Kumbukumbu 3 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 3:1-29

Kushindwa Kwa Ogu Mfalme Wa Bashani

(Hesabu 21:31-35)

13:1 Hes 21:33; 32:19Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei. 23:2 Yos 10:8; 2Fal 19:6; Isa 7:4Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”

33:3 Hes 21:24; 21:35Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja. 43:4 Hes 21:24, 33; 1Fal 4:13Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani. 5Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta. 63:6 Kum 2:24; Za 135:10-12; 136:19-21Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto. 73:7 Kum 2:35Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.

83:8 Hes 32:33; Yos 13:8-12; Kum 4:48; Yos 11:3; 12:1; 13:5; Amu 3:3; 1Nya 5:23; Za 42:6; 89:12; 133:3; Wim 4:8Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni. 93:9 Za 29:6; 89:12; 1Nya 5:23; Wim 4:8; Eze 27:5; Kum 4:48(Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.) 103:10 Yos 12:5; 13:11; 1Nya 5:11; Kum 4:49Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani. 113:11 Mwa 14:5; Yos 13:25; 15:60; 2Sam 11:1; 12:26; 17:27; 1Nya 20:7; Yer 49:2; Eze 21:20; 25:5; Amo 1:14; 2:9(Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa3:11 Dhiraa tisa ni sawa na mita 4. na upana wa dhiraa nne.3:11 Dhiraa nne ni sawa na mita 1.8. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)

Mgawanyo Wa Nchi Mashariki Ya Yordani

(Hesabu 32:1-42)

123:12 Kum 2:36; Hes 32:32-38; Yos 13:8-13Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake. 133:13 Kum 29:8; Mwa 14:5Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai. 143:14 Hes 32:41; Yos 12:5; 13:11-13; 2Sam 10:6; 23:34; 2Fal 25:23; 1Nya 4:19; Yer 40:8; Yos 19:46-47; Za 49:11; 1Nya 2:22Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.) 153:15 Mwa 50:23; Hes 32:39-40Nikampa Makiri nchi ya Gileadi. 163:16 Hes 21:24; 2Sam 24:5; Hes 21:24Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni. 173:17 2Sam 2:29; 4:7; Eze 47:8; Hes 34:11; 14:3; Yos 12:3; 13:27Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.

183:18 Yos 1:13; Hes 32:17Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli. 193:19 Yos 1:14; Hes 32:16Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa, 203:20 Yos 22:4mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”

Mose Akatazwa Kuvuka Yordani

21Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo. 223:22 Kum 1:29; 7:18; 20:4; 31:6; 2Nya 32:8; Za 23:4; Isa 41:10; Kut 14:143:22 Yos 23:10Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”

233:23 Kum 1:37; 31:2; 32:52; 34:4Wakati huo nilimsihi Bwana: 243:24 Kum 5:24; 11:2; 32:3; Kut 8:10; Za 71:16; 86:8; 106:2; 145:12; 150:2; 2Sam 7:22; Neh 9:32; Yer 32:18-21; Kut 15:11“Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe? 253:25 Kum 4:25; 1:7; Yos 1:4; 9:1; 11:17; 12:7; 13:5; Amu 3:3; 9:13; 1Fal 4:33Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”

263:26 Kum 1:37; 31:2Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena. 273:27 Hes 21:20; 27:12; Mwa 13:14; Hes 20:12; Kum 32:52Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani. 283:28 Hes 27:18-23; Kum 31:7; 1:38; 31:3-23Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.” 293:29 Hes 23:28; Kum 4:46; 34:6; Yos 13:20Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Deuteronomio 3:1-29

Derrota de Og, rey de Basán

1»Cuando tomamos la ruta hacia Basán, el rey Og, que gobernaba ese país, nos salió al encuentro en Edrey. Iba acompañado de todo su ejército, dispuesto a pelear. 2Pero el Señor me dijo: “No le tengáis miedo, porque os lo he entregado a vosotros, con todo su ejército y su territorio. Haced con él lo que hicisteis con Sijón, rey de los amorreos, que reinaba en Hesbón”.

3»Y así sucedió. El Señor nuestro Dios también entregó en nuestras manos al rey de Basán y a todo su ejército. Los derrotamos, y nadie vivió para contarlo. 4En aquella ocasión conquistamos todas sus ciudades. Nos apoderamos de las sesenta ciudades que se encontraban en la región de Argob, del reino de Og en Basán. 5Todas esas ciudades estaban fortificadas con altos muros, y con portones y barras, sin contar las muchas aldeas no amuralladas. 6Tal como hicimos con Sijón, rey de Hesbón, destruimos por completo las ciudades con sus varones, mujeres y niños, 7pero nos quedamos con todo el ganado y el botín de sus ciudades.

