Kumbukumbu 32 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 32:1-52

132:1 Za 49:1; Mik 1:2; Yer 2:12; Kum 4:26; Isa 1:2Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitasema;

sikia, ee nchi, maneno ya kinywa changu.

232:2 2Sam 23:4; Za 107:20; Isa 9:8; 55:11; Mik 5:7; Za 65:10; 68:9; 72:8; 147:8Mafundisho yangu na yanyeshe kama mvua,

na maneno yangu na yashuke kama umande,

kama manyunyu juu ya majani mabichi,

kama mvua tele juu ya mimea myororo.

332:3 Za 118:17; 145:6; Kut 33:16-19; 34:4-6; Kum 3:24Nitalitangaza jina la Bwana.

Naam, sifuni ukuu wa Mungu wetu!

432:4 Mwa 49:24; 2Sam 22:31; Za 18:30; 19:7; Kum 4:35; Za 92:15; Mwa 18:25Yeye ni Mwamba, kazi zake ni kamilifu,

njia zake zote ni haki.

Mungu mwaminifu ambaye hakosei,

yeye ni mnyofu na mwenye haki.

532:5 Kum 31:29; Mt 17:17; Lk 9:41; Mdo 2:40Wamefanya mambo ya upotovu mbele zake;

kwa aibu yao, wao si watoto wake tena,

lakini ni kizazi kilicho kiovu na kilichopotoka.

632:6 Za 116:12; 94:8; Yer 5:21; Kut 4:22; 2Sam 7:24; Isa 63:16Je, hii ndiyo njia ya kumlipa Bwana,

enyi watu wajinga na wasio na busara?

Je, yeye siye Baba yenu, Muumba wenu,

aliyewafanya ninyi na kuwaumba?

732:7 Za 44:1; 74:2; 74:2; 77:5; Isa 51:9; 63:9; Kum 4:32; Yos 8:8; 20:4; Za 78:4; Isa 46:9; Kut 10:2; 13:14; Ay 15:18Kumbuka siku za kale;

tafakari vizazi vya zamani vilivyopita.

Uliza baba yako, naye atakuambia,

wazee wako, nao watakueleza.

832:8 Za 7:8; Mwa 11:8; Mdo 8:1; Za 74:17; Hes 23:9; Kum 33:12; 28; Yer 23:6; Mdo 17:26Aliye Juu Sana alipowapa mataifa urithi wao,

alipogawanya wanadamu wote,

aliweka mipaka kwa ajili ya mataifa

sawasawa na hesabu ya wana wa Israeli.

932:9 Za 16:5; 73:26; 119:57; 142:5; Yer 10:16; Kum 9:29; 1Sam 26:19; 1Fal 8:51-53Kwa kuwa fungu la Bwana ni watu wake,

Yakobo kura yake ya urithi.

1032:10 Kum 1:19; 8:15; Ay 12:24; Za 107:40; 32:10; Yer 31:22; Za 17:8; Mit 7:2; Hos 13:5; Zek 2:8Katika nchi ya jangwa alimkuta,

katika nyika tupu ivumayo upepo.

Alimhifadhi na kumtunza;

akamlinda kama mboni ya jicho lake,

1132:11 Kut 19:4; Za 17:8; 18:10-19; 61:4kama tai avurugaye kiota chake,

na kurukaruka juu ya makinda yake,

ambaye hutanda mabawa yake kuwadaka,

na huwachukua kwenye mabawa yake.

1232:12 Za 106:9; Isa 63:13; Yer 31:32; Kum 4:35; Amu 2:12; Za 18:31; 81:9; Isa 43:12; 45:5Bwana peke yake alimwongoza;

hakuwepo mungu mgeni pamoja naye.

1332:13 Kum 33:29; 2Sam 22:34; Za 18:33; Isa 33:16; 58:14; Eze 36:2; Ebr 3:19; Kum 8:8; 33:24; Ay 29:6Akamfanya apande sehemu zilizoinuka za nchi,

akamlisha kwa mavuno ya mashamba.

Akamlea kwa asali toka mwambani,

na kwa mafuta kutoka mwamba mgumu,

1432:14 Hes 21:33; Za 65:9; 81:16; 147:14; Mwa 49:11kwa jibini na maziwa kutoka makundi ya ngʼombe

na kutoka makundi ya mbuzi,

kwa mafuta ya wana-kondoo na mbuzi,

kwa kondoo dume wazuri wa Bashani,

na kwa ngano nzuri.

Ukanywa damu ya zabibu inayotoa povu.

