Luka 11 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 11:1-54

Yesu Afundisha Wanafunzi Wake Kuomba

(Mathayo 6:9-13; 7:7-11)

111:1 Lk 3:21; Yn 13:13Siku moja, Yesu alikuwa mahali fulani akiomba. Alipomaliza kuomba, mmoja wa wanafunzi wake akamwambia, “Bwana, tufundishe kuomba, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.”

211:2 Mt 3:211:2 Mt 6:9-13Akawaambia, “Mnapoomba, semeni:

“ ‘Baba yetu (uliye mbinguni),

jina lako litukuzwe,

ufalme wako uje.

(Mapenzi yako yafanyike

hapa duniani kama huko mbinguni.)

3Utupatie kila siku riziki yetu.

411:4 Mt 18:35; Mk 11:25; Mt 26:41; Yak 1:13Utusamehe dhambi zetu,

kwa kuwa na sisi huwasamehe wote wanaotukosea.

Wala usitutie majaribuni

(bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu).’ ”

5Kisha akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu mwenye rafiki yake, naye akamwendea usiku wa manane na kumwambia, ‘Rafiki, nikopeshe mikate mitatu. 6Kwa sababu rafiki yangu amekuja kutoka safarini, nami sina kitu cha kumpa.’

711:7 Mt 26:10“Kisha yule aliyeko ndani amjibu, ‘Usinisumbue. Mlango umefungwa, nami na watoto wangu tumelala. Siwezi kuamka nikupe chochote.’ 811:8 Lk 18:1-6Nawaambia, ingawa huyo mtu hataamka na kumpa hiyo mikate kwa sababu ni rafiki yake, lakini kwa sababu ya kuendelea kwake kuomba, ataamka na kumpa kiasi anachohitaji.

911:9 Mt 7:711:9 Mt 7:7-11“Kwa hiyo nawaambia: Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango. 10Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.

11“Je, kuna yeyote miongoni mwenu ambaye mtoto wake akimwomba samaki, atampa nyoka badala yake? 12Au mtoto akimwomba yai atampa nge? 13Basi ikiwa ninyi mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa Roho Mtakatifu wale wamwombao!”

Yesu Na Beelzebuli

(Mathayo 12:22-30; Marko 3:20-27)

1411:14 Mt 9:32-3311:14 Mt 12:22Basi Yesu alikuwa anamtoa pepo mchafu kutoka kwa mtu aliyekuwa bubu. Yule pepo mchafu alipomtoka yule mtu aliyekuwa bubu, akaanza kuongea, nao umati wa watu ukashangaa. 1511:15 Mk 3:22; Mt 9:34Lakini wengine wakasema, “Anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli,11:15 Beelzebubu au Beelzebuli; ni mkuu wa pepo wachafu; pia 18, 19. yule mkuu wa pepo wachafu wote.” 1611:16 Mt 12:38Wengine ili kumjaribu wakataka awaonyeshe ishara kutoka mbinguni.

1711:17 Mt 9:34Yesu akajua mawazo yao, naye akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Nayo nyumba iliyogawanyika dhidi yake yenyewe itaanguka. 1811:18 Mt 4:10Kama Shetani amegawanyika mwenyewe, ufalme wake utasimamaje? Nawaambia haya kwa sababu ninyi mnadai ya kuwa mimi ninatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli. 1911:19 Mk 11:24; Yn 15:7; Yak 1:6; Yn 3:32; Mt 7:7Kama mimi natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, wafuasi wenu nao je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu. 2011:20 Kut 8:19; Mt 3:2Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa kidole cha Mungu, basi Ufalme wa Mungu umewajia.

2111:21 Mt 12:29; Mk 3:17“Mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha anapoilinda nyumba yake, mali yake iko salama. 2211:22 Isa 53:12; Kol 2:15Lakini mtu mwenye nguvu zaidi kumliko akimshambulia na kumshinda, yeye humnyangʼanya silaha zake zote alizozitegemea, na kuchukua nyara.

2311:23 Mt 12:30; Mk 9:40“Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.

