Luka 12 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 12:1-59

Maonyo Dhidi Ya Unafiki

(Mathayo 10:26-33)

112:1 Mt 16:6-12; Mk 8:15Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao. 212:2 Mk 4:12; Lk 8:1712:2 Mt 10:26-33Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana. 3Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.

412:4 Yn 15:14-15“Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi. 512:5 Ebr 10:31Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! 6Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao. 712:7 Mt 10:30; 12:12Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.

812:8 Lk 15:10“Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu. 912:9 Mk 8:38; 2Tim 2:12Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu. 1012:10 Mt 8:20; 12:31-32; Mk 3:28-29Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.

1112:11 Mt 10:17-19; Mk 13:11“Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema. 1212:12 Kut 4:12; Mt 10:20Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”

Mfano Wa Tajiri Mpumbavu

13Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”

1412:14 Mdo 7:27Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?” 1512:15 Ay 31:24; Za 62:10Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”

16Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana. 17Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’

18“Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu. 1912:19 Mhu 11:9; 1Kor 15:32; Yak 5:5Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.” ’

2012:20 Yer 17:11; Lk 11:40; Ay 27:8; Za 39:6; 49:19“Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’

2112:21 Mt 6:20; Lk 12:33; 1Tim 6:18, 19; Yak 2:5“Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”

Msiwe Na Wasiwasi

(Mathayo 6:25-34)

2212:22 Mt 6:2512:22 Mt 6:25-33Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini. 23Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi. 2412:24 Ay 38:41; Za 147:9Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege! 25Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake? 26Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?

2712:27 1Fal 10:4-7“Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua. 2812:28 Mt 6:30Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba! 29Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya. 3012:30 Lk 6:36; Mt 6:8Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote. 3112:31 Mt 3:2; 19:29Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.

Utajiri Wa Mbinguni

(Mathayo 6:19-21)

3212:32 Mt 14:27; 25:34“Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme. 3312:33 Mt 19:21; Mdo 2:45; Mt 6:20; Yak 5:2Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu. 3412:34 Mt 6:21Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.

Kukesha

3512:35 Efe 6:14; 1Pet 1:13; Mt 25:1“Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka, 3612:36 Mt 25:1-13kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara. 3712:37 Mt 24:42-46; 25:13; 20:28Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia. 38Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko. 3912:39 1The 5:2; 2Pet 3:10Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa. 4012:40 Mk 13:33; Lk 21:36Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”

Mtumishi Mwaminifu Na Yule Asiye Mwaminifu

(Mathayo 24:45-51)

41Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”

4212:42 Lk 7:13Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa? 43Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo. 4412:44 Mt 24:47Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote. 4512:45 Mt 24:48Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa. 4612:46 Lk 12:40Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.

4712:47 Kum 25:2“Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi. 4812:48 Law 5:17; Hes 15:27-30Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.

Yesu Kuleta Mafarakano

(Mathayo 10:34-36)

4912:49 Lk 12:51“Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa! 5012:50 Mk 10:38; Yn 19:30Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike! 5112:51 Mt 10:34; Lk 12:49; Mik 7:6; Yn 7:46; 9:16Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano. 5212:52 Mt 10:35Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu. 5312:53 Mik 7:6; Mt 10:21Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”

Kutambua Majira

(Mathayo 16:2-3)

5412:54 Mt 16:2-3Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha. 55Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo. 5612:56 Mt 16:3Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?

57“Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki? 5812:58 Mt 5:25Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani. 5912:59 Mt 5:26; Mk 12:42Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”

New International Reader’s Version

Luke 12:1-59

Jesus Gives Words of Warning and Hope

1During that time a crowd of many thousands had gathered. There were so many people that they were stepping on one another. Jesus spoke first to his disciples. “Be on your guard against the yeast of the Pharisees,” he said. “They just pretend to be godly. 2Everything that is secret will be brought out into the open. Everything that is hidden will be uncovered. 3What you have said in the dark will be heard in the daylight. What you have whispered to someone behind closed doors will be shouted from the rooftops.

4“My friends, listen to me. Don’t be afraid of those who kill the body but can’t do any more than that. 5I will show you whom you should be afraid of. Be afraid of the one who has the authority to throw you into hell after you have been killed. Yes, I tell you, be afraid of him. 6Aren’t five sparrows sold for two pennies? But God does not forget even one of them. 7In fact, he even counts every hair on your head! So don’t be afraid. You are worth more than many sparrows.

8“What about someone who says in front of others that he knows me? I tell you, the Son of Man will say in front of God’s angels that he knows that person. 9But what about someone who says in front of others that he doesn’t know me? I, the Son of Man, will say in front of God’s angels that I don’t know him. 10Everyone who speaks a word against the Son of Man will be forgiven. But anyone who speaks evil things against the Holy Spirit will not be forgiven.

11“You will be brought before synagogues, rulers and authorities. But do not worry about how to stand up for yourselves or what to say. 12The Holy Spirit will teach you at that time what you should say.”

The Story of the Rich Fool

13Someone in the crowd spoke to Jesus. “Teacher,” he said, “tell my brother to divide the family property with me.”

