Kutoka 25 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 25:1-40

Sadaka Kwa Ajili Ya Maskani Ya Mungu

(Kutoka 35:4-9)

125:1 Kut 35:21, 29; 36:2; 2Fal 12:4; 1Nya 29:5, 9; 2Nya 24:10; 29:31; Ezr 2:68; Neh 7:70; 2Kor 8:11; 9:7Bwana akamwambia Mose, 2“Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa. 3Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba; 425:4 Kut 28:4-8nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi; 525:5 Hes 4:6-10; Kum 10:3ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo;25:5 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. mbao za mshita; 625:6 Kut 27:20; 30:22-32; 35:28; 39:37; Hes 4:16; Kut 30:11; Law 16:12; Hes 7:14; 2Nya 13:11mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri; 725:7 Kut 28:4-14; 29:5; Amu 8:27; Hos 3:4; Law 8:8; Kut 28:15-30na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.

825:8 Kut 36:1-5; Law 4:6; 10:4-7; 21:12; 23; Hes 3:28; Ebr 9:1-2; Law 26:11-12; Hes 5:3; Kum 12:11; 1Fal 6:13; Zek 2:10; 2Kor 7:16; Ufu 21:3“Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao. 925:9 Kut 26:30; 27:8; 31:11; 39:42-43; 1Nya 28:11, 19; Mdo 7:44; Ebr 8:5; Hes 8:4Tengeneza hema hili na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonyesha.

Sanduku La Agano

(Kutoka 37:1-9)

1025:10 Kum 10:1-5; 1Fal 6:19; Ebr 9:4“Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu,25:10 Dhiraa mbili na nusu ni sawa na sentimita 112.5. upana wa dhiraa moja na nusu,25:10 Dhiraa moja na nusu ni sawa na sentimita 67.5. na kimo cha dhiraa moja na nusu. 1125:11 Kut 30:3-4Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka. 12Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine. 1325:13 Kut 27:6; 30:5; 37:28Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu. 1425:14 Kut 27:7; 40:20; 1Nya 15:15Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba. 1525:15 1Fal 8:8Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa. 1625:16 Kut 16:34; 1Fal 8:8; Kum 31:26Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.

1725:17 Law 16:13; Rum 3:25“Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu. 1825:18 Kut 26:1, 35; 1Fal 6:23-27; 2Nya 3:10-13; Ebr 9:5Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko. 19Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili. 2025:20 Mwa 3:24; Kut 37:9; 1Fal 8:7; 1Nya 28:18; Ebr 9:5Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, yakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko. 2125:21 Kut 26:34; 40:20; Kum 10:5; Kut 16:34; Ebr 9:4Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku. 2225:22 Hes 7:89; 1Sam 4; 4; 2Sam 6:2; 22:11; 2Fal 19:15; 1Nya 13:6; 28:18; Za 18:10; Isa 37:16; Kut 19:3; 29:42; 30:6, 36; Law 16:2; Hes 17:4Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walioko juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakapokutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.

Meza Ya Mikate Ya Wonyesho

(Kutoka 37:10-16)

2325:23 Yer 3:16; Kut 26:35; 40:4, 22; Law 24:6; Hes 3:31; 1Fal 7:48; 1Nya 28:16; 2Nya 4:8, 19; Eze 41:22; 44:16; Ebr 9:2“Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili,25:23 Dhiraa mbili ni sawa na sentimita 90. upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu. 24Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote. 25Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne,25:25 Nyanda nne ni sawa na sentimita 8. na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote. 26Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne. 27Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza. 28Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza. 2925:29 Hes 4:7Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka. 3025:30 Kut 35:13; 39:36; 40:4, 23; Law 24:5-9; Hes 4:7; 1Sam 21:4-6; 1Fal 7:48; 1Nya 23:29Utaweka mikate ya Wonyesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.

Kinara Cha Taa

(Kutoka 37:17-24)

3125:31 Kut 26:35; 31:8; 35:14; 39:37; Law 24:4; Hes 3:31; 1Fal 7:49; 2Nya 4:7; Zek 4:2; Ebr 9:2; Ufu 1:12“Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja. 3225:32 Hes 8:4; Kut 37:18, 19Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine. 33Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa. 34Juu ya kinara chenyewe vitakuwepo vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake. 35Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla. 3625:36 Hes 8:4Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.