Kurudi Kwa Pepo Mchafu

(Mathayo 12:43-45)

2411:24 Mt 12:43“Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati. Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ 25Naye arudipo na kuikuta ile nyumba imefagiliwa na kupangwa vizuri, 2611:26 2Pet 2:20ndipo huenda na kuchukua pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza.”

2711:27 Lk 23:29Ikawa Yesu alipokuwa akisema hayo, mwanamke mmoja katikati ya ule umati wa watu akapaza sauti akasema, “Limebarikiwa tumbo lililokuzaa na matiti uliyonyonya!”

2811:28 Ebr 4:12; Mit 8:32; Yn 14:21Yesu akajibu, “Wamebarikiwa zaidi wale wanaolisikia neno la Mungu na kulitii.”

Ishara Ya Yona

(Mathayo 12:38-42)

2911:29 Mt 12:38; Yn 1:17; Mt 16:4Umati wa watu ulipokuwa unazidi kuongezeka, Yesu akaendelea kusema, “Hiki ni kizazi kiovu. Kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ya Yona. 3011:30 Yn 1:17; 2:10Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ishara kwa watu wa Ninawi, ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa ishara kwa kizazi hiki. 3111:31 1Fal 10:1; 2Nya 9:1Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kuwahukumu watu wa kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni. 3211:32 Yon 3:5Siku ya hukumu, watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.

Taa Ya Mwili

(Mathayo 5:15; 6:22-23)

3311:33 Mt 5:15; Mk 4:21“Hakuna mtu yeyote awashaye taa na kuiweka mahali palipofichika au kuifunikia chini ya bakuli. Badala yake huiweka juu ya kinara chake, ili watu wote wanaoingia waone nuru. 3411:34 Mt 6:22; 2711:34 Mt 6:22; 23Jicho lako ni taa ya mwili wako. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote pia umejaa nuru. Lakini kama jicho ni bovu, mwili wako wote pia umejaa giza. 35Kwa hiyo, hakikisha kwamba nuru iliyoko ndani yako isiwe giza. 36Basi ikiwa mwili wako wote umejaa nuru, bila sehemu yake yoyote kuwa gizani, basi utakuwa na nuru kama vile taa ikuangazavyo kwa nuru yake.”

Yesu Awashutumu Mafarisayo Na Wanasheria

(Mathayo 23:1-36; Marko 12:38-40)

3711:37 Lk 7:36; 14:1Yesu alipomaliza kuzungumza, Farisayo mmoja alimwalika nyumbani mwake kwa chakula. Yesu akaingia na kuketi katika sehemu yake mezani. 3811:38 Mk 7:3-4Yule Farisayo akashangaa kwamba Yesu hakunawa kwanza kabla ya kula.

3911:39 Lk 7:13; Mt 23:25-26; Mk 7:20-23Ndipo Bwana akamwambia, “Sasa, enyi Mafarisayo, mnasafisha kikombe na sahani kwa nje, lakini ndani mmejaa unyangʼanyi na uovu. 4011:40 Lk 12:20; 1Kor 15:36Enyi wapumbavu! Hamjui kuwa yeye aliyetengeneza nje ndiye alitengeneza na ndani pia? 4111:41 Lk 12:33; Mdo 10:15Basi toeni sadaka ya vile mlivyo navyo, na tazama, vitu vyote vitakuwa safi kwenu.

4211:42 Lk 18:12; Kum 6:5; Mik 6:8; Mt 23:23“Lakini ole wenu, Mafarisayo, kwa maana mnampa Mungu zaka za mnanaa, mchicha na kila aina ya mboga, lakini mnapuuza haki na upendo wa Mungu. Iliwapasa kufanya haya ya pili bila kupuuza hayo ya kwanza.

4311:43 Mt 23:6-7; Mk 12:38-39“Ole wenu Mafarisayo, kwa sababu ninyi mnapenda kukalia viti vya mbele katika masinagogi, na kusalimiwa kwa heshima masokoni.

4411:44 Mt 23:27-35“Ole wenu, kwa sababu ninyi ni kama makaburi yasiyokuwa na alama, ambayo watu huyakanyaga pasipo kujua.”

4511:45 Mt 22:35Mtaalamu mmoja wa sheria akamjibu, akasema, “Mwalimu, unaposema mambo haya, unatutukana na sisi pia.”

