Kumbukumbu 4 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 4:1-49

Waamriwa Utii

14:1 Law 18:4-5; Kum 1:3; 30:15-20; Rum 10:5; Eze 20:11; Rum 10:5Sikia sasa, ee Israeli, amri na sheria nitakazokufundisha wewe. Zifuate ili upate kuishi na uingie kuimiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zako anawapa. 24:2 Kum 12:32; Yos 1:7; Mit 30:6; Ufu 22:18-19; Yer 26:2; Law 22:31; Kum 10:12-13; Mhu 12:13Usiongeze wala usipunguze chochote ninachowaamuru ninyi, ila myashike maagizo ya Bwana Mungu wenu ambayo nawapa.

34:3 Hes 25:1-9; Za 106:28Mliona kwa macho yenu wenyewe kile Bwana alichokifanya kule Baal-Peori. Bwana Mungu wenu aliwaangamiza kutoka miongoni mwenu kila mmoja aliyemfuata Baali wa Peori, 4lakini ninyi nyote mlioshikamana na Bwana kwa uthabiti, Mungu wenu, mko hai mpaka leo.

54:5 Za 71:17; 119:102; Yer 32:33; Kut 18:20; Law 27:34; Ezr 9:11Tazama, nimewafundisha amri na sheria kama Bwana Mungu wangu alivyoniamuru mimi, ili mzifuate katika nchi mnayoiingia kuimiliki. 64:6 Kum 29:9; 1Fal 2:3; Kum 30:19-20; 32:46-47; Za 19:7; 119:98; Mit 1:7; 2:5; 2Tim 3:15; Ay 28:28; Za 111:10; Mit 3:7; 9:10; Mhu 12:13; Eze 5:5Zishikeni kwa uangalifu, kwa kuwa hii itaonyesha hekima na ufahamu wenu kwa mataifa, ambayo yatasikia kuhusu amri zote hizi, nao watasema, “Hakika taifa hili kubwa ni watu wenye hekima na ufahamu.” 74:7 2Sam 7:23; Hes 23:21; Za 46:1; Mdo 17:27; Kut 25:8; 29:45; Law 26:12; 1Fal 6:13; Isa 55:6; Zek 2:10; Efe 2:17; Yak 4:8Ni taifa gani jingine lililo kubwa kiasi cha kuwa na miungu yao iliyo karibu nao kama Bwana Mungu wetu alivyo karibu nasi wakati wowote tunapomwomba? 84:8 Za 89:14; 97:2; 119:7, 62, 144, 160, 172; Rum 3:2Nalo ni taifa gani jingine lililo kubwa hivi lenye kuwa na amri na sheria za haki kama hizi ninazoweka mbele yenu leo?

94:9 Kut 23:13; Mwa 14:14; 18:19; Kum 6:20-25; Efe 6:4; Kut 10:2; Mit 4:23; Za 78:5-6; Mit 4:23; 23:19; 3:1, 3; 4:21; Mwa 18:19; Mit 22:6; Efe 6:4Mwe waangalifu, na makini ili msije mkasahau mambo ambayo mliyaona kwa macho yenu, wala kuyaacha yaondoke moyoni mwenu siku zote za uhai wenu. Mwafundishe hayo watoto wenu na watoto wao baada yao.

104:10 Kut 3:1; 19:9, 16; Kum 14:23; 17:19; 31:12-13; Za 2:11; 111:10; 147:11; Isa 8:13; Yer 32:40; Kut 20:20; Kum 12:1Kumbuka siku uliyosimama mbele za Bwana Mungu wako kule Horebu, wakati aliponiambia, “Wakutanishe watu mbele yangu wasikie maneno yangu ili kwamba waweze kujifunza kuniheshimu kwa muda wote watakaoishi katika nchi, nao waweze kuwafundisha watoto wao maneno hayo.” 114:11 Kut 3:1; 19:17-18; 19:9; Za 18:11; 97:2; Ebr 12:18-19Mlisogea karibu na mkasimama chini ya mlima wakati ulipowaka moto mpaka mbinguni juu, pamoja na mawingu meusi na giza nene. 124:12 Kut 20:22; Mt 3:17; Kum 5:4-20; Ebr 12:19; Yn 5:37; Kut 19:9Ndipo Bwana alipozungumza nanyi kutoka moto. Mkasikia sauti ya maneno lakini hamkuona umbo, kulikuwa na sauti tu. 134:13 Kum 9:9-11; Rum 9:4; Kut 24:12; 31:18; 4:14; 21:1Aliwatangazia Agano lake na Amri Kumi, ambazo aliwaamuru mzifuate, kisha akaziandika juu ya vibao viwili vya mawe. 14Naye Bwana alinielekeza wakati huo kuwafundisha ninyi sheria na amri ambazo mnapaswa kuzifuata katika nchi ambayo mnavuka Yordani kuimiliki.