1532:15 Kum 33:5; 26; Isa 44:2; Kum 31:20; Yer 5:28; Kum 31:16; Isa 1:4, 28; 58:2; 65:11; Yer 15:6; Eze 14:5; Mwa 49:24Yeshuruni32:15 Yeshuruni maana yake ni Yeye aliye mnyofu, yaani Israeli (ona pia Kum 33:26; Isa 44:2). alinenepa na kupiga teke;

alikuwa na chakula tele,

akawa mzito na akapendeza sana.

Akamwacha Mungu aliyemuumba,

na kumkataa Mwamba Mwokozi wake.

1632:16 1Kor 10:22; Kum 31:17; 1Fal 14:9Wakamfanya Mungu kuwa na wivu kwa miungu yao migeni,

na kumkasirisha kwa sanamu zao

za machukizo.

1732:17 Kut 32:8; 22:20; 1Kor 10:20; Kum 28:64; Amu 5:8Wakatoa dhabihu kwa pepo, ambao si Mungu:

miungu wasiyoijua,

miungu iliyojitokeza siku za karibuni,

miungu ambayo baba zenu hawakuiogopa.

1832:18 Amu 3:7; 1Sam 12:9; Za 44:17, 20; 106:21; Yer 2:32; Eze 23:35; Hos 8:14; 13:6Mkamwacha Mwamba, aliyewazaa ninyi;

mkamsahau Mungu aliyewazaa.

1932:19 Law 26:30; Za 78:59; Amo 6:8; Yer 44:21-23; Za 106:40Bwana akaona hili, akawakataa,

kwa sababu alikasirishwa

na wanawe na binti zake.

2032:20 Kum 31:17; Za 4:6; 44:24; Kum 9:23Akasema, “Nitawaficha uso wangu,

nami nione mwisho wao utakuwa nini,

kwa kuwa wao ni kizazi kilichopotoka,

watoto ambao si waaminifu.

2132:21 Hes 25:11; 1Kor 10:22; 1Fal 16:13, 26; 2Fal 17:15; Yer 8:19; Yon 2:8; Rum 10:19; Za 31:6; Yer 2:8; 10:8; 16:19Wamenifanya niwe na wivu

kwa kile ambacho si mungu,

na kunikasirisha kwa sanamu zao

zisizokuwa na thamani.

Nitawafanya wawaonee wivu wale ambao si taifa.

Nitawafanya wakasirishwe

na taifa lile lisilo na ufahamu.

2232:22 Za 7:11; Hes 16:31-35; Za 18:7-8; Yer 15:14; Mao 4:11; Amo 7:4; Law 26:20Kwa maana moto umewashwa kwa hasira yangu,

ule uwakao hadi kwenye vina vya mauti.

Utateketeza dunia pamoja na mazao yake,

na kuwasha moto katika misingi ya milima.

2332:23 Kum 29:21; 2Sam 22:15; Ay 6:4; Za 7:13; 18:14; 45:5; 77:17; 120:4; Isa 5:28; 49:2; Eze 5:16; Hab 3:9-11“Nitalundika majanga juu yao

na kutumia mishale yangu dhidi yao.

2432:24 Mwa 26:1; 41:55; 42:5; 2Sam 24:13; 1Nya 21:12; Kum 28:22; Za 91:6; Mwa 37:20; Ay 20:16; Za 58:4; Yer 8:17; Amo 5:18-19; Mik 7:17; Ay 20:16Nitatuma njaa kali dhidi yao maradhi mabaya,

yateketezayo na tauni ya kufisha;

nitawapelekea meno makali ya wanyama mwitu,

na sumu ya nyoka wale watambaao mavumbini.

2532:25 Isa 24:17; Yer 14:18; Mao 1:20; Eze 7:15; 2Kor 7:5; 2Nya 36:17; Isa 13:18; Yer 4:31; Mao 2:21Barabarani upanga utawakosesha watoto;

nyumbani mwao hofu itatawala.

Vijana wao wa kiume na wa kike wataangamia,

pia watoto wachanga na wazee wenye mvi.

2632:26 Kum 4:27; Hes 14:12; Ay 18:17; Za 34:16; 37:28; 109:15; Isa 14:20Nilisema ningewatawanya

na kufuta kumbukumbu lao

katika mwanadamu.

2732:27 Kum 9:26-28; Za 140:8; Isa 11:13; Yer 40:2-3Lakini nilihofia dhihaka za adui,

adui asije akashindwa kuelewa,

na kusema, ‘Mikono yetu imeshinda;

Bwana hakufanya yote haya.’ ”

2832:28 Isa 1:3; 5:13; 27:11; Yer 8:7Wao ni taifa lisilo na akili,

hakuna busara ndani yao.

