Kutoka 9 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 9:1-35

Pigo La Tano: Vifo Vya Mifugo

19:1 Kut 8:1Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie, ‘Hili ndilo Bwana, Mungu wa Waebrania asemalo: “Waachie watu wangu waende ili wapate kuniabudu.” 2Kama ukikataa kuwaachia waende, nawe ukiendelea kuwashikilia, 39:3 Kut 7:4; 1Sam 5:6; Ay 13:21; Za 32:4; 39:10; 78:50; Mdo 13:11; Law 26:25; Amo 4:10mkono wa Bwana utaleta pigo baya kwa mifugo yako, juu ya farasi wako, punda, ngamia, ngʼombe wako, kondoo na mbuzi. 49:4 Kut 8:23Lakini Bwana ataweka tofauti kati ya mifugo ya Israeli na ile ya Misri, kwamba hakuna mnyama wa Mwisraeli atakayekufa.’ ”

5Bwana akaweka wakati na kusema, “Kesho Bwana atalitenda hili katika nchi.” 69:6 Kut 11:5; 12:29; Za 78:48-50Siku iliyofuata Bwana akalitenda: Mifugo yote ya Wamisri ikafa, lakini hakuna hata mnyama mmoja wa wana wa Israeli aliyekufa. 79:7 Kut 7:14, 22; 8:32Farao akatuma watu kuchunguza, nao wakakuta kuwa hakuna hata mnyama mmoja wa Waisraeli aliyekufa. Lakini moyo wa Farao haukukubali kuwaachia watu waende.

Pigo La Sita: Majipu

8Kisha Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Chukueni majivu ya tanuru, naye Mose ayarushe angani mbele ya Farao. 99:9 Law 13:18-19; 2Fal 20:7; Ay 2:7; Isa 38:21; Ufu 16:2Yatakuwa vumbi jepesi juu ya nchi yote ya Misri, pia yatatokea majipu yenye kufura juu ya watu na wanyama katika nchi yote.”

10Basi wakachukua majivu kwenye tanuru na kusimama mbele ya Farao. Mose akayarusha hewani, nayo majipu yenye kufura yakatokea miilini mwa watu na wanyama. 119:11 Kut 8:18Waganga hawakuweza kusimama mbele ya Mose kwa sababu ya majipu yale yaliyokuwa miilini mwao na juu ya miili ya Wamisri wote. 129:12 Kut 4:21; 7:4Lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amemwambia Mose.

Pigo La Saba: Mvua Ya Mawe

139:13 Kut 3:18Kisha Bwana akamwambia Mose, “Amka mapema asubuhi, usimame mbele ya Farao, umwambie, ‘Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Waebrania: Waachie watu wangu waende, ili kwamba waweze kuniabudu, 149:14 Kut 8:10; 15:11; 1Sam 2:2; 2Sam 7:22; 1Fal 8:23; 1Nya 17:20; Za 35:10; 71:19; 86:8; 89:6; Isa 46:9; Yer 10:6; Mik 7:18au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote. 159:15 Kut 3:20Kwa kuwa mpaka sasa ningelikuwa nimenyoosha mkono wangu na kukupiga wewe na watu wako kwa pigo ambalo lingekufutilia mbali juu ya nchi. 169:16 Mit 16:4; Kut 14:4, 17, 31; Za 20:6; 25:11; 68:28; 71:18; 106:8; 109:21; Rum 9:17Lakini nimekuinua wewe kwa kusudi hili hasa, ili nipate kukuonyesha uwezo wangu, na ili Jina langu lipate kutangazwa duniani yote. 17Bado unaendelea kujiinua juu ya watu wangu, wala hutaki kuwaachia waende. 189:18 Yos 10:11; Za 78:47-48; 105:32; 148:8; Isa 30:30; Eze 38:22; Hag 2:17; Kut 9:24; 10:6Kwa hiyo, kesho wakati kama huu nitaleta mvua mbaya sana ya mawe ambayo haijapata kunyesha katika nchi ya Misri, tangu siku ilipoumbwa mpaka leo. 19Sasa toa amri urudishe wanyama wote watoke malishoni na chochote ambacho kipo mashambani waje mpaka mahali pa usalama, kwa sababu mvua ya mawe itanyesha juu ya kila mtu na kila mnyama ambaye hajaletwa ndani ambao bado wako nje mashambani, nao watakufa.’ ”