Kuabudu Sanamu Kwakatazwa

154:15 Isa 40:18; 41:22-24; Kut 3:1; Yos 23:11; Mal 2:15; Mit 4:23, 27; Yer 17:21; Mdo 17:24-29Hamkuona umbo la aina yoyote siku ambayo Bwana alizungumza nanyi kule Horebu kutoka kwenye moto. Kwa hiyo mjihadhari kwa uangalifu sana, 164:16 Mwa 6:11-12; Kum 9:12; 31:29; 32:5; Amu 2:19; Kut 20:4-5; 32:7; Rum 1:23ili msije mkajichafua na kujitengenezea sanamu au kinyago chenye umbo lolote kama la mwanaume au mwanamke, 174:17 Rum 1:23au kama mnyama aliye juu ya nchi au ndege yeyote arukaye angani, 18au kama kiumbe kitambaacho juu ya ardhi au samaki yeyote aliye ndani ya maji. 194:19 2Fal 23:11; Kum 17:3; Ay 31:26; Yer 8:2; 43:13; Eze 8:16; Mwa 1:16; 2:1; 37:9; Rum 1:25; Kum 13:5; Hes 25:3Na utazamapo juu angani na ukaliona jua, mwezi na nyota na vyote vinavyoipamba mbingu, usije ukashawishiwa kuviinamia na kuviabudu vile ambavyo Bwana Mungu wenu alivyogawia mataifa yote chini ya mbingu. 204:20 Kut 1:13; 3:10; Mwa 17:7; Kut 8:22; 34:9; Tit 2:14; Kut 19:5Lakini kwenu ninyi, Bwana amewatoa kutoka kwenye tanuru ya kuyeyushia chuma, katika Misri kuwa watu wa urithi wake kama mlivyo sasa.

214:21 Hes 20:12; Kum 1:37Bwana alinikasirikia kwa sababu yenu na akaapa kwamba sitavuka Yordani kuingia katika nchi nzuri Bwana Mungu wenu anayowapa kuwa urithi wenu. 224:22 Hes 27:13-14; Kum 3:25Nitakufa katika nchi hii; sitavuka Yordani, lakini ninyi ni karibu mvuke mkaimiliki ile nchi nzuri. 234:23 Kut 20:4Jihadharini msilisahau Agano la Bwana Mungu wenu lile alilofanya nanyi; msijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote ambacho Bwana Mungu wenu amewakataza. 244:24 Kut 15:7; 19:18; Ebr 12:29; Kut 20:5Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni moto ulao, Mungu mwenye wivu.

