Kumbukumbu 8 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 8:1-20

Usimsahau Bwana

18:1 Kum 4:1; Kut 19:5; Ay 36:11; Za 16; 11; Eze 20:19Uwe mwangalifu kufuata kila agizo ninalokupa wewe leo, ili mweze kuishi, kuongezeka na mweze kuingia mkamiliki nchi ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zenu. 28:2 Kum 29:5; Za 136:16; Amo 2:10; Mwa 22:1; Yos 6:17; 11:11; Kut 23:32; Amu 1:24; 2:2Kumbuka jinsi Bwana Mungu wenu alivyowaongoza katika njia yote katika jangwa kwa miaka hii arobaini, kukunyenyekeza na kukujaribu ili ajue lililoko moyoni mwako, kwamba utayashika maagizo yake au la. 38:3 Isa 2:11; Yer 44:10; Kut 16:14; 1Fal 8:36; Za 25:5; 94:12; 119:171; Mwa 3:19; Ay 23:12; Za 104:15; Mit 28:21; Isa 51:14; Yer 42:14; Ay 22:22; Za 119:13; 138:4; Kut 16:2-3; Mt 4:4; Lk 4:4Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Bwana. 48:4 Kum 29:5; Neh 9:21Nguo zenu hazikuchakaa wala miguu yenu haikuvimba kwa miaka hii arobaini. 58:5 Kum 4:36; 2Sam 7:14; Ay 5:17; 33:19; Mit 3:11-12; Ebr 12:5-11; Ufu 3:19Mjue basi ndani ya mioyo yenu kama mtu anavyomwadibisha mwanawe, ndivyo Bwana Mungu wako atawaadibisha ninyi.

68:6 Kut 33:13; 1Fal 3:14; Za 81:13; 95:10; Kum 5:33Shikeni maagizo ya Bwana Mungu wenu mtembee katika njia zake na kumheshimu. 78:7 Za 106:24; Yer 3:19; Eze 20:6; Kum 11:9-12; Yer 2:7Kwa kuwa Bwana Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi yenye vijito na mabwawa ya maji, yenye chemchemi zinazotiririka mabondeni na katika vilima; 88:8 Kut 9:31; Mwa 49:11; Hes 13:23; 1Fal 4:25; Kum 32:13; Za 81:16nchi yenye ngano na shayiri, mizabibu na mitini, mikomamanga, mafuta ya zeituni na asali; 98:9 Amu 18:10; Ay 28:2nchi ambayo chakula hakitapungua na hamtakosa chochote; nchi ambayo miamba yake ni chuma na mnaweza kuchimba shaba kutoka kwenye vilima.

108:10 Kum 6:10-12Wakati mtakapokwisha kula na kushiba, msifuni Bwana Mungu wenu kwa ajili ya nchi nzuri aliyowapa. 118:11 Kum 4:9Jihadharini msimsahau Bwana Mungu wenu, mkashindwa kushika maagizo yake, sheria na amri zake ambazo ninawapa leo. 128:12 Mit 30:9; Hos 13:6Angalia wakati mtakapokuwa mmekula na kushiba, mkajenga nyumba nzuri na kukaa humo, 13na wakati makundi yenu ya ngʼombe na mbuzi na kondoo yatakapoongezeka na fedha na dhahabu yenu itakapoongezeka na vyote mlivyo navyo vitakapozidishwa, 148:14 Za 78:7; 106:21basi mioyo yenu isiwe na kiburi mkamsahau Bwana Mungu wenu aliyewatoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa. 158:15 Kum 1:19; 32:13; 32:10; Hes 21:6; Isa 14:29; 30:6; Kut 17:6; Ay 28:9; Za 78:15; 114:8Aliwaongoza kupitia jangwa lile kubwa na la kutisha, nchi ile ya kiu isiyo na maji, yenye nyoka wa sumu na nge. Aliwatolea maji kutoka kwenye mwamba mgumu. 168:16 Kut 16:14; 16:15; Mwa 22:1; Rum 8:28; 2Kor 4:17; Ebr 12:11; Yak 1:12; 1Pet 1:7Aliwapa mana ya kula jangwani, kitu ambacho baba zenu hawakukijua, ili kuwanyenyekesha na kuwajaribu ninyi ili mwishoni apate kuwatendea mema. 178:17 Kum 9:4, 24; 31:27; Amu 7:2; Za 44:3; Isa 10:13Mnaweza kusema, “Uwezo wangu na nguvu za mikono yangu ndizo zilizonipatia utajiri huu.” 188:18 Mwa 26:13; Kum 26:10; 28:4; 1Sam 2:7; Za 25:13; 112:3; Mit 8:18; 10:22; Mhu 9:11; Hos 2:8Lakini kumbukeni Bwana Mungu wenu, ndiye ambaye huwapa uwezo wa kupata utajiri, na hivyo kulithibitisha Agano lake, ambalo aliwaapia baba zenu, kama ilivyo leo.

