Kutoka 36 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 36:1-38

136:1 Kut 28:3; 25:8; Ay 32:8; Isa 28:26; Mit 2:6; Kut 25:8; Law 4:6; 19:30; Hes 18:5; 30:8; 1Fal 6:16; Za 96:6; 134:2; Isa 63:18; Eze 5:11; Dan 8:13, 14; Ebr 9:1, 2Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”

236:2 Kut 31:2, 6; 25:2; 35:2, 26; 1Nya 29:5Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi. 336:3 Kut 35:29Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi. 4Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao, 536:5 2Nya 24:14; 31:10; 2Kor 8:2-3wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”

6Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi, 736:7 1Fal 7:47kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.

Maskani Ya Mungu

(Kutoka 26:1-37)

836:8 Kut 26:1; Ay 32:8; Mit 10:8; 15:14; 21:1; Mwa 3:24; 1Fal 6:23; 2Nya 3:10; Eze 1:5-28; 10:1Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo. 9Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane,36:9 Dhiraa 28 ni sawa na mita 12.6. na upana wa dhiraa nne36:9 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. 10Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano. 11Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho. 1236:12 Kut 26:5Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana. 13Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.

1436:14 Kut 26:7Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani. 15Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini,36:15 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. na upana wa dhiraa nne. 16Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine. 17Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine. 18Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja. 1936:19 Kut 26:14Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.36:19 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili.

2036:20 Kut 26:15; 25:5, 10; Hes 25:1; Kum 10:3; Yos 2:1Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani. 21Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi,36:21 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. na upana wa dhiraa moja na nusu,36:21 Dhiraa moja na nusu ni sawa na sentimita 67.5. 22zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii. 23Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani, 24na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi. 25Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini 26na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili. 27Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani, 28na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali. 2936:29 Kut 26:24; Za 133:1; Mdo 2:46; 1Kor 1:10Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana. 30Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.

3136:31 Kut 26:26Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani, 32matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani. 33Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine. 34Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.

3536:35 Kut 39:38; Mt 27:51; Lk 23:45; Ebr 9:5; 6:19; 10:20Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia. 36Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha. 3736:37 Kut 27:16; Law 16:2Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. 3836:38 1Fal 7:16; 2Nya 4:12; Yer 52:22Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.

New International Reader’s Version

Exodus 36:1-38

1Bezalel and Oholiab must do the work just as the Lord has commanded. So must every skilled worker to whom the Lord has given skill and ability. They know how to do all the work for every purpose connected with the sacred tent. And that includes setting it up.”

2Then Moses sent for Bezalel and Oholiab. He sent for every skilled worker to whom the Lord had given ability and who wanted to come and do the work. 3They received from Moses all the offerings the people of Israel had brought. They had brought the offerings for all the work for every purpose connected with the holy tent. That included setting it up. The people kept bringing the offerings they chose to give. They brought them morning after morning. 4So all the skilled workers working on the holy tent stopped what they were doing. 5They said to Moses, “The Lord commanded us to do the work. And the people are bringing more than enough for us to do it.”

6Then Moses gave an order. A message was sent through the whole camp. It said, “No man or woman should make anything else and offer it for the holy tent.” And so the people were kept from bringing more offerings. 7There was already more than enough to do all the work.

The Holy Tent

8All the skilled workers made the holy tent. They made ten curtains out of finely twisted linen. They made them with blue, purple and bright red yarn. A skilled worker sewed cherubim into the pattern. 9All the curtains were the same size. They were 42 feet long and six feet wide. 10The workers joined five of the curtains together. They did the same thing with the other five. 11Then they made loops out of blue strips of cloth along the edge of the end curtain in one set. They did the same thing with the end curtain in the other set. 12They also made 50 loops on the end curtain of the one set. They did the same thing on the end curtain of the other set. They put the loops across from each other. 13Then they made 50 gold hooks. They used them to join the two sets of curtains together so that the holy tent was all one piece.

14The workers made a total of 11 curtains out of goat hair to put over the holy tent. 15All 11 curtains were the same size. They were 45 feet long and six feet wide. 16The workers joined five of the curtains together into one set. They did the same thing with the other six. 17Then they made 50 loops along the edge of the end curtain in the one set. They did the same thing with the other set. 18They made 50 bronze hooks. They used them to join the tent together all in one piece. 19They made a covering for the tent. They made it out of ram skins dyed red. Over that, they put a covering of another kind of strong leather.

20The workers made frames out of acacia wood for the holy tent. 21Each frame was about 15 feet long and two feet three inches wide. 22The workers added two small wooden pins to each frame. The pins stuck out so that they were even with each other. The workers made all the frames of the holy tent in the same way. 23The workers made 20 frames for the south side of the holy tent. 24And they made 40 silver bases to go under them. They made two bases for each frame. They put one under each pin that stuck out. 25For the north side of the holy tent they made 20 frames 26and 40 silver bases. They put two bases under each frame. 27The workers made six frames for the west end of the holy tent. 28They made two frames for the corners of the holy tent at the far end. 29At those two corners the frames were double from top to bottom. They were fitted into a single ring. The workers made both of them the same. 30So there were eight frames and 16 silver bases. There were two bases under each frame.

31The workers also made crossbars out of acacia wood. They made five for the frames on one side of the holy tent. 32They made five for the frames on the other side. And they made five for the frames on the west, at the far end of the holy tent. 33The center crossbar reached from end to end at the middle of the frames. 34The workers covered the frames with gold. They made gold rings to hold the crossbars. They also covered the crossbars with gold.

35They made the curtain out of blue, purple and bright red yarn and finely twisted linen. A skilled worker sewed cherubim into the pattern. 36The workers made four posts out of acacia wood for the curtain. They covered the posts with gold. They made gold hooks and four silver bases for the posts. 37For the entrance to the tent the workers made a curtain. They made it out of blue, purple and bright red yarn and finely twisted linen. A person who sewed skillfully made it. 38The workers made five posts with hooks for the curtains. They covered the tops of the posts and their bands with gold. And they made five bronze bases for them.