Kutoka 37 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 37:1-29

Sanduku La Agano

(Kutoka 25:10-22)

137:1 Kut 31:2; 30:6; 39:35; Kum 10:3; Kut 35:30; 25:10Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu,37:1 Dhiraa moja na nusu ni sawa na mita 1.13. upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu. 2Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu. 3Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine. 437:4 Hes 4:6Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu. 537:5 Hes 1:50; 2Sam 6:3Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.

637:6 Kut 26:34; 31:7; Ebr 9:5; Kut 25:17Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu. 737:7 Eze 41:18Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko. 8Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili. 937:9 Ebr 9:5; Kum 10:3; Mwa 3:24; Kut 25:22; 1Fal 6:23; 2Nya 3:10; Za 80:1; Eze 1:5-28; 10:1; Yn 1:51; Flp 2:10; 1Tim 3:16; 1Pet 1:12Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.

Meza

(Kutoka 25:23-30)

1037:10 Kum 31:8; Ebr 9:2; Kut 15:23; Mal 1:7, 12Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili,37:10 Dhiraa mbili ni sawa na sentimita 90. upana wa dhiraa moja,37:10 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45. na kimo cha dhiraa moja na nusu. 11Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote. 12Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne,37:12 Nyanda nne ni sawa na sentimita 8. na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote. 13Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne. 1437:14 Ebr 9:4Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza. 15Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu. 1637:16 Kut 25:29Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.

Kinara Cha Taa

(Kutoka 25:31-40)

1737:17 Ebr 9:2; Ufu 1:12; Kut 25:31; Law 24:4; 1Nya 28:15; Zek 4:2; Mt 5:15, 16; Yn 5:35; Flp 2:15; 1Pet 2:9; Ufu 1:20Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja. 18Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine. 19Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa. 2037:20 Hes 17:8; Yer 1:11Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake. 21Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla. 2237:22 Hes 8:4Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.

2337:23 Kut 40:4, 25; Ufu 1:20; 4:5Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi. 24Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta37:24 Talanta moja ya dhahabu ni sawa na kilo 34. moja ya dhahabu safi.

Madhabahu Ya Kufukizia Uvumba

(Kutoka 30:1-5)

2537:25 Kut 30:34-36; Lk 1:11; Ebr 9:4; Ufu 8:3; Kut 27:2; Ufu 9:13; 1Fal 9:25; 1Nya 29:6, 7; Isa 60:6; Mal 1:11; 1Pet 2:5Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo. 26Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka. 27Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu. 2837:28 Kut 25:13Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.

2937:29 Kut 31:11; 30:1, 25; 39:38; Isa 61:1; 11:2; Za 133:2; 1Yn 2:20; Za 141:2; Wim 4:14; Mal 1:11; Ebr 5:7; 7:25; Ufu 5:8; 8:3, 4Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.

Swedish Contemporary Bible

2 Moseboken 37:1-29

Arken tillverkas

(2 Mos 25:10-22)

1Därefter tillverkade Besalel arken av akacieträ, 125 centimeter lång och 75 centimeter bred och 75 centimeter hög. 2Den var klädd med rent guld både invändigt och utvändigt och hade en rand av guld runt omkring. 3Fyra ringar av guld sattes fast ovanför arkens fyra fötter, två på var sida. 4Sedan gjorde han stänger av akacieträ och drog över dem med guld 5och sköt in dem genom ringarna på arkens sidor, så att man kunde bära den.

6Sedan gjorde han ett lock av rent guld. Det var 125 centimeter långt och 75 centimeter brett. 7Han gjorde två keruber av hamrat guld vid de båda ändarna av försoningsstället, 8en kerub vid den ena och en vid den andra ändan av locket. De var gjorda i ett stycke med locket. 9Keruberna hade sina vingar utbredda över locket så att de täckte den och de hade ansiktena vända mot varandra nedåt mot försoningsstället.

Bordet

(2 Mos 25:23-30)

10Han gjorde också ett bord av akacieträ, en meter långt, en halv meter brett och 75 centimeter högt. 11Det var överdraget och kantat med guld. 12Runt omkring det gjorde han en list lika bred som en hand och runt den en rand av guld. 13Och han göt fyra ringar av rent guld och satte dem i hörnen vid de fyra bordsbenen 14tätt intill listen, så att man skulle kunna bära bordet med stängerna som sköts in i ringarna. 15Stängerna gjordes av akacieträ överdraget med guld till att bära bordet med. 16Av rent guld gjorde han sedan kärlen till bordet, faten, skålarna, bägarna och kannorna för dryckesoffren.

Lampstället tillverkas

(2 Mos 25:31-40)

17Lampstället gjorde han också av rent, hamrat guld. Det var gjort i ett enda stycke: fot, stam, grenar och utsmyckningar med blad, knoppar och blommor. 18Det hade sex armar, tre på var sida av stammen. 19Till varje arm gjordes tre utskurna skålar, formade som mandelträdsblommor. Så gjorde man med alla sex armarna som gick ut från stammen. 20På mittstammen fanns fyra skålar, formade som mandelblommor och knoppar, 21en blomma under varje armpar som gick ut från stammen, gjorda i ett stycke, sammanlagt sex armar. 22Dekorationerna och armarna var alla gjorda i ett stycke av rent hamrat guld. 23Sedan gjorde han sju oljelampor till den och tänger och brickor till dessa, allt av rent guld. 24Hela lampstället var gjort av 34 kilo renaste guld.

Rökelsealtaret tillverkas

(2 Mos 30:1-5; 30:22-38)

25Rökelsealtaret gjordes av akacieträ. Det var en halv meter i fyrkant och en meter högt och dess horn var gjorda i ett stycke med själva altaret. 26Han drog rent guld över dess överdel, sidor och horn och gjorde en guldkant runt det. 27Sedan gjorde han två guldringar som sattes fast nedanför kanten på två motsatta sidor för att hålla stängerna som man kunde bära altaret med. 28De var av akacieträ, överdragna med guld.

29Han gjorde den heliga smörjelseoljan och den rena, välluktande rökelsen, konstfärdigt tillredda.