Kutoka 36 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 36:1-38

136:1 Kut 28:3; 25:8; Ay 32:8; Isa 28:26; Mit 2:6; Kut 25:8; Law 4:6; 19:30; Hes 18:5; 30:8; 1Fal 6:16; Za 96:6; 134:2; Isa 63:18; Eze 5:11; Dan 8:13, 14; Ebr 9:1, 2Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”

236:2 Kut 31:2, 6; 25:2; 35:2, 26; 1Nya 29:5Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi. 336:3 Kut 35:29Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi. 4Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao, 536:5 2Nya 24:14; 31:10; 2Kor 8:2-3wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”

6Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi, 736:7 1Fal 7:47kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.

Maskani Ya Mungu

(Kutoka 26:1-37)

836:8 Kut 26:1; Ay 32:8; Mit 10:8; 15:14; 21:1; Mwa 3:24; 1Fal 6:23; 2Nya 3:10; Eze 1:5-28; 10:1Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo. 9Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane,36:9 Dhiraa 28 ni sawa na mita 12.6. na upana wa dhiraa nne36:9 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. 10Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano. 11Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho. 1236:12 Kut 26:5Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana. 13Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.

1436:14 Kut 26:7Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani. 15Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini,36:15 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. na upana wa dhiraa nne. 16Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine. 17Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine. 18Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja. 1936:19 Kut 26:14Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.36:19 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili.

2036:20 Kut 26:15; 25:5, 10; Hes 25:1; Kum 10:3; Yos 2:1Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani. 21Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi,36:21 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. na upana wa dhiraa moja na nusu,36:21 Dhiraa moja na nusu ni sawa na sentimita 67.5. 22zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii. 23Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani, 24na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi. 25Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini 26na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili. 27Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani, 28na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali. 2936:29 Kut 26:24; Za 133:1; Mdo 2:46; 1Kor 1:10Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana. 30Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.

3136:31 Kut 26:26Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani, 32matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani. 33Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine. 34Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.

3536:35 Kut 39:38; Mt 27:51; Lk 23:45; Ebr 9:5; 6:19; 10:20Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia. 36Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha. 3736:37 Kut 27:16; Law 16:2Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. 3836:38 1Fal 7:16; 2Nya 4:12; Yer 52:22Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.

O Livro

Êxodo 36:1-38

1Todos os outros artistas, com capacidades dadas pelo Senhor, deverão prestar assistência a Bezalel e a Aoliabe na construção e no mobiliário do tabernáculo.”

2Moisés chamou Bezalel, Aoliabe e todos os homens capazes, que o Senhor dotou de sabedoria e que se tinham oferecido voluntariamente para ajudar neste trabalho, e mandou que começassem. 3Moisés entregou-lhes o material oferecido pelo povo, mas este ainda trazia em cada manhã mais ofertas voluntárias. 4Por fim, todos os que trabalhavam naquela tarefa vieram ter com Moisés 5e disseram-lhe: “Já temos muito mais do que é necessário para esta obra!” 6Moisés então enviou uma mensagem, através do campo, anunciando que não eram precisas mais ofertas. E o povo teve mesmo de ser impedido de trazer mais coisas, 7porque aquilo que eles já tinham era mais do que suficiente para realizar todo o serviço.

O tabernáculo

(Êx 26.1-37)

8Os artistas tecelãos fizeram primeiramente dez véus de linho fino retorcido, em azul, púrpura e vermelho, com querubins habilmente bordados. 9O comprimento de cada véu era de 14 metros e de largura, 2 metros. Eram todos da mesma medida. 10Cinco destes véus eram ligados entre si, lado a lado, e outros cinco também da mesma maneira, de forma a fazerem duas peças retangulares. 11-12Cinquenta laços azuis foram cosidos na bainha de cada uma dessas duas longas peças. 13Depois fizeram-se cinquenta colchetes de ouro para prender os laços, atando assim as duas peças de maneira a formarem um todo único.

14Por cima desse teto havia uma segunda coberta feita de onze mantas de pelo de cabra, 15cada uma delas uniformemente com 15 metros de comprimento por 2 de largura. 16Bezalel juntou cinco destas cobertas, formando uma peça retangular, e as outras seis também as uniu da mesma forma. 17Depois fez cinquenta laços na bainha dum dos lados de cada uma dessas peças, 18assim como cinquenta pequenos colchetes de bronze para poder atar os laços uns aos outros, a fim de que as duas peças ficassem bem unidas. 19A última camada deste telhado era feita de pele de carneiro tingida de vermelho e ainda de pele de couro fino.

20Para os lados do tabernáculo empregou tábuas de madeira de acácia, postas ao alto. 21A altura de cada tábua era de 5 metros, e a largura de 75 centímetros. 22Cada tábua tinha uma ranhura para poder encaixar na seguinte. 23Havia vinte tábuas do lado sul, 24com as extremidades enfiando, ao todo, em quarenta bases de prata. Cada tábua estava fixada à base por duas braçadeiras. 25Havia também vinte tábuas do lado norte do tabernáculo, 26com quarenta bases de prata, duas sob cada tábua. 27O lado ocidental, que era a parte de trás, tinha seis tábuas, 28-29mais uma para cada canto. Estas tábuas, incluindo as dos cantos, ligavam-se umas às outras em ambas as extremidades por meio de argolas. 30Assim, no lado ocidental, havia oito tábuas nos cantos da construção, com dezasseis bases de prata; duas bases para cada tábua.

31Depois fez cinco conjuntos de barras de madeira de acácia para prender as tábuas entre si; cinco barras para cada lado do tabernáculo. 32Cinco traves para cada lado do tabernáculo, mais cinco para a retaguarda, do lado do ocidente. 33A barra do meio, que ficará a meia altura das tábuas, atravessá-las-á de uma ponta à outra. 34Tanto as tábuas como as barras foram cobertas de ouro, mas as argolas eram de ouro puro.

35O véu interior, de azul, púrpura e vermelho, foi feito de linho, com querubins artisticamente bordados. 36Depois foi atado a quatro ganchos postos em quatro colunas de madeira de acácia, cobertas de ouro e assentes em quatro bases de prata.

37Seguidamente, fez o véu para a entrada da tenda sagrada, de linho fino retorcido, bordado a azul, púrpura e vermelho. 38Este véu estava suspenso por cinco postes ou colunas. Estes postes, os seus capitéis e hastes foram revestidos de ouro. As suas cinco bases foram moldadas em bronze.