Kutoka 20 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 20:1-26

Amri Kumi

(Kumbukumbu 5:1-21)

120:1 Kum 10:4; Neh 9:13; Za 119:9; 147:19; Mal 4:4Ndipo Mungu akasema maneno haya yote:

220:2 Mwa 17:7; Kut 16:12; Law 19:2; 20:7; Isa 43:3; Eze 20:19; Mwa 15:7; Kut 6:6; 13:3; Eze 20:6“Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa Misri, kutoka nchi ya utumwa.

320:3 Kut 34:14; Kum 6:14; 13; 10; 2Fal 17:35; Za 44:20; 81:9; Yer 1:16; 7:6-9; 11:13; 19:4; 25:6Usiwe na miungu mingine ila mimi.

420:4 Kut 32:8; 34:17; Law 19:4; 26:1; Kum 4:15-23; 27:15; 2Sam 7:22; 1Fal 14:9; 2Fal 17:12; Isa 42:8; 44:9Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni, au duniani chini, au ndani ya maji. 520:5 Kut 23:13; Yos 23:7; Amu 6:10; 2Fal 17:35; Isa 44:15-19; 46:6; Kut 34:14; Kum 4:24; Yos 24:19; Mwa 9:25; Law 26:39; Kut 34:7; Hes 14:18; Yer 32:18Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 620:6 Kut 34:7; Hes 14:18; Kum 7:9; Yer 32:18; Lk 1:50; Rum 11:28lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.

720:7 Kut 22:28; Law 18:21; 19:12; 22:2; 24:11, 16; Kum 6:13; 10:20; Ay 2:5-9; Za 63:11; Isa 8:21; Eze 20:39; 39:7; Mt 5:33Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.

820:8 Kut 16:23; 31:13-16; 35:3; Law 19:3, 30; 26:2; Isa 56:2; Yer 17:21-27; Eze 22:8Ikumbuke siku ya Sabato, uitakase. 920:9 Kut 23:12; 31:13-17; 34:21; 35:2-3; Law 23:3; Lk 13:14Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote, 1020:10 Mwa 2:3; Kut 31:14; Law 23:38; Hes 28:9; Isa 56:2; Eze 20:12, 20lakini siku ya saba ni Sabato kwa Bwana Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wako wa kiume au wa kike, wala wanyama wako, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. 1120:11 Mwa 1:3–2:1; 2:2; Kut 31:17; Eze 4:4Kwa kuwa kwa siku sita, Bwana aliumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo, lakini akapumzika siku ya saba. Kwa hiyo Bwana akaibariki siku ya Sabato na kuifanya takatifu.

1220:12 Kum 5:16; Mt 15:4; 19:19; Mk 7:10; 10:19; Lk 18:20; Efe 6:2; Kum 6:2; Efe 6:3; Kum 11:9; 25:15; Yer 35:7Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.

1320:13 Mwa 4:23; Mt 5:21; 19:18; Lk 18:20; Rum 13:8-9; Yak 2:11Usiue.

1420:14 Law 18:20; 20:10; Hes 5:12, 13, 29; Mit 6:29-32; Mt 5:27; 19:18; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9; Yak 2:11Usizini.

1520:15 Law 19:11-13; Eze 18:7; Mt 19:18; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9Usiibe.

1620:16 Law 19:11; Yer 9:3-5; Kut 23:1, 7; Law 19:18; Za 50:20; 101:5; 119:29; Mt 19:18; Mk 10:19; Lk 3:14; 18:20Usimshuhudie jirani yako uongo.

1720:17 Lk 12:15; Rum 7:7; 13:9; Efe 5:3; Ebr 13:5Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wa kiume au wa kike, wala ngʼombe wake au punda wake, wala chochote kile alicho nacho jirani yako.”

Watu Wanaogopa

(Kumbukumbu 5:22-33)

1820:18 Kut 19:16-19; Kum 4:36; Isa 58:1; Yer 6:17; Eze 33:3; Ebr 12:1-19; Ufu 1:10; Kut 19:18; Mwa 3:10; Kut 14:31; 19:16Watu walipoona ngurumo na radi, na kusikia mlio wa tarumbeta, na kuuona mlima katika moshi, walitetemeka kwa woga. Wakasimama mbali 1920:19 Ay 37:4-5; 40:9; Za 29:3-4; Kum 5:23-27; 18:16; Gal 3:19na wakamwambia Mose, “Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini usimwache Mungu aseme nasi, la sivyo tutakufa.”

