Luka 13 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 13:1-35

Tubu, La Sivyo Utaangamia

113:1 Mt 27:2Wakati huo huo, kulikuwa na watu waliomwambia Yesu habari za Wagalilaya ambao Pilato aliwaua, na damu ya hao watu akaichanganya na dhabihu yao waliyokuwa wanatoa. 213:2 Yn 9:2-3Yesu akawauliza, “Mnadhani kwamba hawa Wagalilaya ambao walikufa kifo cha namna hiyo walikuwa na dhambi kuwazidi Wagalilaya wengine wote? 313:3 Za 7:12La hasha! Ninyi nanyi msipotubu, mtaangamia vivyo hivyo. 413:4 Yn 9:7-11Au wale watu kumi na wanane waliokufa walipoangukiwa na mnara huko Siloamu: mnadhani wao walikuwa waovu kuliko watu wote waliokuwa wanaishi Yerusalemu? 513:5 Mt 3:2; Mdo 2:38Nawaambia, la hasha! Ninyi nanyi msipotubu, wote mtaangamia vivyo hivyo.”

Mfano Wa Mti Usiozaa Matunda

613:6 Isa 5:2; Mt 21:19Kisha Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu, akaja ili kutafuta tini kwenye mti huo, lakini hakupata hata moja. 713:7 Mt 3:10Hivyo akamwambia mtunza shamba: ‘Tazama, kwa muda wa miaka mitatu sasa nimekuwa nikija kutafuta matunda kwenye mtini huu, nami sikupata hata moja. Ukate! Kwa nini uendelee kuharibu ardhi?’

813:8 2Pet 3:9, 15“Yule mtunza shamba akamjibu, ‘Bwana, uache tena kwa mwaka mmoja zaidi, nami nitaupalilia na kuuwekea mbolea. 9Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vyema, la sivyo uukate.’ ”

Yesu Amponya Mwanamke Kilema Siku Ya Sabato

1013:10 Mt 4:23Basi Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo siku ya Sabato. 1113:11 Lk 13:16Wakati huo huo akaja mwanamke mmoja aliyekuwa na pepo mchafu, naye alikuwa amepinda mgongo kwa muda wa miaka kumi na minane, wala alikuwa hawezi kunyooka wima. 12Yesu alipomwona, akamwita, akamwambia, “Mwanamke, uwe huru, umepona ugonjwa wako.” 1313:13 Mt 5:23Yesu alipomwekea mikono yake, mara akasimama wima akaanza kumtukuza Mungu.

1413:14 Mt 12:2; Lk 14:3; Kut 20:9; Mk 5:22Lakini kiongozi wa sinagogi akakasirika kwa sababu Yesu alikuwa ameponya mtu siku ya Sabato. Akaambia ule umati wa watu, “Kuna siku sita ambazo watu wanapaswa kufanya kazi. Katika siku hizo, njooni mponywe, lakini si katika siku ya Sabato.”

1513:15 Lk 14:5Lakini Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Je, kila mmoja wenu hamfungulii ngʼombe wake au punda wake kutoka zizini akampeleka kumnywesha maji siku ya Sabato? 1613:16 Lk 3:8; 19:9; Mt 4:10Je, huyu mwanamke, ambaye ni binti wa Abrahamu, aliyeteswa na Shetani akiwa amemfunga kwa miaka yote hii kumi na minane, hakustahili kufunguliwa kutoka kifungo hicho siku ya Sabato?”

1713:17 Isa 66:5Aliposema haya, wapinzani wake wakaaibika, lakini watu wakafurahi kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyoyafanya.

Mfano Wa Punje Ya Haradali

(Mathayo 13:31-32; Marko 4:30-32)

1813:18 Mt 3:2; 13:24Kisha Yesu akauliza, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaufananisha na nini? 1913:19 Lk 17:6; Mt 13:32Umefanana na punje ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake. Nayo ikakua, ikawa mti nao ndege wa angani wakatengeneza viota vyao kwenye matawi yake.”

