Kutoka 38 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 38:1-31

Madhabahu Ya Sadaka Ya Kuteketezwa

(Kutoka 27:1-8)

138:1 Kut 27:1; 2Nya 29:23, 24; Za 51:15-19; Isa 61:8; Eze 44:11; 45:17; Ebr 9:14; 13:10Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu;38:1 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano38:1 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. 238:2 2Nya 1:5; 1Fal 7:45Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba. 338:3 Kut 31:9; 35:16Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto. 4Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu. 5Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba. 6Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba. 7Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.

Sinia La Kunawia

(Kutoka 30:18)

838:8 Kut 30:18; 40:7; Kum 23:17; 1Sam 2:22; 1Fal 14:24; 2Fal 16:17; 2Nya 4:2; Za 26:6; Zek 13:1; Eze 36:25; 2Kor 7:1; Ebr 10:22; 1Yn 5:6Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.

Ua Wa Hema La Kukutania

(Kutoka 27:9-19)

938:9 Kut 27:9; Za 84:2; 92:13Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja,38:9 Dhiraa 100 ni sawa na mita 45. na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri, 10pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 11Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.

12Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini38:12 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 13Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini. 14Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano38:14 Dhiraa 15 ni sawa na mita 6.75. yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 15Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 16Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri. 17Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.

1838:18 2Nya 3:14Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano, 19likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha. 2038:20 Kut 35:18; 38:20; 27:10; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.

Vifaa Vilivyotumika

2138:21 Hes 1:50-53; 8:24; 9:15; 10:11; 17:7; 1Nya 23:32; 2Nya 24:6; Mdo 7:44; Ufu 15:5; Hes 4:28-33Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni. 2238:22 Kut 31:2(Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose, 2338:23 Kut 31:6akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.) 2438:24 Kut 30:12-16; 12:37; Hes 3:47Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730,38:24 Talanta 29 na shekeli 730 ni sawa na tani moja. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.

2538:25 Kut 12:37; 30:12Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775,38:25 Talanta 100 na shekeli 1,775 za fedha ni sawa na tani 3.4. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 2638:26 Kut 30:12-16; 12:36-37; Hes 1:46Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550. 2738:27 Kut 26:19Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako. 28Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.

29Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.38:29 Talanta 70 na shekeli 2,400 ni sawa na tani 2.4. 30Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote, 3138:31 Kut 27:19; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.

Bibelen på hverdagsdansk

2. Mosebog 38:1-31

Brændofferalteret bygges

1Brændofferalteret blev også konstrueret af akacietræ. Det var 2,25 m langt, 2,25 m bredt og 1,35 m højt. 2Der blev lavet et horn i hvert af dets fire hjørner, ud i ét stykke med hjørnestolpen, og det hele blev belagt med bronze. 3Dernæst blev der lavet bronzeredskaber til brug ved alteret, bakker til at fjerne asken i, diverse skovle, stænkeskåle, kødgafler og bakker til gløder. 4Et bronzegitter blev lavet og anbragt udvendig under alterets pynteliste, så det nåede halvvejs op ad alteret. 5Ved gitterets fire hjørner blev der lavet fire ringe, hvor bærestængerne kunne stikkes ind. 6Bærestængerne blev lavet af akacietræ belagt med bronze 7og blev stukket gennem ringene på hver side af alteret, der var lavet som en hul trækasse.

8Vaskefadet af bronze med tilhørende bronzestativ blev lavet af bronzespejle, som var en gave fra de kvinder, der gjorde tjeneste ved åbenbaringsteltets indgang.

Indhegningen omkring forgården

9Derpå blev indhegningen omkring forgården lavet. Til sydsiden blev der lavet en 45 m lang stofvæg af fintvævet linned. 10Til at holde stofvæggen blev der lavet 20 stolper med dertil hørende bronzesokler, sølvkroge og sølvstænger. 11Nordvæggen var også 45 m lang med 20 stolper, bronzesokler, sølvkroge og sølvstænger. 12Vestsiden bestod af en 22,5 m lang stofvæg hængt op ved hjælp af sølvkroge og sølvstænger på ti stolper med dertil hørende bronzesokler. 13Østsiden med indgangen til boligen var ligeledes 22,5 m lang.

14På den ene side af indgangen blev der opsat tre stolper på hver sin sokkel og lavet en 6,75 m lang stofvæg, som blev hængt op på stolperne. 15Det samme blev der gjort på den anden side af indgangen. 16Stofvæggen rundt om forgården blev lavet af fintvævet linned. 17Hver stolpe stod på en bronzesokkel, mens krogene til stolperne og tværstængerne, som stoffet blev hængt op på, blev lavet af sølv. Stolpernes hoveder blev overtrukket med sølv.

18Stoffet til forhænget ved indgangen blev lavet af fintvævet linned med broderier i blåt, violet og purpurrødt garn. Det var 9 m langt og havde samme højde som resten af forgårdens vægge, nemlig 2,25 m, 19og blev ved hjælp af sølvkroge og sølvstænger hængt op på fire stolper med tilhørende bronzesokler. Stolpernes hoveder var af sølv, 20men samtlige teltpløkker, der blev brugt til boligen og til forgården, var af bronze.

Omfanget af de brugte materialer

21Her følger en rapport over arbejdet og en liste over de materialer, som blev brugt ved opførelsen af boligen, hvor pagtens ark fremover skulle have til huse. Moses gav levitterne opgaven med at holde regnskab over materialerne, og han udpegede Arons søn Itamar til at forestå det arbejde. 22Betzalel havde det overordnede ansvar for alt det arbejde, der blev udført. 23Han blev assisteret af Oholiab, som også var specielt dygtig til design, indgravering, vævning og broderi.

24Totalvægten af alt det guld, folket bragte, og som blev brugt til projektet, var næsten 900 kg.38,24 På hebraisk: 29 talenter og 730 shekel. En talent er 3000 shekel, og den, der her er brugt, menes at veje ca. 10 g. 25-26Af sølv blev der brugt over 3 tons,38,25-26 På hebraisk: 100 talenter og 1775 shekel, altså 301.775 shekel eller 3018 kg. hvilket svarede til den inddrevne personskat på alle registrerede personer over 20 år, nemlig ½ shekel sølv gange 603.550 personer. 27Sølvet blev brugt til at støbe de 100 sokler, der skulle bruges til vægmodulerne og til de stolper, der skulle bære forhænget foran det allerhelligste. Hver sokkel vejede ca. 30 kg.38,27 På hebraisk: en talent. 28Til sølvkrogene, stolpehovederne og tværstængerne gik der 18 kg38,28 På hebraisk: 1775 shekel. sølv.

29Den indkomne bronze beløb sig til lidt over 2 tons.38,29 På hebraisk: 70 talenter og 2400 shekel, dvs. ca. 2100 kg. 30Den blev brugt til soklerne ved åbenbaringsteltets indgang, til bronzealteret, gitterværket, alterredskaberne, 31soklerne under forgårdens vægge og samtlige teltpløkker.