Luka 12 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 12:1-59

Maonyo Dhidi Ya Unafiki

(Mathayo 10:26-33)

112:1 Mt 16:6-12; Mk 8:15Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao. 212:2 Mk 4:12; Lk 8:1712:2 Mt 10:26-33Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana. 3Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.

412:4 Yn 15:14-15“Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi. 512:5 Ebr 10:31Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! 6Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao. 712:7 Mt 10:30; 12:12Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.

812:8 Lk 15:10“Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu. 912:9 Mk 8:38; 2Tim 2:12Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu. 1012:10 Mt 8:20; 12:31-32; Mk 3:28-29Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.

1112:11 Mt 10:17-19; Mk 13:11“Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema. 1212:12 Kut 4:12; Mt 10:20Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”

Mfano Wa Tajiri Mpumbavu

13Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”

1412:14 Mdo 7:27Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?” 1512:15 Ay 31:24; Za 62:10Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”

16Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana. 17Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’

18“Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu. 1912:19 Mhu 11:9; 1Kor 15:32; Yak 5:5Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.” ’

2012:20 Yer 17:11; Lk 11:40; Ay 27:8; Za 39:6; 49:19“Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’

2112:21 Mt 6:20; Lk 12:33; 1Tim 6:18, 19; Yak 2:5“Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”

Msiwe Na Wasiwasi

(Mathayo 6:25-34)

2212:22 Mt 6:2512:22 Mt 6:25-33Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini. 23Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi. 2412:24 Ay 38:41; Za 147:9Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege! 25Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake? 26Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?

2712:27 1Fal 10:4-7“Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua. 2812:28 Mt 6:30Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba! 29Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya. 3012:30 Lk 6:36; Mt 6:8Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote. 3112:31 Mt 3:2; 19:29Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.

Utajiri Wa Mbinguni

(Mathayo 6:19-21)

3212:32 Mt 14:27; 25:34“Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme. 3312:33 Mt 19:21; Mdo 2:45; Mt 6:20; Yak 5:2Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu. 3412:34 Mt 6:21Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.

Kukesha

3512:35 Efe 6:14; 1Pet 1:13; Mt 25:1“Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka, 3612:36 Mt 25:1-13kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara. 3712:37 Mt 24:42-46; 25:13; 20:28Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia. 38Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko. 3912:39 1The 5:2; 2Pet 3:10Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa. 4012:40 Mk 13:33; Lk 21:36Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”

Mtumishi Mwaminifu Na Yule Asiye Mwaminifu

(Mathayo 24:45-51)

41Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”

4212:42 Lk 7:13Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa? 43Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo. 4412:44 Mt 24:47Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote. 4512:45 Mt 24:48Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa. 4612:46 Lk 12:40Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.

4712:47 Kum 25:2“Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi. 4812:48 Law 5:17; Hes 15:27-30Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.

Yesu Kuleta Mafarakano

(Mathayo 10:34-36)

4912:49 Lk 12:51“Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa! 5012:50 Mk 10:38; Yn 19:30Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike! 5112:51 Mt 10:34; Lk 12:49; Mik 7:6; Yn 7:46; 9:16Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano. 5212:52 Mt 10:35Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu. 5312:53 Mik 7:6; Mt 10:21Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”

Kutambua Majira

(Mathayo 16:2-3)

5412:54 Mt 16:2-3Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha. 55Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo. 5612:56 Mt 16:3Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?

57“Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki? 5812:58 Mt 5:25Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani. 5912:59 Mt 5:26; Mk 12:42Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”

New Russian Translation

Луки 12:1-59

Иисус осуждает лицемерие

(Мат. 10:26-27)

1Тем временем собрались огромные толпы, и люди теснили друг друга. Иисус начал говорить, обращаясь сначала к Своим ученикам:

– Берегитесь фарисейской закваски, то есть лицемерия. 2Нет ничего скрытого, что не открылось бы, и нет ничего тайного, что не стало бы известным. 3Поэтому то, что вы говорите в темноте, будет услышано при свете дня, и что вы прошептали на ухо во внутренней комнате, будет провозглашено с крыш.

Имейте страх только перед Богом

(Мат. 10:28-33)

4Я говорю вам, Моим друзьям: не бойтесь тех, кто убивает тело и ничего больше сделать не может. 5Я скажу вам, Кого бояться: бойтесь Того, Кто, убив, имеет власть ввергнуть в ад12:5 Греч.: «в геену».. Да, говорю вам, Его бойтесь. 6Не продают ли пять воробьев всего за две мелкие монеты?12:6 Букв.: «за два ассария». Однако ни один из них не забыт Богом. 7А у вас даже и волосы на голове все сосчитаны! Не бойтесь – вы дороже множества воробьев!

Не стыдитесь Иисуса

8– Говорю вам: каждого, кто открыто признает Меня перед людьми, того и Сын Человеческий признает перед Божьими ангелами, 9а кто отречется от Меня перед людьми, от того и Я отрекусь перед Божьими ангелами. 10Всякий, кто скажет что-либо против Сына Человеческого, будет прощен, но тот, кто кощунствует над Святым Духом, не будет прощен.

11Когда вас приведут на суд в синагоги, к правителям и власть имущим, не беспокойтесь о том, как вам защитить себя или что вам говорить, 12потому что Святой Дух в тот самый час научит вас, что вам говорить.

Притча о безумном богаче

13Кто-то в толпе сказал Иисусу:

– Учитель, скажи моему брату, чтобы он разделил со мной наследство.

14Иисус ответил:

– Друг, кто Меня назначил судьей или посредником между вами?

15И Он сказал им:

– Смотрите, берегитесь жадности. Как бы ни был богат человек, его жизнь от этого не зависит.

