Kumbukumbu 5 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 5:1-33

Amri Kumi

(Kutoka 20:1-17)

15:1 Kut 18:20Mose akawaita Israeli wote, akawaambia:

Ee Israeli, sikilizeni amri na sheria ninazowatangazia leo. Jifunzeni, na mwe na hakika kuzifuata. 25:2 Kut 19:5Bwana Mungu wetu alifanya Agano nasi katika mlima wa Horebu. 35:3 Kum 11:2-7; Hes 26:63-65; Ebr 8:9; Mt 13:17Si kwamba Bwana alifanya Agano na baba zetu, bali alifanya nasi, nasi sote ambao tuko hai hapa leo. 45:4 Kut 19:9, 18-19; 20:22; Kum 4:33, 36; 34:10; Hes 14:4Bwana alisema nanyi uso kwa uso kutoka moto juu ya mlima. 55:5 Gal 3:19; Mwa 3:10; Ebr 12:18-21; Kut 20:18-21; 20:18-21; Hes 16:48; Za 106:23; Yer 30:21(Wakati huo nilisimama kati ya Bwana na ninyi kuwatangazia neno la Bwana, kwa sababu mliogopa ule moto, nanyi hamkupanda mlimani.) Naye Mungu alisema:

65:6 Kut 13:3; 29:46; Law 26:1; Kum 6:4; Za 81:10“Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.

75:7 Kut 20:3“Usiwe na miungu mingine ila mimi.

85:8 Law 26:1; Kum 4:15-16; Za 78:58; 97:7; Kut 20:4; Mdo 17:29Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji. 95:9 Hes 26:11; Kut 34:7; Hes 10:35; 14:18; Kut 34:7Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 105:10 Kut 34:2; Hes 14:18; Kum 7:9; Neh 1:5; Yer 32:18; Dan 9:4lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.

115:11 Za 139:20; Law 19:12; Kum 10:20; Mt 5:33-37Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.

125:12 Kut 16:23-30; 31:13; Mk 2:27-28; Kut 20:8Adhimisha siku ya Sabato na kuiweka takatifu, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza. 13Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote. 145:14 Mwa 2:2; Mt 12:2; Mk 2:17; Ebr 4:4; Ay 31:13; Yer 34:9-11; 17:21-24Lakini siku ya Saba ni Sabato kwa Bwana, Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wa kiume au mtumishi wa kike, wala ngʼombe wako, punda wako au mnyama wako yeyote, wala mgeni aliyeko malangoni mwako, ili kwamba mtumishi wako wa kiume na wa kike wapate kupumzika kama wewe. 155:15 Mwa 15:13; Kut 6:1; Za 108:6; Yer 32:21; Kum 4:34Kumbuka mlikuwa watumwa huko Misri, na Bwana Mungu wenu aliwatoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa. Kwa hiyo Bwana Mungu wako amekuagiza kuiadhimisha siku ya Sabato.

165:16 Mal 1:6; Kut 21:17; Law 19:3; Eze 22:7; Mt 15:4; 19:19; Mk 7:10; 10:19; Lk 18:20; Efe 6:2-3; Kum 4:40; 11:9; Mit 3:1-2Waheshimu baba yako na mama yako, kama Bwana Mungu wako alivyokuagiza, ili siku zako zipate kuwa nyingi na kufanikiwa katika nchi Bwana Mungu wako anayokupa.

175:17 Mwa 9:6; Law 24:17; Mhu 3:3; Yer 40:15; 41:3; Mt 5:21-22; 19:19; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9; Yak 2:11Usiue.

185:18 Law 20:10; Mt 5:27-30; 19:18; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9; Yak 2:11Usizini.

195:19 Law 19:11; Mt 19:19; Mk 10:19; Lk 18:20; Rum 13:9Usiibe.

205:20 Kut 23:1; Mt 19:18; Mk 10:19; Lk 18:20Usimshuhudie jirani yako uongo.

