Luka 11 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 11:1-54

Yesu Afundisha Wanafunzi Wake Kuomba

(Mathayo 6:9-13; 7:7-11)

111:1 Lk 3:21; Yn 13:13Siku moja, Yesu alikuwa mahali fulani akiomba. Alipomaliza kuomba, mmoja wa wanafunzi wake akamwambia, “Bwana, tufundishe kuomba, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.”

211:2 Mt 3:211:2 Mt 6:9-13Akawaambia, “Mnapoomba, semeni:

“ ‘Baba yetu (uliye mbinguni),

jina lako litukuzwe,

ufalme wako uje.

(Mapenzi yako yafanyike

hapa duniani kama huko mbinguni.)

3Utupatie kila siku riziki yetu.

411:4 Mt 18:35; Mk 11:25; Mt 26:41; Yak 1:13Utusamehe dhambi zetu,

kwa kuwa na sisi huwasamehe wote wanaotukosea.

Wala usitutie majaribuni

(bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu).’ ”

5Kisha akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu mwenye rafiki yake, naye akamwendea usiku wa manane na kumwambia, ‘Rafiki, nikopeshe mikate mitatu. 6Kwa sababu rafiki yangu amekuja kutoka safarini, nami sina kitu cha kumpa.’

711:7 Mt 26:10“Kisha yule aliyeko ndani amjibu, ‘Usinisumbue. Mlango umefungwa, nami na watoto wangu tumelala. Siwezi kuamka nikupe chochote.’ 811:8 Lk 18:1-6Nawaambia, ingawa huyo mtu hataamka na kumpa hiyo mikate kwa sababu ni rafiki yake, lakini kwa sababu ya kuendelea kwake kuomba, ataamka na kumpa kiasi anachohitaji.

911:9 Mt 7:711:9 Mt 7:7-11“Kwa hiyo nawaambia: Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango. 10Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.

11“Je, kuna yeyote miongoni mwenu ambaye mtoto wake akimwomba samaki, atampa nyoka badala yake? 12Au mtoto akimwomba yai atampa nge? 13Basi ikiwa ninyi mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa Roho Mtakatifu wale wamwombao!”

Yesu Na Beelzebuli

(Mathayo 12:22-30; Marko 3:20-27)

1411:14 Mt 9:32-3311:14 Mt 12:22Basi Yesu alikuwa anamtoa pepo mchafu kutoka kwa mtu aliyekuwa bubu. Yule pepo mchafu alipomtoka yule mtu aliyekuwa bubu, akaanza kuongea, nao umati wa watu ukashangaa. 1511:15 Mk 3:22; Mt 9:34Lakini wengine wakasema, “Anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli,11:15 Beelzebubu au Beelzebuli; ni mkuu wa pepo wachafu; pia 18, 19. yule mkuu wa pepo wachafu wote.” 1611:16 Mt 12:38Wengine ili kumjaribu wakataka awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.

1711:17 Mt 9:34Yesu akajua mawazo yao, naye akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Nayo nyumba iliyogawanyika dhidi yake yenyewe itaanguka. 1811:18 Mt 4:10Kama Shetani amegawanyika mwenyewe, ufalme wake utasimamaje? Nawaambia haya kwa sababu ninyi mnadai ya kuwa mimi ninatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli. 1911:19 Mk 11:24; Yn 15:7; Yak 1:6; Yn 3:32; Mt 7:7Kama mimi natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, wafuasi wenu nao je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu. 2011:20 Kut 8:19; Mt 3:2Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa kidole cha Mungu, basi Ufalme wa Mungu umewajia.

2111:21 Mt 12:29; Mk 3:17“Mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha anapoilinda nyumba yake, mali yake iko salama. 2211:22 Isa 53:12; Kol 2:15Lakini mtu mwenye nguvu zaidi kumliko akimshambulia na kumshinda, yeye humnyangʼanya silaha zake zote alizozitegemea, na kuchukua nyara.

2311:23 Mt 12:30; Mk 9:40“Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.

