Kutoka 28 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 28:1-43

Mavazi Ya Kikuhani

(Kutoka 39:1-7)

128:1 Law 8:30; Za 99:9; Ebr 5; 4; Kut 6:23; 24:9; Law 8:2; 21:1; Hes 18:1-7; Kum 18:5; 1Sam 2:28; Ebr 5:1“Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani. 228:2 Kut 29:5; 31:10; 35:19; Law 8:7-9; 16:32; Hes 20:26-28Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima. 328:3 Kut 31:6; 35:10, 25, 35; 36:1; 31:3; Kum 34:9; Isa 11:2Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili awekwe wakfu, anitumikie katika kazi ya ukuhani. 428:4 Kut 25:7; Law 10:5Haya ndiyo mavazi watakayoshona: kifuko cha kifuani, kisibau, kanzu, joho lililorembwa, kilemba na mshipi. Mavazi haya yatashonwa kwa ajili ya ndugu yako Aroni na wanawe ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani. 528:5 Kut 25:4-7; 25:4-7Waambie watumie dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani safi.

Kisibau

628:6 Kut 39:2; Law 8:7“Tengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kazi ya fundi stadi. 7Kitakuwa na vipande viwili vya mabegani vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kufungia kisibau. 828:8 Kut 29:5Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi utafanana nacho: utakuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao utengenezwe kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri.

928:9 Wim 8:6; Isa 44:16; Hag 2:23“Chukua vito viwili vya shohamu, na uchore juu yake majina ya wana wa Israeli 10kufuatana na walivyozaliwa: majina sita katika kito kimoja, na mengine sita katika kito kingine. 11Yachore majina ya wana wa Israeli juu ya vito hivyo viwili kama vile sonara anavyochonga muhuri. Kisha uvitie vito hivyo katika vijalizo vya dhahabu, 1228:12 Kum 33:12; Ay 31:36; Kut 30:16; Hes 10:10; 31:54; Yos 4:7; Zek 6:14; Kut 39:7; Mwa 9:12-17; Kut 12:14; Mk 14:9; Mdo 10:4; 1Kor 11:24, 25na uvifungie juu ya vipande vya mabega ya kisibau yawe kama vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli. Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake kama kumbukumbu mbele za Bwana. 13Tengeneza vijalizo vya dhahabu 14na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba, na uifunge mikufu hiyo kwenye vijalizo.

Kifuko Cha Kifuani

(Kutoka 39:8-21)

1528:15 Kut 25:7; 39:8; Law 8:8; Isa 59:17; 1The 5:7; Efe 6:14“Fanyiza kifuko cha kifuani kwa ajili ya kufanya maamuzi, kazi ya fundi stadi. Kitengeneze kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa. 16Kitakuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja28:16 Shibiri moja ni sawa na sentimita 22. na upana wa shibiri moja, na kikunjwe mara mbili. 1728:17 Eze 28:13; Ufu 21:19-20; Kut 30:10; Mal 3:17Kisha weka safu nne za vito vya thamani juu yake. Safu ya kwanza itakuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi; 18katika safu ya pili itakuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi; 19safu ya tatu itakuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto; 2028:20 Eze 1:16; 10:9; Dan 10:6na safu ya nne itakuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Yote yatiwe kwenye vijalizo vya dhahabu. 2128:21 Yos 4:8; Ufu 21:12; Hes 1:5; 2:3; Ufu 7:4-8; 21:12Patakuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kwa jina mojawapo la wana wa Israeli, kila kimoja kichorwe kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.

22“Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani, tengeneza mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba. 23Tengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili yake, uzifungie kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani. 24Funga ile mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete zilizo katika pembe za hicho kifuko cha kifuani, 25nazo zile ncha nyingine za mkufu zifunge kwenye vile vijalizo viwili, na uzishikamanishe na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele. 26Tengeneza pete mbili za dhahabu, uzishikamanishe kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau. 27Tengeneza pete nyingine mbili za dhahabu, na uzishikamanishe sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau. 28Pete za kifuko cha kifuani zitafungwa kwenye pete zile za kisibau kwa kamba ya buluu, ziunganishwe na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau.

2928:29 Wim 8:6; Isa 49:15, 16; Ebr 9:24“Wakati wowote Aroni aingiapo Mahali Patakatifu, atakuwa na yale majina ya wana wa Israeli moyoni mwake juu ya kile kifuko cha kifuani cha uamuzi kama kumbukumbu ya kudumu mbele za Bwana. 3028:30 Law 8:8; Hes 27:21; Kum 33:8; 1Sam 28:6; Ezr 2:63; Neh 7:65Pia weka Urimu na Thumimu28:30 Urimu na Thumimu maana yake ni Nuru na Kweli; vifaa hivi viliwekwa kwenye kifuko cha juu cha kisibau cha kuhani mkuu ili kujua mapenzi ya Mungu kwenye mambo ya kutatanisha. ndani ya kifuko cha kifuani, yawe juu ya moyo wa Aroni kila mara aingiapo mbele za Bwana. Kwa hiyo siku zote Aroni atakuwa na uwezo kufanya maamuzi kwa ajili ya wana wa Israeli mbele za Bwana.

