Kutoka 35 – NEN & TNCV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 35:1-35

Masharti Ya Sabato

135:1 Kut 34:32Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye: 235:2 Law 23:3; Mwa 2:3; Kut 34:21; Kum 5:13-14; Kut 31:14, 15; Hes 15:32; Lk 13:14Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe. 335:3 Kut 16:23Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”

Vifaa Kwa Ajili Ya Maskani Ya Mungu

(Kutoka 25:1-9)

435:4 Kut 25:1, 2Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru: 535:5 Kut 25:2; 2Kor 9:7Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba; 6nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi; 7ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo;35:7 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. mbao za mshita; 835:8 Kut 25:6mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri; 9vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.

1035:10 Kut 31:6; 39:43; 1Fal 7:14; Isa 28:26“Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru: 1135:11 Kut 26:1-37; 36:8-38; Mdo 7:44, 45; Ebr 8:2, 5; 9:2-11; Ufu 21:3Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako; 1235:12 Kut 25:10-22; 37:1-9; 26:33Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia; 1335:13 Kut 25:23-30; 37:10-16meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho; 1435:14 Kut 25:31kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga; 1535:15 Kut 30:1-6; 37:26-28; 30:34-38; 26:36; 1Sam 2:28; 1Nya 23:13; 2Nya 29:11; Lk 1:9madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani; 1635:16 Kut 27:1-8; 38:1-7; 30:18madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake; 1735:17 Kut 27:9; 38:9-20pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua; 1835:18 Kut 27:19; 38:20vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake; 1935:19 Kut 28:2; 31:10; 39:1mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”

20Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose, 2135:21 Kut 25:2; 36:2; 1Nya 28:2, 9; 29:9; Ezr 7:27; 2Kor 8:12; 9:7na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu. 22Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana. 2335:23 Kut 39:1; 1Nya 29:8Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta. 24Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta. 2535:25 Kut 28:3; 31:6; 36:1; 2Fal 23:7; Mit 31:19-24Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi. 2635:26 Kut 25:2; 1Nya 29:6-8Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi. 27Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani. 2835:28 Kut 25:6Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri. 2935:29 Kut 25:2-7; 36:3; 2Fal 12:4Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.

Bezaleli Na Oholiabu

(Kutoka 31:1-11)

30Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, 3135:31 2Nya 2:7, 14naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi, 32ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba, 33kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza. 3435:34 Kut 31:6; 2Nya 2:14Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine. 3535:35 Kut 31:3, 6; 36:1, 2; 1Fal 7:14; 1Nya 2:14; Isa 28:26; Yak 1:5Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.

Thai New Contemporary Bible

อพยพ 35:1-35

ระเบียบวันสะบาโต

1โมเสสจึงเรียกชนอิสราเอลทั้งหมดมาประชุมและกล่าวกับพวกเขาว่า “ต่อไปนี้คือสิ่งที่องค์พระผู้เป็นเจ้าทรงบัญชาให้ท่านทั้งหลายทำ 2จงทำงานเพียงหกวัน ส่วนวันที่เจ็ดจะเป็นวันบริสุทธิ์ เป็นสะบาโตแห่งการหยุดพักถวายแด่องค์พระผู้เป็นเจ้าผู้ใดทำงานในวันนั้นจะต้องตาย 3ในวันสะบาโตอย่าก่อไฟในที่พักของพวกเจ้า”

วัสดุสำหรับพลับพลา

(อพย.25:1-7; 39:32-41)

4โมเสสกล่าวแก่ชุมชนอิสราเอลทั้งหมดว่า “องค์พระผู้เป็นเจ้าทรงบัญชาว่า 5ทุกคนที่เต็มใจ จงนำสิ่งต่างๆ ที่เจ้ามีดังต่อไปนี้มาถวายองค์พระผู้เป็นเจ้าได้แก่ทองคำ เงิน และทองสัมฤทธิ์ 6ด้ายสีน้ำเงิน สีม่วง และสีแดง ผ้าลินินเนื้อดี ขนแพะ 7หนังแกะตัวผู้ย้อมสีแดง หนังพะยูน ไม้กระถินเทศ 8น้ำมันมะกอกสำหรับจุดประทีป เครื่องเทศสำหรับปรุงน้ำมันเพื่อใช้เจิมและสำหรับเครื่องหอม 9โกเมนและอัญมณีอื่นๆ เพื่อใช้ทำเอโฟดและทับทรวง

