Kutoka 37 – NEN & NVI-PT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 37:1-29

Sanduku La Agano

(Kutoka 25:10-22)

137:1 Kut 31:2; 30:6; 39:35; Kum 10:3; Kut 35:30; 25:10Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu,37:1 Dhiraa moja na nusu ni sawa na mita 1.13. upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu. 2Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu. 3Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine. 437:4 Hes 4:6Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu. 537:5 Hes 1:50; 2Sam 6:3Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.

637:6 Kut 26:34; 31:7; Ebr 9:5; Kut 25:17Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu. 737:7 Eze 41:18Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko. 8Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili. 937:9 Ebr 9:5; Kum 10:3; Mwa 3:24; Kut 25:22; 1Fal 6:23; 2Nya 3:10; Za 80:1; Eze 1:5-28; 10:1; Yn 1:51; Flp 2:10; 1Tim 3:16; 1Pet 1:12Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.

Meza

(Kutoka 25:23-30)

1037:10 Kum 31:8; Ebr 9:2; Kut 15:23; Mal 1:7, 12Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili,37:10 Dhiraa mbili ni sawa na sentimita 90. upana wa dhiraa moja,37:10 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45. na kimo cha dhiraa moja na nusu. 11Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote. 12Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne,37:12 Nyanda nne ni sawa na sentimita 8. na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote. 13Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne. 1437:14 Ebr 9:4Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza. 15Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu. 1637:16 Kut 25:29Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.

Kinara Cha Taa

(Kutoka 25:31-40)

1737:17 Ebr 9:2; Ufu 1:12; Kut 25:31; Law 24:4; 1Nya 28:15; Zek 4:2; Mt 5:15, 16; Yn 5:35; Flp 2:15; 1Pet 2:9; Ufu 1:20Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja. 18Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine. 19Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa. 2037:20 Hes 17:8; Yer 1:11Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake. 21Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla. 2237:22 Hes 8:4Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.

2337:23 Kut 40:4, 25; Ufu 1:20; 4:5Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi. 24Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta37:24 Talanta moja ya dhahabu ni sawa na kilo 34. moja ya dhahabu safi.

Madhabahu Ya Kufukizia Uvumba

(Kutoka 30:1-5)

2537:25 Kut 30:34-36; Lk 1:11; Ebr 9:4; Ufu 8:3; Kut 27:2; Ufu 9:13; 1Fal 9:25; 1Nya 29:6, 7; Isa 60:6; Mal 1:11; 1Pet 2:5Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo. 26Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka. 27Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu. 2837:28 Kut 25:13Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.

2937:29 Kut 31:11; 30:1, 25; 39:38; Isa 61:1; 11:2; Za 133:2; 1Yn 2:20; Za 141:2; Wim 4:14; Mal 1:11; Ebr 5:7; 7:25; Ufu 5:8; 8:3, 4Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.

Nova Versão Internacional

Êxodo 37:1-29

A Arca da Aliança

1Bezalel fez a arca com madeira de acácia, com um metro e dez centímetros de comprimento, setenta centímetros de largura e setenta centímetros de altura37.1 Hebraico: 2,5 côvados de comprimento e 1,5 côvados de largura e de altura. O côvado era uma medida linear de cerca de 45 centímetros.. 2Revestiu-a de ouro puro, por dentro e por fora, e fez uma moldura de ouro ao seu redor. 3Fundiu quatro argolas de ouro para ela, prendendo-as a seus quatro pés, com duas argolas de um lado e duas do outro. 4Depois fez varas de madeira de acácia, revestiu-as de ouro 5e colocou-as nas argolas laterais da arca para que pudesse ser carregada.

6Fez a tampa de ouro puro com um metro e dez centímetros de comprimento por setenta centímetros de largura. 7Fez também dois querubins de ouro batido nas extremidades da tampa. 8Fez ainda um querubim numa extremidade e o segundo na outra, formando uma só peça com a tampa. 9Os querubins tinham as asas estendidas para cima, cobrindo com elas a tampa. Estavam de frente um para o outro, com o rosto voltado para a tampa.

A Mesa e seus Utensílios

10Fez a mesa com madeira de acácia com noventa centímetros de comprimento, quarenta e cinco centímetros de largura e setenta centímetros de altura. 11Revestiu-a de ouro puro e fez uma moldura de ouro ao seu redor. 12Fez também ao seu redor uma borda com a largura de quatro dedos e uma moldura de ouro para essa borda. 13Fundiu quatro argolas de ouro para a mesa e prendeu-as nos quatro cantos, onde estavam os seus quatro pés. 14As argolas foram presas próximas da borda, para que sustentassem as varas usadas para carregar a mesa. 15Fez as varas para carregar a mesa de madeira de acácia, revestidas de ouro. 16E de ouro puro fez os utensílios para a mesa: seus pratos e recipientes para incenso, as tigelas e as bacias nas quais se derramam as ofertas de bebidas37.16 Veja Nm 28.7..

O Candelabro de Ouro

17Fez o candelabro de ouro puro e batido. O pedestal, a haste, as taças, as flores e os botões formavam com ele uma só peça. 18Seis braços saíam do candelabro: três de um lado e três do outro. 19Havia três taças com formato de flor de amêndoa, num dos braços, cada uma com botão e flor, e três taças com formato de flor de amêndoa no braço seguinte, cada uma com botão e flor. Assim era com os seis braços que saem do candelabro. 20Na haste do candelabro havia quatro taças com formato de flor de amêndoa, cada uma com flor e botão. 21Havia um botão debaixo de cada par dos seis braços que saíam do candelabro. 22Os braços com seus botões formavam uma só peça com o candelabro; tudo feito de ouro puro e batido.

23Fez de ouro puro suas sete lâmpadas, seus cortadores de pavio e seus apagadores. 24Com trinta e cinco quilos37.24 Hebraico: 1 talento. de ouro puro fez o candelabro com seus botões e todos esses utensílios.

O Altar do Incenso

25Fez ainda o altar do incenso de madeira de acácia. Era quadrado, com quarenta e cinco centímetros de cada lado e noventa centímetros de altura; suas pontas formavam com ele uma só peça. 26Revestiu de ouro puro a parte superior, todos os lados e as pontas, e fez uma moldura de ouro ao seu redor. 27Fez também duas argolas de ouro de cada lado do altar, abaixo da moldura, para sustentar as varas utilizadas para carregá-lo, 28e usou madeira de acácia para fazer as varas e revestiu-as de ouro.

29Fez ainda o óleo sagrado para as unções e o incenso puro e aromático—obra de perfumista.