2932:29 Kum 5:29; Za 81:13; Isa 47:7; Mao 1:9Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili,

na kutambua mwisho wao utakuwa aje!

3032:30 Law 26:8; Amu 2:14; 3:8; 4:2; 10:7; 1Sam 12:9; Hes 21:34; 1Sam 23:7; Za 31:18; 44:12; 106:41; Isa 50:1; 54:6Mtu mmoja angewezaje kufukuza elfu moja,

au wawili kufukuza elfu kumi,

kama si kwamba Mwamba wao amewauza,

kama si kwamba Bwana amewaacha?

3132:31 Mwa 49:24; Kut 14:25Kwa kuwa mwamba wao si kama Mwamba wetu,

sawasawa na vile adui zetu wanavyokiri.

3232:32 Yer 23:14; Ay 6:4; 20:16; Kum 29:18Mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma,

na kutoka kwenye mashamba ya Gomora.

Zabibu zake zimejaa sumu,

na vishada vyake vimejaa uchungu.

3332:33 Za 58:4Mvinyo wao ni sumu ya nyoka,

sumu yenye kufisha ya swila.

3432:34 Ay 14:17; Yer 2:22; Hos 13:12“Je, hili sikuliweka akiba

na kulifungia kwenye vyumba vyangu vya hazina?

3532:35 Mwa 4:24; Yer 51:6; Mwa 30:2; Kut 32:34; Za 54:5; Rum 12:19; Ebr 10:30; Za 17:5; 35:6; 37:31; 38:16; 66:9; 73:2; 94:18; 121:3; Mit 4:19; Yer 23:12; Eze 7:8-9Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.

Wakati utakapowadia, mguu wao utateleza;

siku yao ya maafa ni karibu,

na maangamizo yao yanawajia haraka.”

3632:36 Ebr 10:30; Amo 7:3; Law 26:43-45; Kum 30:1-3; Amu 2:18; Za 90:13; 102:13; 103:13; 106:45; 135:14; Yoe 2:14; 1Fal 14:10; 21:21; 2Fal 9:8Bwana atawahukumu watu wake,

na kuwahurumia watumishi wake

atakapoona nguvu zao zimekwisha

wala hakuna yeyote aliyebaki,

mtumwa au aliye huru.

3732:37 Amu 10:14; Yer 2:28; 11:12Atasema: “Sasa iko wapi miungu yao,

mwamba walioukimbilia,

3832:38 Hes 25:1-2; Yer 11:12; 44:8; 25miungu wale waliokula mafuta ya dhabihu zao

na kunywa mvinyo wa sadaka zao za vinywaji?

Wainuke basi, wawasaidie!

Wawapeni basi ulinzi!

3932:39 Isa 41:4; 43:10; 44:7; 46:4; 48:12; 1Sam 2:6; 2Fal 5:7; Za 68:20; Yn 11:25-26; Kut 15:26; Ay 5:18; 15:11; Za 147:3; Isa 6:10; 19:22; 30:26; 53:5; 57:18; Yer 33:6; Hos 6:1; Mal 4:2; 1Pet 2:24; Ay 9:12; 10:7; Za 7:2; 50:22; Isa 43:13; Dan 4:35; Hos 5:14“Tazama basi, Mimi mwenyewe, Mimi Ndiye!

Hakuna mungu mwingine ila Mimi.

Mimi ninaua na Mimi ninafufua,

Mimi nimejeruhi na Mimi nitaponya,

wala hakuna awezaye kuokoa kutoka mkononi mwangu.

4032:40 Mwa 14:22; 21:23; Ufu 1:18Ninainua mkono wangu kuelekea mbinguni na kusema:

Hakika kama niishivyo milele,

4132:41 Amu 7:20; Za 7:12; 45:3; Isa 27:1; 34:6; 66:16; Yer 12:12; Eze 21:9-10; Za 149:7; Yer 46:10; Neh 1:2; Za 137:8; Yer 25:14; 50:29; 51:24, 56wakati ninapounoa upanga wangu unaometameta

na mkono wangu unapoushika ili kutoa hukumu,

nitalipiza kisasi juu ya adui zangu

na kuwalipiza wale wanaonichukia.

4232:42 2Sam 2:26; Yer 12:12; 44:1; 46:10-14Nitailevya mishale yangu kwa damu,

wakati upanga wangu ukitafuna nyama:

damu ya waliochinjwa pamoja na mateka,

vichwa vya viongozi wa adui.”