16И Он рассказал им притчу:

– Земля одного богатого человека принесла ему хороший урожай. 17«Что мне делать? Мне негде хранить весь собранный урожай, – подумал он. 18– Вот что я сделаю, – решил он тогда, – я снесу мои хранилища и построю большие, в них будет достаточно места для моего зерна и другого имущества. 19Тогда я смогу сказать себе: теперь у тебя полно добра на много лет. Отдыхай, ешь, пей, веселись». 20Но Бог сказал ему: «Глупец! Сегодня же ночью твою жизнь возьмут у тебя. Кому достанется все, что ты приготовил?» 21Так будет с каждым, кто копит богатство для себя, но не приобретает богатства для Бога.

Иисус говорит о беспокойстве

(Мат. 6:25-34)

22Затем Иисус сказал Своим ученикам:

– Поэтому Я говорю вам: не тревожьтесь о своей жизни, что вам есть, или о своем теле, во что вам одеться. 23Ведь жизнь важнее пищи, и тело важнее одежды. 24Посмотрите на воронов, они не сеют и не жнут, у них нет ни хранилищ, ни амбаров, однако Бог питает их. Насколько же вы ценнее этих птиц! 25И кто из вас, беспокоясь, может продлить себе жизнь хотя бы на час?12:25 Или.: «прибавить себе роста хотя бы на один локоть?» 26Если вы не можете сделать даже этого, то зачем вам тревожиться об остальном?

27Подумайте о том, как растут лилии. Они не трудятся и не прядут, но говорю вам, что даже Соломон во всем своем величии не одевался так, как любая из них. 28Но если Бог так одевает траву на поле, которая сегодня есть, а завтра будет брошена в печь, то не оденет ли Он и вас, маловеры? 29Не беспокойтесь о том, что вам есть или что пить, не тревожьтесь об этом. 30Ведь все язычники этого мира только об этом и думают, но ваш Отец знает, что вы нуждаетесь в этом. 31Ищите лучше Его Царства, и это тоже будет дано вам.

32Не бойся, малое стадо, ведь вашему Отцу было угодно дать вам Царство! 33Продавайте ваше имущество и давайте милостыню. Приобретайте себе такие кошельки, которые не изнашиваются, сокровища на небесах, где ни вор к ним не подберется, ни моль их не съест. 34Ведь где ваше богатство, там будет и ваше сердце.

Притча о верных слугах

(Мат. 25:1-13; Мат. 24:43-51; Мк. 13:33-37)

35Будьте всегда наготове: одежды подпоясаны, а светильники горящие, 36как у тех слуг, что ждут возвращения своего хозяина со свадебного пира. Когда хозяин придет и постучит, они смогут сразу открыть ему. 37Блаженны те слуги, которых хозяин, возвратившись, найдет бодрствующими. Говорю вам истину, он тогда сам подпояшется, как слуга, пригласит их к столу и будет прислуживать им. 38Блаженны те слуги, которых хозяин застанет готовыми, даже если он придет среди ночи или перед рассветом. 39Знайте, что если бы хозяин дома знал, в котором часу придет вор, то он не позволил бы ему проникнуть в свой дом. 40Вы тоже должны быть готовы, потому что Сын Человеческий придет в час, когда вы Его не ждете.

41Петр спросил:

– Господи, Ты говоришь эту притчу только нам или всем?

42Господь ответил:

– Кто тогда окажется верным и разумным управляющим, которого хозяин поставил над другими слугами, чтобы вовремя раздавать им пищу? 43Блажен тот слуга, которого хозяин, когда вернется, найдет поступающим так. 44Говорю вам истину: он доверит ему все свое имение. 45Но если тот слуга решит: «Мой хозяин придет еще не скоро» – и станет избивать слуг и служанок, есть, пить и пьянствовать, 46то придет его хозяин в тот день, когда он не ожидает, и в тот час, когда он не знает. Он рассечет его надвое и определит ему одну участь с неверными.

47Тот слуга, который знал волю своего хозяина и не приготовился или не сделал того, что хотел хозяин, будет сильно бит, 48а тот, кто делает достойное наказания по незнанию, будет бит меньше. Кому было много дано, с того много и потребуют, и кому было много доверено, с того много и спросится.

Иисус предупреждает о грядущих разделениях

(Мат. 10:34-35)

49Я пришел принести огонь на землю, и как Я хочу, чтобы он уже разгорелся! 50Но Мне еще предстоит пройти крещение, и как Я томлюсь, пока это не совершится! 51Вы думаете, Я пришел, чтобы принести на землю мир? Нет, говорю вам, не мир, а разделение. 52Семья из пяти человек разделится: трое против двоих, и двое против троих. 53Отец будет против сына и сын против отца, мать против дочери и дочь против матери, свекровь против невестки и невестка против свекрови12:53 См. Мих. 7:6..

Иисус говорит о приметах времени

(Мат. 16:2-3; 5:25-26)

54Иисус опять обратился к народу:

– Когда вы видите облако на западе, вы сразу говорите, что будет дождь, и, действительно, идет дождь. 55И когда дует южный ветер, вы говорите: будет жарко, и так и бывает. 56Лицемеры! Вы знаете, что означают приметы земли и неба, так почему же вы не знаете, какое настало время? 57Почему вы сами не рассудите, в чем истина? 58Когда ты идешь со своим обвинителем в суд, постарайся примириться с ним еще по пути, иначе он притащит тебя к судье, а судья отдаст тебя стражнику, и тот бросит тебя в темницу. 59Говорю тебе, что ты не выйдешь оттуда, пока не выплатишь все до самого последнего гроша.