Kutoka 19 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 19:1-25

Waisraeli Kwenye Mlima Sinai

119:1 Kut 6:6; Hes 3:14; 33:15Mnamo mwezi wa tatu baada ya Waisraeli kuondoka Misri, siku kama iyo hiyo, wakafika katika Jangwa la Sinai. 219:2 Kut 17:1; 36:1; Kum 5:2-4Baada ya kuondoka Refidimu, waliingia katika Jangwa la Sinai na Israeli wakapiga kambi pale jangwani mbele ya mlima.

319:3 Kut 20:21; 3:4; 25:22; Mdo 7:38Kisha Mose akakwea kwenda kwa Mungu, naye Bwana akamwita kutoka kwenye ule mlima akasema, “Hivi ndivyo utakavyosema na nyumba ya Yakobo na utakachowaambia watu wa Israeli: 419:4 Kum 29:2; Yos 24:7; Kum 32:11; Za 103:5; Isa 40:31; Yer 4:13; 48:40; Ufu 12:14; Kum 33:12; Isa 31:5; Eze 16:6‘Ninyi wenyewe mmeona nililofanya huko Misri, jinsi nilivyowabeba kwenye mbawa za tai na kuwaleta kwangu. 519:5 Kut 15:26; Kum 6:3; Za 78:10; Yer 7:23; Mwa 17:9; Kut 3:1; 8:22; 34:9; Kum 1:8; Tit 2:14; Kut 9:29; 1Kor 10:26Sasa kama mkinitii kikamilifu na kutunza Agano langu, basi ninyi mtakuwa mali yangu ya thamani kubwa miongoni mwa mataifa yote. Ijapokuwa dunia yote ni mali yangu, 619:6 Isa 61:6; 66; 21; 1Pet 2:5; Mwa 18:19; Law 11:45; Kum 4:27; 7:6; 26:19; 28:9; 29:13; 33:3; Isa 4:3; 62:12; Yer 2:3; Amo 3:2ninyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Haya ndiyo maneno utakayosema kwa wana wa Israeli.”

719:7 Kut 18:12; Law 4:15; 9:1; Hes 16:25; Kut 4:30; Isa 8:10Kwa hiyo Mose akarudi, akawaita wazee wa watu na kuwaambia maneno yote ambayo Bwana alikuwa amemwamuru ayaseme. 819:8 Kut 24:3-7; Kum 5:27; 26:17Watu wote wakajibu kwa pamoja, “Tutafanya kila kitu Bwana alichokisema.” Naye Mose akarudisha majibu yao kwa Bwana.

919:9 Kut 20:21; 24:15-16; 33:9; 34:5; Kum 4:11; 2Sam 22:10-12; 2Nya 6:1; Kut 4:5; Za 18:11; 97:2; 99:7; Mt 17:5; Kum 4:12, 36; Yn 12:29-30Bwana akamwambia Mose, “Nitakujia katika wingu zito, ili watu wanisikie nikinena nawe na kila mara waweke tumaini lao kwako.” Kisha Mose akamwambia Bwana yale ambayo watu walikuwa wamesema.

1019:10 Law 11:44; Hes 11:18; Isa 16:5; Yoe 2:16; Ebr 10:22; Mwa 35:2; Ufu 22:14Naye Bwana akamwambia Mose, “Nenda kwa watu ukawaweke wakfu leo na kesho. Waambie wafue nguo zao 1119:11 Mwa 11:5; Kut 3:1; 24:16; 31:18; 34:2-4, 29-32; Law 7:38; 26:46; 27:34; Hes 3:1; Dan 10:5; Neh 9:13; Gal 4:24-25na wawe tayari siku ya tatu, kwa sababu siku hiyo, Bwana atashuka juu ya mlima Sinai machoni pa watu wote. 12Weka mipaka kuzunguka mlima kwa ajili ya watu, uwaambie, ‘Mwe waangalifu, msije mkapanda mlimani au kuugusa. Yeyote atakayeugusa mlima hakika atauawa. 1319:13 Ebr 12:20; Yos 6:4; 1Nya 15:28; Za 81:3; 98:6; Kut 34:3Hakika atapigwa mawe au kupigwa mishale; mkono wa mtu hautamgusa. Akiwa mwanadamu au mnyama, hataruhusiwa kuishi.’ Ila tu wakati baragumu itakapopigwa kwa mfululizo, ndipo watu wote watakapopanda mlimani.”

1419:14 Mwa 35:2Baada ya Mose kushuka kutoka mlimani akawaendea watu na kuwaweka wakfu, wakafua nguo zao. 1519:15 1Sam 21:4; 1Kor 7:5Kisha akawaambia watu, “Jitayarisheni kwa ajili ya siku ya tatu. Mwanaume yeyote asimkaribie mwanamke.”

