skrivenoga u rupcu. 21Bojao sam te se zato što si strog čovjek. Uzimaš što nije tvoje i žanješ što nisi posijao.’

22‘Zli slugo!’ odgovori mu on. ‘Sudit ću ti prema tvojim vlastitim riječima. Znao si da sam strog, da uzimam što nije moje i da žanjem što nisam posijao? 23Zašto onda nisi moj novac uložio u banku?19:23 U grčkome: kod novčara. Tako bih barem dobio kamate.’ 24Zatim kralj reče: ‘Oduzmite mu to srebro i dajte ga onome koji ima deset!’

25‘Ali, gospodaru, pa on već ima pet kilograma srebra!19:25 U grčkome: deset mina.’ kazali su.

26‘Velim vam,’ odgovori im kralj, ‘onome tko ima dat će se još, a onome tko nema oduzet će se i ono što ima. 27A moje neprijatelje, koji me nisu htjeli za kralja, dovedite ovamo i smaknite ih preda mnom.’”

Mesijanski ulazak u Jeruzalem

(Mt 21:1-11; Mk 11:1-11; Iv 12:12-19)

28Pošto im je to ispričao, Isus krene dalje prema Jeruzalemu. 29Kad se približio mjestima Betfagi i Betaniji na Maslinskoj gori, pošalje naprijed dvojicu učenika. 30“Idite u ono selo pred vama”, reče im, “i čim uđete, vidjet ćete privezano magare koje još nitko nije jahao. Odvežite ga i dovedite ovamo. 31Upita li vas tko: ‘Što to radite?’ recite samo: ‘Treba Gospodinu.’”

32Oni odu i nađu magare kako im je rekao. 33Dok su ga odvezivali, neki ih ljudi upitaju: “Zašto odvezujete magare?”

34“Gospodinu treba”, odgovore oni. 35Dovedu magare Isusu i prebace preko njega svoje ogrtače te posjednu Isusa na njega.

36Mnoštvo je pred Isusom prostiralo svoje ogrtače po putu. 37Kad se već približio obronku Maslinske gore, mnoštvo njegovih sljedbenika počne na sav glas zahvaljivati Bogu za sva slavna djela što su ih vidjeli:

38“Blagoslovljen kralj

koji dolazi u ime Gospodnje!

Na nebu mir!

Slava Bogu na nebu!”19:38 Psalam 118:25-26 i Psalam 148:1.

39Ali neki farizeji među njime kazaše: “Učitelju, opomeni svoje učenike da to ne govore!”

40“Kažem vam,” reče im Isus, “ako oni ušute, klicat će kamenje na cesti!”

Isus tuži nad Jeruzalemom

41Kad se približio Jeruzalemu i ugledao grad, Isus zaplače nad njim: 42“Kako bih volio da si danas pronašao put mira! Ali sada je prekasno i mir je skriven od tebe. 43Doći će dani kada će neprijatelj zauzeti tvoje zidine, opkoliti te i pritisnuti sa svih strana. 44Sravnit će sa zemljom i tebe i tvoju djecu u tebi. Neće od tebe ostati ni kamena na kamenu jer nisi prepoznao da te je Bog pohodio.”

Isus izgoni trgovce iz Hrama

(Mt 21:12-17; Mk 11:15-19; Iv 2:13-22)

45Kad je ušao u Hram, Isus počne iz njega izgoniti trgovce. 46“U Svetome pismu piše: ‘Moj Hram treba biti molitveni dom’, a vi ste ga pretvorili u razbojničku špilju!”,19:46 Izaija 56:7; Jeremija 7:11. reče im.

47Nakon toga Isus je danomice poučavao u Hramu, a svećenički poglavari i pismoznanci smišljali su skupa s narodnim starješinama kako da ga ubiju, 48ali im to nije polazilo za rukom jer je narod upijao svaku njegovu riječ.