Kumbukumbu 30 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 30:1-20

Mafanikio Baada Ya Kumgeukia Bwana

130:1 Kum 11:26; Law 26:40-45; Kum 4:32; 29:28; 1Fal 8:47Wakati baraka hizi zote pamoja na laana nilizoziweka mbele yako zitakapokujia, nawe ukazitafakari moyoni popote Bwana Mungu wako atakapokutawanya miongoni mwa mataifa, 230:2 Kum 4:29-30hapo wewe na watoto wako mtakapomrudia Bwana Mungu wako, na kumtii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote kulingana na kila kitu ninachokuamuru leo, 330:3 Za 14:7; 53:6; 85:1; 126:4; Yer 30:18; 33:11; Eze 16:53; Yoe 3:1; Sef 2:7; Kum 13:17; Mwa 48:21; 11:4; Kum 4:27; Isa 11:11; Yer 12:15; 16:15; 26:4; 29:14; 48:47; 49:6ndipo Bwana Mungu wako atakapokurudisha kutoka utumwani na kukuhurumia, naye atakukusanya tena kutoka mataifa yote kule alikutawanya. 430:4 Isa 17:6; 24:13; 27:12; 40:11; 41:5; 49:5; 56:8; Eze 20:34, 41; 34:13; Za 19:6; Neh 1:8-9; Isa 11:12; 42:10; 43:6; 48:20; 62:11; Yer 31:8, 10; 50:2Hata kama umefukuziwa katika nchi ya mbali kiasi gani chini ya mbingu, kutoka huko Bwana Mungu wako atakukusanya na kukurudisha. 530:5 Yer 29:14; Kum 7:13Yeye Bwana atakurudisha katika nchi iliyokuwa mali ya baba zako, nawe utaimiliki. Naye atakufanya ufanikiwe sana na kukuzidisha kwa idadi kuliko baba zako. 630:6 Kum 6:24; 10:16; 6:5; Yer 32:29Bwana Mungu wako ataitahiri mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu ili mweze kumpenda kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote ukaishi. 730:7 Mwa 12:3; Kum 7:15Bwana Mungu wako ataweka laana hizi zote juu ya adui zako ambao wanakuchukia na kukutesa. 8Utamtii tena Bwana na kuzishika amri zake zote ninazokupa leo. 930:9 Yer 1:10; 24:6; 31:28; 32:41; 42:10; 45:4; Kum 28:63; Eze 34:27; Yer 32:41; 33:9; Sef 3:17; Lk 15:6, 10, 32; Yn 15; 11Ndipo Bwana Mungu wako atakapokufanikisha sana katika kazi zote za mikono yako na katika uzao wa tumbo lako, wadogo wa mifugo yako na mazao ya nchi yako. Bwana atakufurahia tena na kukufanikisha, kama alivyowafurahia baba zako, 1030:10 Kum 28:61; 4:29kama ukimtii Bwana Mungu wako, na kuzishika amri zake na maagizo yake ambayo yameandikwa katika Kitabu hiki cha Sheria, na kumgeukia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote.

Uzima Na Mauti

1130:11 Za 19:8; Isa 45:19-23; 63:1Ninachokuagiza leo sio kigumu sana kwako au usichokiweza. 1230:12 Mit 30:4; Rum 10:6; Yn 3:13Hakiko juu mbinguni, ili uulize, “Ni nani atakayepanda mbinguni kukileta na kututangazia ili tuweze kutii?” 1330:13 Ay 28:14; Rum 10:7Wala hakiko ngʼambo ya bahari, ili uulize, “Ni nani atakayevuka bahari kwenda kukichukua na kututangazia ili tupate kutii?” 1430:14 Kum 6:6; Rum 10:8La hasha! Lile neno liko karibu sana nawe; liko kinywani mwako na ndani ya moyo wako ili uweze kulitii.

1530:15 Mit 10:16; 11:9; 12:28; 3:1-2; Kum 28:11; Za 25:13; 106:5; Mwa 2:17; Kum 11:26Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo. 1630:16 Kum 6:5; 4:1; 32:17; Neh 9:29Ninakuamuru leo kwamba umpende Bwana Mungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, naye Bwana Mungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.

