Kutoka 13 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 13:1-22

Kuwekwa Wakfu Kwa Wazaliwa Wa Kwanza

1Bwana akamwambia Mose, 213:2 Kut 22:29; 34:20; Law 27:26; Hes 3:13; 8:17; 18:15; Kum 15:19; Neh 10:34; Lk 2:23“Niwekeeni wakfu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume. Kila mtoto wa kwanza aliye kifungua tumbo miongoni mwa Waisraeli ni mali yangu, akiwa wa mwanadamu au wa mnyama.”

313:3 Kut 7:4; Law 26:13; Hes 22:5; 26:4; Kum 4:45; 5:6; Za 81:10; 114:1; Kut 3:20; 12:8Ndipo Mose akawaambia watu, “Ikumbukeni siku hii, siku ambayo mlitoka katika nchi ya Misri, katika nchi ya utumwa, kwa sababu Bwana aliwatoa humo kwa mkono wenye nguvu. Msile chochote kilichotiwa chachu. 413:4 Kut 12:2Leo, katika mwezi wa Abibu,13:4 Abibu ni jina la mwezi wa kwanza kwa Wayahudi, ambao ni mwezi wa nne katika kalenda yetu. mnatoka. 513:5 Kut 3:8; 12:25-26Bwana atakapokuleta katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Wahivi na Wayebusi, nchi aliyowaapia baba zako kukupa, nchi itiririkayo maziwa na asali, utaiadhimisha sikukuu hii katika mwezi huu: 613:6 Kut 12:15-20Kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu na katika siku ya saba utamfanyia Bwana sikukuu. 7Kwa muda wa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu, pasionekane kitu chochote kilicho na chachu miongoni mwako, wala chachu yoyote isionekane popote ndani ya mipaka yako. 813:8 Kut 10:2; Za 78:5-6Siku ile utamwambia mwanao, ‘Nafanya hivi kwa sababu ya jambo ambalo Bwana alinitendea nilipotoka katika nchi ya Misri.’ 913:9 Isa 44:5; Kum 6:8; 11:18; Mit 3:3; Mt 23:5; Kut 3:20Adhimisho hili, litakuwa kama alama kwenye mkono wako na ukumbusho katika paji lako la uso, kwamba sheria ya Bwana inapaswa iwe kinywani mwako. Kwa kuwa Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu. 1013:10 Kut 12:14; Za 75:2; 102:13Ni lazima uishike amri hii kwa wakati uliopangwa mwaka baada ya mwaka.

1113:11 Mwa 22:16; Kum 1:8; Mwa 12:7; 17:19; Za 105:42-45“Baada ya Bwana kukuingiza katika nchi ya Wakanaani na kukupa nchi hiyo, kama alivyokuahidi kwa kiapo na kwa baba zako, 1213:12 Mwa 4:4; Law 27:26; Hes 3:13; 18:15-17; Lk 2:23inakupasa kumtolea Bwana mzaliwa wa kwanza wa kila tumbo. Wazaliwa wote wa kwanza wa kiume wa mifugo yako ni mali ya Bwana. 1313:13 Law 27:11; Kut 34:20; Isa 66:3; Hes 3:46-47; 18:15Kila mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa mwana-kondoo, lakini kama hukumkomboa, utamvunja shingo yake. Kila mzaliwa wa kwanza mwanaume miongoni mwa wana wenu utamkomboa.

1413:14 Kut 10:2; 20:2; Kum 7:8; 6:20; 28:68“Katika siku zijazo, mwanao akikuuliza, ‘Hii ina maana gani?’ Mwambie, ‘Kwa mkono wenye nguvu Bwana alitutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa. 15Farao alipokataa kwa ukaidi kuturuhusu kuondoka, Bwana aliua kila mzaliwa wa kwanza wa Wamisri, mwanadamu na wa mnyama. Hii ndiyo sababu ninatoa dhabihu kwa Bwana mzaliwa wa kwanza wa kiume, wa kila tumbo na kumkomboa kila mzaliwa wa kwanza wa wana wangu.’ 16Jambo hili litakuwa kama ishara kwenye mkono wako na kama alama kwenye paji la uso wako, kwamba Bwana alikutoa katika nchi ya Misri kwa mkono wake wenye nguvu.”

Nguzo Ya Wingu Na Moto

1713:17 Kut 14:11; Hes 14:1-4; Kum 17:16; Hos 11:5Farao alipowaachia watu waende, Mungu hakuwaongoza kufuata njia ipitiayo katika nchi ya Wafilisti, ingawa njia hiyo ilikuwa fupi zaidi. Kwa maana Mungu alisema, “Wakikabiliana na vita, wanaweza kubadili mawazo yao na kurudi Misri.” 1813:18 Kut 15:22; Za 136:16; Eze 20:10; Yos 4:13Kwa hiyo Mungu akawaongoza watu kupitia njia ya kuzunguka kupitia jangwani, kuelekea Bahari ya Shamu. Waisraeli walipanda kutoka nchi ya Misri wakiwa wamejiandaa kwa vita.