2020:20 Mwa 15:1; 22:1; Kum 4:10; 6:2; 10:12; Za 111:10; 128:1; Mit 1:7; Mhu 12:13; Isa 8:13; Ay 1:8; 2:3; 28:28; Mit 3:7; 8:13; 14:16; 16:6Mose akawaambia watu, “Msiogope! Mungu amekuja kuwajaribu, ili kwamba hofu ya Mungu iwakalie, msitende dhambi.”

2120:21 Kut 19:9; Kum 5:22; Za 81:8; 68:4; 97:2; Isa 19:1Watu wakabaki mbali, wakati Mose alipolisogelea lile giza nene mahali pale Mungu alipokuwa.

Sanamu Na Madhabahu

2220:22 Kum 5:24-26; Neh 9:13Kisha Bwana akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli hivi: ‘Mmejionea wenyewe kwamba nimesema nanyi kutoka mbinguni: 2320:23 Kut 22:20; 32:4, 8; 34:17; Kum 29:17-18; Neh 9:18Msijifanyizie miungu yoyote na kuilinganisha nami, msijitengenezee miungu ya fedha wala miungu ya dhahabu.

2420:24 Kut 27:1; 40:29; Hes 16:38; Kum 27:5; Yos 8:30; 2Fal 16:14; 2Nya 4:1; Eze 43:13; Mwa 8:20; Kut 18:12; Kum 12:5; 16:6, 11; 26:2; 1Fal 9:3; 2Fal 21:4-7; 2Nya 6:6; 12:13; Ezr 6:12; Mwa 12:2; 22:17“ ‘Utanitengenezea madhabahu ya udongo, na juu yake utoe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani, kondoo zako, mbuzi na ngʼombe zako. Popote nitakapofanya Jina langu liheshimiwe, nitakuja kwenu na kuwabariki. 2520:25 Yos 8:31; 1Fal 6:7Ikiwa unanitengenezea madhabahu ya mawe, usiijenge kwa mawe ya kuchonga, maana mkitumia chombo cha kuchongea mtaitia unajisi. 2620:26 Eze 43:17Msitumie ngazi kupandia kwenye madhabahu yangu, uchi wako usije ukadhihirika kwa chini.’

New International Reader’s Version

Exodus 20:1-26

God Gives His People the Ten Commandments

1Here are all the words God spoke. He said,

2“I am the Lord your God. I brought you out of Egypt. That is the land where you were slaves.

3“Do not put any other gods in place of me.

4“Do not make for yourself statues of gods that look like anything in the sky. They may not look like anything on the earth or in the waters either. 5Do not bow down to them or worship them. I, the Lord your God, am a jealous God. I cause the sins of the parents to affect their children. I will cause the sins of those who hate me to affect even their grandchildren and great-grandchildren. 6But for all time to come I show love to all those who love me and keep my commandments.

7“Do not misuse the name of the Lord your God. The Lord will find guilty anyone who misuses his name.

8“Remember to keep the Sabbath day holy. 9Do all your work in six days. 10But the seventh day is a sabbath to honor the Lord your God. Do not do any work on that day. The same command applies to your sons and daughters, your male and female servants, and your animals. It also applies to any outsiders who live in your towns. 11In six days the Lord made the heavens, the earth, the sea and everything in them. But he rested on the seventh day. So the Lord blessed the Sabbath day and made it holy.

12“Honor your father and mother. Then you will live a long time in the land the Lord your God is giving you.

13“Do not murder.

14“Do not commit adultery.

15“Do not steal.

16“Do not be a false witness against your neighbor.

17“Do not want to have anything your neighbor owns. Do not want to have your neighbor’s house, wife, male or female servant, ox or donkey.”

18The people saw the thunder and lightning. They heard the trumpet. They saw the mountain covered with smoke. They trembled with fear and stayed a long way off. 19They said to Moses, “Speak to us yourself. Then we’ll listen. But don’t let God speak to us. If he does, we’ll die.”

20Moses said to the people, “Don’t be afraid. God has come to test you. He wants you to have respect for him. That will keep you from sinning.”

21Moses approached the thick darkness where God was. But the people remained a long way off.

Worship the Lord

22Then the Lord said to Moses, “Here is what you must tell the people of Israel. Say to them, ‘You have seen for yourselves what I said to you from heaven. 23Do not put any other gods in place of me. Do not make silver or gold statues of them for yourselves.

24“ ‘Make an altar out of dirt for me. Sacrifice your burnt offerings and friendship offerings on it. Sacrifice your sheep, goats and cattle on it. I will come to you and bless you everywhere I cause my name to be honored. 25If you make an altar out of stones to honor me, do not build it with blocks of stone. You will make it “unclean” if you use a tool on it. 26Do not walk up steps to my altar. If you do, someone might see your naked body under your robes.’