Luka 1 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Luka 1:1-80

1Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu, 21:2 Mk 1:1; Mdo 1:21-22; 2Pet 1:16; 1Yn 1:1; Mk 4:14kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana, 31:3 Mdo 11:4; 24:3; 26:25; 1:1mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo, 41:4 Yn 20:31; Mdo 2:42ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.

Kuzaliwa Kwa Yohana Mbatizaji Kwatabiriwa

51:5 1Nya 24:10; Mt 2:1Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni. 61:6 Kum 5:33; Lk 2:25Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama. 7Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.

81:8 1Nya 24:19; 2Nya 8:14Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu, 91:9 2Nya 29:11; Za 141:2alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba. 101:10 Law 16:17Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.

111:11 Mdo 5:19; Kut 30:1-10Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria. 121:12 Amu 6:22-23; 13:22Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu. 131:13 Mt 14:27; 3:1; Lk 1:60-63Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana. 141:14 Lk 1:58Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake. 151:15 Law 10:9; Lk 7:33; Yer 1:5; Gal 1:15Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake. 161:16 Mal 4:5, 6Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao. 171:17 Mt 11:14; Mal 4:4-6Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”

181:18 Mwa 17:17Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”

191:19 Mt 18:10; Lk 1:26Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema. 201:20 Kut 4:11; Eze 3:26Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”

21Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni. 221:22 Lk 1:62Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.

231:23 2Fal 11:5Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake. 24Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.

251:25 Mwa 30:23; Isa 4:1Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”

Kuzaliwa Kwa Yesu Kwatabiriwa

261:26 Lk 1:62; Mt 2:23Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti, 271:27 Mt 1:16-20; Lk 2:4kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria. 281:28 Amu 5:24Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”

291:29 Lk 1:12Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?” 301:30 Mt 14:27Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu. 311:31 Isa 7:14; Mt 1:21-25Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu. 321:32 Mk 5:7Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake. 331:33 Mt 28:18; 2Sam 7:16; Ebr 1:8Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

34Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”

351:35 Mt 1:18; 4:3; Mk 1:24Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu. 361:36 Lk 1:24Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa. 371:37 Mt 19:26; Mwa 18:14; Zek 8:6; Mt 18:26; Mk 10:27; Rum 4:21Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”

38Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.

Maria Aenda Kumtembelea Elizabeti

391:39 Lk 1:65; Yos 21:9, 10, 11Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi. 40Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti. 411:41 Lk 1:15; Mwa 25; 22Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu, 421:42 Amu 5:24akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa. 431:43 Yn 13:13Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu? 44Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha. 451:45 Lk 1:20; 11:28Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”

Wimbo Wa Maria Wa Sifa

461:46 Za 34:2-3Naye Maria akasema:

“Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,

471:47 Za 18:46; 1Tim 4:10nayo roho yangu inamfurahia

Mungu Mwokozi wangu,

481:48 Za 138:5; Lk 11:27kwa kuwa ameangalia kwa fadhili

unyonge wa mtumishi wake.

Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,

491:49 Za 71:19; 111:9kwa maana yeye Mwenye Nguvu

amenitendea mambo ya ajabu:

jina lake ni takatifu.

501:50 Kut 20:6; Za 103:17Rehema zake huwaendea wale wamchao,

kutoka kizazi hadi kizazi.

511:51 Za 98:1; Isa 40:10Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake;

amewatawanya wale wenye kiburi

ndani ya mioyo yao.

521:52 Mt 23:12; 1Sam 2:6; Ay 5:11; Za 11:3, 6Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi,

lakini amewainua wanyenyekevu.

531:53 Za 107:9; 1Sam 3:5Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri,

bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.

541:54 Za 98:3Amemsaidia mtumishi wake Israeli,

kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu

551:55 Za 132:11; Gal 3:16Abrahamu na uzao wake milele,

kama alivyowaahidi baba zetu.”

56Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.

Kuzaliwa Kwa Yohana Mbatizaji

57Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume. 581:58 Lk 1:14Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.

591:59 Law 12:3; Flp 3:5Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake. 601:60 Lk 1:13, 63; Mt 3:1Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”

61Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”

621:62 Lk 1:22Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani. 631:63 Lk 1:13, 60; Mt 3:1Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.” 641:64 Lk 1:20; Eze 24:27Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu. 65Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote. 661:66 Mwa 39:2; Mdo 11:21Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.