Kurudi Kwa Pepo Mchafu

(Mathayo 12:43-45)

2411:24 Mt 12:43“Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati. Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ 25Naye arudipo na kuikuta ile nyumba imefagiliwa na kupangwa vizuri, 2611:26 2Pet 2:20ndipo huenda na kuchukua pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza.”

2711:27 Lk 23:29Ikawa Yesu alipokuwa akisema hayo, mwanamke mmoja katikati ya ule umati wa watu akapaza sauti akasema, “Limebarikiwa tumbo lililokuzaa na matiti uliyonyonya!”

2811:28 Ebr 4:12; Mit 8:32; Yn 14:21Yesu akajibu, “Wamebarikiwa zaidi wale wanaolisikia neno la Mungu na kulitii.”

Ishara Ya Yona

(Mathayo 12:38-42)

2911:29 Mt 12:38; Yn 1:17; Mt 16:4Umati wa watu ulipokuwa unazidi kuongezeka, Yesu akaendelea kusema, “Hiki ni kizazi kiovu. Kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ya Yona. 3011:30 Yn 1:17; 2:10Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ishara kwa watu wa Ninawi, ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa ishara kwa kizazi hiki. 3111:31 1Fal 10:1; 2Nya 9:1Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kuwahukumu watu wa kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni. 3211:32 Yon 3:5Siku ya hukumu, watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.

Taa Ya Mwili

(Mathayo 5:15; 6:22-23)

3311:33 Mt 5:15; Mk 4:21“Hakuna mtu yeyote awashaye taa na kuiweka mahali palipofichika au kuifunikia chini ya bakuli. Badala yake huiweka juu ya kinara chake, ili watu wote wanaoingia waone nuru. 3411:34 Mt 6:22; 2711:34 Mt 6:22; 23Jicho lako ni taa ya mwili wako. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote pia umejaa nuru. Lakini kama jicho ni bovu, mwili wako wote pia umejaa giza. 35Kwa hiyo, hakikisha kwamba nuru iliyoko ndani yako isiwe giza. 36Basi ikiwa mwili wako wote umejaa nuru, bila sehemu yake yoyote kuwa gizani, basi utakuwa na nuru kama vile taa ikuangazavyo kwa nuru yake.”

Yesu Awashutumu Mafarisayo Na Wanasheria

(Mathayo 23:1-36; Marko 12:38-40)

3711:37 Lk 7:36; 14:1Yesu alipomaliza kuzungumza, Farisayo mmoja alimwalika nyumbani mwake kwa chakula. Yesu akaingia na kuketi katika sehemu yake mezani. 3811:38 Mk 7:3-4Yule Farisayo akashangaa kwamba Yesu hakunawa kwanza kabla ya kula.

3911:39 Lk 7:13; Mt 23:25-26; Mk 7:20-23Ndipo Bwana akamwambia, “Sasa, enyi Mafarisayo, mnasafisha kikombe na sahani kwa nje, lakini ndani mmejaa unyangʼanyi na uovu. 4011:40 Lk 12:20; 1Kor 15:36Enyi wapumbavu! Hamjui kuwa yeye aliyetengeneza nje ndiye alitengeneza na ndani pia? 4111:41 Lk 12:33; Mdo 10:15Basi toeni sadaka ya vile mlivyo navyo, na tazama, vitu vyote vitakuwa safi kwenu.

4211:42 Lk 18:12; Kum 6:5; Mik 6:8; Mt 23:23“Lakini ole wenu, Mafarisayo, kwa maana mnampa Mungu zaka za mnanaa, mchicha na kila aina ya mboga, lakini mnapuuza haki na upendo wa Mungu. Iliwapasa kufanya haya ya pili bila kupuuza hayo ya kwanza.

4311:43 Mt 23:6-7; Mk 12:38-39“Ole wenu Mafarisayo, kwa sababu ninyi mnapenda kukalia viti vya mbele katika masinagogi, na kusalimiwa kwa heshima masokoni.

4411:44 Mt 23:27-35“Ole wenu, kwa sababu ninyi ni kama makaburi yasiyokuwa na alama, ambayo watu huyakanyaga pasipo kujua.”

