Kutoka 39 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 39:1-43

Mavazi Ya Kikuhani

(Kutoka 28:1-14)

139:1 Kut 35:19-23; 28:2; Za 93:5; Eze 43Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Kisibau

239:2 Kut 28:6; Law 8:7Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri. 3Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi. 439:4 Law 24:7; Yos 4:7Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau. 539:5 Isa 11:5; Ufu 1:13Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

639:6 Kut 28:9; Ay 28:16; Isa 49:16; Ufu 1:17Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa. 739:7 Law 24:7; Yos 4:7; Kut 28:12; Yos 4:7; Neh 2:20Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Kifuko Cha Kifuani

(Kutoka 28:15-30)

839:8 Law 8:8; Kut 28:15; Isa 59:17Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa. 9Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja39:9 Shibiri moja ni sawa na sentimita 22. na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili. 1039:10 Kut 28:17; Eze 28:13; Ufu 21:19, 20; Isa 54:12Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi; 1139:11 Ufu 4:3; Isa 54:11; Yer 17:1safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi; 12safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto; 1339:13 Dan 10:6; Ay 28:16; Ufu 21:11katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu. 1439:14 Ufu 21:12Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.

15Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba. 16Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani. 17Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani, 18nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele. 19Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau. 20Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau. 21Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Mavazi Mengine Ya Kikuhani

(Kutoka 28:31-43)

2239:22 Kut 28:31; Law 8:7; 1Sam 2:18; 2Sam 6:14Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji, 23na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike. 24Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho. 2539:25 Kut 28:33Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga. 26Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

2739:27 Kut 28:39, 40; 39:27; Law 8:13; Kut 28:4; Isa 61:10; Rum 3:22; Gal 3:27Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji, 2839:28 Law 6:10; 8:2; Kut 28:39, 42; Eze 44:17, 18na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri. 29Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

3039:30 Isa 23:18; Zek 14:20; Za 93:5; Isa 23:18Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana. 31Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Mose Akagua Maskani Ya Mungu

(Kutoka 35:10-19)

3239:32 Kut 25:9; 25:40Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose. 3339:33 Kut 25:8-40; 36:10-16; Ebr 9:1-28Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake; 34kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo,39:34 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. pazia la kufunikia; 3539:35 Kut 30:6; 37:1Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema, 3639:36 Kut 25:23-30; 37:10-16meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho; 3739:37 Kut 25:31-39; 25:6; Ufu 1:13-20; Mt 5:14; Flp 2:15kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa; 3839:38 Kut 31:1-10; 37:25-28; 30:22-32; 37:29; 30:34-38; 36:35madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema; 3939:39 Kut 37:1-8; 38:1-7; 30:18madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake; 4039:40 Kut 27:9-19; 38:9-20; Ufu 3:12mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania; 41na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.

4239:42 Kut 25:9Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose. 4339:43 Kut 25:9; 35:10; Mwa 31:55; Law 9:22-23; Hes 6:23-27; Kum 26:15; 2Sam 6:18; 1Fal 8:14, 55; 1Nya 16:2; 2Nya 30:27Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.

New International Version – UK

Exodus 39:1-43

The priestly garments

1From the blue, purple and scarlet yarn they made woven garments for ministering in the sanctuary. They also made sacred garments for Aaron, as the Lord commanded Moses.

The ephod

2They39:2 Or He; also in verses 7, 8 and 22 made the ephod of gold, and of blue, purple and scarlet yarn, and of finely twisted linen. 3They hammered out thin sheets of gold and cut strands to be worked into the blue, purple and scarlet yarn and fine linen – the work of skilled hands. 4They made shoulder pieces for the ephod, which were attached to two of its corners, so that it could be fastened. 5Its skilfully woven waistband was like it – of one piece with the ephod and made with gold, and with blue, purple and scarlet yarn, and with finely twisted linen, as the Lord commanded Moses.