Unabii Wa Zekaria

671:67 Yoe 2:28Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:

681:68 Mwa 24:27; 1Fal 8:15; Za 111:9; Lk 7:16“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli,

kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.

691:69 2Sam 22:23; Za 132:17Naye ametusimamishia pembe1:69 Pembe hapa inamaanisha nguvu. ya wokovu

katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,

701:70 Yer 23:3; Za 132:17kama alivyonena kwa vinywa vya manabii

wake watakatifu tangu zamani,

711:71 Za 106:10kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu,

na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:

721:72 Mik 7:20; Za 106:45; Eze 16:60ili kuonyesha rehema kwa baba zetu

na kukumbuka Agano lake takatifu,

731:73 Mwa 22:16-18kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:

741:74 Ebr 9:14kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu,

tupate kumtumikia yeye pasipo hofu

751:75 Efe 4:24katika utakatifu na haki mbele zake,

siku zetu zote.

761:76 Mt 11:9; Mk 5:7; Mal 3:1; Mt 3:3“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana;

kwa kuwa utamtangulia Bwana

na kuandaa njia kwa ajili yake,

771:77 Yer 31:34; Mt 1:21kuwajulisha watu wake juu ya wokovu

utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,

781:78 Mal 4:2kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu,

nuru itokayo juu itatuzukia

791:79 Za 107:14; Mdo 26:18ili kuwaangazia wale waishio gizani

na katika uvuli wa mauti,

kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”

801:80 Lk 2:40, 52Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.

Korean Living Bible

누가복음 1:1-80

1존경하는 데오빌로 각하에게: 1:1 원문에는 ‘로고스’ (말씀)예수님이 하신 일을 처음부터 목격하고 그분의 말

2씀을 직접 들은 사람들이 우리 가운데 전한 말을 그대로 기록하려고 붓을 든 사람이 많습니다.

3나도 이 모든 일을 처음부터 자세히 조사해 보았으므로 데오빌로 각하에게 차례대로 써 보내는 것이 좋을 것이라고 생각했습니다.

4그래서 내가 각하께서 이미 들으신 일들이 사실임을 알게 하려고 이 글을 드립니다.

천사가 사가랴에게 나타남

5헤롯이 유대 왕으로 있을 때 아비야 반에 사가랴란 제사장이 있었는데 그의 아내 엘리사벳도 아론의 후손이었다.

6이들 부부는 하나님이 보시기에 의로운 사람들이었으며 주의 모든 계명과 규정을 빈틈없이 지켰다.

7그러나 엘리사벳은 임신을 못하는 몸이어서 그들에게는 아기가 없었고 두 사람이 모두 나이가 많았다.

8사가랴가 자기 반의 차례에 따라 하나님 앞에서 제사장의 직무를 수행할 때였다.

9제사장직의 관습대로 제비를 뽑은 결과 사가랴가 성전에 들어가 분향하는 일을 맡게 되었다.

10그리고 그가 분향하는 동안 많은 사람들이 밖에서 기도하고 있었다.

11그때 주의 천사가 사가랴에게 나타나 향단 오른쪽에 서자

12그는 천사를 보고 놀라며 무서워하였다.

13그러나 천사는 그에게 이렇게 말하였다. “사가랴야, 두려워하지 말아라. 하나님께서 네 기도를 들으셨다. 네 아내 엘리사벳이 아들을 낳을 것이니 ‘요한’ 이라고 불러라.

14너도 기쁘고 즐겁겠지만 많은 사람들이 그가 태어난 것을 기뻐할 것이다.

15그 아기는 주 앞에서 위대한 사람이 될 것이며 포도주와 독한 술을 마시지 않을 것이다. 그리고 그는 1:15 어떤 역본에는 ‘태어나자마자’모태에 있을 때부터 성령이 충만하여

16많은 이스라엘 사람을 그들의 주 하나님께로 돌아오게 할 것이다.

17그는 엘리야의 정신과 능력을 가지고 주님보다 먼저 와서 1:17 말4:6아버지의 마음이 자녀들에게 돌아서게 하고 순종치 않는 사람들이 의로운 사람의 지혜를 갖게 하여 백성들이 주님을 맞이할 준비를 갖추게 할 것이다.”