254:25 1Fal 11:6; 15:26; 16:25-30; 2Fal 17:2; 17:21Baada ya kuwa na watoto na wajukuu na kuishi katika nchi hiyo siku nyingi, tena kama mkijichafua na kutengeneza sanamu ya aina yoyote, mkifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wenu na kumfanya awe na hasira, 264:26 Mwa 31:50; Mit 14:5; Kum 30:18-19; 31:28; 32:1; Za 50:4; Isa 1:2; 34:1; Yer 6:19; Mik 6:2; Kum 6:15; 7:4ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yenu siku hii kwamba mtaangamia mara moja kutoka nchi ile ambayo mnavuka Yordani kuimiliki. Hamtaishi kule kwa muda mrefu bali kwa hakika mtaangamizwa. 274:27 Law 26:23; Kum 28:36-64; 29:28; 1Fal 8:46; 2Fal 17:16; Za 44:11; 106:27; Yer 3:8; Mik 1:16; Isa 17:6; 21:17; Oba 1:5; Neh 1:8Bwana atawatawanya miongoni mwa mataifa, na ni wachache wenu tu watakaosalia miongoni mwa mataifa hayo ambayo Bwana atawafukuzia. 284:28 Kum 13:2; 28:36-64; 1Sam 26:19; Yer 5:19; 16:13; Mdo 19:26; Kum 29:17; Za 115:4-8; 135:15-18; Isa 8:19; 26:14; 44:17-20; Ufu 9:20Huko mtaabudu miungu ya miti na mawe iliyotengenezwa na watu, ambayo haiwezi kuona au kusikia wala kula au kunusa. 294:29 1Sam 13:12; 2Fal 13:4; 2Nya 7:14; 15:4; 33:12; Za 78:34; 119:58; Isa 45:19, 22; 55:6; Yer 26:19; Dan 9:13; Hos 3:5; Amo 5:4; 1Sam 7:3; 1Fal 8:48; Yer 29:13; Kum 6:5; 30:1-3, 10Lakini kama mtamtafuta Bwana Mungu wenu, mtampata; kama mtamtafuta kwa moyo wenu wote na kwa roho yote. 304:30 Hos 3:5; Law 26:41; Kum 31:17-21; Za 4:1; 18:6; 48:1; 59:16; 107:6; Kum 31:29; Yer 23:20; 3:1-12, 22; 4:1; 18:11; Ebr 1:2; Kum 30:2; 1Fal 8:48; Neh 1:9; Yoe 2:12Wakati mnapokuwa katika dhiki, nayo mambo haya yote yamewatokea siku hizo, ndipo mtamrudia Bwana Mungu wenu na kumtii. 314:31 Kut 34:6; Neh 9:31; Za 111:9; Kum 31:6-8; Yoe 1:5; 1Fal 8:57; 1Nya 28:9-20; Za 9:10; 27:9; 71:9; Isa 42:16; Ebr 13:5; Law 26:44-45; Yon 4:2Kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu mwenye huruma, hatawaacha au kuwaangamiza wala kusahau Agano alilofanya na baba zenu, alilowathibitishia kwa kiapo.

Bwana Ndiye Mungu

324:32 Kum 32:7; Mwa 1:27; Isa 45:12; Kum 28:64; 30:1; Yer 9:16; Mt 24:31; 2Sam 7:23; Ay 8:8Sasa uliza kuhusu siku za zamani, zamani kabla ya wakati wako, tangu siku ile Mungu alipomuumba mtu juu ya nchi, uliza kutoka mwisho mmoja wa mbingu mpaka mwisho mwingine wa mbingu. Je, kumepata kutokea jambo jingine lililo kubwa kama hili, au kuna jambo jingine kama hilo limepata kusikiwa? 334:33 Kut 20:22; Kum 5:24-26Je, kuna watu wengine wowote waliosikia sauti ya Mungu ikizungumza kwenye moto, kama mlivyosikia, nao wakaishi? 344:34 Kut 14:30; Isa 7:12; Kut 4:17; Kum 7:19; 26:8; 29:3; 1Nya 16:12; Za 9:1; 40:5; Yer 32:20; Kut 32:20; 3:20; Kum 5:15; 6:21; 15:15; Kut 15:1; Kum 34:12; Za 45:4; 65:5Je, kuna mungu yeyote amepata kujaribu mwenyewe kuchukua taifa moja kutoka taifa lingine, kwa mapigo, kwa ishara za miujiza na maajabu, kwa vita, kwa mkono wenye nguvu na mkono ulionyooshwa au kwa matendo makuu ya kutisha, kama yale ambayo Bwana Mungu wenu aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu?

354:35 Kum 4:39; 7:9; 32:4-12; Kut 8:10; 1Sam 2:2; 1Fal 8:60; 2Fal 19:19; Isa 3:10; Mk 12:32Mlionyeshwa mambo haya ili mpate kujua kuwa Bwana ndiye Mungu; hakuna mwingine ila yeye. 364:36 Kut 19:19; Kum 8:5; Kut 19:20; 18:22; 24:16; 1Nya 29:1; 2Nya 20:6; Ebr 12:18, 25Kutoka mbinguni amewasikizisha sauti yake ili kuwaadilisha. Hapa duniani aliwaonyesha moto wake mkubwa, nanyi mlisikia maneno yake kutoka kwenye ule moto. 374:37 Kum 7:8; 10:15; 23:5; 33:3; Za 44:3; Yer 31:3; Hos 11:1; Mal 1:2; 2:11; Kut 3:20; 13:3, 9-14Kwa sababu aliwapenda baba zenu na alichagua wazao wao baada yao, aliwatoa katika nchi ya Misri kwa Uwepo wake na kwa uwezo wake mkuu, 384:38 Hes 34:14-15; Kum 7:1; 9:5aliwafukuza mbele yenu mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi na kuwaleta ninyi katika nchi yao na akawapa ninyi kuwa urithi wenu, kama ilivyo leo.