8»Fue así como en aquella ocasión nos apoderamos del territorio de esos dos reyes amorreos, es decir, de toda la porción al este del Jordán, desde el arroyo Arnón hasta el monte Hermón, 9al que los sidonios llaman Sirión y los amorreos, Senir. 10También nos apoderamos de todas las ciudades de la meseta, todo Galaad y todo Basán, hasta Salcá y Edrey, ciudades del reino de Og en Basán. 11Por cierto, el rey Og de Basán fue el último de los gigantes. Su cama3:11 cama. Alt. sarcófago. era de hierro y medía cuatro metros y medio de largo por dos de ancho.3:11 cuatro … ancho. Lit. nueve codos de largo y cuatro codos de ancho según el codo de un hombre. Todavía se la puede ver en Rabá de los amonitas.

División de la tierra

12»Una vez que nos apoderamos de esa tierra, a los rubenitas y a los gaditas les entregué el territorio que está al norte de Aroer y junto al arroyo Arnón, y también la mitad de la región montañosa de Galaad con sus ciudades. 13El resto de Galaad y todo el reino de Og, es decir, Basán, se los entregué a la media tribu de Manasés.

»Ahora bien, a toda la región de Argob en Basán se la conoce como tierra de gigantes. 14Yaír, uno de los descendientes de Manasés, se apoderó de toda la región de Argob hasta la frontera de los guesureos y los macateos, y a esa región de Basán le puso su propio nombre, llamándola Javot Yaír,3:14 Javot Yaír. Alt. poblados de Yaír. nombre que retiene hasta el día de hoy. 15A Maquir le entregué Galaad, 16y a los rubenitas y a los gaditas les entregué el territorio que se extiende desde Galaad hasta el centro del arroyo Arnón, y hasta el río Jaboc, que marca la frontera de los amonitas. 17Su frontera occidental era el Jordán en el Arabá, desde el lago Quinéret3:17 lago Quinéret. Es decir, lago de Galilea. hasta el mar del Arabá, que es el Mar Muerto, en las laderas del monte Pisgá.

18»En aquel tiempo os di esta orden: “El Señor vuestro Dios os ha dado posesión de esta tierra. Vosotros, los hombres fuertes y guerreros, pasad al otro lado al frente de vuestros hermanos israelitas. 19En las ciudades que os he entregado permanecerán solamente vuestras mujeres, vuestros niños y el mucho ganado que yo sé que tenéis. 20No podréis volver al territorio que os he entregado hasta que el Señor haya dado reposo a vuestros hermanos, como os lo ha dado a vosotros, y hasta que ellos hayan tomado posesión de la tierra que el Señor vuestro Dios les entregará al otro lado del Jordán”.

Instrucciones a Josué

21»En aquel tiempo le ordené a Josué: “Con tus propios ojos has visto todo lo que vuestro Señor y Dios ha hecho con esos dos reyes. Y lo mismo hará con todos los reinos por donde vas a pasar. 22No les tengas miedo, que el Señor tu Dios pelea por ti”.

Dios le prohíbe a Moisés cruzar el Jordán

23»En aquella ocasión le supliqué al Señor: 24“Tú, Señor y Dios, has comenzado a mostrarle a tu siervo tu grandeza y tu poder; pues ¿qué dios hay en el cielo o en la tierra capaz de hacer las obras y los prodigios que tú realizas? 25Déjame pasar y ver la buena tierra al otro lado del Jordán, esa hermosa región montañosa y el Líbano”. 26Pero por vuestra causa el Señor se enojó conmigo y no me escuchó, sino que me dijo: “¡Basta ya! No me hables más de este asunto. 27Sube hasta la cumbre del Pisgá y mira al norte, al sur, al este y al oeste. Contempla la tierra con tus propios ojos, porque no vas a cruzar este río Jordán. 28Dale a Josué las debidas instrucciones; anímalo y fortalécelo, porque será él quien pasará al frente de este pueblo y quien les dará en posesión la tierra que vas a ver”.

29»Y permanecimos en el valle, frente a Bet Peor.