198:19 Kum 6:14; 4:26; 30:18; Za 16:4; Yer 7:6; 13:10; 25:6Ikiwa mtamsahau Bwana Mungu wenu, mkaifuata miungu mingine, mkaiabudu na kuisujudia, ninashuhudia dhidi yenu leo kwamba hakika mtaangamizwa. 208:20 2Fal 21:2; Za 10:16; Eze 5:5-17; Mao 1:1-22; 2:17; Dan 9:12; Zek 1:6Kama mataifa Bwana aliyoyaangamiza mbele yenu, ndivyo ninyi mtakavyoangamizwa kwa kutokumtii Bwana Mungu wenu.

New International Reader’s Version

Deuteronomy 8:1-20

Remember What the Lord Has Done

1Make sure you obey every command I’m giving you today. Then you will live, and there will be many of you. You will enter the land and take it as your own. It’s the land the Lord promised to your people of long ago. 2Remember how the Lord your God led you all the way. He guided you in the desert for these 40 years. He wanted to take your pride away. He wanted to test you to know what was in your hearts. He wanted to see whether you would obey his commands. 3He took your pride away. He let you go hungry. Then he gave you manna to eat. You and your parents had never even known anything about manna before. He tested you to teach you that man doesn’t live only on bread. He also lives on every word that comes from the mouth of the Lord. 4Your clothes didn’t wear out during these 40 years. Your feet didn’t swell. 5Here is what I want you to know in your hearts. The Lord your God guides you, just as parents guide their children.

6Obey the commands of the Lord your God. Live as he wants you to live. Have respect for him. 7The Lord your God is bringing you into a good land. It has brooks, streams and deep springs of water. Those springs flow in its valleys and hills. 8It has wheat, barley, vines, fig trees, pomegranates, olive oil and honey. 9There is plenty of food in that land. You will have everything you need. Its rocks have iron in them. And you can dig copper out of its hills.

10When you have eaten and are satisfied, praise the Lord your God. Praise him for the good land he has given you. 11Make sure you don’t forget the Lord your God. Don’t fail to obey his commands, laws and rules. I’m giving them to you today. 12But suppose you don’t obey his commands. And suppose you have plenty to eat. You build fine houses and live in them. 13The number of your herds and flocks increases. You also get more and more silver and gold. And everything you have multiplies. 14Then your hearts will become proud. And you will forget the Lord your God. The Lord brought you out of Egypt. That’s the land where you were slaves. 15He led you through that huge and terrible desert. It was a dry land. It didn’t have any water. It had poisonous snakes and scorpions. The Lord gave you water out of solid rock. 16He gave you manna to eat in the desert. Your people had never even known anything about manna before. The Lord took your pride away. He tested you. He did it so that things would go well with you in the end. 17You might say to yourself, “My power and my strong hands have made me rich.” 18But remember the Lord your God. He gives you the ability to produce wealth. That shows he stands by the terms of the covenant he made with you. He promised it to your people of long ago. And he’s still faithful to his covenant today.

19Don’t forget the Lord your God. Don’t serve other gods. Don’t worship them and bow down to them. I am a witness against you today that if you do, you will certainly be destroyed. 20You will be destroyed just like the nations the Lord your God is destroying to make room for you. That’s what will happen if you don’t obey him.