Kutoka 40 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 40:1-38

Kuweka Wakfu Maskani Ya Mungu

1Kisha Bwana akamwambia Mose: 240:2 Kut 26:30; Law 3:2; 6:26; 9:23; 16:16; Hes 7:89; 11:16; 17:4; 20:6; Yos 18:1; 19:51; Yer 7:12; Kut 12:2; Hes 9:1“Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza. 340:3 Kut 26; 33; Hes 4:5Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake. 440:4 Kut 25:23; 25:30-31; 26:33Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake. 540:5 Kut 30:1Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.

640:6 Kut 27:1; 2Fal 16:14; 2Nya 4:1“Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania; 740:7 Kut 30:18weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake. 840:8 Kut 27:9Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.

940:9 Kut 30:26; Hes 7:1; Law 8:10“Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu. 1040:10 Kut 29; 36Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana. 11Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.

1240:12 Hes 8:9; Kut 29:4; 30:19“Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji. 1340:13 Kut 28:41; Law 8:1-12Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani. 1440:14 Kut 28:40; Law 10:5Walete wanawe na uwavike makoti. 1540:15 Kut 29:9; Hes 25:13Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.” 1640:16 Mwa 6:22Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.

1740:17 Hes 7:10Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili. 1840:18 2Nya 1:3; Kut 36:20-34Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo. 1940:19 Kut 36:19; Mwa 6:22Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.

2040:20 Kut 16:34; Ebr 9:4; 1Fal 8:9; Kut 25:17-22; 26:34; 31:7Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake. 2140:21 Kut 26:33; Mwa 6:22Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.

2240:22 Kut 25:23Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia 2340:23 Kut 25:30; Law 24:5-8; Mwa 6:22na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.

2440:24 Kut 25:31; 26:35Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu 2540:25 Kut 25:37; 37:23; Mwa 6:22na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.

2640:26 Kut 30:1Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia 2740:27 Mwa 6:22; Kut 30:7na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza. 2840:28 Kut 26:36Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.

2940:29 Kut 20:24; 29:38-42; Mwa 6:22Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.

3040:30 Kut 30:18Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia, 3140:31 Kut 30:19-21Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao. 3240:32 Kut 30:20; Mwa 6:22Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.

3340:33 Kut 27:9; 38:9-20; 27:16Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.

Utukufu Wa Bwana

(Hesabu 9:15-23)

3440:34 Kut 19:16; 16:7; Law 16:2; Hes 9:15-23; 1Fal 8:12; 2Nya 5:13; Isa 6:4; Eze 10:4; Kut 19:16; 23; 2Nya 5:13; Yn 1:14; 12:41; Ufu 15:8Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu. 3540:35 Kut 16:10; 1Fal 8:11; 2Nya 5:13-14; 7:2Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.

3640:36 Hes 9:17-23; 10:13; Neh 9:19Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka; 37lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka. 3840:38 Hes 9:15; Kut 13:21; 1Kor 10:1Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.

New International Version – UK

Exodus 40:1-38

Setting up the tabernacle

1Then the Lord said to Moses: 2‘Set up the tabernacle, the tent of meeting, on the first day of the first month. 3Place the ark of the covenant law in it and shield the ark with the curtain. 4Bring in the table and set out what belongs on it. Then bring in the lampstand and set up its lamps. 5Place the gold altar of incense in front of the ark of the covenant law and put the curtain at the entrance to the tabernacle.

6‘Place the altar of burnt offering in front of the entrance to the tabernacle, the tent of meeting; 7place the basin between the tent of meeting and the altar and put water in it. 8Set up the courtyard around it and put the curtain at the entrance to the courtyard.

9‘Take the anointing oil and anoint the tabernacle and everything in it; consecrate it and all its furnishings, and it will be holy. 10Then anoint the altar of burnt offering and all its utensils; consecrate the altar, and it will be most holy. 11Anoint the basin and its stand and consecrate them.

12‘Bring Aaron and his sons to the entrance to the tent of meeting and wash them with water. 13Then dress Aaron in the sacred garments, anoint him and consecrate him so that he may serve me as priest. 14Bring his sons and dress them in tunics. 15Anoint them just as you anointed their father, so that they may serve me as priests. Their anointing will be to a priesthood that will continue throughout their generations.’ 16Moses did everything just as the Lord commanded him.

17So the tabernacle was set up on the first day of the first month in the second year. 18When Moses set up the tabernacle, he put the bases in place, erected the frames, inserted the crossbars and set up the posts. 19Then he spread the tent over the tabernacle and put the covering over the tent, as the Lord commanded him.

20He took the tablets of the covenant law and placed them in the ark, attached the poles to the ark and put the atonement cover over it. 21Then he brought the ark into the tabernacle and hung the shielding curtain and shielded the ark of the covenant law, as the Lord commanded him.

22Moses placed the table in the tent of meeting on the north side of the tabernacle outside the curtain 23and set out the bread on it before the Lord, as the Lord commanded him.

24He placed the lampstand in the tent of meeting opposite the table on the south side of the tabernacle 25and set up the lamps before the Lord, as the Lord commanded him.

26Moses placed the gold altar in the tent of meeting in front of the curtain 27and burned fragrant incense on it, as the Lord commanded him.

28Then he put up the curtain at the entrance to the tabernacle. 29He set the altar of burnt offering near the entrance to the tabernacle, the tent of meeting, and offered on it burnt offerings and grain offerings, as the Lord commanded him.

30He placed the basin between the tent of meeting and the altar and put water in it for washing, 31and Moses and Aaron and his sons used it to wash their hands and feet. 32They washed whenever they entered the tent of meeting or approached the altar, as the Lord commanded Moses.

33Then Moses set up the courtyard around the tabernacle and altar and put up the curtain at the entrance to the courtyard. And so Moses finished the work.

The glory of the Lord

34Then the cloud covered the tent of meeting, and the glory of the Lord filled the tabernacle. 35Moses could not enter the tent of meeting because the cloud had settled on it, and the glory of the Lord filled the tabernacle.

36In all the travels of the Israelites, whenever the cloud lifted from above the tabernacle, they would set out; 37but if the cloud did not lift, they did not set out – until the day it lifted. 38So the cloud of the Lord was over the tabernacle by day, and fire was in the cloud by night, in the sight of all the Israelites during all their travels.