209:20 Mit 13:13Wale maafisa wa Farao ambao waliliogopa neno la Bwana wakafanya haraka kuwaleta watumwa wao na mifugo yao ndani. 219:21 Mwa 19:14; Eze 33:4-5Lakini wale waliopuuza neno la Bwana wakawaacha watumwa wao na mifugo yao shambani.

22Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili kwamba mvua ya mawe inyeshe juu ya Misri yote, juu ya watu, wanyama na juu ya kila kitu kiotacho katika mashamba ya Misri.” 239:23 Kut 20:18; 1Sam 12:17; Za 18:13; 29:3; 68:33; 77:17; 104:7; Ufu 8:7; 16:21Mose alipoinyoosha fimbo yake kuelekea angani, Bwana akatuma ngurumo na mvua ya mawe, umeme wa radi ulimulika hadi nchi. Kwa hiyo Bwana akaifanya mvua ya mawe kunyesha juu ya nchi ya Misri, 24mvua ya mawe ikanyesha na radi ikamulika pote. Ikawa dhoruba ya kutisha ambayo haijakuwako katika nchi ya Misri, tangu nchi hiyo iwe taifa. 259:25 Za 105:32-33; Eze 13:13Mvua ya mawe ikaharibu kila kitu katika nchi ya Misri kilichokuwa katika mashamba, watu na wanyama, ikaharibu kila kitu kinachoota mashambani na kuvunja kila mti. 269:26 Isa 32:18-20; Kut 10:23; 11:7; 12:13; Amo 4:7Mahali pekee ambapo mvua ya mawe haikunyesha ni nchi ya Gosheni, ambako Waisraeli waliishi.

279:27 Kut 10:16; Hes 14:40; Kum 1:41; Yos 7:11; Amu 10:10; 1Sam 15:24; 24:17; 26:21; Za 11:7; 116:5; 119:135; 129:4; 145:17; Yer 12:1; Mao 1:18Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni akawaambia, “Wakati huu nimetenda dhambi. Bwana ni mwenye haki, mimi na watu wangu ni wakosaji. 289:28 Kut 8:8; Mdo 8:24Mwombeni Bwana, kwa kuwa tumepata ngurumo na mvua za mawe za kututosha. Nitawaachia mwondoke; hamtahitaji kungoja zaidi.”

299:29 1Fal 8:22; Ay 11:13; Za 77:2; 88:9; 143:6; Isa 1:15; Kut 19:5; Ay 41:11; Za 24:1; 50:12; 1Kor 10:26Mose akamjibu, “Nitakapokuwa nimetoka nje ya mji, nitanyoosha mikono yangu juu kumwomba Bwana. Ngurumo zitakoma na hapatakuwepo mvua ya mawe tena, ili upate kujua kuwa, nchi ni mali ya Bwana. 309:30 Kut 8:29Lakini ninajua kuwa wewe na maafisa wako bado hammwogopi Bwana Mungu.”

319:31 Kum 8:8; Rut 1:22; 2:23; 2Sam 14:30; 17:28; Isa 28:25; Eze 4:9(Kitani na shayiri viliharibiwa, kwa kuwa shayiri ilikuwa na masuke, na kitani ilikuwa katika kutoa maua. 329:32 Isa 28:25Hata hivyo, ngano na jamii nyingine ya ngano hazikuharibiwa kwa sababu zilikuwa hazijakomaa bado.)

