Kutoka 14 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 14:1-31

Kuvuka Bahari Ya Shamu

1Ndipo Bwana akamwambia Mose, 2“Waambie Waisraeli wageuke nyuma na wapige kambi karibu na Pi-Hahirothi, kati ya Migdoli na bahari. Watapiga kambi kando ya bahari, mkabala na Baal-Sefoni. 3Farao atafikiri kwamba, ‘Hao Waisraeli wanatangatanga katika nchi kwa kuchanganyikiwa, nalo jangwa limewafungia.’ 414:4 Kut 4:21; Za 71:11; Kut 9:16; Rum 9:17, 22-23; Kut 6:2; 7:5; Eze 32:15Nami nitaufanya moyo wa Farao mgumu, naye atawafuatilia. Lakini nitajipatia utukufu kwa ajili yangu mwenyewe kupitia Farao na jeshi lake lote, nao Wamisri watajua kuwa mimi ndimi Bwana.” Kwa hiyo Waisraeli wakafanya hivyo.

514:5 Mwa 31:21; Za 105:25Mfalme wa Misri alipoambiwa kuwa Waisraeli wamekimbia, Farao na maafisa wake wakabadili nia zao kuhusu Waisraeli, wakasema, “Tumefanya nini? Tumewaachia Waisraeli waende zao na tumeukosa utumishi wao!” 6Kwa hiyo akaandaliwa gari lake la vita, naye akaenda pamoja na jeshi lake. 714:7 Kut 15:4Akachukua magari bora mia sita, pamoja na magari mengine yote ya Misri, pamoja na maafisa wa magari hayo yote. 814:8 Kut 11:10; Hes 33:2; Mdo 13:17Bwana akaufanya mgumu moyo wa Farao, mfalme wa Misri, kwa hiyo akawafuatia Waisraeli, waliokuwa wakiondoka Misri kwa ujasiri. 914:9 Mwa 47:17; Yos 24:6; Isa 43:17; Kut 15:9Nao Wamisri, yaani farasi wote wa Farao na magari ya vita, wapanda farasi na vikosi vya askari, wakawafuatia Waisraeli, wakawakuta karibu na Pi-Hahirothi, mkabala na Baal-Sefoni walipokuwa wamepiga kambi kando ya bahari.

1014:10 Kut 15:25; Yos 24:7; Neh 9:9; Za 5:2; 34:17; 50:15; 107:6, 28Farao alipokaribia, Waisraeli wakainua macho yao, wakawaona Wamisri wakija nyuma yao. Wakashikwa na hofu, wakamlilia Bwana. 1114:11 Kut 5:21; 16:13; 17:3; Hes 11:1; 14:22; 20:4; 21:5; Kum 9:7Wakamwambia Mose, “Je, ni kwamba hayakuwako makaburi huko Misri hata umetuleta tufe huku jangwani? Umetufanyia nini kututoa Misri? 1214:12 Kut 5:21; 15:24; 17:2; Za 106:7-8Hatukukuambia tulipokuwa huko Misri, tuache tuwatumikie Wamisri? Ingekuwa vyema zaidi kwetu kuwatumikia Wamisri kuliko kufa jangwani!”

1314:13 Mwa 15:1; 1Sam 12:16; 2Nya 20:17; Isa 41:10-14Mose akawajibu Waisraeli, “Msiogope. Simameni imara, nanyi mtauona wokovu Bwana atakaowapatia leo. Hao Wamisri mnaowaona leo kamwe hamtawaona tena. 1414:14 Kut 15:3; Kum 1:30; 3:22; 20:4; Yos 10:14; 23:3; 2Sam 5:24; 2Nya 20:29; Neh 4:20; Za 24:8; Isa 42:13; Yer 41:12; 1Sam 12:16; Za 37:7; 46:10; 116:7; Isa 28:12; 30:15; Zek 2:13Bwana atawapigania ninyi, nanyi mnatakiwa kutulia tu.”

1514:15 Yos 7:10Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Kwa nini wewe unanililia? Waambie Waisraeli waendelee mbele. 1614:16 Kut 4:2, 17; Isa 10:26; Hes 20:8-11Inua fimbo yako na unyooshe mkono wako juu ya bahari ili kuyagawa maji, hivyo kwamba Waisraeli wapate kupita mahali pakavu baharini. 1714:17 Kut 4:21Nitaifanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu kusudi waingie baharini wakiwafuatia. Nami nitajipatia utukufu kupitia Farao pamoja na jeshi lake lote, kupitia magari yake ya vita na wapanda farasi wake. 1814:18 Kut 6:2; Eze 32:15Nao Wamisri watajua kwamba Mimi ndimi Bwana nitakapojipatia utukufu kupitia Farao, magari yake ya vita na wapanda farasi wake.”

