Kutoka 38 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 38:1-31

Madhabahu Ya Sadaka Ya Kuteketezwa

(Kutoka 27:1-8)

138:1 Kut 27:1; 2Nya 29:23, 24; Za 51:15-19; Isa 61:8; Eze 44:11; 45:17; Ebr 9:14; 13:10Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu;38:1 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano38:1 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. 238:2 2Nya 1:5; 1Fal 7:45Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba. 338:3 Kut 31:9; 35:16Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto. 4Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu. 5Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba. 6Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba. 7Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.

Sinia La Kunawia

(Kutoka 30:18)

838:8 Kut 30:18; 40:7; Kum 23:17; 1Sam 2:22; 1Fal 14:24; 2Fal 16:17; 2Nya 4:2; Za 26:6; Zek 13:1; Eze 36:25; 2Kor 7:1; Ebr 10:22; 1Yn 5:6Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.

Ua Wa Hema La Kukutania

(Kutoka 27:9-19)

938:9 Kut 27:9; Za 84:2; 92:13Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja,38:9 Dhiraa 100 ni sawa na mita 45. na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri, 10pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 11Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.

12Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini38:12 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 13Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini. 14Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano38:14 Dhiraa 15 ni sawa na mita 6.75. yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 15Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 16Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri. 17Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.

1838:18 2Nya 3:14Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano, 19likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha. 2038:20 Kut 35:18; 38:20; 27:10; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.

Vifaa Vilivyotumika

2138:21 Hes 1:50-53; 8:24; 9:15; 10:11; 17:7; 1Nya 23:32; 2Nya 24:6; Mdo 7:44; Ufu 15:5; Hes 4:28-33Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni. 2238:22 Kut 31:2(Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose, 2338:23 Kut 31:6akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.) 2438:24 Kut 30:12-16; 12:37; Hes 3:47Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730,38:24 Talanta 29 na shekeli 730 ni sawa na tani moja. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.

2538:25 Kut 12:37; 30:12Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775,38:25 Talanta 100 na shekeli 1,775 za fedha ni sawa na tani 3.4. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 2638:26 Kut 30:12-16; 12:36-37; Hes 1:46Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550. 2738:27 Kut 26:19Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako. 28Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.

29Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.38:29 Talanta 70 na shekeli 2,400 ni sawa na tani 2.4. 30Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote, 3138:31 Kut 27:19; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.

O Livro

Êxodo 38:1-31

O altar do holocausto

(Êx 27.1-8)

1O altar dos holocaustos, foi igualmente construído em madeira de acácia, quadrado, com 2,5 metros de lado e 1,5 metros de altura. 2Tinha quatro chifres em cada canto, tudo de uma só peça com o resto. Este altar foi revestido de bronze. 3Depois fez em bronze os utensílios a serem usados no serviço do altar: as caldeiras, as pás, as bacias, os garfos e os braseiros. 4Seguidamente, fez uma grelha de bronze que ficou apoiada numa cercadura, na parte inferior, a meia altura. 5Foram feitas ainda quatro argolas para cada lado da grelha, para nelas se porem as varas para o transporte. 6Estas varas eram feitas de madeira de acácia, revestidas de bronze. 7Pôs também duas varas nas argolas nos lados do altar, a fim de ser transportado. Este altar, feito de pranchas, era oco por dentro.

A bacia de bronze

(Êx 30.18)

8A bacia de bronze e o seu pé, da mesma liga, foi feita com os espelhos das mulheres que se juntaram à entrada da tenda do encontro.

O pátio

(Êx 27.9-19)

9Em seguida, foi a vez do pátio. A parede do sul tinha 50 metros de comprimento e consistia em véus de linho fino retorcido. 10Havia vinte postes, para manter os véus, que assentavam em bases de bronze e tinham ganchos e hastes de prata. 11A parede no norte media, da mesma forma, 50 metros, com vinte colunas e bases de bronze, e também ganchos e hastes de prata. 12O lado ocidental ficou com 25 metros. Os véus foram suspensos em dez postes, com as suas bases, e com ganchos e hastes de prata. 13O lado oriental tinha igualmente 25 metros.

14-15Os véus de ambos os lados da entrada tinham 7,5 metros de comprimento com três postes e três bases. 16Todos os véus que formavam as paredes do pátio eram tecidos com linho fino retorcido. 17Cada poste tinha uma base de bronze e todos os ganchos e hastes foram feitos de prata maciça.

18Os véus da entrada do pátio foram feitos também em linho fino retorcido, artisticamente bordados em azul, púrpura e vermelho. Tinha essa entrada 10 metros de comprimento e 2,5 metros de altura, a largura do tecido, tal como a parede do pátio. 19Os véus desta porta eram sustentados por quatro colunas com quatro bases de bronze e com ganchos e hastes de prata. Os cimos dos postes eram de prata.

20Todas as estacas, tanto do tabernáculo como do pátio, eram de bronze.

Os materiais utilizados

21Esta é a enumeração do material empregado na construção do tabernáculo da aliança, registada por ordem de Moisés pelos levitas, sob direção de Itamar, filho de Aarão, o sacerdote. 22Bezalel, filho de Uri e neto de Hur, da tribo de Judá, executou tudo o que o Senhor tinha ordenado a Moisés; 23foi assistido por Aoliabe, filho de Aisamaque da tribo de Dan, que também era um hábil artífice e perito em trabalhos de gravação, de tecelagem e bordados em azul, púrpura e vermelho, e em tecidos de linho fino.

24Os donativos que o povo trouxe ascenderam a 1000 quilos de ouro; todo ele foi usado no tabernáculo.

25O montante da prata recolhida foi de mais de 3600 quilos, segundo o peso oficial do santuário, 26que vieram da taxa paga de 6 gramas de prata por todos os que estavam registados, segundo o censo do povo, de 20 anos para cima, num total de 603 550 homens. 27As bases para as tábuas das paredes do santuário e para os postes que sustentavam o véu requereram 3500 quilos de prata, ou seja, 34 quilos por cada base. 28O resto da prata foi usada nos postes e no revestimento dos seus cimos, assim como nos ganchos e hastes.

29O povo trouxe mais de 2500 quilos de bronze 30que foi usado na fundição das bases dos postes da entrada da tenda do encontro e na construção do altar de bronze, na sua grelha e seus utensílios, 31nas bases das colunas que suportam os véus da entrada do pátio e nas estacas usadas na montagem do tabernáculo e do pátio.