18사가랴가 천사에게 “나는 늙었고 내 아내도 나이가 많은데 어떻게 이런 일이 있을 수 있습니까?” 하고 묻자

19천사가 대답하였다. “나는 하나님을 모시고 있는 가브리엘이다. 하나님께서 이 기쁜 소식 을

너에게 알리라고 나를 보내셨다.

20네가 내 말을 믿지 않았으므로 이런 일이 일어날 때까지 벙어리가 되어 말을 못할 것이다. 그러나 때가 되면 내 말이 그대로 이루어질 것이다.”

21사람들은 사가랴를 기다리다가 그가 성전 안에 너무 오래 있는 것을 이상하게 여겼다.

22사가랴가 드디어 밖으로 나왔으나 말을 하지 못하므로 사람들은 그가 성전 안에서 환상을 본 줄로 알았다. 사가랴는 사람들에게 손짓만 하고 말을 하지 못한 채 그대로 있다가

23그의 직무 기간이 끝난 다음에 집으로 돌아갔다.

24그 후에 그의 아내 엘리사벳은 임신하여 다섯 달 동안 숨어 지내면서

25“이처럼 주께서 나를 보살펴 주셔서 나에게 아이를 주심으로 모든 사람들이 다 아는 내 부끄러움을 씻어 주셨다” 하였다.

마리아에게 아들을 약속함

26엘리사벳이 임신한 지 여섯 달이 되었을 때 하나님께서는 가브리엘 천사를 갈릴리 나사렛이라는 마을에 사는

27다윗의 후손 요셉과 약혼한 처녀 마리아에게 보내셨다.

28천사가 그 집에 들어가 마리아에게 “은혜를 받은 처녀여, 기뻐하여라. 주님께서 너와 함께 계신다” 라고 하였다.

29마리아는 이런 인사말이 무슨 뜻인지 몰라 어리둥절하였다.

30그러자 천사가 말하였다. “마리아야, 무서워하지 말아라. 너는 하나님의 은혜를 받았다.

31이제 네가 임신하여 아들을 낳을 것이다. 이름을 ‘예수’ 라고 불러라.

32그는 위대한 인물이 될 것이며 가장 높으신 하나님의 아들이라고 불릴 것이다. 주 하나님께서 그의 조상 다윗의 보좌를 그에게 주실 것이니

33그가 영원히 야곱의 집을 다스릴 것이며 그의 나라는 끝없이 계속될 것이다.”

34마리아가 천사에게 “저는 처녀인데 어떻게 이런 일이 있을 수 있겠습니까?” 하고 묻자

35천사가 이렇게 대답하였다. “성령님이 네 위에 내려오시고 하나님의 능력이 너를 덮어 주실 것이다. 그러므로 태어나실 거룩한 분은 하나님의 아들이라고 불릴 것이다.

36네 친척 엘리사벳을 보아라. 그녀는 아이를 낳지 못하는 여자로 알려졌으나 그처럼 늙은 나이에도 임신한 지 여섯 달이나 되었다.

37하나님에게는 불가능한 일이 아무것도 없다.”

38그때 마리아가 “저는 주의 종입니다. 말씀하신 대로 되기를 바랍니다” 하고 말하였다. 그러자 천사는 떠나갔다.

39그 후에 마리아는 유대 산골 사가랴가 사는 마을로 급히 가서

40엘리사벳을 방문하였다.

41엘리사벳이 마리아의 인사하는 소리를 듣는 순간 엘리사벳의 태중의 아기가 뛰었다. 엘리사벳은 성령으로 충만하여

42큰 소리로 이렇게 말하였다. “너는 여자들 중에 가장 복받은 사람이며 네 태중의 1:42 원문에는 ‘열매’아기도 복받은 분이다.

43내 주님의 어머니가 나를 찾아오다니 이 얼마나 영광스러운 일인가!

44네가 인사하는 소리를 듣는 순간 내 태중의 아기가 기뻐서 뛰었다.

45주께서 말씀하신 것이 이루어질 것을 믿은 여자는 정말 행복하다.”