215:21 Rum 7:7; 13:9Usitamani mke wa jirani yako. Usitamani nyumba ya jirani yako au shamba lake, mtumishi wake wa kiume au wa kike, ngʼombe au punda wake, wala kitu chochote cha jirani yako.”

225:22 Kut 20:21; 24:12; 31:18; Kum 4:13Hizi ndizo amri alizozitangaza Bwana kwa sauti kubwa kwa kusanyiko lenu lote huko mlimani kutoka kwenye moto, wingu na giza nene, wala hakuongeza chochote zaidi. Kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe, naye akanipa mimi.

Woga Wa Watu Mlimani

(Kutoka 20:18-21)

235:23 Kut 3:16Mliposikia sauti kutoka kwenye giza, mlima ulipokuwa ukiwaka moto, viongozi wenu wote wa makabila yenu na wazee wenu walinijia mimi. 245:24 Kum 4:34; 8:5; 11:2; Isa 53:4; Kum 3:24; Kut 19:19Nanyi mkasema, “Bwana Mungu wetu ametuonyesha utukufu na enzi yake, nasi tumesikia sauti yake kutoka kwenye moto. Leo tumeona kwamba mwanadamu anaweza kuishi hata kama Mungu akizungumza naye. 255:25 Kut 20:18-19; Kum 18:16; Ebr 12:19Lakini sasa, kwa nini tufe? Moto huu mkubwa utatuteketeza sisi na tutakufa kama tukiendelea kusikia sauti ya Bwana Mungu wetu zaidi. 265:26 Kut 33:20; Kum 4:33; Amu 6:22-23; 13:22; Isa 6:5Ni mtu yupi mwenye mwili ambaye amewahi kuisikia sauti ya Mungu aliye hai akizungumza kutoka kwenye moto, kama sisi tulivyoisikia, naye akaishi? 275:27 Kut 19:8; 24:7Sogea karibu usikie yale yote asemayo Bwana Mungu wetu. Kisha utuambie chochote kile ambacho Bwana Mungu wetu anakuambia. Tutasikiliza na kutii.”

285:28 Kum 18:17Bwana aliwasikia wakati mlipozungumza nami, na Bwana akaniambia, “Nimesikia kile hawa watu walichokuambia. Kila kitu walichokisema ni kizuri. 295:29 Za 81:8, 13; Yos 22:5; Za 78:7; Kum 4:1-40; 12:25; 22:7; Isa 48:18; Kum 12:25; Yer 44:4; Mt 23:37; Lk 19:42; 2Kor 5:20; 6:1; 7:1; Ebr 12:25; Yn 15:14; Ufu 22:14Laiti kama mioyo yao ingekuwa na mwelekeo wa kuniogopa na kuzishika amri zangu zote daima, ili kwamba wafanikiwe wao pamoja na watoto wao milele!

305:30 Mal 4:4; Gal 3:19“Nenda uwaambie warudi kwenye mahema yao. 315:31 Kut 24:12Lakini wewe baki hapa pamoja nami ili niweze kukupa maagizo yote, amri na sheria ambazo utawafundisha wazifuate katika nchi ninayokwenda kuwapa waimiliki.”

325:32 Kum 4:29; 10:12; 17:11, 20; 28:14; Yos 1:7; 1Fal 15:5; 2Fal 22:2; Mit 4:27; Kum 10:12; Za 119:6; Mhu 8:12; 1Tim 4:8; Efe 6:3Hivyo kuweni waangalifu kuyafanya yale Bwana Mungu wenu aliyowaagiza; msigeuke upande wa kuume wala wa kushoto. 335:33 Isa 3:10; Yer 7:23; 38:20; Lk 1:6; Kum 4:40Fuateni yale yote ambayo Bwana Mungu wenu aliwaagiza, ili mpate kuishi, kustawi na kuziongeza siku zenu katika nchi mtakayoimiliki.