33Kisha Mose akaondoka kwa Farao akaenda nje ya mji. Mose akanyoosha mikono yake kuelekea kwa Bwana, ngurumo na mvua ya mawe vikakoma, mvua haikuendelea tena kunyesha nchini. 34Farao alipoona kwamba mvua ya mawe na ngurumo zimekoma, akafanya dhambi tena. Yeye na maafisa wake wakafanya mioyo yao kuwa migumu. 359:35 Kut 4:2Kwa hiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waende, kama vile Bwana alivyokuwa amesema kupitia Mose.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

出埃及記 9:1-35

瘟疫之災

1耶和華對摩西說:「你再進宮見法老,告訴他,『希伯來人的上帝耶和華說,讓我的子民去事奉我。 2如果你不讓他們走,繼續扣留他們, 3我就會使你田間所有的牲畜,包括馬、驢、駱駝和牛羊,都染上嚴重的瘟疫。 4但我要把埃及以色列的牲畜分開,以色列人的牲畜必絲毫無損。』」 5耶和華定了日期,說:「明天耶和華必在此地行這事。」 6第二天,耶和華就這樣行了,埃及的牲畜都死了,但以色列人的牲畜一頭也沒死。 7法老派人去探查,發現以色列人的牲畜真的安然無恙。可是,他仍然頑固,不肯讓以色列人離開。

膿瘡之災

8耶和華對摩西亞倫說:「你們去取幾把窯裡的灰,摩西要在法老面前把灰拋向空中。 9這灰要變成塵土,散佈在埃及每一個角落,落在人或牲畜身上,就會起皰長瘡。」 10摩西亞倫便取了一些窯裡的灰,站在法老面前,摩西把灰拋向空中,埃及人和牲畜身上就開始起皰長瘡。 11埃及的巫師無法與摩西對抗,因為他們及所有埃及人身上都長了膿瘡。 12耶和華使法老的心剛硬,他就不聽他們的話,正如耶和華對摩西說的。

冰雹之災

13耶和華對摩西說:「明天一早你再去見法老,對他說,『希伯來人的上帝耶和華這樣說,你要讓我的子民出去事奉我。 14這一次,我要降下大災禍在你及你的臣僕和百姓身上,好叫你知道普天之下我獨一無二。 15我若用瘟疫攻擊你和你的百姓,你們早就滅亡了。 16我讓你活到現在,是為了向你彰顯我的權能,使我的名傳遍天下。 17但你竟然在我的子民面前狂傲自大,不讓他們離開。 18明天這個時候,我要使天上降下大冰雹,是你們埃及立國以來從沒有見過的。 19現在,你要叫人趕快到田間把牲畜和屬於你的一切都帶到安全的地方。凡留在田間的人或牲畜都會被冰雹打死。』」 20有些法老的臣僕聽了耶和華的話就很害怕,趕忙把在田間的僕人和牲畜都召回屋裡。 21但那些不把耶和華的話放在心上的,仍把他們的奴僕和牲畜留在田間。 22耶和華對摩西說:「你向天伸杖,天就會降下冰雹,落在埃及的一切人畜身上,摧毀田間的一切農作物。」 23摩西向天伸出手杖,耶和華就發出雷電和冰雹,火光飛向大地。耶和華在埃及降下冰雹。 24那時冰雹夾雜著火降下來,極為嚴重,在埃及史無前例。 25冰雹摧毀了埃及境內田間的一切,包括人和牲畜,摧毀了田裡的一切作物,打斷了所有的樹木, 26只有以色列人所住的歌珊沒有冰雹。 27法老派人召來摩西亞倫,對他們說:「這次我犯罪了,耶和華是對的,我和我的百姓錯了。 28請你們向耶和華禱告,好止住雷電和冰雹。我准許以色列人出去,你們不必再留在這裡了。」 29摩西回答說:「我一出城,就向耶和華舉手禱告,雷電和冰雹必立刻停止,這樣你就知道普天下都屬於耶和華。 30但我知道你和你的臣僕還是不敬畏上帝耶和華。」

31這場冰雹發生在大麥吐穗和亞麻開花的時候。 32小麥和粗麥較晚成熟,沒有被冰雹打壞。 33摩西離開法老,走出城外向耶和華舉手禱告,雷和冰雹便停止了,豪雨也不下了。 34法老看見災禍停止,就又犯罪,他和他的臣僕都心裡頑固。 35法老硬著心,不讓以色列人離開,正如耶和華藉摩西所言。