1914:19 Mwa 16:7; Isa 63:9; Kut 13:2; 1Kor 10:1; Isa 26:7; 42:16; 49:10; 52:10; 58:8Ndipo malaika wa Mungu, aliyekuwa akisafiri mbele ya jeshi la Israeli, akaondoka akakaa nyuma yao. Pia ile nguzo ya wingu ikaondoka hapo mbele yao na kusimama nyuma, 2014:20 Yos 24:7ikakaa kati ya majeshi ya Misri na Israeli. Usiku kucha wingu likaleta giza upande mmoja na nuru kwa upande mwingine, kwa hiyo hakuna aliyemkaribia mwenzake usiku kucha.

2114:21 Kut 7:19; 4:2; Ay 26:12; Isa 14:27; 23:11; 51:15; Yer 31:35; Mdo 7:36; Mwa 41:6; Kut 15:8; 2Sam 22:16; 1Fal 19:11; Ay 38:1; 40:6; Yer 23:19; Nah 1:3; Mwa 8:1; 2Fal 2:8; Za 74:13; 78:13; 114:5; 136:13; Isa 63:12Ndipo Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, naye Bwana akayasukuma maji ya bahari nyuma kwa upepo mkali wa mashariki usiku ule wote na kupafanya nchi kavu. Maji yakagawanyika, 2214:22 Hes 33:8; Yos 24:6; Isa 43:16; 63:11; 1Kor 10:1; Kut 3:12; 15:19; Kum 31:6-8; Yos 3:16; 4:22; Neh 9:11; Za 66:6; 77:19; 106:9; Isa 11:15; 41:10; 43:5; 44:27; 50:2; 51:10; 63:13; Yer 46:28; Nah 1:4; Ebr 11:29; Kut 15:8; Yos 3:13nao Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, maji yakiwa ukuta upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto.

23Wamisri wakawafuatia ndani ya bahari, pamoja na farasi wote wa Farao, magari ya vita na wapanda farasi. 2414:24 Kut 13:21; 1Kor 10:1; Kut 23:27; Yos 10:10; 1Sam 5:9; 5:9; 7:10; 14:15; 2Sam 5:24; 2Fal 7:6; 19:7Karibia mapambazuko, Bwana akaliangalia jeshi la Wamisri kutoka ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha. 2514:25 Kum 32:31; 1Sam 2:2; 4:8; Kut 14:14Mungu akayaondoa magurudumu ya magari yao, kwa hivyo wakayaendesha kwa shida. Nao Wamisri wakasema, “Tuachane na Waisraeli! Bwana anawapigania dhidi ya Misri.”

Wafuatiaji Wazama

26Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Nyoosha mkono wako juu ya bahari ili maji yarudiane yawafunike Wamisri, magari yao ya vita na wapanda farasi wao.” 2714:27 Yos 4:18; Kut 15:1; Kum 1:40; 11:4; Za 78:53; 106:11; 136:15; Ebr 11:29Mose akanyoosha mkono wake juu ya bahari, wakati wa mapambazuko bahari ikarudiana na kuwa kama kawaida. Wamisri wakajaribu kuyakimbia maji, lakini Bwana akawasukumia ndani ya bahari. 2814:28 Kut 15:19; Yos 24:7; Kut 15:5; Amu 4:16; Neh 9:11Maji yakarudiana na kuyafunika magari ya vita na wapanda farasi pamoja na jeshi lote la Farao lililokuwa limewafuata Waisraeli ndani ya bahari. Hakuna hata mmoja wao aliyenusurika.

2914:29 Yos 24:11; 2Fal 2:8; Za 74:15; 78:13Lakini Waisraeli wakapita baharini mahali pakavu, ukiwepo ukuta wa maji upande wao wa kuume na upande wao wa kushoto. 3014:30 1Sam 14:23; 1Nya 11:14; Za 44:7; 106:8-10; Isa 43:3; 50:2; 51:9-10; 60:16Siku ile Bwana akawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wamisri, nao Waisraeli wakawaona Wamisri wamelala ufuoni mwa bahari wakiwa wamekufa. 3114:31 Kut 9:16; Za 147:5; Kut 20:18; Kum 31:13; Yos 4:24; 1Sam 12:18; Za 76:6-7; 112:1; Kut 4:5; Za 22:4; 40:3; 106:12; Yn 2:11; 11:45Basi Waisraeli walipoona uwezo mkubwa Bwana aliodhihirisha dhidi ya Wamisri, watu wakamwogopa Bwana na wakaweka tumaini lao kwake na kwa Mose mtumishi wake.