4332:43 Za 137:6; Isa 25:9; 65:18; 66:10; Rum 15:10; 2Fal 9:7; Ufu 6:10; Isa 1:24; Yer 9:9; Za 65:3; 79:9Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake,

kwa kuwa atailipiza damu ya watumishi wake,

atalipiza kisasi juu ya adui zake

na kufanya upatanisho

kwa ajili ya nchi na watu wake.

4432:44 Hes 13:8, 16Mose na Yoshua32:44 Yoshua, yaani Yehoshea kwa Kiebrania, maana yake ni Yehova ni Mwokozi. mwana wa Nuni wakaja, wakanena maneno yote ya wimbo watu wakiwa wanasikia. 45Mose alipomaliza kuyasoma maneno haya yote kwa Israeli wote, 4632:46 Kum 6:6; Yn 1:17; 7:19; Kum 6:7akawaambia, “Yawekeni moyoni maneno yote ambayo nimewatangazia kwa makini siku hii ya leo, ili kwamba mpate kuwaagiza watoto wenu wayatii kwa bidii maneno yote ya sheria hii. 4732:47 Kum 30:20; 33:25; Kut 23:26; Isa 65:22Siyo maneno matupu tu kwenu, bali ni uzima wenu. Kwa hayo mtaishi maisha marefu katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”

Mose Aelezwa Kuhusu Kifo Chake

4832:48 Hes 27:12Siku hiyo hiyo Bwana akamwambia Mose, 4932:49 Hes 27:12; 32:3; 22:1; Law 14:34“Kwea katika mapangano ya Mlima Abarimu hadi kilima cha Nebo kilichoko Moabu, ngʼambo ya Yeriko, na uitazame Kanaani, nchi ninayowapa Waisraeli kama milki yao wenyewe. 5032:50 Mwa 25:8; Hes 27:13; 20:22; 29Utafia kwenye mlima huo unaokwea na kukusanyika pamoja na watu wako, kama ndugu yako Aroni alivyofia juu ya Mlima Hori naye akakusanyika kwa watu wake. 5132:51 Eze 47:19; Hes 13:21; 20:11-13; 27:14Hii ni kwa sababu ninyi wawili mlivunja uaminifu nami mbele ya Waisraeli kwenye maji ya Meriba-Kadeshi katika Jangwa la Sini, na kwa sababu hamkuuinua utakatifu wangu miongoni mwa Waisraeli. 5232:52 Kum 34:1-3; 3:27Kwa hiyo, utaiona tu nchi kwa mbali; wewe hutaingia nchi ninayowapa watu wa Israeli.”

New International Reader’s Version

Deuteronomy 32:1-52

1Heavens, listen to me. Then I will speak.

Earth, hear the words of my mouth.

2Let my teaching fall like rain.

Let my words come down like dew.

Let them be like raindrops on new grass.

Let them be like rain on tender plants.

3I will make known the name of the Lord.

Praise God! How great he is!

4He is the Rock. His works are perfect.

All his ways are right.

He is faithful. He doesn’t do anything wrong.

He is honest and fair.

5Israel, you have sinned against him very much.

It’s too bad for you that you aren’t his children anymore.

You have become a twisted and evil nation.

6Is that how you thank the Lord?

You aren’t wise. You are foolish.

Remember, he’s your Father. He’s your Creator.

He made you. He formed you.

7Remember the days of long ago.

Think about what the Lord did through those many years.

Ask your father. He will tell you.

Ask your elders. They’ll explain it to you.

8The Most High God gave the nations their lands.

He divided up the human race.

He set up borders for the nations.

He did it based on the number of the angels in his heavenly court.

9The Lord’s people are his share.

Jacob is the nation he has received.

10The Lord found Israel in a desert.

He found them in an empty and windy land.

He took care of them and kept them safe.

He guarded them as he would guard his own eyes.

11He was like an eagle that stirs up its nest.

It hovers over its little ones.

It spreads out its wings to catch them.

It carries them up in the air on its feathers.

12The Lord was the only one who led Israel.

No other god was with them.

13The Lord made them ride on the highest places in the land.

He fed them what grew in the fields.

He gave them the sweetest honey.

He fed them olive oil from a rocky hillside.

14He gave them butter and milk from the herds and flocks.

He fed them the fattest lambs and goats.

He gave them the best of Bashan’s rams.

He fed them the finest wheat.

They drank the bubbling red juice of grapes.

15When Israel grew fat, they became stubborn.

When they were filled with food, they became fat and heavy.

They left the God who made them.

They turned away from the Rock who saved them.