4611:46 Mt 23:4Yesu akamjibu, “Nanyi wataalamu wa sheria, ole wenu, kwa sababu mnawatwika watu mizigo mizito ambayo hawawezi kubeba, wala ninyi wenyewe hamwinui hata kidole kimoja kuwasaidia.

4711:47 Mt 23:29“Ole wenu, kwa sababu ninyi mnajenga makaburi ya manabii waliouawa na baba zenu. 4811:48 Mt 23:29-32; Mdo 7:51-53Hivyo ninyi mwashuhudia na mnathibitisha kile baba zenu walichofanya. Wao waliwaua manabii, nanyi mnawajengea makaburi. 4911:49 1Kor 1:24; Kol 2:3Kwa sababu ya jambo hili, Mungu katika hekima yake alisema, ‘Tazama, nitatuma kwao manabii na mitume, nao watawaua baadhi yao na wengine watawatesa.’ 50Kwa hiyo kizazi hiki kitawajibika kwa ajili ya damu ya manabii iliyomwagwa tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, 5111:51 Mwa 4:8; 2Nya 24:20-21; Mt 23:35-36tangu damu ya Abeli mpaka damu ya Zekaria, aliyeuawa kati ya madhabahu na mahali patakatifu. Naam, nawaambia, kizazi hiki kitawajibika kwa haya yote.

5211:52 Mt 23:13“Ole wenu ninyi wataalamu wa sheria, kwa sababu mmeuondoa ufunguo wa maarifa. Ninyi wenyewe hamkuingia, na wale waliokuwa wanaingia mkawazuia.”

53Yesu alipoondoka huko, walimu wa sheria na Mafarisayo wakaanza kumpinga vikali na kumsonga kwa maswali, 5411:54 Mt 12:10; Mk 12:13wakivizia kumkamata kwa kitu atakachosema ili wamshtaki.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

路加福音 11:1-54

教导门徒祷告

1有一天,耶稣在某地祷告完毕,有个门徒对祂说:“主啊,请教导我们祷告,像约翰教他的门徒一样。”

2耶稣对他们说:“你们应该这样祷告,

“‘天父,愿人都尊崇你的圣名,

愿你的国度降临,

愿你的旨意在地上成就,

就像在天上成就一样11:2 有古卷无“愿你的旨意在地上成就,就像在天上成就一样”。

3愿你天天赐给我们日用的饮食。

4求你饶恕我们的罪,

因为我们也饶恕那些亏欠我们的人。

不要让我们遇见诱惑,

拯救我们脱离那恶者11:4 有古卷无“拯救我们脱离那恶者”。。’”

5耶稣又对他们说:“假设你在半夜跑去朋友家请求说,‘朋友,请借给我三个饼吧, 6因为有一位朋友远道而来,我家没有什么可以招待他。’ 7那个人在屋里应声说,‘请别打搅我,门已经锁上了,我和孩子们也已经上床了,我不能起来给你拿饼。’

8“我告诉你们,那人虽不念朋友之情,但是倘若你不肯罢休,继续请求,他最终会起来满足你的愿望。

9“我告诉你们,祈求,就会给你们;寻找,就会寻见;叩门,就会给你们开门。 10因为凡祈求的,就得到;寻找的,就寻见;叩门的,就给他开门。

11“你们中间做父亲的,如果孩子要饼,你会给他石头吗?11:11 有古卷无“如果孩子要饼,你会给他石头吗?”要鱼,你会给他蛇吗? 12要鸡蛋,你会给他蝎子吗? 13你们虽然邪恶,尚且知道把好东西给儿女,天父岂不更要赐圣灵给那些求祂的人吗?”

