Kumbukumbu 30 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 30:1-20

Mafanikio Baada Ya Kumgeukia Bwana

130:1 Kum 11:26; Law 26:40-45; Kum 4:32; 29:28; 1Fal 8:47Wakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popote Bwana Mungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa, 230:2 Kum 4:29-30hapo wewe na watoto wako mtakapomrudia Bwana Mungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo, 330:3 Za 14:7; 53:6; 85:1; 126:4; Yer 30:18; 33:11; Eze 16:53; Yoe 3:1; Sef 2:7; Kum 13:17; Mwa 48:21; 11:4; Kum 4:27; Isa 11:11; Yer 12:15; 16:15; 26:4; 29:14; 48:47; 49:6ndipo Bwana Mungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya. 430:4 Isa 17:6; 24:13; 27:12; 40:11; 41:5; 49:5; 56:8; Eze 20:34, 41; 34:13; Za 19:6; Neh 1:8-9; Isa 11:12; 42:10; 43:6; 48:20; 62:11; Yer 31:8, 10; 50:2Hata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka huko Bwana Mungu wako atakukusanya na kukurudisha. 530:5 Yer 29:14; Kum 7:13Yeye Bwana atakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako. 630:6 Kum 6:24; 10:16; 6:5; Yer 32:29Bwana Mungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi. 730:7 Mwa 12:3; Kum 7:15Bwana Mungu wako ataweka laana hizi zote juu ya adui zako ambao wanakuchukia na kukutesa. 8Utamtii tena Bwana na kuzishika amri zake zote ninazokupa leo. 930:9 Yer 1:10; 24:6; 31:28; 32:41; 42:10; 45:4; Kum 28:63; Eze 34:27; Yer 32:41; 33:9; Sef 3:17; Lk 15:6, 10, 32; Yn 15; 11Ndipo Bwana Mungu wako atakapokufanikisha sana katika kazi zote za mikono yako na katika uzao wa tumbo lako, wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako. Bwana atakufurahia tena na kukufanikisha, kama alivyowafurahia baba zako, 1030:10 Kum 28:61; 4:29kama ukimtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake ambayo yameandikwa katika Kitabu hiki cha Sheria, na kumgeukia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.

Uzima Na Mauti

1130:11 Za 19:8; Isa 45:19-23; 63:1Ninachokuagiza leo sio kigumu sana kwako au usichokiweza. 1230:12 Mit 30:4; Rum 10:6; Yn 3:13Hakiko juu mbinguni, ili uulize, “Ni nani atakayepanda mbinguni kukileta na kututangazia ili tuweze kutii?” 1330:13 Ay 28:14; Rum 10:7Wala hakiko ngʼambo ya bahari, ili uulize, “Ni nani atakayevuka bahari kwenda kukichukua na kututangazia ili tupate kutii?” 1430:14 Kum 6:6; Rum 10:8La hasha! Lile neno liko karibu sana nawe; liko kinywani mwako na ndani ya moyo wako ili uweze kulitii.

1530:15 Mit 10:16; 11:9; 12:28; 3:1-2; Kum 28:11; Za 25:13; 106:5; Mwa 2:17; Kum 11:26Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo. 1630:16 Kum 6:5; 4:1; 32:17; Neh 9:29Ninakuamuru leo kwamba umpende Bwana Mungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, naye Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.

17Lakini kama moyo wako ukigeukia mbali ukawa huna utii, kama umevutwa kuisujudia miungu mingine na kuiabudu, 1830:18 Kum 8:19nakutangazia leo hii kwamba hakika utaangamizwa. Hutaishi maisha marefu katika nchi unayovuka Yordani kuiingia na kuimiliki.

1930:19 Kum 4:26; 11:26Leo ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yako kwamba nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana. Basi sasa chagueni uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi, 2030:20 Kum 6:5; 4:1; 8:3; 32:47; 10:20; Za 27:1; Yn 5:26; Mdo 17:28; Mit 3:22; Mwa 12:7; Za 37:3na ili upate kumpenda Bwana Mungu wako, uisikilize sauti yake na kuambatana naye. Kwa kuwa Bwana ndiye uzima wako, na atakupa wingi wa siku ili upate kuishi katika nchi aliyoapa kuwapa baba zako Abrahamu, Isaki na Yakobo.

New International Version

Deuteronomy 30:1-20

Prosperity After Turning to the Lord

1When all these blessings and curses I have set before you come on you and you take them to heart wherever the Lord your God disperses you among the nations, 2and when you and your children return to the Lord your God and obey him with all your heart and with all your soul according to everything I command you today, 3then the Lord your God will restore your fortunes30:3 Or will bring you back from captivity and have compassion on you and gather you again from all the nations where he scattered you. 4Even if you have been banished to the most distant land under the heavens, from there the Lord your God will gather you and bring you back. 5He will bring you to the land that belonged to your ancestors, and you will take possession of it. He will make you more prosperous and numerous than your ancestors. 6The Lord your God will circumcise your hearts and the hearts of your descendants, so that you may love him with all your heart and with all your soul, and live. 7The Lord your God will put all these curses on your enemies who hate and persecute you. 8You will again obey the Lord and follow all his commands I am giving you today. 9Then the Lord your God will make you most prosperous in all the work of your hands and in the fruit of your womb, the young of your livestock and the crops of your land. The Lord will again delight in you and make you prosperous, just as he delighted in your ancestors, 10if you obey the Lord your God and keep his commands and decrees that are written in this Book of the Law and turn to the Lord your God with all your heart and with all your soul.

The Offer of Life or Death

11Now what I am commanding you today is not too difficult for you or beyond your reach. 12It is not up in heaven, so that you have to ask, “Who will ascend into heaven to get it and proclaim it to us so we may obey it?” 13Nor is it beyond the sea, so that you have to ask, “Who will cross the sea to get it and proclaim it to us so we may obey it?” 14No, the word is very near you; it is in your mouth and in your heart so you may obey it.

15See, I set before you today life and prosperity, death and destruction. 16For I command you today to love the Lord your God, to walk in obedience to him, and to keep his commands, decrees and laws; then you will live and increase, and the Lord your God will bless you in the land you are entering to possess.

17But if your heart turns away and you are not obedient, and if you are drawn away to bow down to other gods and worship them, 18I declare to you this day that you will certainly be destroyed. You will not live long in the land you are crossing the Jordan to enter and possess.

19This day I call the heavens and the earth as witnesses against you that I have set before you life and death, blessings and curses. Now choose life, so that you and your children may live 20and that you may love the Lord your God, listen to his voice, and hold fast to him. For the Lord is your life, and he will give you many years in the land he swore to give to your fathers, Abraham, Isaac and Jacob.