394:39 Kum 8:10; Kut 15:11; Yos 2:11; Isa 42:8; Dan 4:35Kubalini na mweke moyoni leo kuwa Bwana ndiye Mungu mbinguni juu na duniani chini. Hakuna mwingine. 404:40 Law 22:31; Mwa 26:5; Kum 5:29; 11:1; Za 105:45; Isa 48:18; Kum 5:16; 12:25; Isa 3:10; Kut 23:26; Efe 6:2-3Mshike amri na maagizo yake ninayowapa leo, ili mpate kufanikiwa ninyi na watoto wenu baada yenu, na mpate kuishi maisha marefu katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu siku zote.

Miji Ya Makimbilio

414:41 Hes 35:6Kisha Mose akatenga miji mitatu mashariki ya Yordani, 424:42 Kut 21:13ambayo mtu yeyote aliyemuua mtu angeweza kukimbilia ikiwa amemuua jirani yake bila kukusudia na bila kuwa na chuki naye siku zilizopita. Angeweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake. 434:43 Yos 21:38; 1Fal 22:3; 2Fal 8:28; 9:14Miji hiyo ilikuwa: Bezeri katika tambarare ya jangwa kwa ajili ya Wareubeni; Ramothi katika nchi ya Gileadi kwa ajili ya Wagadi; nao mji wa Golani katika nchi ya Bashani kwa ajili ya Wamanase.

Utangulizi Wa Sheria

44Hii ndiyo sheria Mose aliyoweka mbele ya Waisraeli. 45Haya ndiyo masharti, amri na sheria Mose aliyowapa wana wa Israeli wakati walitoka Misri, 464:46 Hes 21:26; Kum 3:29nao walikuwa katika bonde karibu na Beth-Peori mashariki ya Yordani, katika nchi ya Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, naye alishindwa na Mose na Waisraeli walipokuja toka Misri. 474:47 Hes 21:25; Kum 3:3, 4Waliimiliki nchi yake na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, wafalme wawili Waamori waliotawala mashariki ya Yordani. 484:48 Kum 2:36; 3:8-9; Za 133:3Nchi hii ilienea kutoka Aroeri ukingoni mwa Bonde la Arnoni mpaka Mlima Sioni (yaani Hermoni), 49pamoja na eneo lote la Araba mashariki ya Yordani, na kuenea mpaka Bahari ya Araba kwenye miteremko ya Pisga.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

申命記 4:1-49

當守律法

1以色列人啊,要聆聽我傳授給你們的律法,要切實遵行,以便你們可以存活,並進入你們祖先的上帝耶和華賜給你們的那片土地。 2我吩咐你們的,你們不可做任何增減,這是你們的上帝耶和華的命令,你們要遵守。 3你們親眼看見耶和華在巴力·毗珥事件中的作為,你們的上帝耶和華毀滅了你們中間所有拜巴力·毗珥的人, 4但你們這些信靠你們的上帝耶和華的人至今還活著。 5看啊,遵照我的上帝耶和華的吩咐,我把律例和典章傳授給你們,好讓你們在將要佔領的土地上遵守。 6你們要謹遵這些律例和典章,因為這樣就會讓外族人看見你們的智慧和聰明。他們聽見這些律法後,必說,『這偉大的民族真有智慧和聰明!』 7我們的上帝耶和華與我們如此親近,隨時垂聽我們的呼求,有哪個偉大民族的神明能與之相比? 8有哪個偉大的民族擁有我今天所傳授給你們的如此公義的律例和典章?

