Kutoka 38 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 38:1-31

Madhabahu Ya Sadaka Ya Kuteketezwa

(Kutoka 27:1-8)

138:1 Kut 27:1; 2Nya 29:23, 24; Za 51:15-19; Isa 61:8; Eze 44:11; 45:17; Ebr 9:14; 13:10Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu;38:1 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano38:1 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. 238:2 2Nya 1:5; 1Fal 7:45Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba. 338:3 Kut 31:9; 35:16Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto. 4Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu. 5Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba. 6Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba. 7Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.

Sinia La Kunawia

(Kutoka 30:18)

838:8 Kut 30:18; 40:7; Kum 23:17; 1Sam 2:22; 1Fal 14:24; 2Fal 16:17; 2Nya 4:2; Za 26:6; Zek 13:1; Eze 36:25; 2Kor 7:1; Ebr 10:22; 1Yn 5:6Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.

Ua Wa Hema La Kukutania

(Kutoka 27:9-19)

938:9 Kut 27:9; Za 84:2; 92:13Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja,38:9 Dhiraa 100 ni sawa na mita 45. na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri, 10pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 11Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.

12Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini38:12 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 13Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini. 14Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano38:14 Dhiraa 15 ni sawa na mita 6.75. yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 15Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 16Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri. 17Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.

1838:18 2Nya 3:14Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano, 19likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha. 2038:20 Kut 35:18; 38:20; 27:10; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.

Vifaa Vilivyotumika

2138:21 Hes 1:50-53; 8:24; 9:15; 10:11; 17:7; 1Nya 23:32; 2Nya 24:6; Mdo 7:44; Ufu 15:5; Hes 4:28-33Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni. 2238:22 Kut 31:2(Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose, 2338:23 Kut 31:6akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.) 2438:24 Kut 30:12-16; 12:37; Hes 3:47Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730,38:24 Talanta 29 na shekeli 730 ni sawa na tani moja. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.

2538:25 Kut 12:37; 30:12Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775,38:25 Talanta 100 na shekeli 1,775 za fedha ni sawa na tani 3.4. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 2638:26 Kut 30:12-16; 12:36-37; Hes 1:46Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550. 2738:27 Kut 26:19Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako. 28Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.

29Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.38:29 Talanta 70 na shekeli 2,400 ni sawa na tani 2.4. 30Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote, 3138:31 Kut 27:19; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.

La Bible du Semeur

Exode 38:1-31

L’autel des holocaustes et ses accessoires38.1 titre Pour les v. 1-7, voir 27.1-8. En hébreu, les mesures sont en coudées (une coudée = 50 cm).

1Betsaléel fit l’autel des holocaustes en bois d’acacia, carré, de deux mètres cinquante de côté, et d’un mètre cinquante de hauteur. 2A ses quatre angles, il fit quatre cornes en saillie de l’autel, et il le plaqua de bronze. 3Il fabriqua aussi en bronze tous les ustensiles de l’autel : les récipients destinés à recueillir les cendres, les pelles, les bassines, les fourchettes et les brasiers. 4Il munit l’autel d’une grille faite d’un treillis de bronze et la plaça sous la bordure de l’autel, depuis le bas jusqu’à mi-hauteur. 5Il fondit quatre anneaux qu’il fixa aux quatre coins de la grille de bronze pour recevoir les barres. 6Il fit des barres en bois d’acacia et les recouvrit de bronze. 7Il introduisit dans les anneaux sur les côtés de l’autel les barres qui devaient servir à le transporter ; il le fit avec des panneaux et l’autel était creux à l’intérieur.

La cuve de bronze38.8 Voir 30.17-21.

8Il fit aussi la cuve de bronze avec son socle de même métal en employant les miroirs des femmes qui s’assemblaient à l’entrée de la tente de la Rencontre.

Le parvis38.9 Pour les v. 9-20, voir 27.9-19.

9Après cela, il fabriqua le parvis. Du côté sud, sur une longueur de cinquante mètres, il était délimité par des tentures de lin retors. 10Elles étaient soutenues par vingt piliers, reposant sur vingt socles de bronze et munis de crochets et de tringles en argent. 11Du côté nord, il y avait également cinquante mètres de tentures soutenues par vingt piliers reposant sur vingt socles de bronze et munis de crochets et de tringles en argent. 12A l’ouest, vingt-cinq mètres de tentures, soutenues par dix piliers reposant sur dix socles et munis de crochets et de tringles en argent. 13Du côté est, le parvis avait aussi vingt-cinq mètres de largeur. 14-15De chaque côté de la porte, sur sept mètres cinquante, il fit des tentures soutenues par trois piliers reposant sur leurs trois socles. 16Toutes les tentures formant l’enceinte du parvis étaient en fin lin retors. 17Les socles des piliers étaient de bronze, mais leurs crochets et les tringles qui les reliaient étaient en argent ainsi que leurs chapiteaux. Toutes les colonnes du parvis étaient équipées de tringles d’argent. 18Le rideau de la porte du parvis était un ouvrage brodé en fils de pourpre violette et écarlate, de rouge éclatant et de fin lin retors ; il avait dix mètres de long et deux mètres cinquante de haut comme les tentures du parvis. 19Ses quatre piliers et leurs quatre socles étaient en bronze, leurs crochets et leurs tringles en argent, et leurs chapiteaux étaient revêtus d’argent. 20Tous les piquets du tabernacle et ceux du parvis étaient faits de bronze.

Les comptes38.21 En hébreu, les poids sont en talents (un talent = 300 sicles) et en sicles (un sicle = 11,4 g).

21Voici les comptes du tabernacle, de la Demeure de l’acte de l’alliance, établis sur l’ordre de Moïse, par les soins des lévites, sous la direction d’Itamar, fils du prêtre Aaron. 22Betsaléel, fils d’Ouri, descendant de Hour, de la tribu de Juda, fit tout ce que l’Eternel avait ordonné à Moïse, 23assisté par Oholiab, fils d’Ahisamak de la tribu de Dan qui était sculpteur, concepteur et brodeur en pourpre violette et écarlate, en rouge éclatant et en fin lin.

24Quantité d’or utilisée pour la construction et tous les ouvrages du sanctuaire, or qui avait été présenté à l’Eternel : 1 000 kilogrammes, pesé selon l’unité de poids (le sicle) en vigueur au sanctuaire. 25L’argent apporté par les membres de la communauté dont on fit le recensement pesait 3 440 kilogrammes, selon l’unité de poids en vigueur au sanctuaire, 26ce qui représentait une demi-unité de poids, soit 5,7 grammes par tête pour tous les hommes de vingt ans et au-dessus qui furent recensés, c’est-à-dire 603 550 hommes38.26 Pour les v. 25-26, voir 30.11-16.. 273 420 kilogrammes furent utilisés pour les cent socles du sanctuaire et ceux du voile, soit 34,20 kilogrammes par socle. 28Les 20 kilogrammes restants furent utilisés pour les crochets et les tringles reliant les piliers, ainsi que pour le revêtement des chapiteaux. 29Le peuple avait présenté à l’Eternel 2 421 kilogrammes de bronze. 30On en fit les socles de l’entrée de la tente de la Rencontre et l’autel de bronze avec sa grille et tous ses ustensiles, 31les socles du parvis tout autour, ceux de l’entrée du parvis et tous les piquets du tabernacle et du parvis.