46그러자 마리아는 이렇게 노래하였다. “내 영혼이 주를 찬양하며

47내 마음이 내 구주 하나님을 기뻐하는 것은

48그가 이 천한 종을 돌아보셨음이라. 지금부터는 모든 세대가 나를 행복하다 하겠네.

49능력 있는 분이 나를 위해 큰 일을 하셨으니 그의 이름 거룩하여라!

50그를 두려워하는 사람들에게 자손 대대로 자비를 베푸시는구나.

51그가 권능의 팔을 펴서 교만한 자들을 흩으시고

52권력자들을 높은 자리에서 끌어내리셨지만 낮고 천한 사람들은 높여 주셨네.

53굶주린 사람들에게는 좋은 것으로 배불리 먹이셨으나 부자들은 빈손으로 보내셨네.

54그의 종 이스라엘에게 자비 베푸는 것을 잊지 않으시고 기억하여 그를 도우셨으니

55우리 조상들에게 말씀하신 대로 아브라함과 그 후손에게 하신 영원한 약속이었네.”

56마리아는 엘리사벳의 집에서 석 달 동안 지내다가 자기 집으로 돌아갔다.

세례 요한의 출생

57엘리사벳은 달이 차서 아들을 낳았다.

58이웃과 친척들은 주님께서 엘리사벳에게 큰 자비를 베푸셨다는 소식을 듣고 함께 기뻐하였다.

59아기가 난 지 8일 만에 1:59 포피를자르는의식.할례식이 베풀어졌다. 식에 참석한 사람들은 아버지의 이름을 따서 아기 이름을 사가랴로 부르려고 하였다.

60그러나 아기 어머니는 “아니오, 요한이라고 불러야 합니다” 하고 대답하였다.

61사람들이 “친척 중에는 이런 이름을 가진 사람이 없는데” 하며

62사가랴에게 손짓으로 아기 이름을 뭐라고 지었으면 좋겠느냐고 물었다.

63사가랴가 필기 도구를 달라고 하여 아기 이름을 ‘요한’ 이라고 쓰자 사람들은 모두 놀랐다.

64바로 그 순간에 사가랴의 입이 열리고 혀가 풀려서 말을 하게 되어 하나님을 찬양하였다.

65그래서 이웃 사람들이 다 두려워하였고 또 이 소문이 온 유대 산골에 쫙 퍼졌다.

66그리고 듣는 사람마다 모두 이 말을 마음에 새기며 “이 아기가 앞으로 어떤 사람이 될까?” 하고 말했는데 이것은 주의 손길이 그 아기와 함께하였기 때문이었다.

67아기 아버지 사가랴는 성령님의 감동을 받아 이렇게 예언하였다.

68“이스라엘의 주 하나님을 찬양하여라. 그가 오셔서 자기 백성을 1:68 또는 ‘속량하시며’죄에서 건져 주셨고

69그의 종 다윗의 집에서 우리를 위하여 1:69 원문에는 ‘구원의뿔’구원의 주를 일으키셨으니

70오래 전에 그의 거룩한 예언자들을 통해서 말씀하신 대로

71우리 원수들과 우리를 미워하는 모든 사람들의 손에서 우리를 구원하는 구원이라.

72그가 우리 조상들에게 자비를 베풀고 그의 거룩한 계약을 기억하겠다고 말씀하셨으며

73우리 조상 아브라함에게 엄숙하게 맹세하심으로

74우리를 원수들의 손에서 구해 내고

75우리가 주 앞에서 일평생 두려움 없이 거룩함과 의로움으로 주를 섬기게 하겠다고 약속하셨다.

76“아가야, 너는 가장 높으신 하나님의 예언자가 될 것이다. 너는 주님보다 미리 와서 그의 길을 준비하여

77죄를 용서받음으로써 얻는 구원의 길을 그의 백성들에게 전할 것이다.

78이 모든 일은 우리 하나님의 자비로 된 것이니 하늘에서 떠오르는 태양이 우리를 찾아와

79어두움과 죽음의 그늘에 사는 사람들을 비추고 우리를 평화의 길로 인도하리라.”

80아기는 무럭무럭 자라 마음이 굳세어지고 이스라엘 백성들 앞에 나타날 때까지 광야에서 살았다. 예수님의 탄생