1913:19 Yos 24:32; Mdo 7:16; Ebr 11:22; Mwa 47:29-30Mose akachukua mifupa ya Yosefu kwa sababu Yosefu alikuwa amewaapisha wana wa Israeli. Alikuwa amewaambia, “Hakika Mungu atakuja kuwasaidia, nanyi ni lazima mwiichukue mifupa yangu mwende nayo kutoka mahali hapa.”

2013:20 Kut 12:37; Hes 33:6Baada ya Waisraeli kuondoka Sukothi wakapiga kambi huko Ethamu pembeni mwa jangwa. 2113:21 Kut 32:1; 33:14; Kum 2:7; 31:8; Amu 4:14; 5:4; Za 68:7; 72:20; Yer 2:2; Hab 3:13; Kut 14:19, 24; 24:16; 33:9-10; 34:5; 40:38; Hes 9:16; 12:5; 14:14; Kum 1:33; Neh 9:12, 19; Za 78:14; 99:7; 105:39; Isa 4:5; 1Kor 10:1Wakati wa mchana Bwana aliwatangulia kwa nguzo ya wingu kuwaongoza katika njia yao, na wakati wa usiku aliwatangulia kwa nguzo ya moto kuwaangazia, ili waweze kusafiri mchana au usiku. 2213:22 Neh 9:19; Hes 33:7; Yer 44:1; Eze 29:10Ile nguzo ya wingu wakati wa mchana au ile nguzo ya moto wakati wa usiku haikuondoka mahali pake mbele ya watu.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

出埃及记 13:1-22

奉献头胎

1耶和华对摩西说: 2以色列人中的长子和头生的牲畜都属于我,因此要把他们分别出来,使他们圣洁,归给我。”

3摩西对百姓说:“你们要记住离开埃及的这一天,因为耶和华用大能的手把你们从受奴役的地方解救出来。不可吃带酵的食物。 4你们是在亚笔月13:4 亚笔月是犹太历的第一个月,约在阳历三月中旬到四月中旬,相当于中国的春分时节。的这一天从埃及出来的, 5将来耶和华带领你们进入迦南以后,你们每逢此月都要为祂守节期。那里现在住着迦南人、人、亚摩利人、希未人和耶布斯人。耶和华已经向你们祖先起誓,应许赐给你们那奶蜜之乡。 6在节期的七天之内,你们只可以吃无酵饼,到了第七天,你们要为耶和华守节期。 7七天之内要吃无酵饼,你们境内不得有酵或是带酵的东西。 8那时,要告诉你们的子孙,‘这节期是纪念我们离开埃及时耶和华为我们所做的一切。’ 9这节期就好像在你们手上或额上作的记号,叫你们记得耶和华的律法,祂曾经用大能的手把你们带出埃及10因此,每一年你们都要按时守这节期。

11“将来耶和华成就祂起誓给你们祖先的应许,领你们进入迦南人的土地,把那里赐给你们以后, 12你们要把所有长子和头生的公畜归给祂。 13所有头生的公驴必须用羊羔赎回,不然就要打断它的脖子。要赎回你们所有的长子。 14将来你们的子孙问起这件事的意义,你们就回答,‘耶和华曾经用大能的手把我们从受奴役之地——埃及领出来。 15当时法老硬着心不肯放我们走,所以耶和华就把埃及人的长子和头生的牲畜全都杀了。因此,我们把所有头生的公畜当作祭牲献给耶和华,只把长子赎回来。’ 16这事就像在你们手上作记号,额上作标记,以牢记耶和华曾用大能的手领我们离开埃及。”

云柱和火柱

17法老让以色列人离开埃及后,上帝没有带领他们穿越非利士地区,虽然那是条捷径。因为上帝说:“如果他们遇上战争,就会改变主意,返回埃及。” 18所以,上帝领他们绕道而行,走旷野的路,前往红海13:18 红海”或译“芦苇湖”,确切地点约在今红海北端苏伊士运河附近。以色列人离开埃及时都带着兵器。 19摩西约瑟的骸骨一起带走,因为约瑟曾叫以色列人郑重发誓,对他们说:“上帝必眷顾你们,把你们带出埃及,那时你们要把我的骸骨也一起带走。” 20以色列人从疏割启程,来到旷野边缘的以倘安营。 21耶和华走在他们前面,白天用云柱为他们指示道路,晚上用火柱照亮他们,这样他们可以日夜赶路。 22白天的云柱和晚上的火柱从不离开他们。