17Lakini kama moyo wako ukigeukia mbali ukawa huna utii, kama umevutwa kuisujudia miungu mingine na kuiabudu, 1830:18 Kum 8:19nakutangazia leo hii kwamba hakika utaangamizwa. Hutaishi maisha marefu katika nchi unayovuka Yordani kuiingia na kuimiliki.

1930:19 Kum 4:26; 11:26Leo ninaziita mbingu na nchi kama mashahidi dhidi yako kwamba nimeweka mbele yako uzima na mauti, baraka na laana. Basi sasa chagueni uzima, ili wewe na watoto wako mpate kuishi, 2030:20 Kum 6:5; 4:1; 8:3; 32:47; 10:20; Za 27:1; Yn 5:26; Mdo 17:28; Mit 3:22; Mwa 12:7; Za 37:3na ili upate kumpenda Bwana Mungu wako, uisikilize sauti yake na kuambatana naye. Kwa kuwa Bwana ndiye uzima wako, na atakupa wingi wa siku ili upate kuishi katika nchi aliyoapa kuwapa baba zako Abrahamu, Isaki na Yakobo.

Het Boek

Deuteronomium 30:1-20

Een belofte van zegen

1‘Als al deze dingen over u komen, de zegeningen en vervloekingen die ik heb opgenoemd, zult u tot het juiste inzicht komen terwijl u onder de volken leeft waarheen de Here u heeft verdreven. 2En als u in die tijd naar de Here, uw God, wilt terugkeren en u en uw kinderen zijn begonnen met heel hun hart de wetten en regels die ik u vandaag geef, te gehoorzamen, 3dan zal de Here, uw God, u uit uw gevangenschap redden. Hij zal u genade schenken, naar u toekomen en u bijeenbrengen uit alle volken waaronder Hij u heeft verspreid. 4Ook al zou u zich in de verste uithoeken van het heelal bevinden, Hij zal u vinden en terugbrengen naar het land van uw voorouders. 5Hij zal ervoor zorgen dat het u goed gaat, nog meer dan uw voorouders, en u in aantal doen toenemen.

6Hij zal de harten van u, uw kinderen en uw kleinkinderen reinigen, zodat u weer met hart en ziel van de Here, uw God, kunt houden. Zo zal Israël weer tot leven komen! 7-8 Als u terugkeert naar de Here en alle wetten en regels die ik u vandaag geef, gehoorzaamt, zal de Here uw God zijn vervloekingen van u afnemen en deze tegen uw vijanden richten, tegen hen die u haten en vervolgen. 9De Here, uw God, zal u voorspoed geven bij alles wat u doet. Hij zal u veel kinderen, veel vee en grote oogsten geven, want de Here zal opnieuw vreugde over u hebben, net als over uw voorouders. 10Hij zal blij met u zijn als u zijn geboden die in dit wetboek zijn geschreven, gehoorzaamt en u met hart en ziel wendt tot de Here, uw God.

11Want deze geboden zijn niet te moeilijk om nageleefd te worden. 12Deze wetten zijn niet hoog in de hemel zodat u ze niet kunt zien of horen en er niemand is die ze bij u kan brengen. 13Ze zijn ook niet aan de overkant van de zee, zo ver weg dat niemand u hun boodschap kan overbrengen. 14Nee, zij zijn vlakbij—in uw hart en op uw lippen—zodat u ze kunt gehoorzamen.

15Luister, vandaag heb ik u de keus gegeven tussen leven en dood, geluk en ellende. 16Ik heb u vandaag opdracht gegeven de Here, uw God, lief te hebben, zijn paden te volgen en zijn wetten na te leven. Dan zult u leven en een groot volk worden. De Here, uw God, zal u en het land dat u in bezit gaat nemen, dan zegenen. 17Maar als uw hart zich afwendt en u niet wilt luisteren—als u zich laat verleiden andere goden te aanbidden— 18dan verklaar ik u hier vandaag dat u zeker zult worden vernietigd, u zult geen lang en goed leven hebben in het land aan de overkant van de Jordaan. 19Hemel en aarde zijn mijn getuigen dat ik u vandaag de keus heb gegeven tussen leven en dood, zegen en vloek. Kies dan toch het leven, zodat u en uw kinderen mogen leven! 20Kies voor het liefhebben en gehoorzamen van de Here, uw God. Houd u aan Hem vast, want dat is uw leven. Dat verzekert u van een lang leven in het land dat de Here beloofde aan uw voorouders Abraham, Isaak en Jakob.’