14Jesus replied, “Friend, who made me a judge or umpire between you?” 15Then he said to them, “Watch out! Be on your guard against wanting to have more and more things. Life is not made up of how much a person has.”

16Then Jesus told them a story. He said, “A certain rich man’s land produced a very large crop. 17He thought to himself, ‘What should I do? I don’t have any place to store my crops.’

18“Then he said, ‘This is what I’ll do. I will tear down my barns and build bigger ones. I will store my extra grain in them. 19I’ll say to myself, “You have plenty of grain stored away for many years. Take life easy. Eat, drink and have a good time.” ’

20“But God said to him, ‘You foolish man! Tonight I will take your life away from you. Then who will get what you have prepared for yourself?’

21“That is how it will be for whoever stores things away for themselves but is not rich in the sight of God.”

Do Not Worry

22Then Jesus spoke to his disciples. He said, “I tell you, do not worry. Don’t worry about your life and what you will eat. And don’t worry about your body and what you will wear. 23There is more to life than eating. There are more important things for the body than clothes. 24Think about the ravens. They don’t plant or gather crops. They don’t have any barns at all. But God feeds them. You are worth much more than birds! 25Can you add even one hour to your life by worrying? 26You can’t do that very little thing. So why worry about the rest?

27“Think about how the wild flowers grow. They don’t work or make clothing. But here is what I tell you. Not even Solomon in his royal robes was dressed like one of those flowers. 28If that is how God dresses the wild grass, how much better will he dress you! After all, the grass is here only today. Tomorrow it is thrown into the fire. Your faith is so small! 29Don’t spend time thinking about what you will eat or drink. Don’t worry about it. 30People who are ungodly run after all those things. Your Father knows that you need them. 31But put God’s kingdom first. Then those other things will also be given to you.

32“Little flock, do not be afraid. Your Father has been pleased to give you the kingdom. 33Sell what you own. Give to those who are poor. Provide purses for yourselves that will not wear out. Store up riches in heaven that will never be used up. There, no thief can come near it. There, no moth can destroy it. 34Your heart will be where your riches are.

Be Ready

35“Be dressed and ready to serve. Keep your lamps burning. 36Be like servants waiting for their master to return from a wedding dinner. When he comes and knocks, they can open the door for him at once. 37It will be good for those servants whose master finds them ready when he comes. What I’m about to tell you is true. The master will then dress himself so he can serve them. He will have them take their places at the table. And he will come and wait on them. 38It will be good for those servants whose master finds them ready. It will even be good if he comes in the middle of the night or toward morning. 39But here is what you must understand. Suppose the owner of the house knew at what hour the robber was coming. He would not have let his house be broken into. 40You also must be ready. The Son of Man will come at an hour when you don’t expect him.”

41Peter asked, “Lord, are you telling this story to us, or to everyone?”

42The Lord answered, “Suppose a master puts one of his servants in charge of his other servants. The servant’s job is to give them the food they are to receive at the right time. The master wants a faithful and wise manager for this. 43It will be good for the servant if the master finds him doing his job when the master returns. 44What I’m about to tell you is true. The master will put that servant in charge of everything he owns. 45But suppose the servant says to himself, ‘My master is taking a long time to come back.’ Suppose that servant begins to beat the other servants, both men and women. Suppose he feeds himself. And suppose he drinks until he gets drunk. 46The master of that servant will come back on a day the servant doesn’t expect him. The master will return at an hour the servant doesn’t know. Then the master will cut him to pieces. He will send the servant to the place where unbelievers go.

47“Suppose a servant knows the master’s wishes. But the servant doesn’t get ready and doesn’t do what the master wants. Then that servant will receive a heavy beating. 48But suppose the servant does not know his master’s wishes. And suppose the servant does things for which he should be punished. He will receive a lighter beating. Much will be required of everyone who has been given much. Even more will be asked of the person who is supposed to take care of much.

Jesus Will Separate People From One Another

49“I have come to bring fire on the earth. How I wish the fire had already started! 50But I have a baptism of suffering to go through. And I must go through it. 51Do you think I came to bring peace on earth? No, I tell you. I have come to separate people. 52From now on there will be five members in a family, each one against the other. There will be three against two and two against three. 53They will be separated. Father will turn against son and son against father. Mother will turn against daughter and daughter against mother. Mother-in-law will turn against daughter-in-law and daughter-in-law against mother-in-law.”

Understanding the Meaning of What Is Happening

54Jesus spoke to the crowd. He said, “You see a cloud rising in the west. Right away you say, ‘It’s going to rain.’ And it does. 55The south wind blows. So you say, ‘It’s going to be hot.’ And it is. 56You pretenders! You know how to understand the appearance of the earth and the sky. Why can’t you understand the meaning of what is happening right now?

57“Why don’t you judge for yourselves what is right? 58Suppose someone has a claim against you, and you are on your way to court. Try hard to settle the matter on the way. If you don’t, that person may drag you off to the judge. The judge may turn you over to the officer. And the officer may throw you into prison. 59I tell you, you will not get out until you have paid the very last penny!”