9「要謹慎、小心,不可忘記親眼所見的事,要一生銘記在心,並且告訴子子孫孫。 10那天,你們在何烈山站在你們的上帝耶和華面前,耶和華對我說,『把民眾招聚起來,讓他們聽我的教誨,學習一生敬畏我,並傳授給自己的兒女。』 11你們來到山腳下,站在那裡,山上烈焰沖天、烏雲密佈、極其幽暗。 12耶和華在火焰中對你們說話,你們只聽見祂的聲音,卻看不見祂的形像。 13祂向你們宣告祂的約,就是祂吩咐你們遵守的十誡,並寫在兩塊石版上。 14那時,耶和華吩咐我把律例和典章傳授給你們,好讓你們在將要佔領的土地上遵守。

不可拜偶像

15「你們要格外小心,耶和華在何烈山的火焰中對你們說話時,你們沒有看見任何形像, 16所以不可墮落,去為自己製造任何形狀的神像——男人、女人、 17飛禽走獸、 18爬蟲或魚類。 19當你們舉目觀看你們的上帝耶和華賜給天下萬民的日、月、星辰等天上萬象時,不要受誘惑去跪拜、供奉它們。 20耶和華拯救你們脫離埃及那座熔鐵爐,讓你們做祂自己的子民,正如今日的情形。 21因你們的緣故,耶和華向我發怒,起誓不讓我過約旦河、進入祂賜給你們作產業的那片佳美之地。 22我將死在約旦河這邊,過不了約旦河。但你們必過去得到那片佳美之地。 23你們要謹慎,不可忘記你們的上帝耶和華與你們所立的約,不可違背你們上帝耶和華的禁令,去製造任何形狀的神像。 24因為你們的上帝耶和華是烈火,是痛恨不貞的上帝。

25「將來,即使你們在那裡安頓已久、子孫滿堂,也不可墮落、製造任何形狀的神像,不可做你們的上帝耶和華視為邪惡的事,惹祂發怒。 26否則,今天我叫天地作證,你們必很快從約旦河對面將要佔領的土地上滅亡,你們必被徹底消滅,不得在那裡長久居住。 27耶和華必把你們驅散到列邦,使你們在列邦中的人數所剩無幾。 28你們必在那裡供奉人用木石造的不會看、不會聽、不會吃、不會聞的神像。 29但你們若在那裡尋求你們的上帝耶和華,全心全意地尋求祂,就必尋見。 30日後,當你們遭遇這些事,受盡苦難的時候,必歸向你們的上帝耶和華,聽從祂。 31因為你們的上帝耶和華充滿憐憫,祂不會拋棄你們,滅絕你們,也不會忘記祂與你們祖先所立的誓約。

獨一的上帝

32「你們可以查考歷史,自上帝創造世人以來,這樣的奇事,天地之間何曾有過?誰曾聽聞? 33有哪個民族像你們一樣,聽見了上帝在火中說話,還活了下來? 34有哪個神明像你們的上帝耶和華那樣在埃及當著你們的面降災禍、行神蹟奇事、興起戰爭、伸出臂膀、施展大能的手、以偉大而可畏的作為拯救一族脫離異邦? 35耶和華行這樣的事,是要叫你們知道祂是上帝,除祂以外,別無他神。 36祂讓你們聽見祂從天上來的聲音,好教導你們,又在地上讓你們看見祂的烈火,並聽見祂在烈火中說的話。 37因為祂愛你們的祖先,所以揀選你們,親自用大能把你們從埃及領出來, 38趕走比你們強大的民族,領你們進入他們的土地,把他們的土地賜給你們作產業,正如今日的情形。 39所以,今天你們要知道並謹記,耶和華是天上地下的上帝,此外別無他神。 40我今天將祂的律例和誡命傳授給你們,你們要遵守,以便你們及子孫都蒙福,在你們上帝耶和華所賜的土地上得享長壽。」

設立避難城

41那時,摩西約旦河東劃出三座城作避難城, 42供素無冤仇卻誤殺他人者逃往避難。 43三座城分別是曠野高原的比悉——供呂便人避難,基列拉末——供迦得人避難,巴珊哥蘭——供瑪拿西人避難。

重申律法

44以下是摩西頒佈給以色列人的律法, 45即在離開埃及後傳授給他們的法度、律例和典章。 46當時他們在約旦河以東伯·毗珥對面的山谷,那裡原屬於希實本亞摩利西宏摩西以色列人離開埃及後消滅了西宏47佔領了他的土地,還佔領了巴珊的土地。西宏約旦河東亞摩利人的兩個王, 48其國土從亞嫩谷邊的亞羅珥一直到西雲山,即黑門山, 49包括約旦河東的整個亞拉巴,遠至毗斯迦山腳的亞拉巴海。