Mavazi Mengine Ya Kikuhani

(Kutoka 39:22-31)

3128:31 Kut 39:22; Law 8:7; 2Sam 6:14; Hos 3:4“Shona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, 32na katikati uweke nafasi ya kuingizia kichwa. Kutakuwa na utepe uliofumwa, unaofanana na ukosi kuizunguka nafasi hiyo, ili isichanike. 3328:33 Hes 13:23; 1Sam 14:2; 1Fal 7:18; Wim 4:3; Yer 52:22; Yoe 1:12; Hag 2:19Tengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu kuzunguka pindo la hilo joho, na uweke pia vikengele vya dhahabu kati ya hayo makomamanga. 34Hivyo vikengele vya dhahabu na makomamanga vitapishana kuzunguka upindo wa joho lile. 35Ni lazima Aroni alivae anapofanya huduma. Sauti ya hivyo vikengele itasikika anapoingia na kutoka Mahali Patakatifu mbele za Bwana, ili asije akafa.

3628:36 Kut 29:6; Law 8:9; Zek 14:20; Kut 39:30; 1Nya 16:29; Za 29:2; 93:5; Ebr 4:15; 7:26“Tengeneza bamba la dhahabu safi na uchore juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana. 37Lifunge hilo bamba kwa kamba ya buluu kwenye kilemba, nalo ni lazima liwe mbele ya kilemba. 3828:38 Law 5:1; 10:17; 16:22; 22:9, 16; Hes 18:1; Isa 53:5-11; Eze 4:4-6; Ebr 9:28; 1Pet 2:24; Mwa 32:20; Law 22:20, 27; 23:11; Isa 56:7Aroni alivae bamba hilo kwenye paji la uso wake, naye atachukua hatia kuhusu sadaka takatifu za Waisraeli wanazoweka wakfu, sadaka za aina yoyote. Litakuwa kwenye paji la uso wa Aroni daima ili zikubalike kwa Bwana.

3928:39 Kut 29:6; Law 16:4; Eze 24:17-23; 44:18“Fuma koti la kitani safi na ufanye kilemba cha kitani safi. Mshipi uwe ni kazi ya mtarizi. 4028:40 Kut 29:8-9; 39:41; 40:14; Law 8:13; Eze 44:17Watengenezee wana wa Aroni makoti, mishipi na kofia, ili kuwapa ukuu na heshima. 4128:41 Kut 40:13; 29:7; Law 6:20; 10:7; 21:12; Hes 35:25; Kut 29:7-9; 30:30; 40:15; Law 4:3; 6:22; 8:1-36; Hes 3:3; Ebr 7:28Baada ya kumvika Aroni ndugu yako pamoja na wanawe nguo hizi, watie mafuta na kuwabariki. Waweke wakfu ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani.

4228:42 Law 6:10; 16:4, 23; Eze 44:18“Watengenezee nguo za ndani za kitani zitakazofunika mwili, kutoka kiunoni hadi mapajani. 4328:43 Kut 27:21; 30:20-21; Law 16:13; 22:9; Hes 1:51; 4:15-20; 18:22Aroni na wanawe ni lazima wavae haya kila wanapoingia katika Hema la Kukutania au wanaposogelea madhabahu wakati wa kutoa huduma katika Mahali Patakatifu, ili wasije wakafanya kosa wakafa.

“Haya yawe maagizo ya kudumu kwa Aroni na vizazi vyake.

King James Version

Exodus 28:1-43

1And take thou unto thee Aaron thy brother, and his sons with him, from among the children of Israel, that he may minister unto me in the priest’s office, even Aaron, Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar, Aaron’s sons. 2And thou shalt make holy garments for Aaron thy brother for glory and for beauty. 3And thou shalt speak unto all that are wise hearted, whom I have filled with the spirit of wisdom, that they may make Aaron’s garments to consecrate him, that he may minister unto me in the priest’s office. 4And these are the garments which they shall make; a breastplate, and an ephod, and a robe, and a broidered coat, a mitre, and a girdle: and they shall make holy garments for Aaron thy brother, and his sons, that he may minister unto me in the priest’s office. 5And they shall take gold, and blue, and purple, and scarlet, and fine linen.