Mfano Wa Chachu

(Mathayo 13:33)

20Yesu akauliza tena, “Nitaufananisha Ufalme wa Mungu na nini? 2113:21 1Kor 5:6Unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”

Mlango Mwembamba

(Mathayo 7:13-14, 21-23)

2213:22 Lk 9:51Yesu akapita katika miji na vijiji, akifundisha wakati alisafiri kwenda Yerusalemu. 23Mtu mmoja akamuuliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?”

2413:24 Mt 7:13Yesu akawaambia, “Jitahidini sana kuingia kupitia mlango mwembamba, kwa maana nawaambia wengi watajaribu kuingia, lakini hawataweza. 2513:25 Mt 7:23; 25:10-12Wakati mwenye nyumba atakapoondoka na kufunga mlango, mtasimama nje mkibisha mlango na kusema, ‘Bwana! Tufungulie mlango!’

“Lakini yeye atawajibu, ‘Siwajui ninyi, wala mtokako.’

2613:26 Mt 7:22, 23“Ndipo mtamjibu, ‘Tulikula na kunywa pamoja nawe, tena ulifundisha katika mitaa yetu.’

2713:27 Mt 25:41“Lakini yeye atawajibu, ‘Siwajui ninyi, wala mtokako. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’

2813:28 Mt 8:11-12“Ndipo kutakuwako kilio na kusaga meno, mtakapowaona Abrahamu, Isaki, Yakobo na manabii wote wakiwa katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi mkiwa mmetupwa nje. 2913:29 Mal 1:11; Isa 49:12; 59:19; Za 107:3; Lk 14:15Watu watatoka mashariki na magharibi, kaskazini na kusini, nao wataketi kwenye sehemu walizoandaliwa karamuni katika Ufalme wa Mungu. 3013:30 Mt 19:30Tazama, kunao walio wa mwisho watakaokuwa wa kwanza, nao wa kwanza watakaokuwa wa mwisho.”

Yesu Aomboleza Kwa Ajili Ya Yerusalemu

(Mathayo 23:37-39)

3113:31 Mt 14:1Wakati huo huo baadhi ya Mafarisayo wakamwendea Yesu na kumwambia, “Ondoka hapa uende mahali pengine kwa maana Herode anataka kukuua.”

3213:32 Ebr 2:10Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie yule mbweha, ‘Ninafukuza pepo wachafu na kuponya wagonjwa leo na kesho, nami siku ya tatu nitaikamilisha kazi yangu.’ 3313:33 Mt 21:11Sina budi kuendelea na safari yangu leo, kesho na kesho kutwa: kwa maana haiwezekani nabii kufa mahali pengine isipokuwa Yerusalemu.

3413:34 Mt 23:37“Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka! 3513:35 Yer 12:17; 25:2; Za 118:26; Mt 21:9Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa. Ninawaambia, hamtaniona tena mpaka wakati ule mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana.’ ”

Knijga O Kristu

Luka 13:1-35

Isus poziva na obraćenje

1Tada Isusa obavijeste da je Pilat dao smaknuti neke Galilejce dok su prinosili žrtve u jeruzalemskome Hramu. 2“Mislite li da su ti Galilejci koji su nastradali bili veći grešnici od ostalih Galilejaca? 3Nipošto! Kažem vam, i vi ćete tako izginuti ako se ne obratite! 4Ili onih osamnaest na koje se srušila kula u Siloamu i ubila ih, zar mislite da su oni bili grešniji od svih stanovnika Jeruzalema? 5Nipošto. Kažem vam, svi ćete tako izginuti ako se ne obratite.”

Prispodoba o neplodnoj smokvi

6Ispriča im zatim prispodobu: “Imao neki čovjek u vinogradu zasađenu smokvu. Dolazio je vidjeti je li rodila, ali nije na njoj našao roda. 7Reče zato vinogradaru: ‘Već tri godine dolazim tražiti roda na ovoj smokvi, ali ga ne nalazim. Posijeci ju. Zašto da iscrpljuje zemlju!’

8Vinogradar odgovori: ‘Gospodaru, ostavi ju još ove godine, a ja ću ju okopati i pognojiti. 9Možda će nagodinu ipak roditi. Ako ne, posjeći ćeš ju.’”