New Russian Translation

Исход 14:1-31

Переход через море

1Господь сказал Моисею:

2– Скажи израильтянам, чтобы они повернули назад и остановились у Пи-Гахирота, между Мигдолом и морем. Пусть они расположатся у моря, прямо перед Баал-Цефоном. 3Фараон подумает: «Израильтяне блуждают по этой земле в растерянности, окруженные пустыней». 4Я сделаю сердце фараона упрямым, и он погонится за ними, и этим прославлюсь, победив фараона с его войском. Тогда египтяне узнают, что Я – Господь.

Израильтяне так и сделали. 5Когда царю Египта сказали, что народ убежал, фараон и его приближенные передумали и сказали:

– Что мы сделали? Мы отпустили израильтян и лишились работников!

6Фараон запряг колесницу и взял с собой войско. 7Он взял шестьсот отборных колесниц и все остальные колесницы Египта с их начальниками. 8Господь сделал сердце фараона, царя Египта, упрямым, и он погнался за израильтянами, которые смело покидали Египет. 9Войско египтян со всеми лошадьми фараона, колесницами и всадниками14:9 Или: «колесничими»; также в ст. 17, 18, 23, 26 и 28. погналось за израильтянами и настигло их, когда они расположились лагерем у моря, рядом с Пи-Гахиротом, напротив Баал-Цефона.

10Когда фараон приблизился, израильтяне оглянулись и увидели, что египтяне преследуют их. Они очень испугались и стали взывать к Господу. 11Они сказали Моисею:

– Разве в Египте не было могил, что ты повел нас умирать в пустыню? Что ты сделал с нами, выведя нас из Египта? 12Разве мы не говорили тебе в Египте: «Оставь нас в покое. Дай нам служить египтянам?» Лучше бы нам оставаться рабами у египтян, чем умирать в пустыне!

13Моисей ответил народу:

– Не бойтесь. Стойте твердо, и вы увидите, как Господь спасет вас сегодня. Египтян, которых вы видите сейчас, вы не увидите больше никогда. 14Будьте спокойны, Господь будет сражаться за вас.

15Господь сказал Моисею:

– Зачем ты взываешь ко Мне? Вели израильтянам идти вперед. 16Подними посох, простри руку над морем, и оно разделится. Тогда израильтяне смогут пройти через море, как по суше. 17А Я сделаю египтян упрямыми, и они пойдут за ними. Я прославлюсь, победив фараона и его войско, с его колесницами и всадниками. 18Египтяне узнают, что Я – Господь, когда Я прославлюсь, победив фараона, с его колесницами и всадниками.

19Ангел Бога, Который14:19 Или: «который» шел перед израильским войском, пошел позади него. Облачный столб тоже передвинулся со своего места и оказался позади них, 20между войсками Египта и Израиля. Всю ночь облако давало тьму одной стороне и свет другой, и всю ночь свет и тьма не могли сойтись.

21Моисей простер руку над морем, а Господь всю ночь отгонял море сильным восточным ветром и превратил его в сушу. Воды разделились, 22и израильтяне прошли через море, как по суше: одна стена воды стояла у них справа, а другая – слева. 23Египтяне погнались за ними. Лошади, колесницы и всадники фараона ринулись в море. 24Перед самым рассветом Господь посмотрел из огненного и облачного столба на египетское войско и поверг его в смятение. 25Он застопорил14:25 Или: «снял». колеса их колесниц, и им стало трудно ехать.

Египтяне сказали:

– Бежим отсюда! Господь сражается на стороне израильтян против Египта!

26Тогда Господь сказал Моисею:

– Протяни руку над морем, чтобы воды хлынули назад, на египтян, на их колесницы и всадников. 27Моисей простер руку над морем, и с рассветом воды сомкнулись14:27 Или: «вода поднялась до обычной глубины».. Египтяне бежали навстречу морю, и Господь смел их в воду. 28Вода хлынула назад и накрыла колесницы и всадников – все войско фараона, которое ринулось за израильтянами в море. Не спасся никто.

29Но израильтяне перешли через море, как по суше: одна стена воды стояла у них справа, а другая – слева. 30В тот день Господь спас Израиль от египтян, и Израиль увидел их мертвыми на берегу. 31Когда израильтяне увидели великую силу, которой Господь сразил египтян, то их охватил страх перед Господом. Они поверили Ему и Его слуге Моисею.