4511:45 Mt 22:35Mtaalamu mmoja wa sheria akamjibu, akasema, “Mwalimu, unaposema mambo haya, unatutukana na sisi pia.”

4611:46 Mt 23:4Yesu akamjibu, “Nanyi wataalamu wa sheria, ole wenu, kwa sababu mnawatwika watu mizigo mizito ambayo hawawezi kubeba, wala ninyi wenyewe hamwinui hata kidole kimoja kuwasaidia.

4711:47 Mt 23:29“Ole wenu, kwa sababu ninyi mnajenga makaburi ya manabii waliouawa na baba zenu. 4811:48 Mt 23:29-32; Mdo 7:51-53Hivyo ninyi mwashuhudia na mnathibitisha kile baba zenu walichofanya. Wao waliwaua manabii, nanyi mnawajengea makaburi. 4911:49 1Kor 1:24; Kol 2:3Kwa sababu ya jambo hili, Mungu katika hekima yake alisema, ‘Tazama, nitatuma kwao manabii na mitume, nao watawaua baadhi yao na wengine watawatesa.’ 50Kwa hiyo kizazi hiki kitawajibika kwa ajili ya damu ya manabii iliyomwagwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, 5111:51 Mwa 4:8; 2Nya 24:20-21; Mt 23:35-36tangu damu ya Abeli mpaka damu ya Zekaria, aliyeuawa kati ya madhabahu na mahali patakatifu. Naam, nawaambia, kizazi hiki kitawajibika kwa haya yote.

5211:52 Mt 23:13“Ole wenu ninyi wataalamu wa sheria, kwa sababu mmeuondoa ufunguo wa maarifa. Ninyi wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wanaingia mkawazuia.”

53Yesu alipoondoka huko, walimu wa sheria na Mafarisayo wakaanza kumpinga vikali na kumsonga kwa maswali, 5411:54 Mt 12:10; Mk 12:13wakivizia kumkamata kwa kitu atakachosema ili wamshtaki.

New International Reader’s Version

Luke 11:1-54

Jesus Teaches About Prayer

1One day Jesus was praying in a certain place. When he finished, one of his disciples spoke to him. “Lord,” he said, “teach us to pray, just as John taught his disciples.”

2Jesus said to them, “When you pray, this is what you should say.

“ ‘Father,

may your name be honored.

May your kingdom come.

3Give us each day our daily bread.

4Forgive us our sins,

as we also forgive everyone who sins against us.

Keep us from falling into sin when we are tempted.’ ”

5Then Jesus said to them, “Suppose you have a friend. You go to him at midnight and say, ‘Friend, lend me three loaves of bread. 6A friend of mine on a journey has come to stay with me. I have no food to give him.’ 7And suppose the one inside answers, ‘Don’t bother me. The door is already locked. My children and I are in bed. I can’t get up and give you anything.’ 8I tell you, that person will not get up. And he won’t give you bread just because he is your friend. But because you keep bothering him, he will surely get up. He will give you as much as you need.

9“So here is what I say to you. Ask, and it will be given to you. Search, and you will find. Knock, and the door will be opened to you. 10Everyone who asks will receive. The one who searches will find. And the door will be opened to the one who knocks.

11“Fathers, suppose your son asks for a fish. Which of you will give him a snake instead? 12Or suppose he asks for an egg. Which of you will give him a scorpion? 13Even though you are evil, you know how to give good gifts to your children. How much more will your Father who is in heaven give the Holy Spirit to those who ask him!”

Jesus and Beelzebul

14Jesus was driving out a demon. The man who had the demon could not speak. When the demon left, the man began to speak. The crowd was amazed. 15But some of them said, “Jesus is driving out demons by the power of Beelzebul, the prince of demons.” 16Others tested Jesus by asking for a sign from heaven.

17Jesus knew what they were thinking. So he said to them, “Any kingdom that fights against itself will be destroyed. A family that is divided against itself will fall. 18If Satan fights against himself, how can his kingdom stand? I say this because of what you claim. You say I drive out demons by the power of Beelzebul. 19Suppose I do drive out demons with Beelzebul’s help. With whose help do your followers drive them out? So then, they will be your judges. 20But suppose I drive out demons with the help of God’s powerful finger. Then God’s kingdom has come upon you.

