Kutoka 26 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 26:1-37

Maskani Ya Mungu

(Kutoka 36:8-38)

126:1 Kut 29:42; 40:2; Law 8:10; Hes 1:50; Yos 22:19-20; 2Sam 7:2; 1Fal 1:30; Mdo 7:44; Ebr 8:2-5; 13:10; Ufu 21:3; Kut 25:18“Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo. 2Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane,26:2 Dhiraa 28 ni sawa na mita 13. na upana wa dhiraa nne26:2 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. 326:3 1Kor 12:4-12Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano. 426:4 Efe 4:13; Kol 2:2, 19Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho. 5Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane. 6Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.

726:7 Kut 36:14“Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani. 8Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini,26:8 Dhiraa 30 ni sawa na mita 13.5. na upana wa dhiraa nne. 9Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani. 10Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine. 11Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja. 12Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema. 13Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika. 1426:14 Kut 36:19; Hes 3:25; 4:25Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.26:14 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili.

15“Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani. 16Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi26:16 Dhiraa 10 ni sawa na mita 4.5. na upana wa dhiraa moja na nusu, 17zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii. 18Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani, 1926:19 Kut 38:27kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi. 20Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini 21na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili. 22Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani, 23na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali. 24Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana. 25Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.

2626:26 Kut 36:31; Rum 15:1; Gal 6:2“Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani, 27matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani. 28Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine. 29Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.

3026:30 Kut 40:2; 25:9; Hes 9:15; Ebr 8:5; Mdo 7:44; Ebr 8:5“Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.

3126:31 Hes 4:5; 2Nya 3:14; Mt 27:51; Lk 23:45; Ebr 9:3; Kut 25:18; 36:35; Law 16:2; Kut 25:18; 36:35“Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia. 32Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha. 3326:33 Kut 27:21; 35:12; 40:2-3, 21; Law 16:2; Hes 3:31; 4:5; 2Nya 3:14; Law 16:2, 16; 1Fal 6:16; 7:50; 8:6; 2Nya 3:8; 5:7; Eze 41:5; Ebr 9:2-3Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu. 3426:34 Kut 25:21; 30:6; 37:6; Law 16:2; Ebr 9:5Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu. 3526:35 Kut 25:23; Ebr 9:2; Kut 25:31Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.

3626:36 Kut 35:15; 40:5; 28; Za 45:14; Eze 16:10; 26:16; 27:7“Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. 3726:37 Kut 38:1Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.

Bibelen på hverdagsdansk

2. Mosebog 26:1-37

Den hellige bolig

1Den hellige bolig26,1 Også kaldet „tabernaklet”. Det havde form som en stor kasse, 10 alen høj, 10 alen bred og 30 alen lang. Med andre ord ca. 4,5m x 4,5m x 13,5m. skal have en teltdug lavet af ti stykker fintvævet linned med blå, violette og purpurrøde broderier på. Du skal få en dygtig tekstilkunstner til at lave billeder af keruber på dem. 2Alle de ti stykker skal have samme mål: 12,6 m i længden og 1,8 m i bredden. 3Sy stykkerne sammen fem og fem langs siden, så der bliver to store stykker. 4Lav derefter nogle løkker af blåt garn i kanten af den sidste bane på hvert af de to sammensyede stykker, så de kan hægtes sammen. 5Der skal være 50 løkker på hvert stykke lige over for hinanden. 6Lav dernæst 50 guldkroge, som skal sættes i de 50 par løkker. På den måde kan den hellige bolig dækkes af én inderteltdug.

7-8Yderteltdugen skal laves af gedehårstæpper. Der skal være 11 tæppebaner i alt, hver af dem 13,5 m i længden og 1,8 m i bredden. 9Sy de fem tæppebaner sammen til ét stykke, og de seks til et andet stykke. Den sjette tæppebane skal ligge dobbelt over indgangen til boligen. 10-11Sæt derefter 50 løkker i hver af de yderste baner på de to store tæpper, så de kan hægtes sammen med 50 bronzehægter. På den måde bliver de to stykker sat sammen til ét. 12Yderteltdugen vil rage ud over inderteltet med en halv tæppebane ved bagsiden. 13På de to langsider vil det yderste dække rage 45 cm ud over det inderste.

14Dernæst skal du lave endnu to lag som yderligere tagbeklædning, det nederste af rødfarvede vædderskind og det øverste af kraftigt læder.

15Boligens vægge skal bestå af akacietræsmoduler. 16Hvert modul skal være 4,5 m højt og 67 cm bredt 17og have en tap ved hver side forneden til at samle modulerne med. Sådan skal alle panelerne laves. 18Lav 20 moduler til boligens sydside 19og 40 sokler af sølv, to sokler under hvert modul. 20Nordsiden skal også bestå af 20 moduler 21med tilsvarende 40 sokler af sølv, to sokler under hvert modul. 22Vestsiden skal have seks almindelige moduler 23og to smallere moduler i hvert hjørne. 24Hjørnemodulerne skal kunne samles ved hjælp af beslag forneden og en ring foroven. 25Det vil sige, at der i vestsiden af boligen er otte moduler og 16 sokler af sølv, to sokler under hvert modul.

26-27Lav derefter 15 tværstænger af akacietræ til at sikre rækken af moduler, fem tværstænger til hver af boligens tre trævægge, både de to lange sidevægge og den kortere endevæg. 28De tværstænger som ligger i midten, halvvejs oppe ad væggen, skal gå i hele væggens længde. 29Belæg modulerne med guld og støb guldringe, som stængerne kan sidde fast i. Belæg ligeledes tværstængerne med guld. 30Rejs boligen på den måde, jeg har vist dig her på bjerget.

31Til boligens indre skal du lave et forhæng af fintvævet linned, og du skal få en dygtig tekstilkunstner til at brodere keruber på forhænget med blåt, violet og purpurrødt garn. 32Lav så fire akaciestolper belagt med guld og med kroge øverst oppe af guld. Stolperne skal stå inde i boligen på fire sokler af sølv. 33Forhænget skal så hænge i guldkrogene på stolperne. Bag forhænget skal du stille arken med stentavlerne, hvorpå Guds bud er skrevet. Forhænget skal således adskille det hellige, yderste rum i boligen, og det allerhelligste, inderste rum.

34Læg derefter forsoningslåget på plads oven på arken i det allerhelligste rum. 35Placer bordet og lysestagen på den anden side af forhænget i det hellige rum, bordet langs den nordlige væg og lysestagen ved den sydlige væg.

36Til at lave forhænget ved boligens indgang skal du bruge fintvævet linned og give en dygtig tekstilkunstner frie hænder til at udsmykke forhænget med blåt, violet og purpurrødt garn. 37Ved hjælp af guldkroge skal du hænge forhænget op på fem akaciestolper belagt med guld, og støb fem sokler af bronze til stolperne.