Kutoka 27 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 27:1-21

Madhabahu Ya Sadaka Ya Kuteketezwa

(Kutoka 38:1-7)

127:1 Kut 20:24; 40:6; 1Fal 8:64“Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake kiwe dhiraa tatu;27:1 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tano,27:1 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. na upana wake dhiraa tano. 227:2 Kut 29:12; 30:2; 37:25; Law 4:7; 1Fal 1:50; 2:28; Za 118:27; Yer 17:1; Eze 43:15; Amo 3:14; Zek 9:15Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana, na ufunike madhabahu kwa shaba. 327:3 Hes 7:13; 1Fal 7:40-45; 2Fal 12:13; Hes 4:14; 1Nya 28:17; Yer 52:18Tengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama, na vyombo vya kuchukulia moto. 4Kisha tengenezea hayo madhabahu wavu wa shaba, na utengeneze pete za shaba kwenye kila moja ya hizo pembe nne za huo wavu. 5Weka wavu huo chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu. 627:6 Kut 25:13-14, 28Tengeneza mipiko ya mti wa mshita kwa ajili ya madhabahu, na uifunike kwa shaba. 727:7 Hes 4:15; Isa 52:11Hiyo mipiko itaingizwa kwenye zile pete ili iwe pande mbili za madhabahu inapobebwa. 827:8 Kut 25:9, 40; Ebr 8:5; Mdo 7:44Tengeneza madhabahu yawe na uvungu ndani yake ukitumia mbao. Utaitengeneza sawasawa na vile ulivyoonyeshwa mlimani.

Ua Wa Kukutania

(Kutoka 38:9-20)

927:9 Kut 35:17; 40:8, 33; Law 6:16, 26; Eze 40:14; 42:1“Tengeneza ua kwa ajili ya Hema la Kukutania. Upande wa kusini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja,27:9 Dhiraa 100 ni sawa na mita 45. na utakuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri, 10pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 11Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja, nao utakuwa na mapazia, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.

12“Upande wa magharibi wa ua utakuwa na upana wa dhiraa hamsini,27:12 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. nao utakuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi. 13Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, ua pia utakuwa na upana wa dhiraa hamsini. 14Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yatakuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 15Kutakuwepo tena na mapazia ya dhiraa kumi na tano27:15 Dhiraa 15 ni sawa na mita 6.75. kwa upande mwingine wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu.

1627:16 Kut 40:33; 36:37“Kuhusu ingilio la ua, weka pazia lenye urefu wa dhiraa ishirini27:16 Dhiraa 20 ni sawa na mita 9. la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne na vitako vinne. 17Nguzo zote zinazozunguka ua zitakuwa na tepe na kulabu za fedha, na vitako vya shaba. 18Ua wa kukutania utakuwa na urefu wa dhiraa mia moja na upana wa dhiraa hamsini, ukiwa na mapazia ya kitani yaliyosokotwa vizuri yenye urefu wa dhiraa tano kwenda juu na vitako vya shaba. 19Vyombo vingine vyote vinavyotumika katika maskani kwa shughuli yoyote, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua, vitakuwa vya shaba.

Mafuta Ya Kinara Cha Taa

(Walawi 24:1-4)

2027:20 Kut 25:6; Law 24:2“Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi ya zeituni yaliyokamuliwa kwa ajili ya mwanga ili zile taa ziwake mfululizo. 2127:21 Kut 28:43; 29:42; 30:36; 33:7; Law 6:26; 8:3, 31; Hes 31:54; Yos 18:1; 1Fal 1:38-39; Kut 16:34; 25:37; 29:9; 30:21; Law 3:17; 16:34; 17:7; Hes 18:23; 19:21; 1Sam 30:25Katika Hema la Kukutania, nje ya pazia lililo mbele ya Sanduku la Ushuhuda, Aroni na wanawe watahakikisha kuwa taa hizo zinawaka kuanzia jioni mpaka asubuhi mbele za Bwana. Hili litakuwa agizo la milele miongoni mwa Waisraeli kwa vizazi vyote vijavyo.

New International Version – UK

Exodus 27:1-21

The altar of burnt offering

1‘Build an altar of acacia wood, three cubits27:1 That is, about 1.4 metres high; it is to be square, five cubits long and five cubits wide.27:1 That is, about 2.3 metres long and wide 2Make a horn at each of the four corners, so that the horns and the altar are of one piece, and overlay the altar with bronze. 3Make all its utensils of bronze – its pots to remove the ashes, and its shovels, sprinkling bowls, meat forks and firepans. 4Make a grating for it, a bronze network, and make a bronze ring at each of the four corners of the network. 5Put it under the ledge of the altar so that it is halfway up the altar. 6Make poles of acacia wood for the altar and overlay them with bronze. 7The poles are to be inserted into the rings so they will be on two sides of the altar when it is carried. 8Make the altar hollow, out of boards. It is to be made just as you were shown on the mountain.

The courtyard

9‘Make a courtyard for the tabernacle. The south side shall be a hundred cubits27:9 That is, about 45 metres; also in verse 11 long and is to have curtains of finely twisted linen, 10with twenty posts and twenty bronze bases and with silver hooks and bands on the posts. 11The north side shall also be a hundred cubits long and is to have curtains, with twenty posts and twenty bronze bases and with silver hooks and bands on the posts.

12‘The west end of the courtyard shall be fifty cubits27:12 That is, about 23 metres; also in verse 13 wide and have curtains, with ten posts and ten bases. 13On the east end, towards the sunrise, the courtyard shall also be fifty cubits wide. 14Curtains fifteen cubits27:14 That is, about 6.8 metres; also in verse 15 long are to be on one side of the entrance, with three posts and three bases, 15and curtains fifteen cubits long are to be on the other side, with three posts and three bases.

16‘For the entrance to the courtyard, provide a curtain twenty cubits27:16 That is, about 9 metres long, of blue, purple and scarlet yarn and finely twisted linen – the work of an embroiderer – with four posts and four bases. 17All the posts around the courtyard are to have silver bands and hooks, and bronze bases. 18The courtyard shall be a hundred cubits long and fifty cubits wide,27:18 That is, about 45 metres long and 23 metres wide with curtains of finely twisted linen five cubits27:18 That is, about 2.3 metres high, and with bronze bases. 19All the other articles used in the service of the tabernacle, whatever their function, including all the tent pegs for it and those for the courtyard, are to be of bronze.

Oil for the lampstand

20‘Command the Israelites to bring you clear oil of pressed olives for the light so that the lamps may be kept burning. 21In the tent of meeting, outside the curtain that shields the ark of the covenant law, Aaron and his sons are to keep the lamps burning before the Lord from evening till morning. This is to be a lasting ordinance among the Israelites for the generations to come.