Kutoka 39 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 39:1-43

Mavazi Ya Kikuhani

(Kutoka 28:1-14)

139:1 Kut 35:19-23; 28:2; Za 93:5; Eze 43Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Kisibau

239:2 Kut 28:6; Law 8:7Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri. 3Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi. 439:4 Law 24:7; Yos 4:7Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau. 539:5 Isa 11:5; Ufu 1:13Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

639:6 Kut 28:9; Ay 28:16; Isa 49:16; Ufu 1:17Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa. 739:7 Law 24:7; Yos 4:7; Kut 28:12; Yos 4:7; Neh 2:20Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Kifuko Cha Kifuani

(Kutoka 28:15-30)

839:8 Law 8:8; Kut 28:15; Isa 59:17Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa. 9Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja39:9 Shibiri moja ni sawa na sentimita 22. na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili. 1039:10 Kut 28:17; Eze 28:13; Ufu 21:19, 20; Isa 54:12Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi; 1139:11 Ufu 4:3; Isa 54:11; Yer 17:1safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi; 12safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto; 1339:13 Dan 10:6; Ay 28:16; Ufu 21:11katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu. 1439:14 Ufu 21:12Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.

15Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba. 16Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani. 17Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani, 18nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele. 19Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau. 20Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau. 21Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Mavazi Mengine Ya Kikuhani

(Kutoka 28:31-43)

2239:22 Kut 28:31; Law 8:7; 1Sam 2:18; 2Sam 6:14Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji, 23na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike. 24Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho. 2539:25 Kut 28:33Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga. 26Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

2739:27 Kut 28:39, 40; 39:27; Law 8:13; Kut 28:4; Isa 61:10; Rum 3:22; Gal 3:27Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji, 2839:28 Law 6:10; 8:2; Kut 28:39, 42; Eze 44:17, 18na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri. 29Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

3039:30 Isa 23:18; Zek 14:20; Za 93:5; Isa 23:18Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana. 31Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Mose Akagua Maskani Ya Mungu

(Kutoka 35:10-19)

3239:32 Kut 25:9; 25:40Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose. 3339:33 Kut 25:8-40; 36:10-16; Ebr 9:1-28Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake; 34kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo,39:34 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. pazia la kufunikia; 3539:35 Kut 30:6; 37:1Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema, 3639:36 Kut 25:23-30; 37:10-16meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho; 3739:37 Kut 25:31-39; 25:6; Ufu 1:13-20; Mt 5:14; Flp 2:15kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa; 3839:38 Kut 31:1-10; 37:25-28; 30:22-32; 37:29; 30:34-38; 36:35madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema; 3939:39 Kut 37:1-8; 38:1-7; 30:18madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake; 4039:40 Kut 27:9-19; 38:9-20; Ufu 3:12mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania; 41na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.

4239:42 Kut 25:9Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose. 4339:43 Kut 25:9; 35:10; Mwa 31:55; Law 9:22-23; Hes 6:23-27; Kum 26:15; 2Sam 6:18; 1Fal 8:14, 55; 1Nya 16:2; 2Nya 30:27Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.

Swedish Contemporary Bible

2 Moseboken 39:1-43

Prästernas dräkter

(2 Mos 28:1-43)

1Man gjorde heliga kläder åt Aron av blått, purpurrött och karmosinrött garn för tjänsten i helgedomen, så som Herren hade befallt Mose. 2Efoden gjordes av blått, purpurrött, karmosinrött och tvinnat fint lingarn. 3Man hamrade ut guld till tunna plåtar, som man skar i trådar och vävde in med det blåa, purpurröda, karmosinröda och fina lingarnet till en konstvävnad.

4De gjorde axelstycken till efoden, som skulle fästas i dess båda kanter för att hålla ihop den. 5Efodens bälte vävdes i ett stycke på samma sätt i guld, blått, purpurrött, karmosinrött och tvinnat fint lingarn, så som Herren hade befallt Mose. 6Onyxstenarna var infattade i flätverk av guld, med namnen på Israels söner ingraverade, som på ett sigill. 7Dessa stenar fästes på efodens axelstycken som en påminnelse om Israels söner, så som Herren hade befallt Mose.