Japanese Contemporary Bible

申命記 5:1-33

5

十戒

1モーセはイスラエル人を呼び集めて言いました。「さあ、私の語る律法をよく聞きなさい。それを正しく理解し、きちんと守るのです。 2-3いいですか、私たちの神、主はホレブ山(シナイ山)で、あなたがたと契約を結ばれました。私たちの先祖とではなく、今ここにいる一人一人とです。 4その時、主は炎の中からじきじきにお語りになりました。 5あまりのことにあなたがたは震え上がり、だれ一人、山に登って主のもとへ行こうとしなかったので、私が行って主のおことばを聞き、それをあなたがたに伝えたのです。そのおことばはこうでした。

6『わたしは、エジプトでの奴隷生活からあなたを救い出した、あなたの神、主である。

7わたしのほかは、どんなものも神として拝んではならない。

8決して偶像を造ってはならない。鳥でも動物でも魚でも、どんな像も造ってはならない。 9-10それらを拝んでもならない。どのような方法で礼拝してもならない。あなたがたの神は、このわたしだけだ。わたしはねたみ深いから、わたしとほかの神を同時に愛することは許さない。わたしの罰は、わたしを憎む者の子ども、孫、ひ孫までも及ぶ。しかし、わたしを愛し、わたしの命令を守る者には、千代に至るまでも恵みを与えよう。

11実行するつもりもないのに、むやみにわたしの名を使って誓ってはならない。そのようなことをしたら必ず罰せられる。

12主の定めた安息日を特別の日として守りなさい。 13すべての仕事は六日のうちにすませなさい。 14七日目はあなたの神、主の安息の日だから、その日は一日、人も家畜も仕事をしてはならない。外国人も、ここでいっしょに住んでいる限り、この戒めを守る義務がある。すべての人が休むのだ。 15安息日を守るのは、エジプトで奴隷にされていたあなたを、主であるわたしが力強い手を差し伸べて救い出したことを忘れないためである。

16あなたの両親を尊敬しなさい。そうすれば、主であるわたしが与える国で、長く幸せな一生を送ることができる。

17人を殺してはならない。

18姦淫してはならない。

19盗んではならない。

20うそをついてはならない。

21隣人の家をうらやんではならない。隣人の妻に情欲を燃やしたり、家、土地、使用人、牛、ろば、そのほか何でも、隣人の持ち物を欲しがったり、持ち主をねたんだりしてはならない。』

22暗雲の垂れ込めるシナイ山でこれらのことばを、主は炎の中からあなたがた一人一人に告げられました。主はそれを二枚の石板に記して私に下さいました。 23ところが、あなたがたはどうしたでしょう。暗闇にとどろく主の声を聞き、山頂に燃え上がる無気味な火を見ると、恐ろしさのあまり震え上がったではありませんか。族長たちは私のところへ駆けつけ、 24必死に訴えました。『私たちの神、主がどんなにすばらしいお方か、よくわかりました。何しろ、炎の中からお語りになったのですから。しかも、その声を聞いても、私たちはこうして生きています。 25ですが、もう一度こんなことがあったら、その時はきっと助からず、恐ろしい火で焼き殺されてしまうでしょう。 26-27炎の中から語られる神の声を聞いたら、ただではすみませんから。お願いですから、あなたが代表で聞きに行ってください。どんなことを言われても、そのとおりにします。』

28主はそれを聞き、こう言われました。『みなの気持ちはわかった。願いどおりにしよう。 29わたしの命じるとおりにすると言うが、いつもそのような心がけでいてくれたらどんなにうれしいだろう。そうすれば彼らばかりか、子々孫々に至るまで、何の心配もなく幸せに生きられる。 30さあ、帰って、めいめいの天幕へ戻るように言いなさい。 31そのあとでもう一度、わたしのところへ来て命令を聞き、人々に伝えなさい。わたしが与える国で、それをみな守るのだ。』」

32そこでモーセは人々に命じました。「主の戒めをすべて守りなさい。どんな細かな点もきちんと守りなさい。何もかも、主が定められたとおりに行うのです。 33そうして初めて、約束の地に入ってから末長く幸せに暮らせるのです。