Kutoka 38 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 38:1-31

Madhabahu Ya Sadaka Ya Kuteketezwa

(Kutoka 27:1-8)

138:1 Kut 27:1; 2Nya 29:23, 24; Za 51:15-19; Isa 61:8; Eze 44:11; 45:17; Ebr 9:14; 13:10Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu;38:1 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano38:1 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. 238:2 2Nya 1:5; 1Fal 7:45Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba. 338:3 Kut 31:9; 35:16Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto. 4Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu. 5Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba. 6Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba. 7Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.

Sinia La Kunawia

(Kutoka 30:18)

838:8 Kut 30:18; 40:7; Kum 23:17; 1Sam 2:22; 1Fal 14:24; 2Fal 16:17; 2Nya 4:2; Za 26:6; Zek 13:1; Eze 36:25; 2Kor 7:1; Ebr 10:22; 1Yn 5:6Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.

Ua Wa Hema La Kukutania

(Kutoka 27:9-19)

938:9 Kut 27:9; Za 84:2; 92:13Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja,38:9 Dhiraa 100 ni sawa na mita 45. na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri, 10pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 11Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.

12Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini38:12 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 13Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini. 14Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano38:14 Dhiraa 15 ni sawa na mita 6.75. yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 15Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 16Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri. 17Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.

1838:18 2Nya 3:14Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano, 19likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha. 2038:20 Kut 35:18; 38:20; 27:10; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.

Vifaa Vilivyotumika

2138:21 Hes 1:50-53; 8:24; 9:15; 10:11; 17:7; 1Nya 23:32; 2Nya 24:6; Mdo 7:44; Ufu 15:5; Hes 4:28-33Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni. 2238:22 Kut 31:2(Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose, 2338:23 Kut 31:6akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.) 2438:24 Kut 30:12-16; 12:37; Hes 3:47Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730,38:24 Talanta 29 na shekeli 730 ni sawa na tani moja. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.

2538:25 Kut 12:37; 30:12Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775,38:25 Talanta 100 na shekeli 1,775 za fedha ni sawa na tani 3.4. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 2638:26 Kut 30:12-16; 12:36-37; Hes 1:46Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550. 2738:27 Kut 26:19Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako. 28Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.

29Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.38:29 Talanta 70 na shekeli 2,400 ni sawa na tani 2.4. 30Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote, 3138:31 Kut 27:19; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.

Persian Contemporary Bible

خروج 38:1-31

ساختن قربانگاه برای قربانيهای سوختنی

(خروج 27‏:1‏-8)

1قربانگاه قربانی سوختنی نيز با چوب اقاقيا به شكل چهارگوش ساخته شد. هر ضلع آن دو و نيم متر و بلنديش يک و نيم متر بود. 2آن را طوری ساخت كه در چهار گوشه‌اش چهار زائده به شكل شاخ بود. تمام قربانگاه و شاخها روكشی از مفرغ داشت. 3لوازم آن كه شامل سطلها، خاک‌اندازها، كاسه‌ها، چنگكها و آتشدانها بود، همگی از مفرغ ساخته شد. 4‏-5يک منقل مشبک مفرغی كه در هر گوشهٔ آن يک حلقهٔ فلزی بود، برای قربانگاه ساخت و آن را تا نيمهٔ قربانگاه فرو برد تا روی لبه‌ای كه در آنجا وجود داشت قرار گيرد. 6‏-7برای جابه‌جا كردن قربانگاه چوبهايی از درخت اقاقيا با روكش مفرغ ساخت و چوبها را در حلقه‌هايی كه در دو طرف قربانگاه نصب شده بود، فرو كرد. قربانگاه، درونش خالی بود و از تخته ساخته شده بود.

ساختن حوض مفرغی

(خروج 30‏:18)

8حوض مفرغی و پايهٔ مفرغی‌اش را از آيينه‌های زنانی كه در كنار در خيمه خدمت می‌كردند، ساخت.

