Kutoka 27 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 27:1-21

Madhabahu Ya Sadaka Ya Kuteketezwa

(Kutoka 38:1-7)

127:1 Kut 20:24; 40:6; 1Fal 8:64“Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake kiwe dhiraa tatu;27:1 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tano,27:1 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. na upana wake dhiraa tano. 227:2 Kut 29:12; 30:2; 37:25; Law 4:7; 1Fal 1:50; 2:28; Za 118:27; Yer 17:1; Eze 43:15; Amo 3:14; Zek 9:15Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana, na ufunike madhabahu kwa shaba. 327:3 Hes 7:13; 1Fal 7:40-45; 2Fal 12:13; Hes 4:14; 1Nya 28:17; Yer 52:18Tengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama, na vyombo vya kuchukulia moto. 4Kisha tengenezea hayo madhabahu wavu wa shaba, na utengeneze pete za shaba kwenye kila moja ya hizo pembe nne za huo wavu. 5Weka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu. 627:6 Kut 25:13-14, 28Tengeneza mipiko ya mti wa mshita kwa ajili ya madhabahu, na uifunike kwa shaba. 727:7 Hes 4:15; Isa 52:11Hiyo mipiko itaingizwa kwenye zile pete ili iwe pande mbili za madhabahu inapobebwa. 827:8 Kut 25:9, 40; Ebr 8:5; Mdo 7:44Tengeneza madhabahu yawe na uvungu ndani yake ukitumia mbao. Utaitengeneza sawasawa na vile ulivyoonyeshwa mlimani.

Ua Wa Kukutania

(Kutoka 38:9-20)

927:9 Kut 35:17; 40:8, 33; Law 6:16, 26; Eze 40:14; 42:1“Tengeneza ua kwa ajili ya Hema la Kukutania. Upande wa kusini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja,27:9 Dhiraa 100 ni sawa na mita 45. na utakuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri, 10pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 11Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, nao utakuwa na mapazia, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.

12“Upande wa magharibi wa ua utakuwa na upana wa dhiraa hamsini,27:12 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. nao utakuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi. 13Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, ua pia utakuwa na upana wa dhiraa hamsini. 14Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yatakuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 15Kutakuwepo tena na mapazia ya dhiraa kumi na tano27:15 Dhiraa 15 ni sawa na mita 6.75. kwa upande mwingine wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.

1627:16 Kut 40:33; 36:37“Kuhusu ingilio la ua, weka pazia lenye urefu wa dhiraa ishirini27:16 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne na vitako vinne. 17Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na tepe na kulabu za fedha, na vitako vya shaba. 18Ua wa kukutania utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini, ukiwa na mapazia ya kitani yaliyosokotwa vizuri yenye urefu wa dhiraa tano kwenda juu na vitako vya shaba. 19Vyombo vingine vyote vinavyotumika katika maskani kwa shughuli yoyote, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua, vitakuwa vya shaba.

Mafuta Ya Kinara Cha Taa

(Walawi 24:1-4)

2027:20 Kut 25:6; Law 24:2“Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili zile taa ziwake mfululizo. 2127:21 Kut 28:43; 29:42; 30:36; 33:7; Law 6:26; 8:3, 31; Hes 31:54; Yos 18:1; 1Fal 1:38-39; Kut 16:34; 25:37; 29:9; 30:21; Law 3:17; 16:34; 17:7; Hes 18:23; 19:21; 1Sam 30:25Katika Hema la Kukutania, nje ya pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, Aroni na wanawe watahakikisha kuwa taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Bwana. Hili litakuwa agizo la milele miongoni mwa Waisraeli kwa vizazi vyote vijavyo.

Swedish Contemporary Bible

2 Moseboken 27:1-21

Altaret

(2 Mos 38:1-7)

1Du ska också göra ett fyrkantigt altare av akacieträ, 2,5 meter i kvadrat och 1,5 meter högt. 2Utforma altaret med horn i de fyra hörnen och drag över alltsammans med koppar. 3Du ska göra askhinkar, skovlar, skålar, eldgafflar och fyrfat, allesammans av koppar. 4Sedan ska du göra ett galler, ett kopparnät med en ring i varje hörn 5och sätta gallret nertill, så att nätet når upp till mitten av altaret. 6Gör bärstänger av akacieträ, överdragna med koppar, 7som du skjuter in i ringarna på sidorna av altaret, så att man kan bära det. 8Altaret måste vara öppet inuti, gjort av plankor, och det ska göras precis som du fick se på berget.

Förgården

(2 Mos 38:9-20)

9Du ska göra en förgård till boningen. På södra sidan ska det vara förhängen av tvinnat fint lingarn, och de ska vara 50 meter långa på den sidan, 10med 20 stolpar och 20 socklar av koppar. Stolparnas krokar och band ska vara av silver. 11På samma sätt ska det vara på den norra sidan, 50 meter långa förhängen med 20 stolpar och 20 socklar av koppar och med krokar och band av silver.

12Västra sidan av förgården ska ha förhängen som är 25 meter långa med tio stolpar och tio socklar. 13Östra sidan ska också vara 25 meter. 14Förhängena ska vara sju och en halv meter åt ena hållet med tre stolpar och tre socklar, 15likaså åt andra hållet med tre stolpar och tre socklar.

16Ingången till förgården ska ha ett förhänge som är 10 meter långt och gjort av brokigt tyg med blått, purpurrött, karmosinrött och tvinnat fint lingarn, fäst vid fyra stolpar på fyra socklar. 17Alla stolparna runt förgården ska vara försedda med band och krokar av silver och socklar av koppar. 18Förgården ska vara 50 meter lång och 25 meter bred med ett 2,5 meter högt förhänge av tvinnat fint lingarn. Socklarna ska vara av koppar.

19Alla tillbehör för tjänsten i boningen och alla pluggar där och till förgården ska göras av koppar.

Oljan till lampstället

(3 Mos 24:1-4)

20Säg till Israels folk att skaffa fram ren olja av pressade oliver till lampstället, så att lamporna ständigt kan brinna. 21I uppenbarelsetältet, utanför förhänget som hänger framför förbundstecknet, ska Aron och hans söner sköta om dem varje kväll och morgon så att de brinner natten igenom inför Herren. Detta är en bestående stadga som ska gälla för Israel generation efter generation.