Kutoka 5 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 5:1-23

Matofali Bila Nyasi

15:1 Kut 3:18; 4:23Baadaye Mose na Aroni wakaenda kwa Farao, wakamwambia, “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Waruhusu watu wangu waende, ili waweze kunifanyia sikukuu huko jangwani.’ ”

25:2 Amu 2:10; Ay 21:15; Mal 3:14; Kut 3:19Farao akasema, “Huyo Bwana ni nani, hata nimtii na kuruhusu Israeli uende? Simjui huyo Bwana wala sitawaruhusu Israeli waende.”

35:3 Mwa 30:36; Law 26:25; Hes 14:12; Kum 28:21; 2Sam 24:13Ndipo Mose na Aroni wakasema, “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Sasa turuhusu tuwe na safari ya siku tatu ya jangwani ili tukamtolee Bwana Mungu wetu dhabihu, la sivyo aweza kutupiga sisi kwa tauni au kwa upanga.”

45:4 Kut 1:11; 6:6-7Lakini mfalme wa Misri akasema, “Mbona ninyi Mose na Aroni mnawachukua watu waache kazi zao? Rudini kwenye kazi zenu!” 55:5 Mwa 12:2Kisha Farao akasema, “Tazama, sasa watu hawa ni wengi, nanyi mnawazuia kufanya kazi.”

65:6 Mwa 15:13Siku iyo hiyo Farao akatoa amri hii kwa viongozi wa watumwa na wasimamizi wa watu akawaambia: 75:7 Mwa 11:3“Tangu sasa msiwape hawa watu nyasi za kutengenezea matofali. Wao wakusanye nyasi zao wenyewe. 85:8 Kut 10:11Lakini watakeni kutengeneza matofali kiasi kile kile cha mwanzo, kiwango kisipunguzwe. Wao ni wavivu, ndiyo sababu wanalia, wakisema, ‘Turuhusiwe twende kumtolea Mungu wetu dhabihu.’ 9Fanyeni kazi kuwa ngumu zaidi kwa watu hao ili kwamba wakazane na kazi na kuacha kusikiliza uongo.”

10Basi viongozi wa watumwa na wasimamizi wakaenda kuwaambia watu, “Hivi ndivyo Farao asemavyo: ‘Sitawapa tena nyasi. 11Nendeni mkatafute nyasi wenyewe popote mnapoweza kuzipata, lakini kazi yenu haitapunguzwa hata kidogo.’ ” 12Basi watu wakatawanyika kote nchini Misri kukusanya mabua ya kutumia badala ya nyasi. 13Viongozi wa watumwa wakasisitiza, wakisema, “Timizeni kazi mnayotakiwa kwa kila siku, kama wakati ule mlipokuwa mkipewa nyasi.” 145:14 Isa 10:24Wasimamizi wa Kiisraeli waliochaguliwa na viongozi wa watumwa wa Farao walipigwa na kuulizwa, “Kwa nini hamkutimiza kiwango chenu cha kutengeneza matofali jana na leo, kama mwanzoni?”

15Ndipo wasimamizi wa Kiisraeli wakaenda kumlilia Farao, wakisema: “Mbona umewatendea watumishi wako hivi? 16Watumishi wako hawapewi nyasi, hata hivyo tumeambiwa, ‘Tengenezeni matofali!’ Watumishi wako wanapigwa, lakini kosa ni la watu wako wenyewe.”

17Farao akasema, “Ninyi ni wavivu ndiyo sababu mnasema, ‘Turuhusu twende tukamtolee Bwana dhabihu.’ 185:18 Mwa 15:13Sasa nendeni kazini. Hamtapewa nyasi zozote, nanyi ni lazima mtengeneze matofali.”