Isus iscjeljuje u subotu

10Dok je Isus u subotu poučavao u sinagogi, 11bila je ondje žena koja je osamnaest godina bila zgrbljena i nije se mogla uspraviti. Bila je, naime, opsjednuta duhom. 12Kad ju Isus opazi, pozove ju i reče joj: “Ženo, oslobođena si od svoje bolesti!” 13te položi na nju ruke. Žena se smjesta uspravi i počne slaviti Boga.

14Ali nadstojnik sinagoge, srdit što ju je Isus izliječio u subotu, reče narodu: “Šest dana u tjednu treba raditi. U te se dane dakle dolazite liječiti, a ne subotom!”

15Isus mu odgovori: “Licemjeri! I vi radite subotom. Ne odveže li subotom svatko od vas svojega vola ili magarca od jasala i ne odvede li ga na vodu piti? 16Nije li onda trebalo, iako je subota, odriješiti ovu kćer Abrahamovu spona kojima ju je Sotona držao vezanu osamnaest godina?” 17Nato se njegovi neprijatelji posrame, a sav narod radovao se čudesima koja je Isus učinio.

Prispodoba o gorušičinu sjemenu

(Mt 13:31-32; Mk 4:30-32)

18“Kako da vam još opišem Božje kraljevstvo? S čime da ga usporedim?” reče Isus. 19“S njim je kao s gorušičinim sjemenom koje čovjek baci u svoj vrt. Ono izraste i razvije se u stablo te se ptice nebeske dolaze gnijezditi u njegovim granama.”

Prispodoba o kvascu

20Upita opet: “Kako da vam još opišem Božje kraljevstvo? 21Ono je poput kvasca koji žena umijesi u golemu količinu brašna,13:21 U grčkome: tri mjere (otprilike 20 kilograma). a on ipak sve ukvasi.”

Uska vrata

(Mt 7:13-14, 22-23; 8:11-12)

22Putujući u Jeruzalem, Isus je prolazio gradovima i selima i putem poučavao. 23Netko ga upita: “Gospodine, je li malo onih koji se spašavaju?”

24“Vrata neba su uska”, odgovori Isus. “Trudite se da uđete kroz njih jer će mnogi željeti ući, ali neće moći. 25Kad gospodar kuće zaključa vrata, bit će prekasno. Tada ćete stajati vani i kucati ištući: ‘Gospodine, otvori nam!’ ali on će odgovoriti: ‘Ne znam vas odakle ste.’

26Onda ćete početi govoriti: ‘Ali mi smo s tobom jeli i pili, poučavao si po našim trgovima!’

27A on će vam odgovoriti: ‘Kažem vam da vas ne poznajem. Odlazite od mene, svi zlotvori!’

28Bit će velikog plača i škrguta zubi kad ugledate Abrahama, Izaka i Jakova i sve proroke u kraljevstvu Božjemu, a vi ćete biti izbačeni. 29Tada će ljudi odasvud, s istoka i zapada, sa sjevera i juga, doći sjesti u Božjemu kraljevstvu. 30Oni koji su sada prvi tada će biti na zadnjemu mjestu, a oni koje ovdje smatraju zadnjima ondje će biti najveći.”13:30 U grčkome: Mnogi prvi bit će zadnji, a zadnji prvi.

Isus tuži nad Jeruzalemom

(Mt 23:37-39)

31Odmah zatim neki mu farizeji dođu reći: “Otiđi odavde jer te Herod hoće ubiti!”

32On im reče: “Idite i recite toj lisici da ću ja izgoniti zloduhe i iscjeljivati danas i sutra, a trećega ću dana završiti što imam. 33Danas, sutra i prekosutra valja mi nastaviti put jer ne priliči da prorok bude ubijen izvan Jeruzalema.

34Jeruzaleme, Jeruzaleme, koji ubijaš proroke i kamenuješ Božje poslanike! Koliko sam puta htio okupiti tvoju djecu kao što kvočka skuplja piliće pod krila, ali niste htjeli! 35A sada će ti, eto, kuća biti napuštena. I kažem vam, nećete me više vidjeti sve dok ne uzviknete: ‘Blagoslovljen koji dolazi u ime Gospodnje!’”13:35 Vidjetii Psalam 118:26.