1619:16 1Sam 2:10; Isa 29:6; Ebr 12:18-19; Ufu 4:1; Mwa 3:10; 1Sam 13:7; 14:15; 28:5; Za 99:1; Ebr 12:21Asubuhi ya siku ya tatu kulikuwa na ngurumo na radi pamoja na wingu nene juu ya mlima na mlio mkubwa sana wa tarumbeta. Kila mmoja aliyekuwa kambini akatetemeka. 1719:17 Kum 4:11Kisha Mose akawaongoza watu kutoka kambini kukutana na Mungu, nao wakasimama chini ya mlima. 1819:18 Kut 20:18; Za 104:32; Isa 6:4; Ufu 15:8; Kut 3:2; 24:17; Law 9:24; Kum 4:11, 24, 33; 5:4; 9:3; 1Fal 18:24, 38; 1Nya 21:26; 2Nya 7:1; Za 18:8; Ebr 12:18; Mwa 19:28; Ufu 9:2; Amu 5:5; 2Sam 22:8; Za 68:8; Isa 2:19; 5:25; 41:15; 64:1; Yer 4:24; 10:10; Mik 1:4; Nah 1:5; Hab 3:6-10; Hag 2:6Mlima Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi, kwa sababu Bwana alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi kutoka kwenye tanuru kubwa na mlima wote ukatetemeka kwa nguvu nyingi, 1919:19 Kum 4:33; Neh 9:13; Za 81:7nayo sauti ya tarumbeta ikawa kubwa zaidi na zaidi. Kisha Mose akazungumza na sauti ya Bwana ikamjibu.

20Bwana akashuka juu ya Mlima Sinai na akamwita Mose apande juu mlimani. Kwa hiyo Mose akapanda juu, 2119:21 Kut 24:10-11; Hes 4:20; 1Sam 6:19naye Bwana akamwambia Mose, “Shuka ukawaonye watu ili wasijipenyeze kutafuta kumwona Bwana na wengi wao wakafa. 2219:22 Law 10:3; 1Sam 16:5; 2Nya 29:5; Yoe 2:16; 2Sam 6:7Hata makuhani, watakaomkaribia Bwana ni lazima wajiweke wakfu, la sivyo Bwana atawaadhibu.”

23Mose akamwambia Bwana, “Watu hawawezi kupanda mlima Sinai kwa sababu wewe mwenyewe ulituonya ukisema, ‘Wekeni mipaka kuuzunguka mlima na kuutenga kama patakatifu.’ ”

2419:24 Kut 24:1, 9Bwana akajibu, “Shuka ukamlete Aroni pamoja nawe. Lakini makuhani pamoja na watu wasije wakalazimisha kuja kwa Bwana, nisije nikawaadhibu.”

25Basi Mose akashuka kwa watu na kuwaambia lile aliloambiwa.

King James Version

Exodus 19:1-25

1In the third month, when the children of Israel were gone forth out of the land of Egypt, the same day came they into the wilderness of Sinai. 2For they were departed from Rephidim, and were come to the desert of Sinai, and had pitched in the wilderness; and there Israel camped before the mount. 3And Moses went up unto God, and the LORD called unto him out of the mountain, saying, Thus shalt thou say to the house of Jacob, and tell the children of Israel; 4Ye have seen what I did unto the Egyptians, and how I bare you on eagles’ wings, and brought you unto myself. 5Now therefore, if ye will obey my voice indeed, and keep my covenant, then ye shall be a peculiar treasure unto me above all people: for all the earth is mine: 6And ye shall be unto me a kingdom of priests, and an holy nation. These are the words which thou shalt speak unto the children of Israel.

7¶ And Moses came and called for the elders of the people, and laid before their faces all these words which the LORD commanded him. 8And all the people answered together, and said, All that the LORD hath spoken we will do. And Moses returned the words of the people unto the LORD.

9And the LORD said unto Moses, Lo, I come unto thee in a thick cloud, that the people may hear when I speak with thee, and believe thee for ever. And Moses told the words of the people unto the LORD.

10¶ And the LORD said unto Moses, Go unto the people, and sanctify them to day and to morrow, and let them wash their clothes, 11And be ready against the third day: for the third day the LORD will come down in the sight of all the people upon mount Sinai. 12And thou shalt set bounds unto the people round about, saying, Take heed to yourselves, that ye go not up into the mount, or touch the border of it: whosoever toucheth the mount shall be surely put to death: 13There shall not an hand touch it, but he shall surely be stoned, or shot through; whether it be beast or man, it shall not live: when the trumpet soundeth long, they shall come up to the mount.19.13 trumpet: or, cornet

14¶ And Moses went down from the mount unto the people, and sanctified the people; and they washed their clothes. 15And he said unto the people, Be ready against the third day: come not at your wives.

16¶ And it came to pass on the third day in the morning, that there were thunders and lightnings, and a thick cloud upon the mount, and the voice of the trumpet exceeding loud; so that all the people that was in the camp trembled. 17And Moses brought forth the people out of the camp to meet with God; and they stood at the nether part of the mount. 18And mount Sinai was altogether on a smoke, because the LORD descended upon it in fire: and the smoke thereof ascended as the smoke of a furnace, and the whole mount quaked greatly. 19And when the voice of the trumpet sounded long, and waxed louder and louder, Moses spake, and God answered him by a voice. 20And the LORD came down upon mount Sinai, on the top of the mount: and the LORD called Moses up to the top of the mount; and Moses went up. 21And the LORD said unto Moses, Go down, charge the people, lest they break through unto the LORD to gaze, and many of them perish.19.21 charge: Heb. contest 22And let the priests also, which come near to the LORD, sanctify themselves, lest the LORD break forth upon them. 23And Moses said unto the LORD, The people cannot come up to mount Sinai: for thou chargedst us, saying, Set bounds about the mount, and sanctify it. 24And the LORD said unto him, Away, get thee down, and thou shalt come up, thou, and Aaron with thee: but let not the priests and the people break through to come up unto the LORD, lest he break forth upon them. 25So Moses went down unto the people, and spake unto them.