16They made him jealous by serving false gods.

They made him angry by worshiping statues of gods.

He hated those gods.

17The people sacrificed to those false gods, not to God.

They hadn’t known anything about those false gods.

Those gods were new to them.

Their people of long ago didn’t worship them.

18But then they deserted the Rock. He was their Father.

They forgot the God who created them.

19When the Lord saw this, he turned away from them.

His sons and daughters made him angry.

20“I will turn my face away from them,” he said.

“I will see what will happen to them in the end.

They are sinful people.

They are unfaithful children.

21They made me jealous by serving what is not even a god.

They made me angry by worshiping worthless statues of gods.

I will use people who are not a nation to make them jealous.

A nation that has no understanding will make them angry.

22My anger will start a fire.

It will burn all the way down to the kingdom of the dead.

It will eat up the earth and its crops.

It will set the base of the mountains on fire.

23“I will pile troubles on my people.

I will shoot all my arrows at them.

24I will send them hunger. It will make them weak.

I will send terrible sickness. I will send deadly plagues.

I will send wild animals that will tear them apart.

Snakes that glide through the dust will bite them.

25In the streets their children will be killed by swords.

Their homes will be filled with terror.

The young men and women will die.

The babies and old people will die.

26I said I would scatter them.

I said I would erase their name from human memory.

27But I was afraid their enemies would make fun of that.

I was afraid their attackers would not understand.

I was sure they would say, ‘We’re the ones who’ve beaten them!

The Lord isn’t the one who did it.’ ”

28Israel is a nation that doesn’t have any sense.

They can’t understand anything.

29I wish they were wise. Then they would understand what’s coming.

They’d realize what would happen to them in the end.

30How could one person chase a thousand?

How could two make ten thousand run away?

It couldn’t happen unless their Rock had deserted them.

It couldn’t take place unless the Lord had given them up.

31Their rock is not like our Rock.

Even our enemies know that.

32Their vine comes from the vines of Sodom.

It comes from the vineyards of Gomorrah.

Their grapes are filled with poison.

Their bunches of grapes taste bitter.

33Their wine is like the poison of snakes.

It’s like the deadly poison of cobras.

34The Lord says, “I have kept all those terrible things stored away.

I have kept them sealed up in my strongbox.

35I punish people. I will pay them back.

The time will come when their feet will slip.

Their day of trouble is near.

Very soon they will be destroyed.”

36The Lord will come to the aid of his people.

He’ll show tender love to those who serve him.

He will know when their strength is gone.

He’ll see that no one at all is left.

37He’ll say, “Where are their gods now?

Where is the rock they went to for safety?

38Where are the gods who ate the fat of their sacrifices?

Where are the gods who drank the wine of their drink offerings?

Let those gods rise up to help you!

Let them keep you safe!

39“Look! I am the One!

There is no other God except me.

I put some people to death. I bring others to life.

I have wounded, and I will heal.

No one can save you from my power.

40I raise my hand to heaven. Here is the promise I make.

You can be sure that I live forever.

41And you can be just as sure

that I will sharpen my flashing sword.

My hand will hold it when I judge.

I will get even with my enemies.

I will pay back those who hate me.

42I will make my arrows drip with blood.

My sword will destroy people.

It will kill some. It will even kill prisoners.

It will cut off the heads of enemy leaders.”

43You nations, be full of joy. Be joyful together with God’s people.

The Lord will get even with his enemies.

He will pay them back for killing those who serve him.

He will wipe away the sin of his land and people.

44Moses spoke all the words of this song to the people. Joshua, the son of Nun, was with him. 45Moses finished speaking all these words to all the Israelites. 46Then he said to them, “Think carefully about all the words I have announced to you today. I want you to command your children to be careful to obey all the words of this law. 47They aren’t just useless words for you. They are your very life. If you obey them, you will live in the land for a long time. It’s the land you are going across the Jordan River to take as your own.”

Moses Will Die on Mount Nebo

48On that same day the Lord said to Moses, 49“Go up into the Abarim mountains. Go to Mount Nebo in Moab. It is across from Jericho. From there look out over Canaan. It is the land I am giving the Israelites to take as their own. 50You will die there on the mountain you have climbed. You will join the members of your family who have already died. In the same way, your brother Aaron died on Mount Hor. He joined the members of his family who had already died. 51You and Aaron disobeyed me in front of the Israelites. It happened at the waters of Meribah Kadesh in the Desert of Zin. You did not honor me among the Israelites as the holy God. 52So you will see the land, but only from far away. You will not enter the land I am giving to the Israelites.”