6They mounted the onyx stones in gold filigree settings and engraved them like a seal with the names of the sons of Israel. 7Then they fastened them on the shoulder pieces of the ephod as memorial stones for the sons of Israel, as the Lord commanded Moses.

The breastpiece

8They fashioned the breastpiece – the work of a skilled craftsman. They made it like the ephod: of gold, and of blue, purple and scarlet yarn, and of finely twisted linen. 9It was square – a span39:9 That is, about 23 centimetres long and a span wide – and folded double. 10Then they mounted four rows of precious stones on it. The first row was carnelian, chrysolite and beryl; 11the second row was turquoise, lapis lazuli and emerald; 12the third row was jacinth, agate and amethyst; 13the fourth row was topaz, onyx and jasper.39:13 The precise identification of some of these precious stones is uncertain. They were mounted in gold filigree settings. 14There were twelve stones, one for each of the names of the sons of Israel, each engraved like a seal with the name of one of the twelve tribes.

15For the breastpiece they made braided chains of pure gold, like a rope. 16They made two gold filigree settings and two gold rings, and fastened the rings to two of the corners of the breastpiece. 17They fastened the two gold chains to the rings at the corners of the breastpiece, 18and the other ends of the chains to the two settings, attaching them to the shoulder pieces of the ephod at the front. 19They made two gold rings and attached them to the other two corners of the breastpiece on the inside edge next to the ephod. 20Then they made two more gold rings and attached them to the bottom of the shoulder pieces on the front of the ephod, close to the seam just above the waistband of the ephod. 21They tied the rings of the breastpiece to the rings of the ephod with blue cord, connecting it to the waistband so that the breastpiece would not swing out from the ephod – as the Lord commanded Moses.

Other priestly garments

22They made the robe of the ephod entirely of blue cloth – the work of a weaver – 23with an opening in the centre of the robe like the opening of a collar,39:23 The meaning of the Hebrew for this word is uncertain. and a band around this opening, so that it would not tear. 24They made pomegranates of blue, purple and scarlet yarn and finely twisted linen round the hem of the robe. 25And they made bells of pure gold and attached them around the hem between the pomegranates. 26The bells and pomegranates alternated round the hem of the robe to be worn for ministering, as the Lord commanded Moses.

27For Aaron and his sons, they made tunics of fine linen – the work of a weaver – 28and the turban of fine linen, the linen caps and the undergarments of finely twisted linen. 29The sash was made of finely twisted linen and blue, purple and scarlet yarn – the work of an embroiderer – as the Lord commanded Moses.

30They made the plate, the sacred emblem, out of pure gold and engraved on it, like an inscription on a seal:

Holy to the Lord.

31Then they fastened a blue cord to it to attach it to the turban, as the Lord commanded Moses.

Moses inspects the tabernacle

32So all the work on the tabernacle, the tent of meeting, was completed. The Israelites did everything just as the Lord commanded Moses. 33Then they brought the tabernacle to Moses:

the tent and all its furnishings, its clasps, frames, crossbars, posts and bases;

34the covering of ram skins dyed red and the covering of another durable leather39:34 Possibly the hides of large aquatic mammals and the shielding curtain;

35the ark of the covenant law with its poles and the atonement cover;

36the table with all its articles and the bread of the Presence;

37the pure gold lampstand with its row of lamps and all its accessories, and the olive oil for the light;

38the gold altar, the anointing oil, the fragrant incense, and the curtain for the entrance to the tent;

39the bronze altar with its bronze grating, its poles and all its utensils;

the basin with its stand;

40the curtains of the courtyard with its posts and bases, and the curtain for the entrance to the courtyard;

the ropes and tent pegs for the courtyard;

all the furnishings for the tabernacle, the tent of meeting;

41and the woven garments worn for ministering in the sanctuary, both the sacred garments for Aaron the priest and the garments for his sons when serving as priests.

42The Israelites had done all the work just as the Lord had commanded Moses. 43Moses inspected the work and saw that they had done it just as the Lord had commanded. So Moses blessed them.