21“When a strong man is completely armed and guards his house, what he owns is safe. 22But when someone stronger attacks, he is overpowered. The attacker takes away the armor the man had trusted in. Then he divides up what he has stolen.

23“Whoever is not with me is against me. And whoever does not gather with me scatters.

24“What happens when an evil spirit comes out of a person? It goes through dry areas looking for a place to rest. But it doesn’t find it. Then it says, ‘I will return to the house I left.’ 25When it arrives there, it finds the house swept clean and put in order. 26Then the evil spirit goes and takes seven other spirits more evil than itself. They go in and live there. That person is worse off than before.”

27As Jesus was saying these things, a woman in the crowd called out. She shouted, “Blessed is the mother who gave you birth and nursed you.”

28He replied, “Instead, blessed are those who hear God’s word and obey it.”

The Sign of Jonah

29As the crowds grew larger, Jesus spoke to them. “The people of today are evil,” he said. “They ask for a sign from God. But none will be given except the sign of Jonah. 30He was a sign from God to the people of Nineveh. In the same way, the Son of Man will be a sign from God to the people of today. 31The Queen of the South will stand up on judgment day with the people now living. And she will prove that they are guilty. She came from very far away to listen to Solomon’s wisdom. And now something more important than Solomon is here. 32The men of Nineveh will stand up on judgment day with the people now living. And the Ninevites will prove that those people are guilty. The men of Nineveh turned away from their sins when Jonah preached to them. And now something more important than Jonah is here.

The Eye Is the Lamp of the Body

33“No one lights a lamp and hides it. No one puts it under a bowl. Instead, they put a lamp on its stand. Then those who come in can see the light. 34Your eye is like a lamp for your body. Suppose your eyes are healthy. Then your whole body also is full of light. But suppose your eyes can’t see well. Then your body also is full of darkness. 35So make sure that the light inside you is not darkness. 36Suppose your whole body is full of light. And suppose no part of it is dark. Then your body will be full of light. It will be just as when a lamp shines its light on you.”

Six Warnings

37Jesus finished speaking. Then a Pharisee invited him to eat with him. So Jesus went in and took his place at the table. 38But the Pharisee was surprised. He noticed that Jesus did not wash before the meal.

39Then the Lord spoke to him. “You Pharisees clean the outside of the cup and dish,” he said. “But inside you are full of greed and evil. 40You foolish people! Didn’t the one who made the outside make the inside also? 41Give freely to poor people to show what is inside you. Then everything will be clean for you.

42“How terrible it will be for you Pharisees! You give God a tenth of your garden plants, such as mint and rue. But you have forgotten to be fair and to love God. You should have practiced the last things without failing to do the first.

43“How terrible for you Pharisees! You love the most important seats in the synagogues. You love having people greet you with respect in the market.

44“How terrible for you! You are like graves that are not marked. People walk over them without knowing it.”

45An authority on the law spoke to Jesus. He said, “Teacher, when you say things like that, you say bad things about us too.”

46Jesus replied, “How terrible for you authorities on the law! You put such heavy loads on people that they can hardly carry them. But you yourselves will not lift one finger to help them.

47“How terrible for you! You build tombs for the prophets. It was your people of long ago who killed them. 48So you show that you agree with what your people did long ago. They killed the prophets, and now you build the prophets’ tombs. 49So God in his wisdom said, ‘I will send prophets and apostles to them. They will kill some. And they will try to hurt others.’ 50So the people of today will be punished. They will pay for all the prophets’ blood spilled since the world began. 51I mean from the blood of Abel to the blood of Zechariah. He was killed between the altar and the temple. Yes, I tell you, the people of today will be punished for all these things.

52“How terrible for you authorities on the law! You have taken away the key to the door of knowledge. You yourselves have not entered. And you have stood in the way of those who were entering.”

53When Jesus went outside, the Pharisees and the teachers of the law strongly opposed him. They threw a lot of questions at him. 54They set traps for him. They wanted to catch him in something he might say.