Kutoka 39 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 39:1-43

Mavazi Ya Kikuhani

(Kutoka 28:1-14)

139:1 Kut 35:19-23; 28:2; Za 93:5; Eze 43Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Kisibau

239:2 Kut 28:6; Law 8:7Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri. 3Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi. 439:4 Law 24:7; Yos 4:7Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau. 539:5 Isa 11:5; Ufu 1:13Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

639:6 Kut 28:9; Ay 28:16; Isa 49:16; Ufu 1:17Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa. 739:7 Law 24:7; Yos 4:7; Kut 28:12; Yos 4:7; Neh 2:20Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Kifuko Cha Kifuani

(Kutoka 28:15-30)

839:8 Law 8:8; Kut 28:15; Isa 59:17Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa. 9Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja39:9 Shibiri moja ni sawa na sentimita 22. na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili. 1039:10 Kut 28:17; Eze 28:13; Ufu 21:19, 20; Isa 54:12Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi; 1139:11 Ufu 4:3; Isa 54:11; Yer 17:1safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi; 12safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto; 1339:13 Dan 10:6; Ay 28:16; Ufu 21:11katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu. 1439:14 Ufu 21:12Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.

15Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba. 16Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani. 17Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani, 18nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele. 19Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau. 20Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau. 21Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Mavazi Mengine Ya Kikuhani

(Kutoka 28:31-43)

2239:22 Kut 28:31; Law 8:7; 1Sam 2:18; 2Sam 6:14Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji, 23na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike. 24Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho. 2539:25 Kut 28:33Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga. 26Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

2739:27 Kut 28:39, 40; 39:27; Law 8:13; Kut 28:4; Isa 61:10; Rum 3:22; Gal 3:27Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji, 2839:28 Law 6:10; 8:2; Kut 28:39, 42; Eze 44:17, 18na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri. 29Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

3039:30 Isa 23:18; Zek 14:20; Za 93:5; Isa 23:18Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana. 31Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Mose Akagua Maskani Ya Mungu

(Kutoka 35:10-19)

3239:32 Kut 25:9; 25:40Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose. 3339:33 Kut 25:8-40; 36:10-16; Ebr 9:1-28Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake; 34kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo,39:34 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. pazia la kufunikia; 3539:35 Kut 30:6; 37:1Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema, 3639:36 Kut 25:23-30; 37:10-16meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho; 3739:37 Kut 25:31-39; 25:6; Ufu 1:13-20; Mt 5:14; Flp 2:15kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa; 3839:38 Kut 31:1-10; 37:25-28; 30:22-32; 37:29; 30:34-38; 36:35madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema; 3939:39 Kut 37:1-8; 38:1-7; 30:18madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake; 4039:40 Kut 27:9-19; 38:9-20; Ufu 3:12mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania; 41na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.

4239:42 Kut 25:9Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose. 4339:43 Kut 25:9; 35:10; Mwa 31:55; Law 9:22-23; Hes 6:23-27; Kum 26:15; 2Sam 6:18; 1Fal 8:14, 55; 1Nya 16:2; 2Nya 30:27Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.

New International Reader’s Version

Exodus 39:1-43

The Clothes for the Priests

1The workers made clothes from the blue, purple and bright red yarn. The clothes were worn by the priests who served in the holy tent. The workers also made sacred clothes for Aaron. They made them just as the Lord had commanded Moses.

The Linen Apron

2The workers made the linen apron. They made it out of thin gold wire, and of blue, purple and bright red yarn, and of finely twisted linen. 3They hammered out thin sheets of gold. They cut it into thin wire. Then they sewed it into the blue, purple and bright red yarn and fine linen. Skilled workers made it. 4The workers made shoulder straps for the apron. The straps were joined to two of its corners. 5Its skillfully made waistband was made like the apron. The waistband was part of the apron itself. It was made out of thin gold wire, and out of blue, purple and bright red yarn, and out of finely twisted linen. The workers made it just as the Lord had commanded Moses.