8Bröstskölden gjordes också i konstvävnad, precis som efoden, av guld, blått, purpurrött, karmosinrött och tvinnat fint lingarn. 9Den var fyrkantig, 25 centimeter bred, 25 centimeter lång och dubbelvikt. 10I den sattes fyra rader stenar, i den första en karneol, en topas och en smaragd, 11i den andra en rubin, en safir och en kalcedon, 12i den tredje en hyacint, en agat och en ametist, 13och i den fjärde en krysolit, en onyx och en jaspis. De var infattade i flätverk av guld. 14I de tolv stenarna var namnen på Israels tolv söner ingraverade, som på sigill, en för varje stam.

15Till bröstskölden gjordes kedjor av rent guld, tvinnade som snören, 16och två flätverk av guld och två guldringar som fästes vid två hörn i bröstskölden. 17De två guldsnoddarna fäste de vid de två ringarna i bröstsköldens hörn 18och de två andra ändarna av snoddarna vid de två flätverken på framsidan i axelstyckena. 19Två guldringar gjordes och sattes fast på bröstsköldens nedre hörn, på insidan närmast efoden. 20De gjorde sedan två andra guldringar som de fäste framtill på efodens axelstycken, längst ner vid sömmen ovanför bältet. 21Bröstskölden bands fast vid sina ringar till efodens ringar med ett blått snöre, så att den satt ovanför efodens bälte och inte skulle lossna från efoden. Så hade Herren befallt Mose.

22Efodkåpan gjordes helt av blått tyg, 23med en öppning i mitten för huvudet, med en krage, för att tyget inte skulle gå sönder. 24Runt fållen fäste man granatäpplen, som var gjorda av blått, purpurrött och karmosinrött tvinnat garn. 25Av rent guld gjorde de bjällror som sattes mellan granatäpplena runt fållen, 26ett granatäpple och en bjällra växelvis runt fållen på kåpan. Denna kåpa skulle bäras vid tjänstgöring så som Herren hade befallt Mose.

27De gjorde tunikor åt Aron och hans söner av fint lingarn. 28Turbanen, huvudbonaderna och underkläderna vävdes alla av fint lingarn, 29likaså vävdes bältet i brokig väv av tvinnat fint lingarn, blått, purpurrött och karmosinrött, så som Herren hade befallt Mose. 30Sedan gjorde de plattan och det heliga diademet av rent guld och graverade in, som man graverar i ett sigill, ”Helgad åt Herren”. 31Man fäste ett blått snöre på den och satte den upptill på turbanen, så som Herren hade befallt Mose.

32Slutligen var allt arbete med boningen, uppenbarelsetältet, färdigt. Israeliterna gjorde allting som Herren befallt Mose.

Mose inspekterar arbetet

(2 Mos 35:10-19)

33Sedan förde man fram hela tältet till Mose: boningen och allt som tillhörde det, hakarna, brädorna, tvärstängerna, stolparna, socklarna, 34överdraget av rödfärgade baggskinn, överdraget av delfinskinn och det skyddande förhänget, 35arken med förbundstecknet, stänger, försoningsstället, 36bordet med dess tillbehör, skådebröden, 37lampstället av rent guld med dess lampor, tillbehör och olja, 38guldaltaret, smörjelseoljan, den välluktande rökelsen, förhänget för ingången till tältet, 39kopparaltaret, kopparnätet, bärstängerna och alla övriga tillbehör, tvättfatet med dess ställning, 40förhängena till förgården, stolparna och deras socklar, förhänget till förgårdens port, linorna och pluggarna och alla redskap som behövs för tjänsten i boningen, i uppenbarelsetältet, 41de vävda dräkterna för helgedomstjänsten, prästen Arons heliga kläder och hans söners prästkläder.

42Israels folk hade utfört allt arbete så som Herren befallt Mose. 43Mose inspekterade allt arbete de utfört och såg att allt var gjort som Herren hade befallt, och han välsignade dem.