3725:37 Kut 27:21; 30:8; Law 24:3-4; Hes 8:2; 1Sam 3:3; 2Nya 13:11; Ufu 1:12“Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake. 3825:38 Hes 4:9Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi. 39Utatumia talanta moja25:39 Talanta moja ya dhahabu ni sawa na kilo 34. ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote. 4025:40 Hes 8:4; Mdo 7:44; Ebr 8:5; Kut 26:30; 1Nya 28:11, 19Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano ulioonyeshwa kule mlimani.

New International Reader’s Version

Exodus 25:1-40

Offerings for the Holy Tent

1The Lord said to Moses, 2“Tell the people of Israel to bring me an offering. You must receive the offering for me from everyone whose hearts move them to give.

3“Here are the offerings you must receive from them.

“gold, silver and bronze

4blue, purple and bright red yarn and fine linen

goat hair

5ram skins that are dyed red

another kind of strong leather

acacia wood

6olive oil for the lights

spices for the anointing oil and for the sweet-smelling incense

7onyx stones and other jewels for the linen apron and chest cloth

8“Have them make a sacred tent for me. I will live among them. 9Make the holy tent and everything that belongs to it. Make them exactly like the pattern I will show you.

The Ark of the Covenant Law

10“Have them make an ark out of acacia wood. It must be a chest three feet nine inches long and two feet three inches wide and high. 11Cover it inside and outside with pure gold. Put a strip of gold around it. 12Make four gold rings for it. Join them to its four bottom corners. Put two rings on one side and two rings on the other. 13Then make poles out of acacia wood. Cover them with gold. 14Put the poles through the rings on the sides of the ark to carry it. 15The poles must remain in the rings of the ark. Do not remove them. 16I will give you the tablets of the covenant law. When I do, put them into the ark.

17“Make its cover out of pure gold. The cover is the place where sin will be paid for. Make it three feet nine inches long and two feet three inches wide. 18Make two cherubim out of hammered gold at the ends of the cover. 19Put one of the cherubim on each end of it. Make the cherubim part of the cover itself. 20They must have their wings spread up over the cover. The cherubim must face each other and look toward the cover. 21Place the cover on top of the ark. I will give you the tablets of the covenant law. Put them in the ark. 22The ark is where the tablets of the covenant law are kept. I will meet with you above the cover between the two cherubim that are over the ark. There I will give you all my commands for the Israelites.

The Table for the Holy Bread

23“Make a table out of acacia wood. Make it three feet long, one foot six inches wide and two feet three inches high. 24Cover it with pure gold. Put a strip of gold around it. 25Also make a rim around it three inches wide. Put a strip of gold around the rim. 26Make four gold rings for the table. Join them to the four corners, where the four legs are. 27The rings must be close to the rim. They must hold the poles that will be used to carry the table. 28Make the poles out of acacia wood. Cover them with gold. Use them to carry the table. 29Make its plates and dishes out of pure gold. Also make its pitchers and bowls out of pure gold. Use the pitchers and bowls to pour out drink offerings. 30Put the holy bread on the table. It must be near my holy throne on the ark of the covenant law at all times.

The Gold Lampstand

31“Make a lampstand out of pure gold. Hammer out its base and stem. Its buds, blossoms and cups must branch out from it. They must be part of the lampstand itself. 32Six branches must come out from the sides of the lampstand. Make three on one side and three on the other. 33On one branch make three cups that are shaped like almond flowers with buds and blossoms. Then put three on the next branch. Do the same with all six branches that come out from the lampstand. 34On the lampstand there must be four cups that are shaped like almond flowers with buds and blossoms. 35One bud must be under the first pair of branches that come out from the lampstand. Put a second bud under the second pair. And put a third bud under the third pair. Make a total of six branches. 36The buds and branches must come out from the lampstand. The whole lampstand must be one piece hammered out of pure gold.

37“Then make its seven lamps. Set them up on it so that they light the space in front of it. 38The trays and wick cutters must be made out of pure gold. 39Use 75 pounds of pure gold to make the lampstand and everything used with it. 40Be sure to make everything just like the pattern I showed you on the mountain.