19Wasimamizi wa Kiisraeli walitambua kuwa wako taabani walipoambiwa, “Hamtakiwi kupunguza idadi ya matofali mliotakiwa kutengeneza kila siku.” 20Walipoondoka kwa Farao, wakawakuta Mose na Aroni wakingojea kukutana nao, 215:21 Mwa 34:30; 16:5; Kut 1:13; 14:11; 16:3; Hes 14:3; 20:3wakawaambia Mose na Aroni, “Bwana na awaangalie awahukumu ninyi! Mmetufanya tunuke kwa Farao na maafisa wake, nanyi mmeweka upanga mikononi mwao ili kutuua sisi.”

Mungu Anaahidi Ukombozi

225:22 Kut 1:12; Yos 7:7; Hes 11:11Mose akarudi kwa Bwana na kumwambia, “Ee Bwana, mbona umewaletea watu hawa taabu? Kwa nini basi ukanituma mimi? 235:23 Yer 4:10; 20:7; Eze 14:9Tangu nilipomwendea Farao kuzungumza naye kwa jina lako, amewaletea taabu watu hawa, nawe kamwe hujawakomboa watu wako.”

New International Reader’s Version

Exodus 5:1-23

Bricks Without Straw

1Later on, Moses and Aaron went to Pharaoh. They said, “The Lord is the God of Israel. He says, ‘Let my people go. Then they will be able to hold a feast to honor me in the desert.’ ”

2Pharaoh said, “Who is the Lord? Why should I obey him? Why should I let Israel go? I don’t even know the Lord. And I won’t let Israel go.”

3Then Moses and Aaron said, “The God of the Hebrews has met with us. Now let us take a journey that lasts about three days. We want to go into the desert to offer sacrifices to the Lord our God. If we don’t, he might strike us with plagues. Or he might let us be killed by swords.”

4But the king of Egypt said, “Moses and Aaron, why are you taking the people away from their work? Get back to work!” 5Pharaoh continued, “There are large numbers of your people in the land. But you are stopping them from working.”

6That same day Pharaoh gave orders to the slave drivers and the overseers in charge of the people. 7He said, “Don’t give the people any more straw to make bricks. Let them go and get their own straw. 8But require them to make the same number of bricks as before. Don’t lower the number they have to make. They are lazy. That’s why they are crying out, ‘Let us go. We want to offer sacrifices to our God.’ 9Make them work harder. Then they will be too busy to pay attention to lies.”

10The slave drivers and the overseers left. They said to the people, “Pharaoh says, ‘I won’t give you any more straw. 11Go and get your own straw anywhere you can find it. But you still have to make the same number of bricks.’ ” 12So the people scattered all over Egypt. They went to gather any pieces of straw left in the fields. 13Pharaoh’s slave drivers kept making the people work hard. They said, “Finish the work you are required to do each day. Make the same number of bricks you made when you had straw.” 14The slave drivers whipped the Israelite overseers they had appointed. The slave drivers asked, “Why haven’t you made the same number of bricks yesterday or today, just as before?”

15Then the Israelite overseers appealed to Pharaoh. They asked, “Why have you treated us like this? 16You didn’t give us any straw. But you told us, ‘Make bricks!’ We are being whipped. But it’s the fault of your own people.”

17Pharaoh said, “You are lazy! That’s why you keep saying, ‘Let us go. We want to offer sacrifices to the Lord.’ 18Now get to work. We won’t give you any straw. But you still have to make the same number of bricks.”

19The Israelite overseers realized they were in trouble. They knew it when they were told, “Don’t reduce the number of bricks you are required to make each day.” 20When they left Pharaoh, they found Moses and Aaron waiting to meet them. 21They said to Moses and Aaron, “We want the Lord to look at what you have done! We want him to judge you for it! We are like a very bad smell to Pharaoh and his officials. You have given them an excuse to kill us with their swords.”

The Lord Promises to Save the Israelites

22Moses returned to talk to the Lord. He said to him, “Why, Lord? Why have you brought trouble on these people? Is this why you sent me? 23I went to Pharaoh to speak to him in your name. Ever since then, he has brought nothing but trouble on these people. And you haven’t saved your people at all.”