Kutoka 37 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 37:1-29

Sanduku La Agano

(Kutoka 25:10-22)

137:1 Kut 31:2; 30:6; 39:35; Kum 10:3; Kut 35:30; 25:10Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu,37:1 Dhiraa moja na nusu ni sawa na mita 1.13. upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu. 2Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu. 3Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine. 437:4 Hes 4:6Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu. 537:5 Hes 1:50; 2Sam 6:3Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.

637:6 Kut 26:34; 31:7; Ebr 9:5; Kut 25:17Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu. 737:7 Eze 41:18Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko. 8Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili. 937:9 Ebr 9:5; Kum 10:3; Mwa 3:24; Kut 25:22; 1Fal 6:23; 2Nya 3:10; Za 80:1; Eze 1:5-28; 10:1; Yn 1:51; Flp 2:10; 1Tim 3:16; 1Pet 1:12Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.

Meza

(Kutoka 25:23-30)

1037:10 Kum 31:8; Ebr 9:2; Kut 15:23; Mal 1:7, 12Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili,37:10 Dhiraa mbili ni sawa na sentimita 90. upana wa dhiraa moja,37:10 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45. na kimo cha dhiraa moja na nusu. 11Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote. 12Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne,37:12 Nyanda nne ni sawa na sentimita 8. na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote. 13Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne. 1437:14 Ebr 9:4Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza. 15Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu. 1637:16 Kut 25:29Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.

Kinara Cha Taa

(Kutoka 25:31-40)

1737:17 Ebr 9:2; Ufu 1:12; Kut 25:31; Law 24:4; 1Nya 28:15; Zek 4:2; Mt 5:15, 16; Yn 5:35; Flp 2:15; 1Pet 2:9; Ufu 1:20Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja. 18Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine. 19Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa. 2037:20 Hes 17:8; Yer 1:11Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake. 21Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla. 2237:22 Hes 8:4Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.

2337:23 Kut 40:4, 25; Ufu 1:20; 4:5Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi. 24Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta37:24 Talanta moja ya dhahabu ni sawa na kilo 34. moja ya dhahabu safi.

Madhabahu Ya Kufukizia Uvumba

(Kutoka 30:1-5)

2537:25 Kut 30:34-36; Lk 1:11; Ebr 9:4; Ufu 8:3; Kut 27:2; Ufu 9:13; 1Fal 9:25; 1Nya 29:6, 7; Isa 60:6; Mal 1:11; 1Pet 2:5Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo. 26Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka. 27Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu. 2837:28 Kut 25:13Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.

2937:29 Kut 31:11; 30:1, 25; 39:38; Isa 61:1; 11:2; Za 133:2; 1Yn 2:20; Za 141:2; Wim 4:14; Mal 1:11; Ebr 5:7; 7:25; Ufu 5:8; 8:3, 4Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.

Nueva Versión Internacional

Éxodo 37:1-29

El arca

37:1-9Éx 25:10-20

1Bezalel hizo el arca de madera de acacia, de dos codos y medio de largo, un codo y medio de ancho, y un codo y medio de alto.37:1 Es decir, aprox. 1.1 m de largo por 68 cm de ancho y 68 cm de alto; también en v. 6. 2La recubrió de oro puro por dentro y por fuera, también puso en su derredor una moldura de oro. 3Fundió cuatro anillos de oro para el arca y se los colocó a sus cuatro patas, colocando dos anillos en un lado y dos en el otro. 4Hizo luego unas varas de madera de acacia, las recubrió de oro, 5y las introdujo en los anillos que van a los costados del arca para transportarla.

6Al arca le hizo una tapa de oro puro, de dos codos y medio de largo por un codo y medio de ancho. 7Para los dos extremos de la tapa del arca hizo dos querubines de oro trabajado a martillo. 8En cada uno de los extremos puso un querubín, y los hizo de modo que ambos formaban una sola pieza con la tapa del arca. 9Los querubines tenían las alas extendidas por encima de la tapa del arca y con ellas lo cubrían. Quedaban el uno frente al otro, mirando hacia la tapa.

La mesa

37:10-16Éx 25:23-29

10Bezalel hizo la mesa de madera de acacia de dos codos de largo por un codo de ancho y un codo y medio de alto.37:10 Es decir, aprox. 90 cm por 45 cm de ancho y 68 cm de alto. 11La recubrió de oro puro y le puso alrededor una moldura de oro. 12También le hizo un reborde de un palmo37:12 Es decir, aprox. 7.5 cm; se trata aquí del palmo menor. de ancho y puso una moldura de oro alrededor del reborde. 13Fundió cuatro anillos de oro para la mesa y se los sujetó a las cuatro esquinas, donde iban las cuatro patas. 14Los anillos fueron colocados junto al reborde para pasar por ellos las varas empleadas para transportar la mesa. 15Esas varas eran de madera de acacia y estaban recubiertas de oro. 16Los utensilios para la mesa, sus platos, bandejas, tazones y jarras para verter las ofrendas líquidas, los hizo de oro puro.

El candelabro

37:17-24Éx 25:31-39

17Bezalel hizo el candelabro de oro puro trabajado a martillo. Su base, su tallo, y sus copas, cálices y flores formaban una sola pieza. 18De los costados del candelabro salían seis brazos, tres de un lado y tres del otro. 19En cada uno de los seis brazos del candelabro había tres copas en forma de flores de almendro, con cálices y pétalos. 20El candelabro mismo tenía cuatro copas en forma de flor de almendro, con cálices y pétalos. 21Debajo del primer par de brazos que salía del candelabro había un cáliz; debajo del segundo par de brazos había un segundo cáliz y debajo del tercer par de brazos había un tercer cáliz —seis brazos en total. 22Los cálices y los brazos formaban una sola pieza con el candelabro, el cual era de oro puro trabajado a martillo.

23Hizo también de oro puro sus siete lámparas, lo mismo que sus cortapabilos y braseros. 24Para hacer el candelabro y todos sus accesorios, usó un talento37:24 Es decir, aprox. 34 kg. de oro puro.

El altar del incienso

37:25-28Éx 30:1-5

25Bezalel hizo de madera de acacia el altar del incienso. Era cuadrado, de un codo de largo por un codo de ancho y dos codos de alto.37:25 Es decir, aprox. 45 cm de largo por 45 cm de ancho y 90 cm de alto. Sus cuernos formaban una pieza con el altar. 26Recubrió de oro puro su parte superior, sus cuatro costados y los cuernos, y puso una moldura de oro alrededor. 27Debajo de la moldura puso dos anillos de oro en cada uno de sus costados, para pasar por ellos las varas usadas para transportarlo. 28Las varas las hizo de madera de acacia y las recubrió de oro.

29Bezalel hizo también el aceite de la unción sagrada y el incienso puro y aromático, como lo hacen los fabricantes de perfumes.