耶稣和别西卜

14有一次,耶稣赶出一个使人哑巴的鬼。鬼一出去,哑巴就能说话了,大家都很惊奇。 15有人却说:“祂是靠鬼王别西卜赶鬼。” 16还有些人想试探耶稣,要求祂行个神迹证明自己是上帝派来的。

17耶稣知道他们的心思,就说:“一个国内部自相纷争,必然灭亡;一个家内部自相纷争,必然崩溃。 18同样,若撒旦内部自相纷争,它的国怎能维持呢?你们说我是靠别西卜赶鬼, 19若我是靠别西卜赶鬼,你们的子弟又是靠谁赶鬼呢?因此,他们要审判你们。 20但若我是靠上帝的能力赶鬼,就是上帝的国已降临在你们中间了。

21“壮汉全副武装地看守自己的住宅,他的财物会很安全。 22但是,来了一个比他更强壮的人,把他制服后,夺去他所依靠的武装,并把他抢来的东西分给了人。 23谁不与我为友,就是与我为敌;谁不和我一起收聚,就是故意拆散。

24“有个污鬼离开了它以前所附的人,在干旱无水之地四处游荡,寻找安歇之处,却没有找到。于是它说,‘我要回到老地方。’ 25它回去后,看见里面打扫得又干净又整齐, 26就去带来了七个比自己更邪恶的鬼一起住在那里。那人的下场比从前更惨了。”

谁更有福

27耶稣说话的时候,人群中有个妇人高喊:“生你养你的人真有福啊!”

28耶稣回答说:“但那听了上帝的话又去遵行的人更有福。”

可悲的邪恶世代

29这时聚集的人越来越多,耶稣说:“这是一个邪恶的世代,人们只想看神迹,但除了约拿的神迹以外,再没有神迹给他们看。 30正如约拿成了尼尼微人的神迹,人子也要成为这世代的神迹。

31“在审判的日子,南方的女王和这世代的人都要起来11:31 起来”或作“复活”,下同32节。,她要定这个世代的罪,因为她曾不远千里来听所罗门王的智言慧语。看啊!这里有一位比所罗门王更伟大。

32“在审判的日子,尼尼微人和这世代的人都要起来,尼尼微人要定这个世代的罪,因为他们听到约拿的宣告,就悔改了。看啊!这里有一位比约拿更伟大。

灯的比喻

33“没有人点了灯却将它放在地窖里或斗底下,人总是把灯放在灯台上,让进来的人可以看见光。 34你的眼睛就是身体的灯,你的眼睛明亮,全身就光明;你的眼睛昏花,全身就黑暗。 35因此要小心,不要让你心里的光变为黑暗。 36如果你全身光明、毫无黑暗,你整个人就熠熠生辉,好像有灯光照在你身上。”

谴责法利赛人

37耶稣说完这番话后,有一个法利赛人来请祂吃饭,祂便应邀入席。 38这位法利赛人看见耶稣饭前没有行犹太人洗手的礼仪,十分诧异。 39主对他说:“你们法利赛人洗净杯盘的外面,你们里面却充满了贪婪和邪恶。 40愚蠢的人啊,人里外不都是上帝所创造的吗? 41只要你们发自内心地去施舍,一切对你们都是洁净的。

42“法利赛人啊,你们有祸了!你们将薄荷、茴香、各样蔬菜献上十分之一,却忽略了上帝的公义和仁爱。后者是你们本该做的,前者也不可忽略。

43“法利赛人啊,你们有祸了!你们喜欢在会堂里坐首位,又喜欢在街市上听到别人的问候。 44你们有祸了!因为你们就像没有墓碑的坟墓,人们从上面走过也不知道。”

谴责律法教师

45一位律法教师对耶稣说:“老师,你这话把我们也侮辱了!”

46耶稣回答说:“你们这些律法教师也有祸了!你们把沉重难负的担子放在别人肩上,自己却连一根指头也不肯动。

47“你们有祸了,你们为先知修造坟墓,而他们正是被你们祖先杀害的! 48所以你们是见证人,你们赞同祖先的行为,因为他们杀了先知,你们为先知造坟墓。 49因此,充满智慧的上帝说,‘我要差遣先知和使徒到他们那里,有些要被杀害,有些要遭迫害’, 50-51使创世以来,自亚伯一直到在祭坛和圣所之间被杀的撒迦利亚等众先知的血债,都由这个世代承担。我实在告诉你们,这些罪责都要由这个世代承担。

52“律法教师啊,你们有祸了!你们拿走了知识的钥匙,自己不进去,还阻挡那些正要进去的人。”

53耶稣离开那里后,法利赛人和律法教师开始激烈地反对祂,用各种问题刁难祂, 54伺机找把柄陷害祂。