10“พวกท่านทุกคนที่มีความเชี่ยวชาญ จงมาช่วยกันทำทุกสิ่งตามที่องค์พระผู้เป็นเจ้าทรงบัญชาเถิด 11คือพลับพลารวมทั้งเต็นท์และเครื่องคลุมพลับพลา ตะขอ ไม้ฝาพลับพลา คานขวาง เสาและฐานเสา 12หีบพร้อมคานหาม พระที่นั่งกรุณา และม่านกั้นอภิสุทธิสถาน 13โต๊ะพร้อมคานหามและภาชนะเครื่องใช้ทุกอย่าง รวมทั้งขนมปังเบื้องพระพักตร์ 14คันประทีปพร้อมกับอุปกรณ์ต่างๆ ตะเกียงและน้ำมันจุดประทีป 15แท่นเผาเครื่องหอมพร้อมคานหาม น้ำมันเจิมและเครื่องหอม ม่านสำหรับทางเข้าพลับพลา 16แท่นบูชาพร้อมตะแกรงทองสัมฤทธิ์ คานหามและเครื่องใช้ไม้สอยทุกอย่าง อ่างทองสัมฤทธิ์และฐานรอง 17ม่านกั้นลานพลับพลาพร้อมเสาและฐานเสา ม่านกั้นทางเข้าลานพลับพลา 18หลักหมุดสำหรับพลับพลา และหลักหมุดสำหรับลานพลับพลาพร้อมกับเชือก 19เครื่องแต่งกายที่ทอสำหรับปุโรหิตเมื่อเข้ามาปฏิบัติหน้าที่ในสถานนมัสการ ทั้งเครื่องแต่งกายบริสุทธิ์สำหรับปุโรหิตอาโรนและเครื่องแต่งกายสำหรับบรรดาบุตรชายของเขาเมื่อทำหน้าที่ปุโรหิต”

20แล้วชุมชนอิสราเอลทั้งหมดก็แยกย้ายกันกลับไปจากโมเสส 21ทุกคนที่เต็มใจและปรารถนาที่จะถวาย ต่างก็นำของมาถวายองค์พระผู้เป็นเจ้าสำหรับการสร้างเต็นท์นัดพบ อุปกรณ์ทุกอย่าง และเครื่องแต่งกายบริสุทธิ์ของปุโรหิต 22ชายหญิงทุกคนที่เต็มใจพากันนำเครื่องประดับทองคำทุกชนิด ได้แก่ เข็มกลัด ตุ้มหู แหวน และเครื่องประดับต่างๆ มาถวายเป็นเครื่องบูชายื่นถวายแด่องค์พระผู้เป็นเจ้า 23ทุกคนที่มีผ้าลินินเนื้อดี ด้ายสีน้ำเงิน สีม่วง และสีแดง ขนแพะ หนังแกะตัวผู้ย้อมสีแดง และหนังพะยูนก็นำมาถวาย 24บางคนก็นำเงินหรือทองสัมฤทธิ์มาถวายเป็นเครื่องบูชาแด่องค์พระผู้เป็นเจ้าและทุกคนที่มีไม้กระถินเทศก็นำมาถวายเพื่อใช้ในการก่อสร้าง 25ผู้หญิงทุกคนที่เชี่ยวชาญการปั่นด้ายและทอผ้าก็นำผ้าลินินเนื้อดี ด้ายสีน้ำเงิน สีม่วง และสีแดงมาถวาย 26และผู้หญิงทุกคนที่เต็มใจและมีความชำนาญก็ปั่นด้ายจากขนแพะมาทอเป็นผ้า 27บรรดาผู้นำก็เอาโกเมนและอัญมณีอื่นๆ มาให้เพื่อใช้ฝังลงบนเอโฟดและทับทรวง 28พวกเขายังได้นำเครื่องเทศและน้ำมันมะกอกมาสำหรับจุดประทีป สำหรับปรุงน้ำมันเพื่อใช้เจิมและสำหรับเครื่องหอมมาด้วย 29ดังนั้นชนอิสราเอลทุกคนทั้งชายและหญิงที่เต็มใจต่างก็นำของมาถวายองค์พระผู้เป็นเจ้าด้วยความสมัครใจเพื่องานทั้งปวงตามที่องค์พระผู้เป็นเจ้าทรงบัญชาพวกเขาไว้ผ่านทางโมเสส

เบซาเลลและโอโฮลีอับ

(อพย.31:2-6)

30แล้วโมเสสกล่าวแก่ชนอิสราเอลว่า “ดูเถิด องค์พระผู้เป็นเจ้าทรงเลือกสรรเบซาเลลบุตรชายของอูรี ซึ่งเป็นบุตรชายของเฮอร์จากเผ่ายูดาห์ 31และพระองค์ทรงให้เขาเปี่ยมด้วยพระวิญญาณของพระเจ้า มีความรู้ความสามารถและความชำนาญในเชิงช่างทุกแบบ 32เพื่อออกแบบเครื่องทอง เงิน และทองสัมฤทธิ์อย่างวิจิตร 33เจียระไนเพชรพลอย แกะสลักไม้ และงานฝีมือทุกแบบ 34และพระเจ้าทรงให้เขากับโอโฮลีอับบุตรชายของอาหิสะมัคจากเผ่าดานสามารถสอนคนอื่นๆ ได้ 35พระเจ้าทรงให้เขาทั้งสองเชี่ยวชาญในงานฝีมือเชิงช่างทุกแบบ เป็นนักออกแบบ ทั้งชำนาญงานปักบนผ้าลินินด้วยด้ายสีน้ำเงิน สีม่วง และสีแดง และงานทอ คนทั้งสองเป็นช่างฝีมือเอกและเป็นนักออกแบบชั้นเยี่ยม