6They put the onyx stones in fancy gold settings. They carved the names of the sons of Israel on the stones. They did it the way a jewel cutter would carve them. 7Then they connected them to the shoulder straps of the linen apron. The stones stood for the sons of Israel and were a constant reminder for them. The workers did those things just as the Lord had commanded Moses.

The Chest Cloth

8Skilled workers made the chest cloth. They made it like the linen apron. They used thin gold wire, and blue, purple and bright red yarn, and finely twisted linen. 9The chest cloth was nine inches square. It was folded in half. 10The workers put four rows of valuable jewels on it. Carnelian, chrysolite and beryl were in the first row. 11Turquoise, lapis lazuli and emerald were in the second row. 12Jacinth, agate and amethyst were in the third row. 13And topaz, onyx and jasper were in the fourth row. The workers put them in fancy gold settings. 14They used a total of 12 stones. There was one stone for each of the names of the sons of Israel. Each stone was carved with the name of one of the 12 tribes.

15The workers made braided chains out of pure gold for the chest cloth. They made them like ropes. 16They made two fancy gold settings and two gold rings. They connected them to two corners of the chest cloth. 17They joined the two gold chains to the rings at the corners of the chest cloth. 18They joined the other ends of the chains to the two settings. They joined them to the shoulder straps on the front of the linen apron. 19The workers made two gold rings. They connected them to the other two corners of the chest cloth. They put them on the inside edge next to the apron. 20Then they made two more gold rings. They connected them to the bottom of the shoulder straps on the front of the apron. They put them close to the seam. They put them right above the waistband of the apron. 21They tied the rings of the chest cloth to the rings of the apron with blue cord. That connected it to the waistband. Then the chest cloth would not swing out from the linen apron. The workers did those things just as the Lord had commanded Moses.

More Clothes for the Priests

22The workers made the outer robe of the linen apron completely out of blue cloth. The cloth was made by a skillful person. 23The workers made an opening in the center of the robe. They made an edge like a collar around the opening. Then it couldn’t tear. 24They made pomegranates out of blue, purple and bright red yarn and finely twisted linen. They sewed them around the hem of the robe. 25They made bells out of pure gold. They sewed them around the hem between the pomegranates. 26They sewed a bell between every two pomegranates all around the hem of the robe. Aaron had to wear the robe when he served as priest. That’s what the Lord commanded Moses.

27The workers made inner robes out of fine linen for Aaron and his sons. The linen cloth was made by a skillful person. 28The workers also made the turban out of fine linen. And they made the caps and the underwear out of finely twisted linen. 29The belt was made out of finely twisted linen and blue, purple and bright red yarn. A person who sewed skillfully made it. The workers did those things just as the Lord had commanded Moses.

30They made the plate out of pure gold. It was a sacred crown. On the plate, they carved the words

Set Apart for the Lord.

31Then they tied the plate to the turban with a blue cord. They did those things just as the Lord had commanded Moses.

The Holy Tent Is Completed

32So all the work on the holy tent, the tent of meeting, was completed. The Israelites did everything just as the Lord had commanded Moses. 33Then they brought the holy tent to Moses along with everything that belonged to it. Here are the things they brought:

hooks, frames, crossbars, posts and bases

34the covering of ram skins dyed red, the covering of another kind of strong leather and the curtain that hides the ark

35the ark where the tablets of the covenant law are kept, the poles and the cover for the ark

36the table for the holy bread with all its things and the holy bread

37the pure gold lampstand with its row of lamps and everything used with it, and the olive oil that gives light

38the gold altar for burning incense, the anointing oil and the sweet-smelling incense

the curtain for the entrance to the tent

39the bronze altar for burnt offerings with its bronze grate, its poles and all its tools

the large bowl with its stand

40the curtains of the courtyard with their posts and bases, and the curtain for the entrance to the courtyard

the ropes and tent stakes for the courtyard

everything that belongs to the holy tent, the tent of meeting

41and the sacred clothes for Aaron the priest and the clothes for his sons when they serve as priests

42The Israelites had done all the work just as the Lord had commanded Moses. 43Moses looked over the work carefully. He saw that the workers had done it just as the Lord had commanded. So Moses gave them his blessing.