6¶ And they shall make the ephod of gold, of blue, and of purple, of scarlet, and fine twined linen, with cunning work. 7It shall have the two shoulderpieces thereof joined at the two edges thereof; and so it shall be joined together. 8And the curious girdle of the ephod, which is upon it, shall be of the same, according to the work thereof; even of gold, of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen.28.8 curious: or, embroidered 9And thou shalt take two onyx stones, and grave on them the names of the children of Israel: 10Six of their names on one stone, and the other six names of the rest on the other stone, according to their birth. 11With the work of an engraver in stone, like the engravings of a signet, shalt thou engrave the two stones with the names of the children of Israel: thou shalt make them to be set in ouches of gold. 12And thou shalt put the two stones upon the shoulders of the ephod for stones of memorial unto the children of Israel: and Aaron shall bear their names before the LORD upon his two shoulders for a memorial.

13¶ And thou shalt make ouches of gold; 14And two chains of pure gold at the ends; of wreathen work shalt thou make them, and fasten the wreathen chains to the ouches.

15¶ And thou shalt make the breastplate of judgment with cunning work; after the work of the ephod thou shalt make it; of gold, of blue, and of purple, and of scarlet, and of fine twined linen, shalt thou make it. 16Foursquare it shall be being doubled; a span shall be the length thereof, and a span shall be the breadth thereof. 17And thou shalt set in it settings of stones, even four rows of stones: the first row shall be a sardius, a topaz, and a carbuncle: this shall be the first row.28.17 set…: Heb. fill in it fillings of stone28.17 sardius: or, ruby 18And the second row shall be an emerald, a sapphire, and a diamond. 19And the third row a ligure, an agate, and an amethyst. 20And the fourth row a beryl, and an onyx, and a jasper: they shall be set in gold in their inclosings.28.20 inclosings: Heb. fillings 21And the stones shall be with the names of the children of Israel, twelve, according to their names, like the engravings of a signet; every one with his name shall they be according to the twelve tribes.

22¶ And thou shalt make upon the breastplate chains at the ends of wreathen work of pure gold. 23And thou shalt make upon the breastplate two rings of gold, and shalt put the two rings on the two ends of the breastplate. 24And thou shalt put the two wreathen chains of gold in the two rings which are on the ends of the breastplate. 25And the other two ends of the two wreathen chains thou shalt fasten in the two ouches, and put them on the shoulderpieces of the ephod before it.

26¶ And thou shalt make two rings of gold, and thou shalt put them upon the two ends of the breastplate in the border thereof, which is in the side of the ephod inward. 27And two other rings of gold thou shalt make, and shalt put them on the two sides of the ephod underneath, toward the forepart thereof, over against the other coupling thereof, above the curious girdle of the ephod. 28And they shall bind the breastplate by the rings thereof unto the rings of the ephod with a lace of blue, that it may be above the curious girdle of the ephod, and that the breastplate be not loosed from the ephod. 29And Aaron shall bear the names of the children of Israel in the breastplate of judgment upon his heart, when he goeth in unto the holy place, for a memorial before the LORD continually.

30¶ And thou shalt put in the breastplate of judgment the Urim and the Thummim; and they shall be upon Aaron’s heart, when he goeth in before the LORD: and Aaron shall bear the judgment of the children of Israel upon his heart before the LORD continually.

31¶ And thou shalt make the robe of the ephod all of blue. 32And there shall be an hole in the top of it, in the midst thereof: it shall have a binding of woven work round about the hole of it, as it were the hole of an habergeon, that it be not rent.

33¶ And beneath upon the hem of it thou shalt make pomegranates of blue, and of purple, and of scarlet, round about the hem thereof; and bells of gold between them round about:28.33 hem: or, skirts 34A golden bell and a pomegranate, a golden bell and a pomegranate, upon the hem of the robe round about. 35And it shall be upon Aaron to minister: and his sound shall be heard when he goeth in unto the holy place before the LORD, and when he cometh out, that he die not.

36¶ And thou shalt make a plate of pure gold, and grave upon it, like the engravings of a signet, HOLINESS TO THE LORD. 37And thou shalt put it on a blue lace, that it may be upon the mitre; upon the forefront of the mitre it shall be. 38And it shall be upon Aaron’s forehead, that Aaron may bear the iniquity of the holy things, which the children of Israel shall hallow in all their holy gifts; and it shall be always upon his forehead, that they may be accepted before the LORD.

39¶ And thou shalt embroider the coat of fine linen, and thou shalt make the mitre of fine linen, and thou shalt make the girdle of needlework.

40¶ And for Aaron’s sons thou shalt make coats, and thou shalt make for them girdles, and bonnets shalt thou make for them, for glory and for beauty. 41And thou shalt put them upon Aaron thy brother, and his sons with him; and shalt anoint them, and consecrate them, and sanctify them, that they may minister unto me in the priest’s office.28.41 consecrate…: Heb. fill their hand 42And thou shalt make them linen breeches to cover their nakedness; from the loins even unto the thighs they shall reach:28.42 their…: Heb. flesh of their nakedness28.42 reach: Heb. be 43And they shall be upon Aaron, and upon his sons, when they come in unto the tabernacle of the congregation, or when they come near unto the altar to minister in the holy place; that they bear not iniquity, and die: it shall be a statute for ever unto him and his seed after him.