حياط خيمهٔ عبادت

(خروج 27‏:9‏-19)

9بعد بصل‌ئيل برای عبادتگاه حياطی درست كرد كه ديوارهايش از پرده‌های كتان لطيف ريزبافت بود. طول پرده‌های سمت جنوب پنجاه متر بود. 10بيست ستون مفرغی برای پرده‌ها ساخت و برای اين ستونها پايه‌های مفرغی و قلابها و پشت‌بندهای نقره‌ای درست كرد. 11برای سمت شمالی حياط نيز همين كار را كرد. 12طول ديوار پرده‌ای سمت غربی بيست و پنج متر بود. ده ستون با ده پايه برای پرده‌ها ساخت و برای هر يک از اين ستونها قلابها و پشت‌بندهای نقره‌ای درست كرد. 13طول ديوار پرده‌ای سمت شرقی هم بيست و پنج متر بود. 14‏-15پرده‌های هر طرف در ورودی هفت و نيم متر بود. برای نگاه داشتن اين پرده‌ها هم سه ستون و سه پايه در هر طرف ساخت. 16تمام پرده‌های ديوار حياط خيمه از كتان لطيف ریز‌بافت بود. 17پايه‌های ستونها از مفرغ، و قلابها و پشت‌بندها و روكش سر ستونها از نقره بود. تمام ستونهای اطراف حياط با پشت‌بندهای نقره‌ای به هم مربوط شدند.

18پردهٔ در ورودی خيمه از كتان لطيف ريزبافت تهيه گرديد و با نخهای آبی، ارغوانی و قرمز گلدوزی شد. طول اين پرده ده متر و بلنديش مانند پرده‌های ديوار حياط، دو و نيم متر بود. 19چهار ستون برای پرده ساخت. پايه‌های ستونها از مفرغ، و قلابها و پشت‌بندها و روكش سر ستونها از نقره بود.

20تمام ميخهايی كه در بنای خيمه و حياط آن به کار رفت، از مفرغ بود.

مقدار فلزی كه در عبادتگاه به کار رفت

21اين است صورت مقدار فلزی كه در ساختن خيمهٔ عبادت به کار رفت. اين صورت به دستور موسی، بوسيلهٔ لاویان و زير نظر ايتامار پسر هارون كاهن تهيه شد. 22(بصل‌ئيل پسر اوری و نوهٔ حور از قبيلهٔ يهودا، آنچه را كه خداوند به موسی دستور داده بود، ساخت. 23دستيار او در اين كار اهولياب پسر اخيسامک از قبيلهٔ دان بود كه در كار طراحی، نساجی و طرازی پارچه‌های آبی، ارغوانی، قرمز و كتان لطيف مهارت داشت.)

24بنی‌اسرائيل جمعاً حدود هزار كيلوگرم طلا هديه كردند كه تمام آن صرف ساختن عبادتگاه شد.

25‏-26مقدار نقرهٔ مصرف شده حدود سه هزار و چهارصد و سی كيلوگرم بود. اين مقدار نقره از ۶۰۳,۵۵۰ نفر دريافت شده بود كه اسامی‌شان در سرشماری نوشته شده و سنشان بيست سال به بالا بود. هر يک از اين افراد حدود شش گرم نقره هديه داده بودند. 27برای پايه‌های چوب‌بست خيمهٔ عبادت و پايه‌های ستونهای پردهٔ داخل آن، سه هزار و چهارصد كيلوگرم نقره مصرف شد، يعنی برای هر پايه سی و چهار كيلوگرم. 28باقی ماندهٔ نقره كه سی كيلوگرم بود برای قلابهای ستونها، پشت‌بندها و روكش سر ستونها مصرف شد.

29‏-31بنی‌اسرائيل دو هزار و چهارصد و بيست و پنج كيلوگرم مفرغ هديه آوردند. اين مقدار مفرغ برای پايه‌های ستونهای در ورودی خيمه، قربانگاه مفرغی، منقل مشبک و ساير لوازم قربانگاه، همچنين برای پايه‌های ستونهای دور حياط و پايه‌های در ورودی آن، و نيز برای ميخهای خيمه و پرده‌های دور حياط به کار رفت.